Mjihadhari na huyu tapeli wa JF

Mjihadhari na huyu tapeli wa JF

Ameweka matangazo kadhaa kwamba anauza kuku/vifaranga, kumbe ni tapeli na anatumia njia ya laghai kudanganya watu humu jf kisha anapotea na pesa.
Naomba wengine waliokua na nia ya kuhitaji bidhaa kutoka kwa huyu bwana wachukue tahadhari.View attachment 655506
Hicho ni kiasi cha pesa nilio mtumia kwaajili ya kusafirishia mzigo.
View attachment 655507View attachment 655509View attachment 655510View attachment 655511View attachment 655512View attachment 655513View attachment 655514
Hizo ni conversations zangu na tapeli huyo wa jf.
User name yake ni nani?
 
Pole sana, tushamjuwa huyo, maana sisi tumo huko huko kwenye ufugaji, ngoja tumtangaze aisumize wengine...
Zuzu tu hilo, halijajuwa bahatai yake, lingeweza tengeneza pesa ya ukweli..
Nikweli mkuu
 
Ni sa hihi.
Jamaa hajataka hata kujua mzigo wake utafikia wapi hadi alipie hiyo nauli kakurupushwa tu akatuma nauli kakosea
Nikweli nilikurupuka mkuu, na ndiomaana nimekuja kutoa tahadhari ili wengine wasije wakakurupuka kama mimi
 
Ujue ni ujinga tu na upumbaf wa watu wachache kuwaharibia wengi...siku izi mambo kidigital just mawasiliano then mzigo unakufikia sema kupitia expansion joint huo wengne wanapiga deal.....mtu nipo Tanzania naagiza simu ya Lenovo naipata sembuse vifaranga, akichomwa moto huyo akili itamkaa sawa huko atakapokuwa anaishi kiroho.
Nikweli mkuu
 
Kwe kwekuna usafi umefanywa humu eeh?

Zile picha za bosi mtoto mbona sizioni?
 
User name yake ni nani?
Screenshot_2017-12-20-13-14-22.png

Hapo anasema yupo Morogoro
Screenshot_2017-12-20-13-14-47.png

Hapo anasema yupo Songea
 
Poleee mkuuu vyuma vimekaza biashara ya mtandaoni ni hatari sana
 
Maagizo kutoka juu...
Wamechelewa wakati wahenga tushazitia mikononi

Kuna mtu kataja hadi muhusika jinsia ke nikataka ku quote ghafla haipo

itakuwa wameliwa wengi kwa tabia zao za kupenda vinono bila sababu.
 
Mkuu....
Kwenye mazungumzo ya sim tulikubaliana kwamba atamkabidhi msafirishaji anae mfaham, kisha baada ya kuuona mzigo nilipaswa kutoa cash kabla sijauchukua
Pole kwa kutapeliwa ila siku nyingine usirudie kutuma fedha kwa mtu usiyemuamini (siyo usiyemjua kwa sababu hata unayemjua anaweza kukutapeli). Na umefnya vizuri kutoa tahadhari. Achana na hawa wanaogeuzia kibao nina uhakika ni hao hao matapeli/tapeli kwani matapeli wana ID hata kumi tofauti na kila moja ina kazi yake. Achana nao kabisa na wala usijieleze zaidi.
 
Nilivyosoma text conservation yenu nimegunduwa wewe ndio ulitaka kumtapeli mwenzako yani upewe vifaranga 100 kwa shilling 17,000/= tu.

acha kumchafuwa mwenzako hata tukienda mahakamani huu siyo ushahidi wa kuthibitisha umetapeliwa ni wewe ndio ulitaka kutapeli na pesa ya tapeli huwa haina refund.
Yani hiyo 17K ni ya usafiri. Kwahiyo jamaa angetoa vifaranga mia bure kabisa....
 
Back
Top Bottom