Mjihadhari na huyu tapeli wa JF

Mjihadhari na huyu tapeli wa JF

Nimesoma mkuu kila kitu! Mi nimestik hapo kwanza...

Na mbaya zaidi wewe nimeona ndie ulieanza kumwita mwenzio tapeli... bila ya kupima kama jamaa nayeye ana imani kiasi gani kwako... ulikurupuka
Huenda alikua muoga hata hiyo nauli kutuma.
Kuana vitu hutakiwi kujihusisha kabisaa kama huna imani.

Yeye ndo mtakaji halafu anataka kuaminiwa dah.
 
Hivi na yeye angetuma hao Vifaranga sijui 100 kwako wewe ambae hakujui, usingeweza na wewe kumtapeli??
Mkuu....
Kwenye mazungumzo ya sim tulikubaliana kwamba atamkabidhi msafirishaji anae mfaham, kisha baada ya kuuona mzigo nilipaswa kutoa cash kabla sijauchukua
 
Watu wamemgeuzia jamaa kibao kuw yeye ndiyo tapeli Aisee. Pole sana ndugu dhamira yako itakushuhudia. Mimi naona nia yako labda ilikuwa kutadharisha wengine lakini mambo yamekuwa tofauti. Kiukweli uluchofanya ni hasa hata mimi ningefanya sasa nikutumie pesa ya mzigo na sijaiona wala hatujuani hii ni ngumu. Yaani ilitakiwa jamaa akifika na mzigo unamkash lakini naoana watu wamekugeukia while nia yako ilikuwa nzuri tuu kufanya biashara na member mwenzako. Bado siamini kama nia yako ilikuwa kutapeli kisha ulete hii habari humu.
Hivi unatumaje nauli kwa mtu usiemjua?

Hivi inawezekana kweli kutuma mzigo bila hata advance yeyote?

Hivi hapo ni nani alitakiwa kua na khofu ya kupoteza anaetaka mzigo au mwenye mzigo?
 
Mwandiko wake tu unajua hamnazo
Ila siamini kama kweli mtu unaweza kufanya kitu serious humu na mtu usiemjua, wakati tunatumia majina fake na avatar fake
Wacha muingizwe mjini tu
Teh teh
 
Huenda alikua muoga hata hiyo nauli kutuma.
Kuana vitu hutakiwi kujihusisha kabisaa kama huna imani.

Yeye ndo mtakaji halafu anataka kuaminiwa dah.

Izi mambo kwa kweli zinahitaji uwe na imani haijalishi ww ni mnunuzi au mnunuaji, pengine jamaa wa watu nae alihisi kwamba mwana bodi hapa anataka amtapeli kwa 17 ndio maana akaomba na yeye alipe ya kuku 20 au 10
 
Nami ndo maana nimesema hvyo cku hz uungwana umepotea.Cjui huyu mwenzetu veep mbna wengine tunafanya biashara za mtandaon.sasa kuna ugumu gan wa mtu kumsafirishia mzgo huku pesa ya transport umesha pewa.
Cku zote uaminifu ni bora zaid ya hyo pesa mtu unayofikir kutapele,coz ukiwa mwaminifu unajiongezea wigo wa biashara yako.
Mimi Jiwedogo ndo na mlaumu si huyu.
Ukiingia vibaya lazima utapeliwe katuma nauli kwa uhakikagani wa kuletewa mzigo hapo tu kanikera?
 
Kazi ipo sijui kwanini kuna watu wana tabia ya kuharibu biashara za mitandaoni kiasi kwamba hata tunaofanya aina hizi za biashara tunaonekana waongo.Mkuu pole kwa yaliyokukuta siku ingine chukua tahadhari unapofanya biashara za mitandaoni ni vizur ujue kwanza ofisi ya muhusika ilipo ndo utume hela.
Kweli kabisa...
 

Nimetoa tahadhari tu mkuu, kwani sioni ubaya kuwatahadharisha wengi kupitia mimi
Pole sana, tushamjuwa huyo, maana sisi tumo huko huko kwenye ufugaji, ngoja tumtangaze aisumize wengine...
Zuzu tu hilo, halijajuwa bahatai yake, lingeweza tengeneza pesa ya ukweli..
 
biashara za mtandaoni zina term kuu 3
1 tukutane sehemu tufanye hiyo biashara mkono kwa mkono
2. tuma ela nikutumie mzigo unafika mpaka mlangoni(hii inategemea source ikiwa ni mtandao ambao unabeba dhamana au kupitia kwa mtu mnafahamiana na kukiwa na halufu ya utapeli
kwa mfano KUPATANA wanakwambia kabisa NEVER PAY IN ADVANCE coz wao hawabebi dhamana ya pesa yako tofauti na mitandao mingne ambapo wanabeba dhamana ya pesa ikiwa mambo yatakwenda sivyo ndivyo )
3.mpaka mzigo niuone ndo natoa ela.
km mnakubaliiana hivyo ni yeye mwenye budhaa kuwa na chanzo cha uhakika sehemu anapotuma bidhaa inamaana ufike sehemu fulani utakuwepo mzigo uone ukiridhika toa ela
tushatuma sana vitu kwenye basi au malori unaongea na konda au dereva huyo mtu mpokeaji akiuona mzigo na akihakikisha upo sawa anakupa cash ndo unampa mzigo
so alichofanya jamaa hadi kuhisi katapeliwa ni sawa coz walikubaliana ilipwe nauri tu!
mzigo ukifika salama mkononi mwake inalipwa pesa yote ya thamani ya mzigo lkn dr ndele akaanza annoying zisizo na mashiko zilizomuogopesha jamaa mpk akaamua ghairi biashara
ilitakiwa tangu mwanzo wa biashara aweke condition kuwa unalipia nauri na asirimia 25 sio mtu ushatuma nauri na kukubalianaa then unaanza mambo mengne ambayo hayakukuapo katika PACT wakati mwanzo mnaanza biashara
ingawa si vema kumuita TAPERI ila dr ndele alikosea ilitakiwa amjibu chochote jamaa kuliko kukaa kimya sms ajibu simu hupokei
lazima uonekane ni mbabaishaji na tapeli
Ni sa hihi.
Jamaa hajataka hata kujua mzigo wake utafikia wapi hadi alipie hiyo nauli kakurupushwa tu akatuma nauli kakosea
 
Ujue ni ujinga tu na upumbaf wa watu wachache kuwaharibia wengi...siku izi mambo kidigital just mawasiliano then mzigo unakufikia sema kupitia expansion joint huo wengne wanapiga deal.....mtu nipo Tanzania naagiza simu ya Lenovo naipata sembuse vifaranga, akichomwa moto huyo akili itamkaa sawa huko atakapokuwa anaishi kiroho.
 
Mimi Jiwedogo ndo na mlaumu si huyu.
Ukiingia vibaya lazima utapeliwe katuma nauli kwa uhakikagani wa kuletewa mzigo hapo tu kanikera?
Ruhsa kunilaumu mkuu, na ninapo kosea sioni ubaya kukubali kosa.
Kikubwa hapa nimeleta tahadhari ili nawengine wasikosee kama mimi
 
Izi mambo kwa kweli zinahitaji uwe na imani haijalishi ww ni mnunuzi au mnunuaji, pengine jamaa wa watu nae alihisi kwamba mwana bodi hapa anataka amtapeli kwa 17 ndio maana akaomba na yeye alipe ya kuku 20 au 10
Inawezekana mkuu
 
Ruhsa kunilaumu mkuu, na ninapo kosea sioni ubaya kukubali kosa.
Kikubwa hapa nimeleta tahadhari ili nawengine wasikosee kama mimi
Nimekusoma mkuu.

Kuna swali nilikuuliza huko juu hujajibu ila lipo nje ya mada
 
Back
Top Bottom