Mji wa Moshi na mavazi ya akina dada!

Filipo

JF-Expert Member
Jan 6, 2011
9,342
5,536
Nipo hapa stand ya mabasi Moshi mjini ambapo dada mmoja amepata msaada kutoka kwa konda aliyemwingiza kwenye basi (kosta) ili kumwokoa kutoka kwenye kundi la vijana waliokuma wakimzomea na kumzodoa kutokana na mavazi aliyokuwa amevaa. Dada huyo aliyekuwa amevaa skin tight inayopita magotini na t shirt iliyombana na inafunika nusu ya makalio alijikuta hana la kufanya hadi alipookolewa na konda kwa kumwingiza kwenye gari yake iliyokuwa kwenye foleni na kufunga vioo vyote. Nilichokigundua baada ya kuuliza mwenyeji nimegundua hilo ni jambo la kawaida kwa mji wa Moshi na limekuwa likifanyika karibu kila siku. Waathirika wakuu ni wageni maana wenyeji wanafahamu. Kina dada mkija Moshi mjipange sawasawa!
 
Hahahaaa!! Wadada nao wamezidi kuvaa hizo Soksi zao cjui mnaziita tyt!!!
Wengine hawana hata shepu wakivaa hvo kama vikatuni vile!!!
 
Vijana walikuwa wanasema "huu ndio mji wa Moshi, hatutaki uhuni hapa". Binafsi nimekosa conclusion. Sijui ndio kutetea utamaduni au ni ushamba maana Moshi hakuna ziwa wala bahari!
 
Vijana walikuwa wanasema "huu ndio mji wa Moshi, hatutaki uhuni hapa". Binafsi nimekosa conclusion. Sijui ndio kutetea utamaduni au ni ushamba maana Moshi hakuna ziwa wala bahari!


Moshi Moshi moshi na Benedict Kinabo! Nilidhani jamaa ni mahodari wa kudhibiti uchafu mjini kwao kwa maana ndio mji ambao huwezi kutema mate, kutupa vichungi vya sigara na hata kukojoa hovyo!

Kumbne mna sifa nyingine? Safi sana, wakomesheni kabisa hao wadada wasio na aibu!
 
Hao vijana wahuni tu.........jioni wa kwanza kwenye hiki kiota

3185426396_6d3d999935.jpg
 
Back
Top Bottom