Lizarazu
JF-Expert Member
- Aug 23, 2015
- 6,331
- 7,885
Nikiangalia zamani na sasa naona utouti mkubwa kwa wanaume na wanawake.
Tofauti na zamani wanaume wengi wa sasa nikienda hospitali au klinic wapo clinic wenyewe wake zao na watoto au wao na watoto, ukitembea pia barabarani au mtaani unaona pia wanaume na watoto wao wamewabeba.
Naona kabsa utandawazi umefanya wanaume wengi kujali wake zao kwa kuwasaidia kazi mbalimbali za kulea na za nyumbani kama kufua, kupika, kuosha vyombo hata kuogesha watoto lakini ukweli ambao ninao wanaume wengi wanaoishi kwa kujali familia zao ndio zinaongoza kwa migogoro na break up.
Sasa hapa ttzo lipo wapi kwa wanaume, wanawake wanapenda Mwanaume wa namna gani.
Nikiangalia familia ambazo wanaume ndio final say ndio zinaongoza kwa kudumu sana.
Hapo tatizo ni la wanawake lakini limeanzia kwa wanaume kwa misingi ifuatayo;
1.Walifanya machaguzi mabaya tangu awali kwa kuoa wanawake waliopoteza haiba ya kike(alpha female) wakitembelea ile dhana isiyokuwa na uhalisia “mwanaume kujiamini” mwisho wa siku wakajikuta wanaishi kwa kuvumlia mwanamke hatimae wakaona ni heri kuuwa ndoa.
2.Kukubali mtu anayetumia hisia(emotion) awe na nguvu sawa au kuliko wewe ya maamuzi ndani ya ndoa, hapo jahazi haliendi na mwisho wa siku lazima lizame tu.
3.kugawana madaraka na mtu ambaye hakuumbwa kushika madaraka hata kidogo, maana hata yeye mwenyewe hajui kutumia hayo madaraka bila kuleta tafrani.
4.kujifanya unaleta diplomasia kwenye mambo yasiohitaji diplomasia hata kidogo na hili ndio mzizi wa yote.
Pongezi kwa wale wote ambao bado wanaishi kwa kufuata mfumo uliowekwa na Mungu tangu dunia inaanzishwa, definitely wao ndio wana enjoy ndoa!