Extrovert
JF-Expert Member
- Feb 29, 2016
- 72,402
- 191,524
Wanaendesha ndoa za kwa katiba ya kiislam ambapo 80% ya vipengele ni mfumo dume. Pia kitabu kimedhibiti sana tamaa, kule ukifanya upumbavu hukawilii kupigwa mawe hadi ufe, hukawili kunyongwa au kuchinjwa kama kuku sasa nani anataka afe kwa tamaa za mda mchache japo maovu yanafanyika ila ni very rare na kwa usiri mkubwa sana.All hail to you master!
Your school of thought deserves some noble accolades.
Na hiki unachokisema ndio msingi wa familia/ndoa nyingi zenye afya yaani zisizokuwa na drama wala mitikisiko ya aina yoyote.
Mfano mzuri ni familia za Middle East huko,Oman,Saudi,Iran,Qatar n.k
Huwezi kuskia kesi au migoro mogoro ya ki familia zimekithiri ukanda ule
Huwezi kuskia wanawake wanaandama eti waruhusiwe kuwa wanatoa mimba huko uarabuni.
Huwezi kuskia wanaandamana eti waruhusiwe kutembea nusu uchi huko uarabuni.
Huwezi kuskia mwanamke anajiamulia kumiliki kitu pasipo kumshirikisha mme wako halafu akizongwa zongwa sana anakimbilia mahakamani.. huko uarabuni.
Huwezi kuskia idadi ya talaka zikiongezeka kihole holela tu huko uarabuni.
Ni ngumu kuskia visa vya ajabu ajabu kama kuuana kwa kuchomana moto sababu ya usaliti huko uarabuni.
Huko uarabuni nadhani ndio sehemu pekee ambapo wanaweza wakajisifu wana Family stability katika dunia hii.
Kikubwa hawatumii mambo ya gender balance kule so lazma mambo yawe mazuri tu.Mke ni pambo na chombo cha starehe kwa mumewe na hilo wanalijua na kuliheshimu. Huku shida ni mfumo wa haki sawa maana kimsingi hakuna mwanaume anaeshindwa kumhudumia mkewe na familia kwa mahitaji muhimu ila tamaa za mke ndio anaona bora afanye kazi awe sawa au zaidi ya mume maana wameaminishwa mume akiwa juu atamnyanyasa so hata kufanya majukumu yake kwa mume anaona manyanyaso. Anataka kama akienda kazini basi wote mpange zamu ya kupika, kudeki na kufua nguo zenu na za watoto.
Just angalia before mifumo ya kijinga ya gender balance ndoa zilikuwa imara na kuolewa ilikuwa kitu kikubwa na cha maana mno so mke na mume walipikwa vizuri na walikuwa wanajua nini maana ya ndoa na utayari ila sikuhizi ndoa ni uwezo wako tu kifedha swala la utayari halizingatiwi.
Ukiweza kulipa mahari na kulisha watu ukumbini basi unakuwa umeoa tayari. Baada ya mwaka mmeshindwana kila mtu anachukua 50 zake.