Mjadala: Muziki sio Haramu. Inategemea na uimbaji wake

Unajua unacho kiandika na unarejea kwenye nini ?

Kwami vipasa sauti ni sharti la kukubaliwa ibada ya mtu ?

Nakuuliza tena unakijua unachokijadili ?


Mkuu mambo haya yanahitaji uelewa mdogo tuu.

Sio kila kitu kilichotumika zamani kwenye dini kitumike sasa hivi.

Muhimu ni zile amri za MUNGU ambazo ndio amri za Asili za ulimwengu.
 
...Hata huo muziki wa Qaswida au injili ukiimbwa kilabuni ni haramu Kwa sababu umeimbwa sehemu isiyosahihi.
Labda hiyo qaswida maana siijui na siwezi kuisemea, lakini muziki wa injili ni halali kuimbwa popote hata kilabuni
 
MUZIKI SIO HARAMU; INATEGEMEA NA UIMBAJI WAKE

Anaandika Robert Heriel.

Ipo kasumba Kwa baadhi ya watu wenye Elimu ndogo ya Kidini na kiroho isemayo muziki mi haramu. Dhana hii ni potofu na upotofu wake unatokana na ufinyu wa elimu zote mbili yaani elimu Dunia na elimu Akhera.

Muziki sio haramu. Muziki ni Sanaa inayotumia ALA/vyombo vya muziki pamoja na sauti ya mwanadamu au kiumbe yeyote.
Muziki Kama Sanaa unalenga kuonyesha uzuri na ustadi wa mchanganyiko wa sauti zenye ladha zinazoburudisha. Muziki husisimua, hutia simanzi, huamsha Raha moyoni. Hata hivyo muziki ukiingiziwa nyimbo, au tenzi, au tendi au aina yoyote ya vipera vya ushairi huwa na dhima kadhaa WA kadha, mathalani; kuburudisha, kuelimisha, kukosoa, kuonya, kufunza, kuhamasisha, kutunza Mila na desturi miongoni mwa dhima zingine.

Muziki haujaanza Jana wala leo, tangu kale na kale na mpaka milele Daima muziki utakuwepo. Matumizi ya Ngoma, zeze, santuri, gitaa, filimbi, kinanda, marimba miongoni mwa ALA zingine za Muziki yatadumu milele zote. Ukuaji wa Teknolojia hukuza muziki na kuubadilisha katika viwango vingine vikuu.

Zipo Aina nyingi za Muziki, miongoni mwazo ni Muziki wa Kidini(muziki wa injili na muziki wa Qaswida Kwa waislam), BongoFleva, RnB, Rumba, Amapiano, Hip hop, Pop miongoni mwa Aina zingine.

Kila muziki Una Aina yake ya uwasilishwaji. Hata hivyo muziki yote lengo lake ni kuijenga jamii.

Muziki ni KAZI Kama KAZI zingine.
Ni KAZI halali na inayopaswa kuheshimiwa.
Na hapa nazungumzia Muziki wa kidunia kuacha hii muziki ya Dini(injili na Qaswida).

Muziki wa kidunia ni Halali ikiwa utatumika Kama ulivyokusudiwa.
Ikiwa wanamuziki watalenga kuweka maudhui yanayojenga jamii katika muziki wao.

Hatuwezi kumtaja Mungu kwenye kila Jambo. Kumtaja Mungu kwenye kila Jambo ni matumizi mabovu ya Uelewa. Mungu mwenyewe katika amri zake keshakataza jina lake lisitajwe bure ikiwa hakuna ulazima wa kufanya hivyo.

Yesu alikuwa anamsemo usemao; Ya Kaisari mpe Kaisari na Yamungu Mpe Mungu.

Kutojua kutenganisha mambo ni Dalili ya ujinga Kama sio upumbavu.

Lazima ujue kutofautisha vitu vilivyowekwa wakfu na vitu vya kawaida. Hiyo ndio Dalili ya werevu.

Muziki ni haramu Kama utashawishi watu kufanya maovu. Muziki ni haramu Kama utahamasisha watu kumuasi Mungu. Muziki ni haramu ikiwa wanamuziki wataimba matusi, watavaa mavazi ya kishetani katika Mazingira yasiyo wataka kufanya hivyo.

Muziki ni Kama ualimu, Udaktari, uhasibu, Uaskari, Uanasheria miongoni mwa KAZI zingine.
Ualimu ni haramu ikiwa mwalimu atafundisha mambo yasiyofaa, mambo yanayoharibu jamii
Udaktari halikadhalika na kazi zingine.

Uharamu ni kitendo cha kufanya Jambo kinyume na inavyotakiwa, kufanya Jambo linalodhuru na kuharibu jamii. Huo ndio uharamu.

Muziki wa kidunia unaokatazwa na Mungu ni ule unapojaribu maadili ya jamii, unaofunza watu roho mbaya, unaodhalilisha utu WA binadamu, unaodhalilisha kazi za uumbaji wa Mungu, huo ndio muziki unaokatazwa.

Watu wa dini wasipotoshe na kuiharibu jamii kuwa watu wasiimbe nyimbo za kidunia kuwa ni dhambi, isipokuwa wawafundishe watu maadili ili wasiimbe mambo yanayoharibu jamii.

Tumezaliwa Duniani, Sisi ni wadunia, Duniani ndio kwetu, kwa nini tusiiimbe nyimbo za kikwetu(kidunia), hatuwezi kuwa na mtazamo Hasi Kwa kila kitu kwenye dunia hii.
Dunia ndio Mama yetu, Baba yetu ni MUNGU. Sio kosa kuimba za kidunia ikiwa hatutukani, hatudhalilishi yeyote, hatuvunji sheria za nchi na maadili yetu kulingana na tamaduni zetu.

Huwezi muimbia mchumba wako nyimbo na muziki mzuri alafu ukaiita hiyo ni yadini utakuwa umechanganyikiwa,
Hata Suleiman katika wimbo uliobora anatupa mfano Bora wa namna nyimbo za kidunia zinavyopaswa kuwa. Kwa maana wimbo uliobora sio wimbo wa dini isipokuwa ni wimbo wa kidunia ambao Suleiman alikuwa akimuimbia Mpenzi wake.

Wito Kwa Wasanii wa muziki;
Jitahidini muimbe nyimbo zenu Kwa kufuata maadili ya utamaduni wa jamii yetu ili kuondoa hii Dhana potofu kuwa muziki ni haramu, Kwa maana Kama mtaimba nyimbo zinazohamasisha mambo haramu basi mnaufanya muziki wenu uitwe haramu.
Na hii itawafanya msiheshimike.

Baadhi ya wanamuziki ndio mnafanya kazi ya muziki idharauliwe na ninyi pia mdharaulike.
Sio ajabu kijana mwanamuziki akakosa mchumba kwenye familia inayojielewa Kwa sababu ya kuimba upumbavu.

Mwanamuziki unaweza kuwa na mafanikio makubwa ya kiuchumi na kufahamika Kwa watu lakini kutokana na nyimbo zenu mkadharaulika tuu.


Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
MPAGANI MKUBWA WEWE. KWAMBA DUNIANI NDIO KWETU WANADAMU! HIVI KWELI WEWE NI MKRISTO UNAYESOMA BIBLIA? UA NYINYI NDIYO WALE WA MISALE NA LITURGIA!
KUNA NYIMBO HATA MIDUNDO YA MUZIKI HAIMPI BWANA YESU KRISTO UTUKUFU. NI CHUKIZO. UNAJUA NYINYI WAKRISTO TANGU MLIPOAMUA KUMWASI ROHO MTAKATIFU AKAWAACHA, MUMEBAKI MNATUMIA AKILI ZENU ZISIZOFAA KUMWABUDU MUNGU.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Sio kila kitu walichofanya mitume nawewe ukifanye ndio kuonyesha kwamba ni halali, au vile ambavyo hawajafanya mitume basi ni dhambi kuvifanya

Mbona mitume haikutumia vipaza sauti na maspeaker kwenye mahubiri, kwa hiyo na hiyo ni dhambi?

Utahitaji kutafuta andiko lililoruhusu matumizi ya speakers na vipaza sauti kwenye mahubiri ili ujue ni halali au haramu?
Unamaanisha nini mkuu kusema hivi ?
 

 
MPAGANI MKUBWA WEWE. KWAMBA DUNIANI NDIO KWETU WANADAMU! HIVI KWELI WEWE NI MKRISTO UNAYESOMA BIBLIA? UA NYINYI NDIYO WALE WA MISALE NA LITURGIA!
KUNA NYIMBO HATA MIDUNDO YA MUZIKI HAIMPI BWANA YESU KRISTO UTUKUFU. NI CHUKIZO. UNAJUA NYINYI WAKRISTO TANGU MLIPOAMUA KUMWASI ROHO MTAKATIFU AKAWAACHA, MUMEBAKI MNATUMIA AKILI ZENU ZISIZOFAA KUMWABUDU MUNGU.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app



😀😀😀😀

Kwenu ni wapi Sheikhe???

Wewe ni mavumbi na mavumbi utarejea.

Hii dunia mnaikana Kwa sababu mumeiharibu 😀😀😀

Embu nijulishe kwenu wapi?
 
Unajua unacho kiandika na unarejea kwenye nini ?

Kwami vipasa sauti ni sharti la kukubaliwa ibada ya mtu ?

Nakuuliza tena unakijua unachokijadili ?
Sirejei kwenye kitu

Sijaelewa ulicho kiandika
 
Watu wamekua wakiishi kwa kuangalia kila kitu walichofanya hao manabii wa kale wakiamini kila kinachoenda kinyume na hapo basi ni dhambi
Kwa namna fulani nakubaliana na wewe.

Japokuwa yako mengi watu wanayasema kwamba ni maamrisho ya manabii lakini uhalisia wake ni maamrisho ya ufahamu wao.

Kwa kiasi fulani nakubali usemacho.
 
MUZIKI SIO HARAMU; INATEGEMEA NA UIMBAJI WAKE

Anaandika Robert Heriel.

Ipo kasumba Kwa baadhi ya watu wenye Elimu ndogo ya Kidini na kiroho isemayo muziki mi haramu. Dhana hii ni potofu na upotofu wake unatokana na ufinyu wa elimu zote mbili yaani elimu Dunia na elimu Akhera.

Muziki sio haramu. Muziki ni Sanaa inayotumia ALA/vyombo vya muziki pamoja na sauti ya mwanadamu au kiumbe yeyote.
Muziki Kama Sanaa unalenga kuonyesha uzuri na ustadi wa mchanganyiko wa sauti zenye ladha zinazoburudisha. Muziki husisimua, hutia simanzi, huamsha Raha moyoni. Hata hivyo muziki ukiingiziwa nyimbo, au tenzi, au tendi au aina yoyote ya vipera vya ushairi huwa na dhima kadhaa WA kadha, mathalani; kuburudisha, kuelimisha, kukosoa, kuonya, kufunza, kuhamasisha, kutunza Mila na desturi miongoni mwa dhima zingine.

Muziki haujaanza Jana wala leo, tangu kale na kale na mpaka milele Daima muziki utakuwepo. Matumizi ya Ngoma, zeze, santuri, gitaa, filimbi, kinanda, marimba miongoni mwa ALA zingine za Muziki yatadumu milele zote. Ukuaji wa Teknolojia hukuza muziki na kuubadilisha katika viwango vingine vikuu.

Zipo Aina nyingi za Muziki, miongoni mwazo ni Muziki wa Kidini(muziki wa injili na muziki wa Qaswida Kwa waislam), BongoFleva, RnB, Rumba, Amapiano, Hip hop, Pop miongoni mwa Aina zingine.

Kila muziki Una Aina yake ya uwasilishwaji. Hata hivyo muziki yote lengo lake ni kuijenga jamii.

Muziki ni KAZI Kama KAZI zingine.
Ni KAZI halali na inayopaswa kuheshimiwa.
Na hapa nazungumzia Muziki wa kidunia kuacha hii muziki ya Dini(injili na Qaswida).

Muziki wa kidunia ni Halali ikiwa utatumika Kama ulivyokusudiwa.
Ikiwa wanamuziki watalenga kuweka maudhui yanayojenga jamii katika muziki wao.

Hatuwezi kumtaja Mungu kwenye kila Jambo. Kumtaja Mungu kwenye kila Jambo ni matumizi mabovu ya Uelewa. Mungu mwenyewe katika amri zake keshakataza jina lake lisitajwe bure ikiwa hakuna ulazima wa kufanya hivyo.

Yesu alikuwa anamsemo usemao; Ya Kaisari mpe Kaisari na Yamungu Mpe Mungu.

Kutojua kutenganisha mambo ni Dalili ya ujinga Kama sio upumbavu.

Lazima ujue kutofautisha vitu vilivyowekwa wakfu na vitu vya kawaida. Hiyo ndio Dalili ya werevu.

Muziki ni haramu Kama utashawishi watu kufanya maovu. Muziki ni haramu Kama utahamasisha watu kumuasi Mungu. Muziki ni haramu ikiwa wanamuziki wataimba matusi, watavaa mavazi ya kishetani katika Mazingira yasiyo wataka kufanya hivyo.

Muziki ni Kama ualimu, Udaktari, uhasibu, Uaskari, Uanasheria miongoni mwa KAZI zingine.
Ualimu ni haramu ikiwa mwalimu atafundisha mambo yasiyofaa, mambo yanayoharibu jamii
Udaktari halikadhalika na kazi zingine.

Uharamu ni kitendo cha kufanya Jambo kinyume na inavyotakiwa, kufanya Jambo linalodhuru na kuharibu jamii. Huo ndio uharamu.

Muziki wa kidunia unaokatazwa na Mungu ni ule unapojaribu maadili ya jamii, unaofunza watu roho mbaya, unaodhalilisha utu WA binadamu, unaodhalilisha kazi za uumbaji wa Mungu, huo ndio muziki unaokatazwa.

Watu wa dini wasipotoshe na kuiharibu jamii kuwa watu wasiimbe nyimbo za kidunia kuwa ni dhambi, isipokuwa wawafundishe watu maadili ili wasiimbe mambo yanayoharibu jamii.

Tumezaliwa Duniani, Sisi ni wadunia, Duniani ndio kwetu, kwa nini tusiiimbe nyimbo za kikwetu(kidunia), hatuwezi kuwa na mtazamo Hasi Kwa kila kitu kwenye dunia hii.

Dunia ndio Mama yetu, Baba yetu ni MUNGU. Sio kosa kuimba za kidunia ikiwa hatutukani, hatudhalilishi yeyote, hatuvunji sheria za nchi na maadili yetu kulingana na tamaduni zetu.

Huwezi muimbia mchumba wako nyimbo na muziki mzuri alafu ukaiita hiyo ni yadini utakuwa umechanganyikiwa,
Hata Suleiman katika wimbo uliobora anatupa mfano Bora wa namna nyimbo za kidunia zinavyopaswa kuwa. Kwa maana wimbo ulio bora sio wimbo wa dini isipokuwa ni wimbo wa kidunia ambao Suleiman alikuwa akimuimbia Mpenzi wake.

Wito Kwa Wasanii wa muziki;
Jitahidini muimbe nyimbo zenu Kwa kufuata maadili ya utamaduni wa jamii yetu ili kuondoa hii Dhana potofu kuwa muziki ni haramu, Kwa maana Kama mtaimba nyimbo zinazohamasisha mambo haramu basi mnaufanya muziki wenu uitwe haramu.
Na hii itawafanya msiheshimike.

Baadhi ya wanamuziki ndio mnafanya kazi ya muziki idharauliwe na ninyi pia mdharaulike.
Sio ajabu kijana mwanamuziki akakosa mchumba kwenye familia inayojielewa Kwa sababu ya kuimba upumbavu.

Mwanamuziki unaweza kuwa na mafanikio makubwa ya kiuchumi na kufahamika Kwa watu lakini kutokana na nyimbo zenu mkadharaulika tuu.

Acha nipumzike sasa

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Si kila halali kwako iwe halali kwa wote, na si kila haramu kwako iwe haramu kwa wote.
Kwetu muziki ni haramu, itabakia kuwa haramu mpaka siku ya mwisho.
kuna wanaofuata matamanio ya nafsi zao, wakatumia mikono yao (KUANDIKA) na vinywa vyao ((KUHUBIRI) wakahalalisha iliyo haramishwa na wakaharamisha iliyohalalishwa hawa ni waovu kupikndukia.
 
Si kila halali kwako iwe halali kwa wote, na si kila haramu kwako iwe haramu kwa wote.
Kwetu muziki ni haramu, itabakia kuwa haramu mpaka siku ya mwisho.
kuna wanaofuata matamanio ya nafsi zao, wakatumia mikono yao (KUANDIKA) na vinywa vyao ((KUHUBIRI) wakahalalisha iliyo haramishwa na wakaharamisha iliyohalalishwa hawa ni waovu kupikndukia.


Nipe Aya ya Qurani iliyoharamisha muziki.

Usinipe hadithi za mtume Muhammad na Mswahaba wake. Hayo tunahachukulia Kama maoni ya Waandishi au manabii na mitume ambao ni Binadamu Kama Sisi tuu
 
Si kila halali kwako iwe halali kwa wote, na si kila haramu kwako iwe haramu kwa wote.
Kwetu muziki ni haramu, itabakia kuwa haramu mpaka siku ya mwisho.
kuna wanaofuata matamanio ya nafsi zao, wakatumia mikono yao (KUANDIKA) na vinywa vyao ((KUHUBIRI) wakahalalisha iliyo haramishwa na wakaharamisha iliyohalalishwa hawa ni waovu kupikndukia.
Mkuu unaweza kunipa marejeo katika uislamu yakielezea nini maana ya muziki ?
 
Nabii tito alishawahi kusema "shetani hawezi kuwa na kila kitu kizuri"

c3288fb2-bb10-4410-9bf7-f6cd34daa697.jpg
 
-Mwanzilishi wa Muziki ni Mungu mwenyewe
-Musiki ulikusudiwa kwa ajili ya Ibada
-Lusifa kabla ya kuasi ndie aliyeumbwa na aina za vyombo vya musiki (Ezekiel 28:13)
-Lusifa alipoasi amegeuza matumizi ya asili ya Musiki wa Ibada kwa mwenyezi Mungu
uwe kwa ajili ya ibada zake

Nguvu ya Muziki
-Musiki unaweza kufukuza mashetani au kukaribisha mashetani
-Musiki wa kimbingu hufukuza mashetani (kumbuka kisa cha sauli kutoka mapepo kwa -muziki tu)
-Musiki unaweza kualika uwepo wa Mungu katika Ibada
-Musiki unaweza kualika uwepo wa mashetani katika ibada (angalia ngoma za mashetani za tanga/pwani zinavyopigwa watu hushikwa na mapepo.
-Musiki unaweza kufanya uue
-Musiki unaweza kukufanya uzini hata kama hukuwa na lengo
-Musiki unaweza kukufanya kumchagua mtu kwenye cheo hata kama hukunia
-Musiki unaweza kukufanya ununue bidhaa fulani hata kama hukudhamiria (ndio maana matangazo ya TV radio huanza na musiki)
Kwa ujumla Muziki huweza kuteka maamuzi yako

13 "Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari." Ezekiel 28:13

-Musiki wa Ibada za Mwenyezi Mungu na Za shetani hutofautiana kwa namna tu unavyopigwa.
1.Mapigo 3/4 na 4/4 ndio mapigo ambayo huendana na mapigo ya moyo na huu ndio muziki ambao haupagawishi.
2. Ukitaka mtu ambaye hachezi musiki acheze ongeza kati ya mapigo kwa kadiri kasi inavyozidi ndivyo kupagawa huzidi basi hapa ndipo ibada huchafuka na kuwa makelele na mazingira hayo ndio rafiki kwa shetani.

Singeli na kupagawa
1.Katika miondoko ya singeli kasi ya vyombo inavyozidi ndivyo kupagawa huongezeka
na wanawake huvua nguo.(kinachofanyika hapa ni kuchanganya vyombo vingi na kuongeza kasi ya mapigo)
2.Kasi ya mapigo ya musiki katika nyimbo za ibada ndio sababu kubwa ya kupagawa katika ibada na hii ndio asili ya makanisa ya wamarekani weusi, ambao tumeiga makanisa yao.
na huu hudhaniwa ni utendaji wa roho mtakatifu.

Nukuu "Nioneshe musiki wa taifa lako, nitakuambia maadili ya taifa lako"
 
Soma kitabu cha wimbo uliobora utaona muziki wa kidunia aliouimba Suleiman.

Daudi yeye alicheza muziki mpaka akavua nguo.

Zipo sherehe nyingi Sana ambazo muziki ulipigwa
Naomba niulize swali? Daudi pia alizini kwa hivyo kuzini ni halali?. Kwa sababu daudi kafanya Jambo baya haihalalishi Hilo Jambo kuwa zuri. Ndio maana tumetakiwa tufanye Yale mapenzi ya Mungu pekee. Jambo unalofanya jiulize je hili Jambo linampendeza Mungu? Kama halimpendezi Mungu liache.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom