ni normal kupiga mnada gari la transit au unazungumzia nini mkuu hao uliosema ni local tunazungumzia transit goods au..nani anaechanganya mada hapo..
Tuweke hivi naongolea UK na DRC nchi ambazo nna experience nazo kikazi.
Kama ukisoma post ya nyuma nikakupigia hesabu namna unavyoweza kuingiza LCD TV 200 Tanzania kutoka UK Na kupata faida ya shs mil 60.
Lakini hizo TV zinakuwa zimepakiliwa kwenye gari ambalo nilikuwekea picha ambalo linakuwa linakwenda Congo via Dar es Salaam Port.
Sasa Bandari ilivyokuwa kwa sababu mzigo upo ndani ya gari Na haujawa declared kwenye Bill of Lading hauulipiikitu, wewe unalipia gharama za gari tu Ambazo ni kama $400 basi gari linatoka nje tayari kwa safari ya kwenda DRC.
2004 TPA wakaanza kusema kama gari za Transit hazitakiwi kubeba mzigo, Sheria haikuwa Kali, wakawa wanabana zaidi kwenye geti namba 3 ambalo ndio lakutolea magari. Mara nyingi ukimpa agent kama 200,000 za kuhonga gari ilikuwa inatoka fresh.
2014/2015 TPA wakaongeza ukali kuhusu mizigo, lakini wale wasiokuwa wanapiga ishu zile wakawa washahama Bandari Na kuamia ZNZ.
Hapo sasa Gari za Transit zenye mizigo ambayo haujaandikwa kwenye Bill of lading zikawa zinatakiwa kukata C11.
Juzi sasa ndio Sheria hii mpya imeanza japo kuwa watu wangu wa ishu washahama Bandari siku nyingi.
Hapo njiani ndio inafaulusha mzigo, Na gari tupu mnaenda kulitupa Tunduma/Nakonde.
Kuhusu mizigo kutelekezwa inatokea kila sehemu iwe ni Local au Transit.
Mtu inaweza kuwa umejipanga kuagiza gari kisha mambo yakatokea pesa ukatumia. Mwisho wa siku gari inafika pesa huna.
Ndio nikakupa mfano wa matajiri ambao wameshindwa kulipia magari japo kuwa wana pesa kibao.
**Uliza ambapo hujaelewa nikueleweshe