Hilo tatizo haliishi ila unaweza kulicontrol na kuishi nalo, Mimi toka nijifahamu nimekua nalo, now nimekua mkubwa najua cha kufanya.
Kwanza lazima ufahamu kuwa unaasili ya ngozi kavu ndio maana unawashwa ikikutana na vitu kama 1.Maji ya baridi sana, 2. Maji ya moto sana. 3. Baridi au upepo mkali baada ya kuoga, 4. Sabuni yenye manukato na kemikali kali, 5.kujifuta mwili na nguo au taulo lenye unyevu, au chafu 6.kujisugua mwili na dodoki gumu au kujisugua sana 7.Kusugua mwili kwa scrub.
Sasa kazi kwako kuavoid hizo situations, Usioge maji ya moto sana au ya baridi sana pendelea ya uvuguvugu, Epuka sabuni za manukato kama alivyosema mdau hapo juu, sugua mwili kwa mikono tu au kitambaa laini, ukimaliza kuoga usikae na maji, jikaushe kwa taulo/nguo safi then paka mafuta mazito yenye moisture then stay hydrated. Halafu tuletee mrejesho.
Mimi hizo measures zimenisaidia siku hizi siwashwi kabisa siku zingine nawashwa kwa mbaali nikikosea step. Waliokwambia juu ya kwenda hospitali, unaweza kujaribu lakini kwangu mimi dawa nilizopewa hazikufanya kazi, Ohh its bad, nilikua sipendi wala sifurahii kuoga.