Mitumba ipo hata nchi zilizoendelea

Mitumba ipo hata nchi zilizoendelea

Na magari mitumba pia izuiwe watu wanunue mapya tu, na spare za magari mitumba nazo zifungiwe watu wanunue mpya tu?????

Inaonekana hakuna ujualo. Magari mitumba tayari yanapigwa vita toka zamani naamini humiliki gari ndiyo maana hujui. FYI ushuru wa gari used ni mkubwa na kadri gari linavyozidi kuwa la zamani ndivyo ushuru wake wake unazidi kuwa mkubwa, hii ni kutaka watu wapunguze kununua vitu chakavu.

Same applies to nguo/viatu na bidhaa zote za mitumba. utaweza kuingiza ila jua ushuru wake utakuwa mkubwa sana na kwa nguo utakuwa mkubwa zaidi sababu serikali inataka kufufua viwanda vyake kama ilivyokuwa hapo awali.
 
Samahani sijakuelewa kizaidi ujumbe wako...nijuze
Wapi hujaelewa? Swali lako lilikuwa kama hiyo mitumba inatoka nje? Nilichokueleza ni kuwa licha ya kuwa ni nguo au vifaa vya makampuni na wabunifu wa Marekani, baadhi au vingi hutengenezwa au kushonwa China na sehemu nyingine.
 
Katika nchi za Northern America yaani United States of America na Canada, kuna maduka makubwa ya kuuza mitumba.

Mfano

Value Villages
Goodwill
Salvation Army
Na mengineyo.

Katika maduka haya wazungu na watu wengine ununua nguo , viatu, furniture, vyombo kama sahani, vikombe, vijiko n.k

Value village kwa mfano, supplier wao mkubwa ni kampuni iitwayo Servers ambayo upata vitu kutoka Canada au Marekani.

Viwanda vipo lakini na mitumba ipo. Mitumba siyo Nguo tu, ni pamoja na vitu kama spare za magari, magari, vitabu, mafriji, n.k.

Miaka ya nyuma, Dr. Salim Ahmed Salim alitumia uzoefu wake wa kukaa nje kuwaelimisha viongozi wenzake serikalini kipindi akiwa waziri mkuu, kwamba mitumba ipo hats nchi zilizo endelea. Ilisaidia sana.

Kwasasa sijui utumuelimisha Nani? Maana ni vurugu.
Kwani lazima kila kitu tufanye kama wao?!kama wao wameendelea waache waendelee na mitumba yao!Ngoja na sisi tuishi maisha yetu!
 
Mpango Ni kufungia uagizwaji/uingizwaji wa mitumba nchini sio kwa wamachinga tu ili kuinua uvaaji wa nguo na viatu vya ndani.
Sio kuvaa vitu vya ndani tu bali tuvae vitu vipya!yani sisi tumekuwa watu wa used kila cku!!!
 
Mleta uzi hayo maduka yote uliyotaja yanafanya kuzungusha mtumba wa ndani yani mtu anatoa nguo yake au kiatu ambacho hana matumizi nacho tena anapeleka goodwill. Huwezi agiza mtumba Indonesia ukapeleka kuuza USA.

Serikali inataka kuinua soko la bidhaa za ndani hasa nguo na viatu kama ilivyokuwa hapo awali.

Kila nchi Lazima ilinde soko lake la ndani ili kukuza uchumi wake.
Ni kweli bt naomba unitajie kiwanda kinachozalisha nguo kwa sasa hapa tz
 
Sio kuvaa vitu vya ndani tu bali tuvae vitu vipya!yani sisi tumekuwa watu wa used kila cku!!!
Wabongo wamekuja kulalamika kwanini wavae vipya wakati wamezoea kuvaa mtumba. Ukizoea shida unaanza kuona ndiyo haki yako
 
Ni kweli bt naomba unitajie kiwanda kinachozalisha nguo kwa sasa hapa tz
Viwanda vinakuja na zuio ka mitumba Bado halijawa effective ndiyo maana Bado unaona mitumba mitaani. Na hata mitumba ikikatazwa bado utaweza kuingiza as long as utalipia ushuru mkubwa utaoweka na kama mitumba itakua inafikia viwango, hivi sasa Tz ni kama dampo tunaletewa mitumba hadi kutoka Malawi
 
Wabongo wamekuja kulalamika kwanini wavae vipya wakati wamezoea kuvaa mtumba. Ukizoea shida unaanza kuona ndiyo haki yako
Unajua ukiwa na negativ thnkng kila kitu utakichukulia negatv!kwann sisi tuwe wamitumba kila kitu?!yanayowezekana kufanywa na sisi wenyewe tufanye jamani!
 
Unajua ukiwa na negativ thnkng kila kitu utakichukulia negatv!kwann sisi tuwe wamitumba kila kitu?!yanayowezekana kufanywa na sisi wenyewe tufanye jamani!
Wabongo watakutoa roho wasikie unasema wafanye wao wenyewe bila kutegemea mwingine. Kama watoto yatima hawaishi malalamiko

Wengi hili swala wanafikiria juu juu tu yani end product ambayo ni nguo ila bdae watakuja kulalamika kwanini bei ya pamba inashuka, kwanini vijana hawana ajira, kwanini viwanda vya zamani vilikufa bila kujua kama wangevaa na kuthamini vyao pamba ingekuwa processed nchini, watu watapata ajira na kila aina ya faida in between. Tuna safari ndefu sana kuendelea
 
ccm wamechanganyikiwa kwa hiyo hata zile mitumba za misaada kanisani au je ni mitumba kwa wauzaji au machinga na je kama ni hivyo kwanini serikali ya CCM hisizuie uwagizaji bali wanafunga kwa watembeza barabarani.huozo huo.


swissme

Mitumba ije ila first class na TBS juu, tatizo tunaletewa malapulapu! Madaraja kwenye jamii yapo na haya kwepeki, tusilazimishane kuvaa nguo kama jezi za wacheza mpira na joto hili! maana hazina viwango. Nakutengeneza nguo zenye ubora bado sanaa , labda tukijitahidi vitenge na batiki na mitindo kama hiyo. Chmsingi tuache blah! blah! kama kutafuta vazi la Taifa.
 
Tunapiga marufuku mitumba wakati hatuna hata kiwanda kimoja cha nguo.Huu ni mwanzo wa kuvaa kaniki.
Umeuliza swali la msingi sana.

Hivi kwa nchi ambayo baada ya zaidi ya miaka 50 baada ya uhuru, tunaagiza hadi socks, handkerchief na underpants, sasa utatokea muujiza gani ndani ya miaka 3 tuwe na viwanda vya nguo vya kuweza kuwavisha waTz milioni 45?!

Wakati mwingine huwa natafakari na kuwaza , hivi moja ya condition ya kupata wadhifa ndani ya serikali ya CCM ni kuweka rehani ufahamu na taaluma yako pale mtaa wa Lumumba?!

Kwa kuwa haiingii akilini kwa mwanataaluma mkubwa na mchumi mkubwa kama huyo Waziri wa viwanda kukuta anatoa pu... mba za kiasi hicho.

Kweli upo uwezekano mkubwa kuwa serikali ya awamu ya 5 imedhamiria wananchi wake masikini waishi kama mashetani!
 
hivi wewe tanzania kuna kiwanda cha nguo bwana acha kutujazia server kwa urojo wako

Hili ndiyo tatizo la kukurupuka, umeambiwa viwanda vikianza kufufuka
Siyo kweli. Nimekupa mfano wa kampuni ya Server ambayo ipo USA lakini inapeleka mitumba Canada.

Kwanza hatuna obligation ya kuiga kila kitu cha nje au US. Wao wanaruhusu ushoga je na sisi turuhusu ushoga? Pili US na Canada wanategemeana kwa kila kitu hasa kwenye biashara. Tayari wanasheria kali za kulinda soko lao la ndani bila kuathiri uhusiano wao wa biashara. US imepakana na Canada na Mexico unadhani mtumba wa Mexico unaweza kwenda kuuzwa US? Unadhani ni kwaninin?

Hili swala la mitumba wengi mnalitafsiri juu juu huku muda huo huo mnalalamika soko baya la zao la pamba, vijana kukosa ajira nk. Kufufua viwanda vya ndani ina maana pamba itauzwa na kuwa processed nchini, viwanda kufufuka na hivyo kuongeza ajira kwa wananchi.

Chukulia katazo la mitumba kama katazo la kuingiza magari chakavu nchini. Je yameachana kabisa kuingia, jibu ni hapana ila kila mtu anajua ushuru wa kuingiza gari la zamani nchini. So bado utaweza kuingiza mitumba kama inafikia viwango na uwe tayari kulipa ushuru mkubwa utaowekwa.

Uminywaji wa uingizaji wa mitumba ya nguo na viatu usichangaywe na uingizwaji wa samani zingine.
 
Watu hamjashtuka tu? Hizi ndo technique alienda kuchukua Rwanda, maana kule napo walikomaa kubana mitumba hadi leo maskini wanapata tabu kuvaa. Tunaigaiga technique za Rwanda, bado safari ni ndefu. Kabla ya kuanza kubana kodi bora tungekuza viwanda kwanza, tukiwa na vichache ambavyo ni competitive na kua na uhakika tunaweza kidhi mahitaji then pandisha kodi.

Trade ni kitu kizuri kwa binadamu, kujaribu kujifanya exporters tu na kubana imports zote kwa mtu aliyesoma uchumi anajua madhara yake. Hii technique waliitumia uingereza miaka ya 1700 ilikua inaitwa mercantilism, na ilifeli baada ya kuona bei ya vitu inapanda badala ya kushuka.

Kama China anaweza manufacture nguo kwa bei 1/100 ya kwako, then import kutoka China, tafuta unachoweza fanya kumzidi yeye then export kwenda kwake, wote mnafaidi. Tunabana sukari, then nguo, then tutabana kila product tukijidanganya kua we can do it ourselves, kama mnafikiri kuexport peke yake ndiko kuna faida then think again. Hawa watu sijui washauri wao wanawatoa wapi, they make decisions very quickly on critical issues, na ni watu wenye elimu zao utakuta PhD na Masters wameziweka mbele, huku ndiko kukariri na sio kuelewa.
 
Unajua ukiwa na negativ thnkng kila kitu utakichukulia negatv!kwann sisi tuwe wamitumba kila kitu?!yanayowezekana kufanywa na sisi wenyewe tufanye jamani!
Mkuu hivi unaijua Tanzania
Yaani hatuzungumzii pposta. Hapa tanzani ya mpitimbi singea. Kakonko Kigoma. Newala mtwara
Pls hiyoo kitu ingeletwa baada ya uzalishaji kuanza mkuu
 
Wapi hujaelewa? Swali lako lilikuwa kama hiyo mitumba inatoka nje? Nilichokueleza ni kuwa licha ya kuwa ni nguo au vifaa vya makampuni na wabunifu wa Marekani, baadhi au vingi hutengenezwa au kushonwa China na sehemu nyingine.

Ok, ila mie kuongelea nje nilimaanisha kwenye hizo nchi za wenzetu aniambie kama nazo zinaingia kutoka nchi za nje au ni zipo hata katika maduka aliyotaja sababu wamanchi wanazipeleka wakitaka kupunguza nguo, au size ya mwili imebadilika au chochote tu... Ndio maana nikakuuliza sababu nilikuwa siongelei nchini hapa.

Hiyo ya kushonwa etc nchi zingine kama China naijua mwisho wa siku quality ya mwenye mali inaweka utofauti kuanzia material etc

Ok cheers
 
Mkuu hivi unaijua Tanzania
Yaani hatuzungumzii pposta. Hapa tanzani ya mpitimbi singea. Kakonko Kigoma. Newala mtwara
Pls hiyoo kitu ingeletwa baada ya uzalishaji kuanza mkuu
Nimekuelewa kiongozi,hata wale wa Litumbandyosi,ha ha haaa!!kumbe unaunga mkono hoja ya kuondoa mitumba ila tu wasifanye haraka mana nguo nazo zinaweza kuadimika kama sukari!!ndo wacwac wako au sio!?
 
Yes kaka mtumba uondoke lakini hii speed ya hapa kazi na geografia haviendani
 
Inaonekana hakuna ujualo. Magari mitumba tayari yanapigwa vita toka zamani naamini humiliki gari ndiyo maana hujui. FYI ushuru wa gari used ni mkubwa na kadri gari linavyozidi kuwa la zamani ndivyo ushuru wake wake unazidi kuwa mkubwa, hii ni kutaka watu wapunguze kununua vitu chakavu.

Same applies to nguo/viatu na bidhaa zote za mitumba. utaweza kuingiza ila jua ushuru wake utakuwa mkubwa sana na kwa nguo utakuwa mkubwa zaidi sababu serikali inataka kufufua viwanda vyake kama ilivyokuwa hapo awali.
Kwa hiyo ndo unataka kusema nini, wewe mwenyewe mbulula tu, wamesema wanazuia au wanapandisha kodi. Na kwenye magari mtumba ni mtumba tu haijalishi umri, inawezekana kweli sijui kwamaana similiki gari la mtumba kama wewe.
 
Back
Top Bottom