Mitumba ipo hata nchi zilizoendelea

Mitumba ipo hata nchi zilizoendelea

Bwana eee nyie serekale msituchosheee! Minguo ya spesho ukilinganisha na mitumba haina uboraa wengine toka tuzaliwe hatujawahi kuvaa hiyo mispesho msitulazimisheee! Fyuuu! Mweeh!
 
Wazuie tu maskin sipati picha polisi watakavyolala macho kupambana na waharifu aisee!! nawahurumia wanaoitwa "wanyonge"!!
 
Shibe ugonjwa mbaya sana. Kuna watu wakiambia Tanzania, akili zao zinaingiwa na picha ya kuanzia Mbagala, inaambaaambaa Posta Mpya, Kivukoni kutokea Kinondoni hadi Bunju, Madale hadi Msakuzi...yaani kwa kifupi hufikiri nje kidooogo ya upeo wa macho plus mji mkuu wa mkoa aliotoka. Mbaya zaidi hadi watunga sera na wasimamizi wanaamini hivyo hivyo.

Hivi, kuna mtu anauziwa nguo mbovu kwa lazima? Kinachoamua soko ni upatikanaji peke yake? Hivi wote ambao hatuvuti bangi tunakuwa hatuvuti kwa kuwa tu tumeshindwa kuipata?

Hivi viwanda vya nguo hapa Tanzania ni vipi? Ni hivi vinavyotengeneza vitenge na khanga?

Nafahamu uwepo wa Mtibwa Suger, Kilombero Sugar, Kagera Suger, TTC Moshi na bado kurupu ya sukari inatuumiza kiasi mamlaka zinajitoa fahamu kubadili bei elekezi angani. Leo hii tunakurupuka na nguo, tutavaa madera kwenda kazini?
 
Shibe ugonjwa mbaya sana. Kuna watu wakiambia Tanzania, akili zao zinaingiwa na picha ya kuanzia Mbagala, inaambaaambaa Posta Mpya, Kivukoni kutokea Kinondoni hadi Bunju, Madale hadi Msakuzi...yaani kwa kifupi hufikiri nje kidooogo ya upeo wa macho plus mji mkuu wa mkoa aliotoka. Mbaya zaidi hadi watunga sera na wasimamizi wanaamini hivyo hivyo.

Hivi, kuna mtu anauziwa nguo mbovu kwa lazima? Kinachoamua soko ni upatikanaji peke yake? Hivi wote ambao hatuvuti bangi tunakuwa hatuvuti kwa kuwa tu tumeshindwa kuipata?

Hivi viwanda vya nguo hapa Tanzania ni vipi? Ni hivi vinavyotengeneza vitenge na khanga?

Nafahamu uwepo wa Mtibwa Suger, Kilombero Sugar, Kagera Suger, TTC Moshi na bado kurupu ya sukari inatuumiza kiasi mamlaka zinajitoa fahamu kubadili bei elekezi angani. Leo hii tunakurupuka na nguo, tutavaa madera kwenda kazini?
Ndo shida ya viongozi kutoijua nchi yao vizuri. Nchi hii ina watu maskini ambao yebo yebo inakatika anaishona hadi inatoboka bado mtu anaivaa.

Mtu ananunua nguo ya elfu nne miezi sita inapita hajanunua nguo nyingine na ikichanika anatia kiraka.

Watu wa vijijini wanaishi kwa msimu. Msimu ukipita si ajabu mtu kupita wiki nzima haijui mia tano inafananaje. Duh! watu watatembea uchi.
 
This week swedes will celebrate MIDSUMMER HOLIDAY na wengi wa raia tutavaa second hand clothes. Sasa Kama wazungu wanavaa nyie mnapiga marufuku na hamna hata kiwanda cha nguo huo nao ni uwendawazimu.
 
Kuna vitu vingine sijui hata tutamlaumu nani. Naona kuna "great misconceptions" hasa kuhusu importation. Hizi theories zinazosema importation is bad sijui zimetoka wapi. Yani hapa kwetu inaonekana hatutaki kukubali kuwa kuna haja ya kuwa selective kwenye mambo kadhaa.
Leo hii ni nguo za aina gani na kwa kiwango gani zinazalishwa hapa tanzania? Na je mahitaji ya nguo tanzania kwa mwaka ni kiwango gani? Je gharama za nguo hizo zipoje? Uwezo wa wananchi kumudu kununua nguo hizo upoje? Hayo yote yamezingitiwa? Hivi leo hima mtu anatumia siku nzima kushona sweta moja (kwakuwa anatumia teknolojia ya zamani ya mkono na kimashine flani hivi,hasa masweta yale wanayovaa wanafunzi wa primary siku hizi) atalazimika kuuza bei ya juu sana ili afidie gharama za chakula,usafiri chumba, umeme nk wakati sweta hilo lingeweza kushonwa na ndani ya sekunde tu na mashine. Tulipaswa kuhakikisha kuwa sio tu tunawazalishaji wa nguo bali wanazalisha kwa teknolojia ya kisasa inayopunguza gharama ili waendane na dunia ilivo. Tulipaswa kuweka standadi za mitumba na sio kusema tumezuia,
Imports sio tu kuwa ni chanzo cha kodi bali inasaidia wazalishaji wa ndani kuongeza ufanisi ili kuweza kushindana. Sasa hapa bongo naoana kila kitu kikizalishwa ndani(hata vile ambavyo bado havizalishwi vya kuto/havizalishwi kabisa) tunataka kuzuia kisiletwe, this is really wrong.
 
Ndo shida ya viongozi kutoijua nchi yao vizuri. Nchi hii ina watu maskini ambao yebo yebo inakatika anaishona hadi inatoboka bado mtu anaivaa.

Mtu ananunua nguo ya elfu nne miezi sita inapita hajanunua nguo nyingine na ikichanika anatia kiraka.

Watu wa vijijini wanaishi kwa msimu. Msimu ukipita si ajabu mtu kupita wiki nzima haijui mia tano inafananaje. Duh! watu watatembea uchi.

Mimi huku naita kukurupuka. Watu hawapendi kununua magari BeForward, bila shaka wangeingia Toyota Tanzania, DT Dobie, CFAO, CMC na kwingineko kuchukua vitu brand new, 0km...lakini ni uwezo.

Mimi siamini kama maisha ya Mtanzania yanaboreka ataendelea kutumia bidhaa duni. Mitumba inalinganishwa na bidhaa za dukani wakati huko dukani kwenyewe udhibiti wa ubora haupo. Hivyo viwanda vya nguo hatunavyo, pili hizo nguo kutoka China hazidumu, ni uongo mtupu.

Kama kuna mtu kawaahidi Wachina kuwa watawatengenezea soko basi Boda Boda zinatosha jamani. Huko kwenye nguo tutadhalilishana. Nanunua tshirt leo size L nikiifua inakuwa XL, sasa sio masihara haya.
 
Incredible hebu niweke bayana: na huko majuu kuna mitumba ya chupi, sidiria, soksi na taulo?
 
katika hatua za maendeleo kwa mtazamo wa Kimagharibi, hatua ya juu kabisa huwa ya "HIGH SELECTIVITY"
yaani kuchagua vilivyobora tu..
Sasa hivi hatutaki copy za simu,hatutaki divisheni III vyuo vikuu, hatutaki mitumba..
lakini bado tunakula kinachojitokeza...kikiwa kiwavi haya, mizizi haya, na wapo wengi wanaokula kwenye madampo.
MI NADHANI TUNGEANZA KUCHAGUA CHAKULA KILICHOBORA KWANZA..
..naanza kukumbuka story za juh na bunuwasi.
 
Tutaona mengi mwaka mpaka umeisha sasa akija mtawala mwingine awamu nyinge atasema mitumba ruksa yaleyale ya UDOM
 
Mitumba ipo ila kuna watanzania wenzetu bado wanaishi kwa kutegemea misaada ya mavazi kwa kuwa hawana uwezo wa kununua hata hiyo mitumba
 
Heheheheee! WAcha nijichekee miye ukistaajabu ya sukari utashaangaa ya mitumbaa! Walaah umenifurahisha we Mwana Mtoka Pabaya ati mtavaa madera?!! Hahah na kanzuu juu ka mnamishipaaaaa!!
 
Tutavaa kanga za urafiki unajifunga freshi tu huyoo job! Wake kwa waume! Hahah ujima!!
 
Mleta uzi hayo maduka yote uliyotaja yanafanya kuzungusha mtumba wa ndani yani mtu anatoa nguo yake au kiatu ambacho hana matumizi nacho tena anapeleka goodwill. Huwezi agiza mtumba Indonesia ukapeleka kuuza USA.

Serikali inataka kuinua soko la bidhaa za ndani hasa nguo na viatu kama ilivyokuwa hapo awali.

Kila nchi Lazima ilinde soko lake la ndani ili kukuza uchumi wake.
hivi wewe tanzania kuna kiwanda cha nguo bwana acha kutujazia server kwa urojo wako
 
Mleta uzi hayo maduka yote uliyotaja yanafanya kuzungusha mtumba wa ndani yani mtu anatoa nguo yake au kiatu ambacho hana matumizi nacho tena anapeleka goodwill. Huwezi agiza mtumba Indonesia ukapeleka kuuza USA.

Serikali inataka kuinua soko la bidhaa za ndani hasa nguo na viatu kama ilivyokuwa hapo awali.

Kila nchi Lazima ilinde soko lake la ndani ili kukuza uchumi wake.

Siyo kweli. Nimekupa mfano wa kampuni ya Server ambayo ipo USA lakini inapeleka mitumba Canada.
 
Kwa hiyo mitumba unayoongelea inaingia nchi hizo kutoka nchi za nje au ni wananchi wanazungusha humo humo nchini kwao?
Tofauti iko wapi? Si zote za ndani na za nje zimeshavaliwa? Huku hatuna za ndani kwa kuwa tunavaa hadi tunatia viraka
 
Mpango Ni kufungia uagizwaji/uingizwaji wa mitumba nchini sio kwa wamachinga tu ili kuinua uvaaji wa nguo na viatu vya ndani.
Viwanda vipi? Matokeo yake tutakosa hata za kuvaa.
 
Watu mnapenda kulalamika bila hata kujua nini hasa kimesemwa. Kitakachofanyika(walichosema) ni kuzuia mitumba ya grade ya chini ambayo mingine kusema ukweli haistahili kabisa kuuziwa mtu,ni takataka.

Hawazuii mitumba yote. Kuna grade 1 ni nzuri kuliko nguo mpya nyingi tu za Kariakoo.
 
Back
Top Bottom