Mitihani ya Big Results Now ni Big Failure Now

Mitihani ya Big Results Now ni Big Failure Now

kwani,inatofauti gani na kilimo kwanza? hyo miradi ya wakubwa.wanajua mapunguf yako wapi,waache tuone.nyumba bila msingi imara,lazima itaanguka tu
 
Kuna shule za vijijini wanafunzi wanalazimishwa kusoma masomo ya sayansi wakati hata walimu hakuna. Wanajaziwa maksi kwenye report zao za muhula wakati hata siku moja hawakusoma hilo somo
 
Kweli haina sera kwani isingewezekana kitu ambacho hata kama ni mimba ndo kwanza inaonekana halafu akina Mulugo wadanganye watu matokeo yake tutayaona kwenye matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu. Hii kweli ni poor results ever.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Ndio tatizo la kuwa na viongozi wajinga wasiojua kuwa the higher they climb the more they reveal their ma------. Hivi a whole professor hawezi kujua kuwa ni ukalulu kuzungumzia big results without big plans? hivi ni upumbavu gani bado amboa hawa viongozi wetu hawajaufanya? it seems they have exhausted everything not to be done by a sane person. Hivi hata huyo bosi wao haoni kwamba hapo wote wanaonekana hawana hata common sense? ni kuwaabudu wazungu ama ni kulongwa?
 
Big Results Now (BRN) = Poor Results Now x 2 (PRN x 2) + Big Salaries Never (BSN).
 
Big Results Now (BRN) = Poor Results Now x 2 (PRN x 2) + Big Salaries Never (BSN).

mafanikio kielimu sio sawa na kubeba magunia ya mahindi kwamba mtu aamue tu kuwa leo nitabeba magunia themanini baada ya jana kubeba magunia sitini,mafanikio katika elimu ni mchakato wa taratibu uliokitwa kwenye makusudio ya dhati hasa kwa kutambua chanzo halisi cha anguko la kielimu na sio mfalme mmoja akurupuke toka usingizini na kusema biiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiigiiiiiiiiiiiii result nooooooooooooww na mambo yabadilike ghafla kama chura arukavyo kutoka eneo A kwenda eneo B.labda kama kuna mazingaombwe ndani yake.
 
Big results can be in either negative or positive direction,nadhaniwanazungumzia big resilts in negative direction,which is equivalent to ”big destruction now”
 
Mmmh but I like the way it sound "Big results" it create imagination of something more than big. I hate these slogans as they rise with no implementations.
 
Kwa haraka haraka baada ya kupitia mitihani yote miwili nimegundua makosa yafuatayo:

SECTION A: GRAMMAR
 Swali namba 4 lina makosa ya kisarufi (swali limeandikwa "a big number of cow" badala ya "a big number of cows"). Nashindwa kuelewa kama hii mitihani ilichapwa kwa type writer au kwa compyuta kwani makosa kama haya husahihishwa na kompyuta yenyewe wakati wa kuchapa.

 Swali namba 17 haliko vizuri kisarufi. Ili liwe sahihi sentensi iliyopo ama ilipaswa kugawanywa katika sentensi mbili kamili au swali ingeandikwa upya kama hivi:
(i) These are our books.(They) are very useful (ambapo jibu lingekuwa D) au
(ii) Our books ARE very useful (au vinginevyo)

 Swali namba 19 (you must be take the punishment)-hii lugha haiweleki kabisa. Sijui kama baada ya kutungwa hii mitihani ilipitiwa kuangaliwa makosa yaliyomo ama vipi!

 Swali namba 20 lina majibu mawili [(a) & (c)]

 Kwa swali namba 24 hakukuwa na haja ya kuweka neno the kabla ya noun ‘tea'- lingeweza kuandikwa neno ‘tea' peke yake na likatosha kuleta maana, i,e: This is the place where tea is manufactured. Kwanza neno "manufactured" sio sahihi hapa-inaonekana watunzi walinakiri sentensi hii moja kwa moja kutoka kwenye vitabu feki vya kina Nyangwine (Kumbuka kilio cha Mbatia Bungeni). In a real sense, tea is not "manufactured" but it is processed-yaani majani ya chai hayatengenezwi kiwandani (manufactured) bali husindikwa (processed). Mpo hapo?

SECTION B: VOCABULARY
 Maelezo ya mwanzo katika hii section sio sahihi kisarufi (For each questions 31-36,………..). Maneno shahihi ambayo yangetumika ni "For each of the questions 31-36,…………….."

 Swali namba 34 (know us)-ni "known as"

 Swali namba 36 (two similar thing)-nadhani walikuwa wanamaanisha "(b) two similar things".

SECTION C: COMPOSITION
 Maelezo ya awali hayaeleweki-"a neaningful story giving then letters A-D". Nadhani hapa walikuwa na maana ya kuandika "a meaningful story, giving them letters A-D".

 Pamoja na makosa haya machache kuna typing errors zimeonekana hapo juu kwa mfano neno ‘shall' limeandikwa ‘shal'; ‘although' limeandikwa ‘althoug'; na ‘three' limeandikwa ‘thre'. Haya makosa yanaweza kuonekana madogo lakini kwa mwanafunzi wa shule ya msingi yanamchanganya na kumpoteza kabisa.

Kwanza nashangaa sana jinsi watoto wanavyokaririshwa maswali bila hata kupimwa kama wanajua kusoma au kuandika. Watoto wanapaswa kufundishwa kuandika insha fupi au composition katika mitihani yao ya Kiswahili na Kiingereza. Tunajenga taifa la watu vilaza wanaojua kugandamizia kila kitu bila kuhitajika kutumia akili wala ubongo. Sijui hasa ni wapi wanasiasa wetu wanataka kulipeleka taifa hili. Tatizo ni kwamba tumewaachia wanasiasa ndio watuamulie kila kitu hata kama hakina tija kwa mendeleo na ustawi wa wananchi.

HESABU
 Swali namba 13 halina jibu. Majibu yote yaliyotolewa sio majibu sahihi.

 Swali namba 14 halieleweki na halina jibu. Haieleweki watunzi walitaka hili swali lirahisishweje. Kama kuna ambaye ameelewa, atufafanulie. Swali lipo katika sehemu mchanganyiko (mixed fraction)-labda kama swali lingeuliza kubadilishwa kuwa improper fraction, hapo lingeeleweka kidogo!

 Swali namba 22 halifanyiki (limekosewa). Huwezi kupata thamani ya y ikiwa thamani ya x haijulikani.

 Swali namba 23 halina jibu sahihi miongoni mwa majawabu yaliyotolewa.

 Swali namba 29 halieleweki na hata kama ukilirekebisha kikakaa vizuri, bado hakuna jawabu sahihi miongoni mwa majawabu yaliyotolewa. Yaani ukilibadilisha likawa hivi 4/5a =21:12 au 4/5:a =21:12 na ukatafuta thamani ya a, bado hakuna jibu sahihi katika majibu yaliyopo.

 Swali namba 31 halijakamilika (limekosewa). Huwezi kupata thamani ya r (nusu kipenyo) ikiwa urefu wa mche duara haujulikani. Kwa maana hiyo ni kwamba huwezi kutafuta vitu viwili ambavyo havijulikani!

 Swali namba 32 limekosewa. Kwa jinsi swali lilivyo, thamani ya n=169º. Jibu haliwezi kuwa dogo kama hayo majibu yaliyotolewa. Kama nimekosea nisahihishe.

 Swali namba 33 linafanyika lakini swali hili ni gumu mno kwa watoto wa darasa la saba.

 Swali namba 35 halina jibu. Jibu sahihi ni 3646.5 sm2

 Swali namba 37 ni gumu sana kwa watoto hawa wadogo.

 Swali namba 38 halina jibu na ni gumu sana kwa watoto.

 Swali namba 45 halijakamilika. Jibu haliwezi kupatikana bila kutaja idadi ya pipi alizopata angalau mmojawapo wa hao marafiki watatu. Pili, majibu yake yamechanganywa. Hili ni kosa la kizembe kabisa.

 Swali namba 47 lina makosa ya kiufundi na halina jibu-eti tani 24,000/=!!!!!?????????? Hivi hawa watunzi huwa hawarudii kusoma haya maswali? Ama kweli walimu wamechoka! Hata kama tukichukulia kwamba hizo ni tani 24,000 bado hakuna jibu sahihi miongoni mwa majibu yaliyotolewa.


 Swali namba 48 halieleweki. Huwezi kupata umri wa yeyote kati yao ikiwa hujapewa umri wa sasa (au wa zamani) wa Anna au mjomba wake.

Katika hali kama hii, tutaimba sana ngonjera ya BRN lakini mwisho wa siku tutegemee matokeo 0; na hali hii itaendelea kuwa hivyo hadi mwisho wa dahari.
Nawasilisha.
 
Acha ujinga wako kuna mtu alimulazimisha kwenda ualimu? si kwasababu ya kufeli kwako sekondari, leo unataka ulipwe mshahara mkubwa wakati hata kufundisha hujui.

Mbona enzi ya UPE wale walimu waliofundisha bila manung'uniko ndio wmetoa maprofesa bora? wanafunzi mnaowafundisha hata kuongea kiswahili hawajui . kama hutaki kazi acha kabebe mizigo sokoni
Waheshimu walimu ndugu maana bila wao usingeweza hata kutumia Computer au kufika hapo ulipo.Ni wajibu wetu watanzania kuwahurumia hao walimu kwa sababu bila wao watoto wetu watakuwaje?Cha msingi ambacho ungeweza kutusaidia ni namna ya kuboresha hiyo elimu ya mwalimu.
 
Serikali inatakiwa kuangalia upya namna wanavyowapata wanafunzi wanaoenda vyuoni kwa ajili ya kuwa waalimu.Kama madaktari,wanasheria,mainjinia hawa wote wanatakiwa wafaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza au la pili kwa nini walimu wachukuliwe hata waliopata Div,IV?Hivi vyuo na serikali vinania njema na elimu ya Watanzania?Hivi mwalimu aliyefeli kidato cha nne au sita leo anaenda kumfundisha mwanafunzi wa kidato cha nne au sita hiyohiyo matokeo yake ni nini?
 
Back
Top Bottom