Mitandao ya simu: Kuna nini nyuma ya pazia?

Mitandao ya simu: Kuna nini nyuma ya pazia?

Usipoteze mda hamia mtandao mwingine,mm nimeshaachana na vodacom!
Tatizo mitandao mingine kuna sehemu hawapo kabisa.

Jana nimenunua kifurushi cha Voda BB cha siku 1 unlimited saa tisa mchana nikiwa na kazi ya kutuma haraka. Hadi nalala usiku nilishindwa kuunganishwa kwenye mtandao. Hasara niliyoipata ni kubwa sana, lakini hakuna anayejali.
 
Ukinunua kifurushi cha internet pekee yake unapata MB 200 kwa sh. 500. Ukiwa unahitaji internet kwa sana bora kununua internet pekee, hivyo vifurushi vingine unanunua kwaajili ya kupiga simu tu na msg, hamna la ziada.

Ila wamepenguza kwa kiasi kikubwa sana. Labda wanatafuta kupunguza wateja, huwezi jua.
 
Mapromisheni yao ndo wanafidia hapo mara jay milionea mara shinda ist
 
Kwa sasa vifurushi vya voda kuanzia 500 mpaka 1000 vinatoa bando yenye mb8. katika hiki kipindi cha mitandao ya kijamii na ulimwengu wa internet kwa ujumla hamtutendei haki wateja wenu this is too much.

Imagine kipindi cha 100mb zilikua zinaisha ikaja 50 tukawa tuna bajeti ila kuanzia jana 8 mb mtatumia mtandao wenu wenyewe. mimi najitoa.

goodbye vodacom.
KWA MWEMDO HUU SOON NITAHAMIA AIRTEL
VODA MMESHINDWA KAZI
Vifushi vya masaa 24 voda kwenda voda
Tsh 150=10 sms
Tsh 500= dk 15+250sms+8mb
Tsh 650= dk 30+300sms+8mb
Tsh 1000= dk 50+300sms+8mb
vodacom kwenda mitandao mingine
Tsh 150= sms 10
Tsh 499= dk 7+300sms+8mb
Tsh 649= dk13 +450sms+8mb
Tsh 999= dk 20+1000sms+8mb
vifurushi vya wiki voda kwenda voda
Tsh 1050= sms 70
Tsh 2000= dk 60+150sms+60mb
Tsh 2800= dk 85+700sms+60mb
Tsh 4000= dk 140+1750 sms+60mb
Tsh 7000= dk 250+2100sms+60mb
Tsh 10000= dk 360+2500sms+60mb
vodacom mitandao yote kwa wiki
Tsh 1050= sms 70
Tsh 1999= dk 29+500sms+6omb
Tsh 3999= dk 49+500sms+60mb
Tsh 4999= dk 91+1000sms+60mb
Tsh 9999= dk 190+1000sms+60mb
 
hii mitandao tanzania imekuja kutumaliza sio kutusaidia na wanatualibia bajeti kwasababu hawaeleweki inamaana saizi mtu uanze kujiunga kifurushi ×2 kwa vipi hii mitandao sasa itaonekana ni kama anasa hasa kwa sisi watu ambao tunatumia smartphone hawawezi wakatupelekesha kama mang'ombe wakati huo hizi internet kuna inchi wanatumia bure
 
bongo kazi mnayo... hizo bei za kijinga ni moja ya sababu Africa ndo wa mwisho kwenye kutumia internet... Someni networking mchakachue tu wenyewe msiwe na mawazo ya bundle.. 10K MB60 ni ujinga, sasa hizo 60MB mtu anafanyia nini? kwa siku nmezoea kupakua zaidi ya 20GB ukiniweka hapo si utaniua
 
Hamia airtel bana,saka kifurushi cha maana piga *148*88# kuna vifurushi vya Mungu wangu (OMG)
 
R.I.P vodacom R.I.P tigo….. Happybirthday AIRTEL…… .. TTCL I miss u.
 
Safi shusheni mpaka 5mb ili umbeya umbeya wa kwenye magroup ya whatsapp yapungue. Hizo kelele zote mnazopiga internet yenyewe huwa mnatumia kwa matumizi ya kimbeya mbeya tu
 
bongo kazi mnayo... hizo bei za kijinga ni moja ya sababu Africa ndo wa mwisho kwenye kutumia internet... Someni networking mchakachue tu wenyewe msiwe na mawazo ya bundle.. 10K MB60 ni ujinga, sasa hizo 60MB mtu anafanyia nini? kwa siku nmezoea kupakua zaidi ya 20GB ukiniweka hapo si utaniua

Mkuu mimi mara ya mwanzo nilinunua unlimited bundle kumbe wamenipa 3GB ndani ya two hours naambiwa bundle imeisha . Daah! Bongo bado sana . Kama wewe uliyezoea kutumia GB nuingi hivyo hautawezana na hawa vichwa maji
 
Back
Top Bottom