Mitandao ya simu: Kuna nini nyuma ya pazia?

Mitandao ya simu: Kuna nini nyuma ya pazia?

Chief-Mkwawa

Mkuu naona kama unanishauri nisilale, hunitakii mema wewe, yaani mchana kutwa nasukuma gurudumu la maendeleo, usiku badala ya kulala ili niamke na kuvu mpya niwe na kasi mpya kutokana na ari mpya wewe unasajesti ndio niingie jeiefu, tunatofautiana ufahamu.
 
Last edited by a moderator:
kunatetesi zimezagaa mitaani,juu ya upunguzwaji wa mb za [internet] katika mitandao ya simu, inasemekana mamlaka ya mawasiliano tanzania [tcra] imeyaagiza makampuni ya simu nchini,kupunguza megabite za vifurushi,vya internet ili kudhibiti utumiaji mbaya wa mitandao,

wanadai watanzania wanatumia mitandao vibaya,sasa mimi najiuliza kwamba zile sera za kupandisha bei ya mafuta ya taa ili kudhibiti uchakachuaji wa petrol ndio sera hizo hizo zimeletwa huku?

lakini mimi nafikiria kwa jicho la mbali kidogo haya yanakuja sio kwa baati mbaya ni kutokana na mambo ya nalo likabili taifa kwa sasa na ili kuwafanya watanzania wasiweze kujua mambo yafuatayo.

1: uandikishwaji wa daftari la mpiga kura
2: upingwaji wa kura ya ndio au hapana katiba pendekezwa
3: uchaguzi mkuu mwezi octoba

kutokana na vyombo vya habari hapa nchini kutokuwa huru na hawa jamaa wanaona kwamba kupitia mitandao ya internet watu wataelimishana njia ni kupunguza mb ili kuwanyima watu wengi fursa ya kujua mambo.

nakumbuka kule misri wakati wa vuguvugu la kuungoa utawala wa hosni mubarrakha serikali ili zima kabisa mawasiliano ya internet ili kuzuia taarifa kuzagaa.hizi zote ni kujilisha upepo,serikali iache kama ni kweli uhu mchezo.

huku ni kuwanjima uhuru wananchi kutoa maoni yao,serikali ishugulike na matatizo ya wananchi nasio kufanya hila badala ya kutibu itazidisha hasira kwa wananchi maana taarifa hizi zimezagaa sana mitaani:

kama ni kweli [tcra] imetumika ni vyema ikajua wajibu wake kuliko kutumiwa na kikundi cha watu wa chache kwa maslahi yao,
 
Tcra ni taasisi ya serikali isiyo huru. Watawala wanataka kuanza kupitishia matakwa yao huko kama wafanyavyo kwenye taasisi zingine za serikali kama tume ya taifa ya uchaguzi. Makamba kwa hili chini ya wizara yake amechemsha sana, na sijui huo urais anaomba wa nini?
 
kunatetesi zimezagaa mitaani,juu ya upunguzwaji wa mb za [internet] katika mitandao ya simu, inasemekana mamlaka ya mawasiliano tanzania [tcra] imeyaagiza makampuni ya simu nchini,kupunguza megabite za vifurushi,vya internet ili kudhibiti utumiaji mbaya wa mitandao,

wanadai watanzania wanatumia mitandao vibaya,sasa mimi najiuliza kwamba zile sera za kupandisha bei ya mafuta ya taa ili kudhibiti uchakachuaji wa petrol ndio sera hizo hizo zimeletwa huku?

lakini mimi nafikiria kwa jicho la mbali kidogo haya yanakuja sio kwa baati mbaya ni kutokana na mambo ya nalo likabili taifa kwa sasa na ili kuwafanya watanzania wasiweze kujua mambo yafuatayo.

1: uandikishwaji wa daftari la mpiga kura
2: upingwaji wa kura ya ndio au hapana katiba pendekezwa
3: uchaguzi mkuu mwezi octoba

kutokana na vyombo vya habari hapa nchini kutokuwa huru na hawa jamaa wanaona kwamba kupitia mitandao ya internet watu wataelimishana njia ni kupunguza mb ili kuwanyima watu wengi fursa ya kujua mambo.

nakumbuka kule misri wakati wa vuguvugu la kuungoa utawala wa hosni mubarrakha serikali ili zima kabisa mawasiliano ya internet ili kuzuia taarifa kuzagaa.hizi zote ni kujilisha upepo,serikali iache kama ni kweli uhu mchezo.

huku ni kuwanjima uhuru wananchi kutoa maoni yao,serikali ishugulike na matatizo ya wananchi nasio kufanya hila badala ya kutibu itazidisha hasira kwa wananchi maana taarifa hizi zimezagaa sana mitaani:

kama ni kweli [tcra] imetumika ni vyema ikajua wajibu wake kuliko kutumiwa na kikundi cha watu wa chache kwa maslahi yao,
Kwa serikali hii ya magamba lolote lawezekana, iwapo wameweza kutengeneza 'movie' ya magaidi kule Amboni, kipi tena watashindwa kukitengeneza?

Lakini watawala wetu watambue kuwa penye ukweli uwongo hujitenga.

Lolote 'watakaloligushi' ni lazima ukweli hatimaye utajulikana.

Kwa namna makampuni ya simu karibu yote yalivyoongeza gharama za vifurushi kimya kimya kwa mpigo, kunaonyesha ipo namna.

Hatua zote hizo zinazofanywa na watawala wetu, zinaonyesha dalili za himaya inayoanguka.

Kuweweseka kwa magamba kunatokana na kufanya tathmini kwenye mitandao ya kijamii na kugundua kuwa 'Lumumba team' yao humu mitandaoni imezidiwa kila idara katika 'mpambano' wao na wazalendo halisi wa nchi hii wanaowazidi kwa hoja 'mamluki' hao wa mitandaoni, hadi sasa wameamua kucheza 'rafu' za kila aina huku refa wao akiangalia tu bila hata ya kutoa kadi ya manjano!
 
Ni bahati mbaya sana Watanzania kwavile hatupo fuku fuku kutafuta ukweli basi utaona mara nyingi huwa tunalilia ama kupigania kile ambacho si haki yetu na kuacha kile ambacho tulipaswa kukipigania!!! Hoja pekee ninayoiona kwenye sakata hili ni upunguzwaji huo wa MB kwa kampuni zote zote, almost at the same time! So long as jambo hili limefanyika kwa pamoja na kampuni zote basi kunaashiria kuwapo kwa collusion among service providers... hili, katika soko huria halikubaliki!


Kinyume chake, tunachololilia, kwamba MB zimeshushwa, hili si haki yetu na hata ukienda mahakamani kampuni za simu zitashinda... WHY? Hizi bundles za internet ambazo huwa tuna-enjoy ni promotional bundles... bei halisi za bundles ni very expensive! Haya ma akina OMG, cjui Cheka Internet na makorokocho mengine sio bundle rasmi sokoni.... hizo zote ni promotional bundles.... hizi za sasa ambazo tunazilalamikia bado ni promotional bundles ambazo bei yake ni chini ya bei halisi ya bundles. Mathalani, Airtel ambayo inaonekana bei yao ni rahisi, bei rasmi ya 1GB ni sh. 15,000 wakati bei ya 500MB ni sh. 12,000/-!!!!! Kwahiyo kilichopo sasa ni sawa, pamoja na bei elekezi ya petrol kwa sasa ni sh. 1,700; vituo vya mafuta vikaamua kuuza sh. 1300 kwa miezi kadhaa lakini baadae wakaamua kupandisha hadi sh. 1,500/- wakati bei inayotamulika ni ile ile ya sh. 1700 halafu tuanze kulalamika kwamba kampuni za mafuta zimepandisha bei kutoka sh. 1,300 hadi sh. 1,500!!!!!

Nasisitiza, mara zote usipofahamu unatakiwa kupigania nini basi kuna uwezekano mkubwa wa kupoteza haki yako! Hapa hoja dhidi ya kampuni za simu sio kushusha bundles coz' bado ni very cheap compared to actual set price... hoja hapa inapaswa kuwa collusion in competitive market is unacceptable!
 
Mimi nina nunua kifurushi cha pembeni cha tigo kwa siku tshs 500 unapata mb 200 kwa matumizi ya simu zinanitosha.
Sms tigo uwa natuma bure siku zote hata nikiwa sina salio.
 
Hata hizo dakika wakikupa, pindi unapoanza kuongea zinapukutika kwa super sonic speed, sijajua dk zao zina uwiano gani na dk za kawaida. Nawaomba airtel wasiwaige hawa vodacom na tigo maana ninyi tu ndo mlobaki wakombozi wangu
 
Naipongeza mitandao make vifurushi vilikuwa vinatumika kwa mambo ya kishenzi kabisa,sahiv imesaidia kuweka nidhamu ya matumizi ya vifurushi,samAhani kutofauriana na wengi huo in mtizamo wangu

Kama wewe itakuwa imekushape umeacha ushenzi au bado?
 
Hii ndo habari vodacom wametoa;

WATANZANIA WAENDELEA KUNUFAIKA NA MAWASILIANO YA GHARAMA NAFUU

-Watanzania waendelea kunufaika na gharama nafuu za mawasiliano
-Nchi nyingine kama Kenya,Afrika Kusini,Ghana,Nigeria na India viwango viko juu.
10985047_941000649257651_7693680316028543952_n.jpg

Watanzania wanaotumia huduma za mawasiliano bado wanaendelea kupata huduma hizo kwa gharama nafuu kwa kupiga simu na matumizi ya interneti ukilinganisha na huduma zinazotozwa kupata mawasiliano katika nchi nyingine za Afrika ikiwemo Afrika ya Kusini,Kenya,Nigeria na hata nchi ya india.


Haya yaemebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza,katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo alitoa mfano kuwa licha ya ongezeko la bei katika vifurushi vya kupata huduma mawasiliano bado katika kifurushi cha gharama ya chini ambayo ni shilingi 500 mteja anaweza kupata MB za kutosha kutumia internet ikiwemo kupiga simu na kutuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS).

Alitoa mfano kuwa mteja akinunua kifurushi cha shilingi 500,kati ya hizo fedha shilingi 138 inakwenda serikalini kwa ajili ya kodi na kampuni kubakia na shilingi 362/- ambapo fedha hizo zinamuwezesha kupata muda wa dakika 15 za maongezi ikiwa kila dakika inatozwa shilingi 24/-,MB za kuperuzi internet 8 kila MB ikiwa inatozwa shilingi 5 na kutuma ujumbe wa maneno (SMS) 250 ambapo kila ujumbe natozwa shilingi 0.12

"Viwango vya malipo kwa Vodacom ni vya gharama nafuu na vimepangwa kulingana na mahitaji ya wateja wetu licha ya mabadiliko madogo katika bei yaliyofanywa hivi karibuni.Hivi sasa tunatoza shilingi 4.9/-kwa kila MB katika kifurushi cha GB5 ambapo bei ya awali kilikuwa kinatozwa shilingi 3.9/-.

Bado malipo ya sasa ni madogo ukilinganisha na mallipo yanayotozwa kwenye kifurushi cha GB5 kwenye soko la huduma za mawasiliano kwa fedha za kitanzania kwa mfano Nigeria inatoza shilingi 17/-/Afrika ya Kusini Shilingi 13/-,Kenya shilingi 12/-,Ghana shilingi 7/-na India shilingi 5/-


Meza pia alielezea mafanikio mbalimbali yaliyofikiwa na kampuni ya Vodacom katika kipindi cha mwaka 2014 amabpo aliwashukuru wateja wote kuwa wamechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa mafanikio hayo ikiwemo zaidi ya wateja 1.7 kujiunga na familia ya Vodacom.

Pia alisema kuna ongezeko la wateja wanaoendelea kufaidika na huduma mbalimbali zinazotolewa na Vodacom ikiwemo huduma ya internet ya gharama nafuu na huduma nyinginezo kama vile M-Pesa ambayo imekuwa na mafanikio kwa kuwa na mtandao wa mawakala 85,000 na kufanya mihamala inayofikia Trioni 1.2 kwa mwaka pia huduma ya M-Pawa imekuwa kwa kasi na inawawezesha wateja wengi kuweka pesa na kukopa.Pia aliongeza kuwa kampuni imeongoza kwa kuwa ya pili kulipa na kukusanya kodi za serikali na kuwa ya kwanza katika sekta ya mawasiliano.

Alisema kwa mwaka jana kampuni iliweza kuwekeza shilingi bilioni 180/- na mwaka huu itawekeza shilingi bilioni 140/- katika kuboresha huduma mbalimbali ikiwemo huduma ya internet na kusambaza huduma bora kwa wateja nchini kote.

Alimalizia kwa kusema kuwa moja ya dhamira ya kampuni ni kuunga mkono juhudi za kusambaza huduma nchini kote hususani sehemu za vijijini ambapo katika kuunga mkono jitihada hizi kampuni imekuwa ikichangia fedha kwenye mfuko wa kusambaza huduma za mawasiliano vijijini ujulikanao kama UCAF.
 
mi nimeunga jana jioni nimepata mb 700 kile kifurushi cha sh 999. labda una matatizo kwenye line wapigie au nenda ofisini kwao


Asante mkuu na mimi nimeiona hiyo ya mb700 na nimejiunga tayari, ila zamani kwa bei hiyo hiyo ilikuwa 1gb, asante sana acha nifanye kazi sasa
 
Vodacom pamoja na Tigo Leo wameshangaza Watanzania, hii ni baada ya kupunguza muda wa maongezi pamoja na MB. Bado hawajaweka bayana nini kinachoendelea chini ya kapeti tumesubiri hata kutumiwa ujumbe ila hakuna kitu.
==================

attachment.php


Vodacom nawajua MB 8 ZIKIISHA KINYEMELA wanaanza kula salio lako lote
 
Wizi wa mchana kweupe unaendelea katika mtandao wa vodacom na nashangaa hata wale tuliowapa dhamana kusimamia mashirika haya wako kimya.ukiweka pesa ili upate kifurushi cha internet,hakuna majibu yanayotolewa na voda kuhusu kupata au kukosa kifurushi ulichokitaka,mbaya zaidi hata pesa uliyoingiza haionekani popote na wala hairudishwi na ukijaribu kuunganisha na internet unaambiwa huna salio la kutosha,uongeze pesa.hii imeanza tangu juzi na jana na nimelizwa karibu shs 5000.yawezekana mimi tu ndio nimelizwa,lakini natoa tahadhali kwa wengine humu,yasiwakute yaliyonikuta.Kwaheri voda,Hodi Airtel au Tigo.:embarrassed::ban:

Karibu airtl,achana na hizo mb8. Huku unapata 1gb kwa sh 1,500 wiki nzima.
 
Mi ni mtumiaji wa Airtel jiungeni kupitia Airtel money unapata DAKIKA 12 MITANDAO YOTE. 500SMS NA 100MB Kwa Sh 499 tu
 
Back
Top Bottom