wapendwa,
kusema ukweli, nilikuwa nataka kuanzisha thread kulaumu hili la kumhusisha binti mwanaasha na kazi ya baba yake. kwa kweli si haki na tuache tabia hii mara moja! jakaya ni jakaya na mwanaasha ni mwanaasha. mimi baba yangu aliishia darasa la pili na mimi sasa nasomea shahada ya uzamivu (PhD) ulaya, na tena sio kwa kubebwa na mtu, bali kwa kushindania na kupata moja ya scholarship adimu kabisa hapa duniani!
tujiulize, kama performance ya baba ingekuwa ina uhusiano na performance ya mtoto, kwangu ingekuwaje?
nimelazimika kulisema hili kwa sababu sioni mantiki ya kumlaumu baba mwanasha kwa matokeo yasiyo mazuri ya binti yake na ambayo naamini yamemsikitikisha pia baba yake (jakaya) tena sana. hebu tujiepushe na siasa kila wakati. tukiendelea na hii tabia, tutakuwa si tu hatumtedei haki baba yake (mzee jakaya kikwete), bali pia mwanaasha mwenyewe.
yeye si wa kwanza kupata matokeo yasiyoridhisha na wala sio wa mwisho. amepata matokeo kama mtoto mwingine yoyote na kama jamii ya wastaarabu, tulipaswa kumtia moyo mdogo wangu mwanaasha ili asikatishwe tamaa na matokeo yake na ikiwezekana tuwashauri wazazi wake kumtafutia fursa nyingine nzuri zaidi za kujiendeleza zaidi.
binafsi namjua kijana mmoja (sasa ni mwanamume wa makamo), alipata div IV form 4 na baada ya kuhangaika ku-reseat, alipata div III form 6 na sasa ninavyoandika hapa ni mmoja wa wahasibu bora kabisa duniani, akiwa amekwishafanya kazi barani ulaya, afrika na arabuni akishinda usaili shindanishi na anazo tuzo kadhaa za utendaji kazi uliotukuka.
hivyo basi wapendwa, bado mwanaasha anazo fursa za kujiendeleza na nawashauri wazazi wake wasikatishwe tamaa na matokeo hayo ya mwana wao ambayo hawakuyatarajia.
nimalizie klwa kumwambia mwanaasha (kama atanisoma hapa), asikatishwe tamaa na maneno ya watu, azungumze na wazazi wake kuona namna gani watamsaidia na asonge mbele.
pole sana baba na mama mwanaasha,
pole sana mwanaasha,
mbarikiwe sana wapendwa,
Glory to God!