We Know Next
JF-Expert Member
- Sep 9, 2010
- 815
- 382
Nadhani si Kumchafua, kumtukana wala kumdhalilisha. Hapa nilazima ieleweke kwamba anayajadiliwa si JK bali ni Rais wa Nchi. Nina maana gani kusema hivi, Raisi wa Nchi ni Kama Mungu wa Nchi hiyo, tunategemea Rais kuwa ni Kiongozi wa mfano, kuanzia ktk maisha yake binafsi, ya kifamilia na hata ya kinchi. ndiyo maana kila anachokifanya jamii lazima ikifahamu na inategemea kiwe ni kizuri cha mfano wa kuigwa. Nitatoa mifano michache,
1. Huko nchi zilizoendelea, bila shaka mnaona mchakato wa kumpata Rais unavyokuwa na upekenyeku, yaana ukikutwa hata na kashfa kidogo tu ya kibinafsi kabisa, unaweza usiwe Rais kwa sababu wanachokipigania watu wa huko ni hadhi ya hiyo nafasi ya Urais na wala si JK,
2. Mwalimu Nyerere ktk moja ya hotuba zake aliwahi kusema, akimtandika kibao mama Maria, ingawa ni jambo dogo kabisa la kibinafsi na kifamilia, lakini wakiipata vyombo vya habari , hiyo itakuwa ni story cover ya magazeti siku hiyo, na akasema story si kumpiga Maria kibao ila ni Rais wa Nchi kumpiga Maria kibao, kwa hiyo suala hapo ni Nafasi ya Urais,
3. Unapokuwa kiongozi wa Nyumba kwa familia zetu za kawaida kabisa, tunategemea uwe kiongozi mwenye busara na wa mfano, sembuse Rais wa nchi? Kwa hiyo mtoto wa Rais akifanya jambo tayari hiyo ni story kwa nchi, Rais mwenyewe akifanya jambo hata kama ni dogo vipi, tayari ni story ya nchi. Suala hapo ni Nafasi na hadhi ya kiti kile cha Uraisi na wala si mtu aliyepo hapo.
Kwa mantiki hiyo basi, Rais ni lazima awe msafi asiwe na dosari inayoweza kuleta picha mbaya ktk jamii ya nchi husika. Ni kweli kabisa ukisikia Rais anawake 7, ni jambo la kushtusha kwa nchi kama yetu, au mtoto wa Rais ni changudoa, tayari inamdharirisha rais, kwa hiyo nadhani, hata watu wanaotaka urais inabidi wajipime kwanza, na waelewe kuwa nafasi hiyo ni ya Public na si ya familia yake.
Kwa hiyo mitandao hii haimchafui Rais, bali nafasi yenyewe inahitaji kuchambuliwa kwa kila upande.
1. Huko nchi zilizoendelea, bila shaka mnaona mchakato wa kumpata Rais unavyokuwa na upekenyeku, yaana ukikutwa hata na kashfa kidogo tu ya kibinafsi kabisa, unaweza usiwe Rais kwa sababu wanachokipigania watu wa huko ni hadhi ya hiyo nafasi ya Urais na wala si JK,
2. Mwalimu Nyerere ktk moja ya hotuba zake aliwahi kusema, akimtandika kibao mama Maria, ingawa ni jambo dogo kabisa la kibinafsi na kifamilia, lakini wakiipata vyombo vya habari , hiyo itakuwa ni story cover ya magazeti siku hiyo, na akasema story si kumpiga Maria kibao ila ni Rais wa Nchi kumpiga Maria kibao, kwa hiyo suala hapo ni Nafasi ya Urais,
3. Unapokuwa kiongozi wa Nyumba kwa familia zetu za kawaida kabisa, tunategemea uwe kiongozi mwenye busara na wa mfano, sembuse Rais wa nchi? Kwa hiyo mtoto wa Rais akifanya jambo tayari hiyo ni story kwa nchi, Rais mwenyewe akifanya jambo hata kama ni dogo vipi, tayari ni story ya nchi. Suala hapo ni Nafasi na hadhi ya kiti kile cha Uraisi na wala si mtu aliyepo hapo.
Kwa mantiki hiyo basi, Rais ni lazima awe msafi asiwe na dosari inayoweza kuleta picha mbaya ktk jamii ya nchi husika. Ni kweli kabisa ukisikia Rais anawake 7, ni jambo la kushtusha kwa nchi kama yetu, au mtoto wa Rais ni changudoa, tayari inamdharirisha rais, kwa hiyo nadhani, hata watu wanaotaka urais inabidi wajipime kwanza, na waelewe kuwa nafasi hiyo ni ya Public na si ya familia yake.
Kwa hiyo mitandao hii haimchafui Rais, bali nafasi yenyewe inahitaji kuchambuliwa kwa kila upande.