Miswada mitatu(3) ya kujadili masuala ya madini na maliasili yafikishwa Bungeni kwa hati ya dharura

Binafsi nafikiri kwa hapa ilipofikia hii miswada.. hamna namna.. Inabidi Wabunge wakakamae na kuipitia kwa uangalifu kila mmoja na kifungu chake kujaribu kuiboresha.
Kwa ujumla ni Sheria moja ya Marekebisho Mbalimbali yenye kurasa 86 na Sheria nyingine mbili mpya zenye kurasa 11 kila moja.
Hapa ndiyo weledi na maslahi ya Taifa yanapotakiwa kwani lazima kuna vipengele tata kwa makusudi au bahati mbaya..

1. The Written Laws(Miscellaneous Amendments) Act, 2017
2.The Natural Wealth and Resources(Permanent Sovereignty) Act, 2017
3.The Natural Wealth and Resources Contracts(Review and Re-negotiation of Unconscionable Terms) Act, 2017.

  • Kwa haraka haraka Sheria ya No. 1 hapo juu katika Madhumuni na Sababu(Objects and Reasons) 'text' ya kiswahili na ya kiingereza zinapishana kwenye vipengele kadhaa
Mfano kipengele e. To eliminate all provisions... wakati 'text' ya kiswahili inasema e. Kuweka Utaratibu wa Bunge kufanya mapitio.. Yanaweza kuwa makosa ya kawaida au 'intentional' ukizingatia 'text' ya kiingereza ndiyo yenye uzito.​

  • Kwenye Sheria ya 2 (Permanent Sovereign.) Ibara ya 12:Review by the National Assembly : All Arrangements or Agreements entailing Extraction,Exploitation of Acquisition and use of Natural wealth and resources may be reviewed by the National Assembly.
Hii 'may be reviewed' kisheria maana yake ni kuwa hailazimishi Bunge kupitia mikataba.. inatoa 'discretion'
Ilitakiwa iwe 'shall be reviewed' ili kuweka ulazima wa Bunge kupitia mikataba.​
  • Limetumika neno National Assembly bila kufafanuliwa mwanzoni kuwa maana yake ni Parliament of Tanzania vinginevyo inaweza kutumika vyovyote.
  • Bado Bunge limenyanganywa Madaraka ya kutunga Sheria kwa Waziri kupewa uwezo wa kutunga Kanuni akiwa 'kajifungia'.. Hasa katika Sheria ya 3(Review and Re-neg.) : Ibara ya 8, Power to Make Regulations: The Minister may make regulations.. Hii inaweza kutumika vibaya..
Kwa ujumla bado mapungufu ni mengi hasa wataalamu wakishaipitia miswada hii..
 
Kumbe,ndio maana wengine wanadai tumeibiwa kidogo tu!

Tena huo ujasiri wametoa wapi?

Tatizo hapa ni utashi wa kutaka kuiona tanzania iliyo bora haupo.Upo wa tumbo tu.
Inatisha kidogo,ila kuna aliye na dodoso kidogo ya kilichomo,au bado ni siri?
 
Itakuwa vizuri ukitusaidia hapa hivyo vipengele vitakavyobadilishwa na sheria zipi mpya zitakazo pitishwa
Inajulikana tunataka kufaidi rasilimali zetu hivyo lazima tuwe wabia (wanahitaji kuweka kiwango labda 40%-50%), Tax holiday badala ya kuwa milele kama sasa wanaweka kipengele tu kwamba ni mwaka wa kwanza tu baada ya hapo wanalipa, ajira za mgodini labda 70% wawe waswahili, hakuna kuchnjua madini nje ya nchi, kila madini yanaposafirishwa lazima yarekodiwe na yapatiwe vibali kutoka benki kuu, etc!Tunahitaji kuunguza hela zetu za kodi kwa kubadilisha hivi vipengele??
Kama muda hautoshi tuwaongeze,ila wakae bila posho si wanalipwa mishahara??
 
Tafsiri ya kutokuwepo nia njema kwa hiyo miswada kama wanavyosema wapinzani inatokana na nini?

1. Content ya hiyo miswada?

AMA

2. Hali ya uharaka wake?
 
Tulisema ccm wanafanya sanaa na siasa kwenye masuala ya madini baadhi ya watu wakashangilia upepo, leo tena wanaleta miswada mitatu kwa hati ya dharura kujadili masuala ya madini na maliasili za nchi, wanataka miswada hii mitatu ijadiliwe kwa siku moja bila wananchi mbalimbali kupata nafasi ya kujua kilichomo hii ni aibu na ccm wanaonesha rangi zao halisi. Yalifanyika kwenye madini 1997 ilifanyika kwenye gas na mafuta 2015 na yakatokea tena leo.haya ndio chanzo cha makinikinia na wizi, Watanzania wakikubali haya ina maana tunakubali kuendelea kuibiwa.
Na bado wanataka ahongezewe muda wa kkaa magongon
 
Jamaa wanapenda posho hawa....!Hivi kweli kuna ambacho hatukijui kwenye kurekebisha sheria za madini, gesi, na mafuta??Sio kwamba inaletwa miswada mipya hapana, ni ile ya zamani ifanyiwe marekebisho ambayo tayari tumeshayapigia makelele sana!Mnataka kuendelea kutafuna kodi zetu mpk lini???Rekebisheni miswada acheni kulalama, kwanza Heche sijui kama atatoa hata mchango!

Laiti kama ungejua maana ya kujadili mswada wa sharia usingeandika hayo!!!!!!!!!
Ni vigumu sana kujadili hata mswada mmoja kuujadili kipengele kwa kipengele (Clause by clause) na kuupitisha kwa siku moja!!!!!!!!!!!!!!
 
Jamaa wanapenda posho hawa....!Hivi kweli kuna ambacho hatukijui kwenye kurekebisha sheria za madini, gesi, na mafuta??Sio kwamba inaletwa miswada mipya hapana, ni ile ya zamani ifanyiwe marekebisho ambayo tayari tumeshayapigia makelele sana!Mnataka kuendelea kutafuna kodi zetu mpk lini???Rekebisheni miswada acheni kulalama, kwanza Heche sijui kama atatoa hata mchango!
Umetumwa we co bure
 
Wakubali kufanya kazi bila posho basi hata kwa wiki mbili tuone uzalendo wao!Otherwise ni wizi wa kodi, let us be honest
Ni wazo zuri lakini ni ombi na si lazima wajitolee!
Kipi bora,walipwe wakae muda utakaotosha kujadiliana au wafukie mashimo?
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Inajulikana tunataka kufaidi rasilimali zetu hivyo lazima tuwe wabia (wanahitaji kuweka kiwango labda 40%-50%), Tax holiday badala ya kuwa milele kama sasa wanaweka kipengele tu kwamba ni mwaka wa kwanza tu baada ya hapo wanalipa, ajira za mgodini labda 70% wawe waswahili, hakuna kuchnjua madini nje ya nchi, kila madini yanaposafirishwa lazima yarekodiwe na yapatiwe vibali kutoka benki kuu, etc!Tunahitaji kuunguza hela zetu za kodi kwa kubadilisha hivi vipengele??
Kama muda hautoshi tuwaongeze,ila wakae bila posho si wanalipwa mishahara??
Umeambiwa Leta contents za hiyo Miswada we unaleta Mambo ya Labda? Haraka ya nini? Au kwa vile maccm yaliyoko Bungeni ukimuondoa Chenge, Zungu na Bashe wengine ni vihiyo wakata mauno? Miswada yenyewe ina Makosa kibao halafu una harisha maupumbavu yako hapa?
 
Tatizo siyo kupeleka bungeni kwa hati ya dharura.Hoja ingekuwa kilichomo ndani ya hiyo miswada.Mhe.Heche angetusaidia kuainisha mapungufu ya miswada hiyo.
Si kila mswada wa dharura huwa na mapungufu.,
 
Tatizo siyo kupeleka bungeni kwa hati ya dharura.Hoja ingekuwa kilichomo ndani ya hiyo miswada.Mhe.Heche angetusaidia kuainisha mapungufu ya miswada hiyo.
Si kila mswada wa dharura huwa na mapungufu.,
Dharura iliyopo hapa nchini kwa Sasa ni MKIRU, sii Rasilimali zetu, hizi zinahitaji Umakini wa hali ya Juu na wenye uwezo wa kuchanganua Mambo wachanganue, sii kina Kibajaji, Mlingwa, Musukuma, na Hawa Ghasia! Maccm mnarudia Makosa yaleyale!
 
  • Thanks
Reactions: SDG

Similar Discussions

Back
Top Bottom