Wabunge wa CCM na miswada kwa hati ya dharura

Bila bila

JF-Expert Member
Dec 20, 2016
21,496
37,789
Zamani Nilikuwa najiuliza Kwa nini miswada ya sheria mbalimbali inapopelekwa Kwa hati ya dharura Wabunge wa upinzani wanapinga Sana huku wale wa CCM wakiunga mkono Kwa nguvu zote na kufikia kuwaita wale wa upinzani hawana Uzalendo.

Naukumbuka vema Muswada wa sheria ya ulinzi wa raslimali za Taifa wa mwaka 2017. John Mnyika akiwa Mbunge wa Kibamba alisimama na kuomba Mwongozo Kwa Spika (Yob Yustino Ndugai) akitaka serikali iondoe udharura wa Muswada huo ili kuwapa nafasi wadau wa sheria na uwekezaji Muda wa kutosha kupitia na kujadili Muswada huo Kwa maslahi mapana ya Taifa siku zijazo.

Jenista Mhagama (Sera, uratibu na Bunge) alimshukia kama Mwewe huku Kibajaji, Mlinga na Msukuma wakiwa wimawima kuomba watoe nyongeza ya Mwongozo Hadi pale Spika aliposema aliyeombwa Mwongozo ni yeye Ila amemruhusu Mhagama Kwa vile ni Chief Whip.

Lakini matokeo ya Tabia ya kuendekeza udharura tumeanza kuyaona kwenye kesi ya juzi tulipopigwa Billion 75 tena Kwa kuomba tumalize nje ya Mahakama.

Nimejiuliza sababu ya Wabunge wa CCM kushangilia miswada inayopelekwa Kwa hati ya dharura nikagundua sababu kubwa ni kwamba inawarahisishia kutolaumiwa. Hawana Muda wa kusoma na kuchambua miswada pale inapoletwa Kwa njia ya kawaida. Kwa hiyo hati ya dharura inawapa kirahisi sababu ya kujitetea.

Niliwahi kuambiwa na rafiki yangu kwamba mwaka 2019 Mbunge mmoja wa Iringa aliombwa elfu 30 na Mtoto wa dada yake ili akalipe faini baada ya pikipiki yake kukamatwa na traffic, yeye akasema faini ya pikipiki ni elfu 5 tu Huyo traffic anataka kumpiga hela.

Akaahidi kumpigia RPC Iringa kulalamika lakini majibu aliyopata ni kwamba, "Mheshimiwa nyie ndo mmepitisha faini hii Bungeni". Kilichofuata ni aibu kwake.
 
Mikataba ya hati za dharura ndio imetumaliza Tz hasa tangu awamu ya kikwete (kumbukeni ya gas na malipo laghai ya IPTL).
Mikataba hii ni ya kifisadi na uhuni mtupu kwa kutumia Bunge la ccm ambalo nalo limetuingiza ktk fisadi nyingi (hata wa DP World)
 
Jenista Mhagama (Sera, uratibu na Bunge) alimshukia kama Mwewe huku Kibajaji, Mlinga na Msukuma wakiwa wimawima kuomba watoe nyongeza ya Mwongozo Hadi pale Spika aliposema aliyeombwa Mwongozo ni yeye Ila amemruhusu Mhagama Kwa vile ni Chief Whip.
Hao wote zero brains
 
Naukumbuka vema Muswada wa sheria ya ulinzi wa raslimali za Taifa wa mwaka 2017. John Mnyika akiwa Mbunge wa Kibamba alisimama na kuomba Mwongozo Kwa Spika (Yob Yustino Ndugai) akitaka serikali iondoe udharura wa Muswada huo ili kuwapa nafasi wadau wa sheria na uwekezaji Muda wa kutosha kupitia na kujadili Muswada huo Kwa maslahi mapana ya Taifa siku zijazo
Muswada huu tuliutolea angalizo Zita Act Retroactively? Tutavunja Mikataba Yote Iliyopo? Can we Stand? Do we have the Guts? tukawaambia the consequences lakini walitia pamba masikioni!. Sasa haya ndio matokeo!.
P
 
Mikataba ya hati za dharura ndio imetumaliza Tz hasa tangu awamu ya kikwete (kumbukeni ya gas na malipo laghai ya IPTL).
Mikataba hii ni ya kifisadi na uhuni mtupu kwa kutumia Bunge la ccm ambalo nalo limetuingiza ktk fisadi nyingi (hata wa DP World)
Sahihi Kwa 100%. Labda anayebisha ni mnufaika.
 
Zamani Nilikuwa najiuliza Kwa nini miswada ya sheria mbalimbali inapopelekwa Kwa hati ya dharura Wabunge wa upinzani wanapinga Sana huku wale wa CCM wakiunga mkono Kwa nguvu zote na kufikia kuwaita wale wa upinzani hawana Uzalendo.

Naukumbuka vema Muswada wa sheria ya ulinzi wa raslimali za Taifa wa mwaka 2017. John Mnyika akiwa Mbunge wa Kibamba alisimama na kuomba Mwongozo Kwa Spika (Yob Yustino Ndugai) akitaka serikali iondoe udharura wa Muswada huo ili kuwapa nafasi wadau wa sheria na uwekezaji Muda wa kutosha kupitia na kujadili Muswada huo Kwa maslahi mapana ya Taifa siku zijazo.

Jenista Mhagama (Sera, uratibu na Bunge) alimshukia kama Mwewe huku Kibajaji, Mlinga na Msukuma wakiwa wimawima kuomba watoe nyongeza ya Mwongozo Hadi pale Spika aliposema aliyeombwa Mwongozo ni yeye Ila amemruhusu Mhagama Kwa vile ni Chief Whip.

Lakini matokeo ya Tabia ya kuendekeza udharura tumeanza kuyaona kwenye kesi ya juzi tulipopigwa Billion 75 tena Kwa kuomba tumalize nje ya Mahakama.

Nimejiuliza sababu ya Wabunge wa CCM kushangilia miswada inayopelekwa Kwa hati ya dharura nikagundua sababu kubwa ni kwamba inawarahisishia kutolaumiwa. Hawana Muda wa kusoma na kuchambua miswada pale inapoletwa Kwa njia ya kawaida. Kwa hiyo hati ya dharura inawapa kirahisi sababu ya kujitetea.

Niliwahi kuambiwa na rafiki yangu kwamba mwaka 2019 Mbunge mmoja wa Iringa aliombwa elfu 30 na Mtoto wa dada yake ili akalipe faini baada ya pikipiki yake kukamatwa na traffic, yeye akasema faini ya pikipiki ni elfu 5 tu Huyo traffic anataka kumpiga hela.

Akaahidi kumpigia RPC Iringa kulalamika lakini majibu aliyopata ni kwamba, "Mheshimiwa nyie ndo mmepitisha faini hii Bungeni". Kilichofuata ni aibu kwake.
Tatizo ni ujinga ytu hapo, wote wapinzania na wasio wa[pinzani.

Mikataba ya Kimataifa, uwe na sheria zako usiwe na sheria zako, mradi umeingia mikataba ya Kimataifa basi itaendeshwa kimataifa bila kujali sheria za nchi yako.


Mara nyingi kwenye mikataba huwa akuna kukumbushana taratibu za kuiendesha tu mikataba, lakini mkienda kinyume kidogo au mliyeingia nae akienda kinyume kidogo, wote mnahukumiwa kwa "arbitration" za Kimartafa.

Mawaziri wetu na wabunge wetu nnakuhakikishai 90% hawafahamu kwanini wao ni wabunge na majukumu ya asasi niyepi. Wawe wa upinzani au wa CCM, wote ni hali kadhalika.

Kwa mtazamo wao wapo pale ili wapige kelele sana waonekane na wapiga kura wao kuwa mahodari.


Wabunge wanaojielewa ni wale ambao wako kimya, wanachapa kazi, siku wakiongea wanaongea mambo yenye maana. Siyo Kina Lema, Halima Mdee, Kibajaji, uharo mtupu.
 
Tatizo ni ujinga ytu hapo, wote wapinzania na wasio wa[pinzani.

Mikataba ya Kimataifa, uwe na sheria zako usiwe na sheria zako, mradi umeingia mikataba ya Kimataifa basi itaendeshwa kimataifa bila kujali sheria za nchi yako.


Mara nyingi kwenye mikataba huwa akuna kukumbushana taratibu za kuiendesha tu mikataba, lakini mkienda kinyume kidogo au mliyeingia nae akienda kinyume kidogo, wote mnahukumiwa kwa "arbitration" za Kimartafa.

Mawaziri wetu na wabunge wetu nnakuhakikishai 90% hawafahamu kwanini wao ni wabunge na majukumu ya asasi niyepi. Wawe wa upinzani au wa CCM, wote ni hali kadhalika.

Kwa mtazamo wao wapo pale ili wapige kelele sana waonekane na wapiga kura wao kuwa mahodari.


Wabunge wanaojielewa ni wale ambao wako kimya, wanachapa kazi, siku wakiongea wanaongea mambo yenye maana. Siyo Kina Lema, Halima Mdee, Kibajaji, uharo mtupu.
Hoja yako ina mantiki kiasi Faiza, lakini unajaribu kutupia lawama wanaokandamizwa na viongozi wa Bunge Kwa makusudi ili kuibeba serikali Bungeni.
Ni mara nyingi wakati angalau Bunge likiwa na Sura ya kibunge hata Kiongozi wa upinzani alikuwa anadharaulika kuliko mhudumu wa Bunge.
Kama ilifikia CCM kutengeneza kundi la Wasema ovyo bungeni (Ally Kesi, Kibajaji, Msukuma na Mlingwa, ulitegemea lolote la maana toka kundi Hilo?
Wabunge wa Chama chako hawaitendei haki Jamii, kabisa hapana.
 
Hoja yako ina mantiki kiasi Faiza, lakini unajaribu kutupia lawama wanaokandamizwa na viongozi wa Bunge Kwa makusudi ili kuibeba serikali Bungeni.
Ni mara nyingi wakati angalau Bunge likiwa na Sura ya kibunge hata Kiongozi wa upinzani alikuwa anadharaulika kuliko mhudumu wa Bunge.
Kama ilifikia CCM kutengeneza kundi la Wasema ovyo bungeni (Ally Kesi, Kibajaji, Msukuma na Mlingwa, ulitegemea lolote la maana toka kundi Hilo?
Wabunge wa Chama chako hawaitendei haki Jamii, kabisa hapana.

Afrika nani umtowe tonge mdomoni? Wote njaa tupu.
 
Afrika nani umtowe tonge mdomoni? Wote njaa tupu.
Ok Sawa. Tukae kimya mpaka na Sisi tutakapopata hayo matonge au tufanyeje? Maana tunapotaka kutafuta usawa Kisheria (kikatba) kuna wenzetu mnatuvuta mashati!!
 
IMG_2819.jpg
 
Back
Top Bottom