Nadhani hujanielewa vizuri wewe umeuliza kama wanalipa vizuri mie nimejaribu kukueleza namna ya mshahara unavyokua, moja, mshahara wa migodini hupanda kadiri wewe mwenyewe unavyojiboresha, mbili ongezeko la mshahara kwa mwaka lakini mshahara wako wewe ni kama nilivyosema haujafika milioni sababu wewe ni mwanafunzi mfanyakazi lakini kwa baadae utakuja kupanda watakapojiridhisha umepata uelewa zaidi na hii lazima wakupe mitihani yao na ufaulu angalau upate 85% hapo wanaweza kukupandisha daraja na mshahara maana Wazungu au migodi haiamini Mavyeti ya huku mashuleni ili wajue unajua lazima ufanye yao ndio wakuelewe, Hata kama wewe ni muendesha mitambo huku mitaani na una vyeti hivyo ni mali yako tu wala si sababu yakutuaminisha unaweza kuendesha mitambo migodi lazima upitie mafunzo kwanza na ufanye mitihani upate kibali ya kuendesha hiyo mitambo wala hiyo leseni yako haihusiki migodini leseni wanaita x, hapa kila unapojifunza mtambo na mkufunzi akakuidhinisha umefuzu unapata x ya hiyo machine hivyo hivyo unaendelea mpaka utafikia hatua ya uongozi kwa kujifunza zaidi, mshahara kama wewe ni mwanafunzi na bado upo kwenye matazamio si kitu chakuangalia sana kikubwa jitahidi kujua vitu vingi maana mgodi ukiwa mjanja ni chuo tena bora sana maana huku mitaani hakuna chuo kilicho na mitambo/machine wanazotumia Wazungu kwenye kazi zao hivyo lazima uwe mpole kwaza upate shule mie nakumbuka mara yangu kuiingia nilikua sijui chochote na watu walinitisha sana utaweza kuiendesha ile mitambo, lakini Mungu alinisimami ndani ya mda mfupi na wazidi vitu vingi watu wakulizika na mishahara na kusahau kujiboresha zaidi ili wafikie kiwango cha kimataifa, mie hapa nilipofika naweza kufanya kazi ya mgodini nchi yeyote na jamii yeyote na wakaelewa kazi yangu maana hawa jamaa wa Wazungu wanakutengeneza uwe wa kimataifa zaidi sababu kazi zao ni zile zile leo watakuwa Tanzania kesho Canada hivyo ni vyema wakawa na timu zao ili kuepusha usumbufu wa kupata watu wanapopata tenda ya kazi lakini hapa naongelea zaidi watu wa kazi za mining sio kukaa ofisini kama yako hiyo utasubiri sana kuona mshahara mnono na production bonus ambazo zaidi huja mnapofanya kazi bila ajari ndani ya kitengo na kuzidi malengo ya uzalishaji taraji unaweza kukutana na bonus hata ya laki tano nje ya mshahara na ukijumlisha na mshahara unatoka na hela nzuri tu...