Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,156
Nimemsikikiza kwa makini Mwanasiasa mkongwe hapa nchini, Abdrahman Kinana, kwa taarifa yake aliyotoa kwa Umma kwa kile alichokiita mwenyewe kuwa anaomba msamaha kwa Rais Magufuli kwa yale maneno yaliyonaswa kwenye video clip, ambayo anaamini yalimkera Mheshimiwa Rais
Nimemsikiliza pia Mheshimiwa huyo Abdrahman Kinana akilalamika kuwa kiukweli alipotamka maneno hayo, alikerekwa, alihuzunika na alikasirishwa sana.
Hakufafanua kuwa ni nini kilichomfanya Mheshimiwa Kinana, akerekwe, ahuzunike na akasirishwe sana na kama vitu hivyo vilivyomkasirisha wakati huo, vimekuwa "solved" kwa wakati huu
Hata hivyo anamalizia kwa kusema kuwa baada ya kufikiria kwa muda mrefu, anadhani ni muda muafaka kwake kumwomba msamaha Rais Magufuli, kwa kitendo alichokitenda ambacho anaamini kilimuudhi Mheshimiwa Rais na kwa kuwa yeye ni muungwana amelazimika kuchukua hatua hiyo ya kumwomba radhi Mheshimiwa Rais.
Hebu tutafakari kwa kina chanzo cha sakata hili zima la hao wazee wastaafu hadi kupelekea wawekwe kitimoto na kujadiliwa kwenye kikao cha juiu kabisa cha chama chao, kikao cha Kamati Kuu ya CCM
Mzozo wote huu chanzo chake ni kutokana na mtu mmoja anayeitwa Crispin Musiba kutoa tuhuma nzito zisizo na ushahidi na ambazo Wazee hao wastaafu waliona kuwa zimewavunjia heshima ndani ya jamii ya watanzania.
Hatua waliyochukua wazee hao ni kupeleka malalamiko yao kwenye uongozi wa chama chao, ambapo walidhani kuwa wangesikilizwa kwa kuitwa huyo mtu anayeitwa Musiba ili atoe ushahidi kwa yale anayowatuhumu
Bila shaka wote tulishuhudia kile kilichojitokeza baada ya hao wazee kuyafikisha kwenye chombo husika cha maamuzi ndani ya chama chao.
Cha kushangaza ni kuwa hao waliopelekewa malalamiko hayo, waliyaona ya moto sana na hivyo kupata "kigugumizi" kuyajadili na hivyo kuyatupilia mbali!
Swali tunalojiuliza ni nani haswa anayemkingia kifua "kivuruge" huyu Cyprian Musiba, hadi vyombo husika vya maamuzi vya chama, hata na vyombo vya sheria vya mahakama vipate "kigugumizi" kutoweza kumjadili kabisa??
Bila "ku-solve root cause" ya tatizo lenyewe ambaye ni huyu mtu amayeitwa Cyprian Musiba, hii misamaha inayodaiwa inaombwa na wahusika itakuwa kiini macho, na bado moshi utakuwa unaendelea kufukuta chini kwa chini na siku moto huo utakapokuja kulipuka, hakuna wa kuweza kuuzima!
Hebu tujiulize ni nani hasa huyu mtu anayemkingia kifua huyu mtu Cyprian Musiba hadi vyombo vya maamuzi vya chama na vyombo vya sheria vishikwe na "mchecheto" na kutoweza kumjadili kabisa??
Ninachotahadharisha ni kuwa kwa kuwa wastaafu hao wamegundua "weakness" yake Mheshimiwa mkubwa kabisa, basi nadhani wameshauriwa na watu wao wa karibu kuwa "bora liishe" kwa kuomba msamaha na huyo Mheshimiwa mkubwa kabisa atafurahi kwa kuamini ya kwamba yeye ndiye anayegopewa kuliko mtu yeyote hapa nchini!
Tahadhari kubwa ninayoitoa hapa ni kuwa misamaha ya aina hiyo haitoki ndani ya mioyo yao hao watu, Bali ni kukubali tu yaishe ili maisha yaendelee na wabaki kwenye "system"
Nimemsikiliza pia Mheshimiwa huyo Abdrahman Kinana akilalamika kuwa kiukweli alipotamka maneno hayo, alikerekwa, alihuzunika na alikasirishwa sana.
Hakufafanua kuwa ni nini kilichomfanya Mheshimiwa Kinana, akerekwe, ahuzunike na akasirishwe sana na kama vitu hivyo vilivyomkasirisha wakati huo, vimekuwa "solved" kwa wakati huu
Hata hivyo anamalizia kwa kusema kuwa baada ya kufikiria kwa muda mrefu, anadhani ni muda muafaka kwake kumwomba msamaha Rais Magufuli, kwa kitendo alichokitenda ambacho anaamini kilimuudhi Mheshimiwa Rais na kwa kuwa yeye ni muungwana amelazimika kuchukua hatua hiyo ya kumwomba radhi Mheshimiwa Rais.
Hebu tutafakari kwa kina chanzo cha sakata hili zima la hao wazee wastaafu hadi kupelekea wawekwe kitimoto na kujadiliwa kwenye kikao cha juiu kabisa cha chama chao, kikao cha Kamati Kuu ya CCM
Mzozo wote huu chanzo chake ni kutokana na mtu mmoja anayeitwa Crispin Musiba kutoa tuhuma nzito zisizo na ushahidi na ambazo Wazee hao wastaafu waliona kuwa zimewavunjia heshima ndani ya jamii ya watanzania.
Hatua waliyochukua wazee hao ni kupeleka malalamiko yao kwenye uongozi wa chama chao, ambapo walidhani kuwa wangesikilizwa kwa kuitwa huyo mtu anayeitwa Musiba ili atoe ushahidi kwa yale anayowatuhumu
Bila shaka wote tulishuhudia kile kilichojitokeza baada ya hao wazee kuyafikisha kwenye chombo husika cha maamuzi ndani ya chama chao.
Cha kushangaza ni kuwa hao waliopelekewa malalamiko hayo, waliyaona ya moto sana na hivyo kupata "kigugumizi" kuyajadili na hivyo kuyatupilia mbali!
Swali tunalojiuliza ni nani haswa anayemkingia kifua "kivuruge" huyu Cyprian Musiba, hadi vyombo husika vya maamuzi vya chama, hata na vyombo vya sheria vya mahakama vipate "kigugumizi" kutoweza kumjadili kabisa??
Bila "ku-solve root cause" ya tatizo lenyewe ambaye ni huyu mtu amayeitwa Cyprian Musiba, hii misamaha inayodaiwa inaombwa na wahusika itakuwa kiini macho, na bado moshi utakuwa unaendelea kufukuta chini kwa chini na siku moto huo utakapokuja kulipuka, hakuna wa kuweza kuuzima!
Hebu tujiulize ni nani hasa huyu mtu anayemkingia kifua huyu mtu Cyprian Musiba hadi vyombo vya maamuzi vya chama na vyombo vya sheria vishikwe na "mchecheto" na kutoweza kumjadili kabisa??
Ninachotahadharisha ni kuwa kwa kuwa wastaafu hao wamegundua "weakness" yake Mheshimiwa mkubwa kabisa, basi nadhani wameshauriwa na watu wao wa karibu kuwa "bora liishe" kwa kuomba msamaha na huyo Mheshimiwa mkubwa kabisa atafurahi kwa kuamini ya kwamba yeye ndiye anayegopewa kuliko mtu yeyote hapa nchini!
Tahadhari kubwa ninayoitoa hapa ni kuwa misamaha ya aina hiyo haitoki ndani ya mioyo yao hao watu, Bali ni kukubali tu yaishe ili maisha yaendelee na wabaki kwenye "system"