Minara ya simu inamilikiwa na nani?

Minara ya simu inamilikiwa na nani?

Uhuru24

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2015
Posts
4,477
Reaction score
5,036
Leo nilikuwa sehemu tukifanya jambo flani hivi,sasa ukaibuka ubishi mkubwa sana juu ya umiliki wa hii minara,makundi yaligawanyika
01:Kundi la kwanza lilikuwa linasema minara ni mali ya kampuni ya simu husika,eg tigo hujenga wao minara yao kwa shughuli zao.
02:Kundi la pili husema kwamba minara ni kampuni ambayo inajitegemea isipokuwa wanaojenga hiyo minara huwakodishia wenye makapuni ya simu eg airtel nk.
Sasa mm nimeona ngoja nije niulize huku,maana JF shule tosha ya kupata majibu ya swali husika,tushirikiane kwenye hili ili tuweze kupata majibu mujarabu kabisa kwa wale ambao wenye A,B,C za hichi kitu.
Nawasilisha
 
Mnara wa tigo au njoo hapa mnara wa voda!
Sogea hapa Minara miwili
ivo yaaani ndio huwa mambo yapo mtaani
 
Kila kampuni inajenga Minara yake aisee...!! Ndo maana kuna minara ya zantel unakuta mingne imekufa sijui ipo ipo tu..
 
Daaah,umenikumbusha mzee mpwagi, jamaa walipima eneo lake bwana ikaonekana ndio sehem sahihi ya kujenga mnara
 
Leo nilikuwa sehemu tukifanya jambo flani hivi,sasa ukaibuka ubishi mkubwa sana juu ya umiliki wa hii minara,makundi yaligawanyika
01:Kundi la kwanza lilikuwa linasema minara ni mali ya kampuni ya simu husika,eg tigo hujenga wao minara yao kwa shughuli zao.
02:Kundi la pili husema kwamba minara ni kampuni ambayo inajitegemea isipokuwa wanaojenga hiyo minara huwakodishia wenye makapuni ya simu eg airtel nk.
Sasa mm nimeona ngoja nije niulize huku,maana JF shule tosha ya kupata majibu ya swali husika,tushirikiane kwenye hili ili tuweze kupata majibu mujarabu kabisa kwa wale ambao wenye A,B,C za hichi kitu.
Nawasilisha
Kimsingi wote wako sahihi ingawa si sahihi sana.

Zamani kila kampuni ya mawasiliano ilikuwa inajenga minara yake yenyewe lakini baada ya mwaka 2010 (sikumbuki mwaka exactly) kampuni ya Helios Towers Tanzania (HTT) iliingia mkataba wa kununua na kumiliki minara yote iliyokuwa ya Vodacom na Tigo na minara mingine pia waliendelea kujenga na kupandiana hayo makampuni pamoja na mengine yanayohusu huduma yao.

Baada ya hapo makampuni ya haya nayo yalijenga minara yake yenyewe na mingine ilijengwa kwa kushirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (USCAF) huu mfuko unashirikiana na Makampuni yote ya simu ikiwemo TTCL, Airtel, Tigo, Vodacom, Zantel including Halotel.

Hivyo kwa shares ya minara iliyopo nchini mingi inamilikiwa na HTT, Airtel (hawa hawakuuza minara yao), Halotel (hawa nao walijenga minara yao, viminara fulani virefu hivi vyembamba), Zantel (hawa nao hawakuuza), TTCL na michache ya Vodacom na Tigo na mingine inayomilikiwa na kampuni husika kwa kushirikiana na USCAF.

NB. Mnara mmoja unaweza kutumia na kampuni zaidi ya moja kwa kitu ambacho wenyewe wanaita site sharing na kimsingi kinachokuwa shared ni huo mnara, power, saa nyingine na transmission links zinakuwa shared.
 
Back
Top Bottom