Minara ya simu inamilikiwa na nani?

Minara ya simu inamilikiwa na nani?

Mi nijuavyo mnara hujengwa na kampuni huska ya simu mfano: hapa kwetu airtel walijenga mnara rakini kampuni ya tigo na voda wakaingia shea kwenye huo mnara

Tigo akaweka vifaa juu ya mnara
Pia ata voda akaweka mtambo yake kwenye huohuo mnara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu mimi kwangu kuna mnara wa kampuni iliyokuwa inaitwa Sasatel, hii kampuni kwa sasa haipo na mnara umebaki kama pambo. Juhudi za kuwatafuta ili nijue nifanyeje ili eneo langu nitumie kwa matumizi mengine siwapati na ofisi zao hazipo tena. Kibaya zaidi tangu 2005 nawadai! Naombeni ushauri wenu kwa wanaojua.
Mkuu Ulishapata Ufumbuzi? Njoo DM
 
Kimsingi wote wako sahihi ingawa si sahihi sana.

Zamani kila kampuni ya mawasiliano ilikuwa inajenga minara yake yenyewe lakini baada ya mwaka 2010 (sikumbuki mwaka exactly) kampuni ya Helios Towers Tanzania (HTT) iliingia mkataba wa kununua na kumiliki minara yote iliyokuwa ya Vodacom na Tigo na minara mingine pia waliendelea kujenga na kupandiana hayo makampuni pamoja na mengine yanayohusu huduma yao.

Baada ya hapo makampuni ya haya nayo yalijenga minara yake yenyewe na mingine ilijengwa kwa kushirikiana na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (USCAF) huu mfuko unashirikiana na Makampuni yote ya simu ikiwemo TTCL, Airtel, Tigo, Vodacom, Zantel including Halotel.

Hivyo kwa shares ya minara iliyopo nchini mingi inamilikiwa na HTT, Airtel (hawa hawakuuza minara yao), Halotel (hawa nao walijenga minara yao, viminara fulani virefu hivi vyembamba), Zantel (hawa nao hawakuuza), TTCL na michache ya Vodacom na Tigo na mingine inayomilikiwa na kampuni husika kwa kushirikiana na USCAF.

NB. Mnara mmoja unaweza kutumia na kampuni zaidi ya moja kwa kitu ambacho wenyewe wanaita site sharing na kimsingi kinachokuwa shared ni huo mnara, power, saa nyingine na transmission links zinakuwa shared.

Masuke mutu mbad...utakuwa mtu wa sites ww. kula 5...USCAF ni kusupport maeneo ya vijijini ili wawe na mawasiliano pia, serikali inatoa mpunga kwa kujenga minara... then kipata kitachpoatikana..kinarudi serikali taratibu then...mnara utabaki kwa kampuni husika....

shortly ttcl ana minara yake,halotel the same na zantel ila Tigo na voda waliuza kwa HTT,wakaibolesha then wanawpangisha wao... kuna stress wanaziondoa especially kwa issue za power and fuel.

Baada ya zantel kuchukuliwa na tigo somes of towers ziko HTT vilevile.... na HTT minara ikikalibiana let say wa voda na tigo..anavunja mmoja anabaki na mmoja then wanafanya joint ndio hiyo unaita site shring ili kupunguza cost...najazilizia tu ila imemaliza kila kitu mkuu.
 
Wakuu mimi kwangu kuna mnara wa kampuni iliyokuwa inaitwa Sasatel, hii kampuni kwa sasa haipo na mnara umebaki kama pambo. Juhudi za kuwatafuta ili nijue nifanyeje ili eneo langu nitumie kwa matumizi mengine siwapati na ofisi zao hazipo tena. Kibaya zaidi tangu 2005 nawadai! Naombeni ushauri wenu kwa wanaojua.
Njoo pm tuyajenge....labda tunaweza badilishana mawazo...location. nina aidea kdg nao hao jamaa
 
Ni kweli kabisa ila tatizo kumbwa makapuni mengi yamepunguza nguvu kwenye kulinda minara yao .ila cha msingi ni kuhakikisha mafundi wanaipitia iyo minara mara kwa mara sio mpaka waone signal azikosawa ndo waende site,kiongoz vp na wewe upo kwenye hii industry nin?
fundi hawezi akawa anazunguka tu wkt mafuta anapewa kwa km...lazima ajustify..huwa anatembelea kwenye siye pm na lost of signal au site ikiwa down...wenyewe wanakata cost kwa kuondoa walinzi so kwanini ajisumbue fundi kwenda kulinda...?
 
Leo nilikuwa sehemu tukifanya jambo flani hivi,sasa ukaibuka ubishi mkubwa sana juu ya umiliki wa hii minara,makundi yaligawanyika
01:Kundi la kwanza lilikuwa linasema minara ni mali ya kampuni ya simu husika,eg tigo hujenga wao minara yao kwa shughuli zao.
02:Kundi la pili husema kwamba minara ni kampuni ambayo inajitegemea isipokuwa wanaojenga hiyo minara huwakodishia wenye makapuni ya simu eg airtel nk.
Sasa mm nimeona ngoja nije niulize huku,maana JF shule tosha ya kupata majibu ya swali husika,tushirikiane kwenye hili ili tuweze kupata majibu mujarabu kabisa kwa wale ambao wenye A,B,C za hichi kitu.
Nawasilisha
ukiachana na mambo ya mitandao hizi minara zimetusaidia sana huku mtaani kwenye swala la marking na location, utasikia tuonane pale karibu na mnara wa tigo,voda, airtel,halotel au zantel ''hadi nimekumbuka tangazo flani inayosema yaone maisha katika mwanga ulio bora''
 
Back
Top Bottom