MIMI : Nikuulize jambo, askofu? ASKOFU: Ndio, uliza mtumishi wa Baba 😀.

MIMI : Nikuulize jambo, askofu? ASKOFU: Ndio, uliza mtumishi wa Baba 😀.

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
2,144
Reaction score
3,459
MIMI : Nikuulize jambo, askofu?

ASKOFU: Ndio, uliza mtumishi wa Baba
😀.
1768474474318.jpg


MIMI: Hivi kati ya Mungu na nyoka nani
aliyemdanganya Mtu pale
‎bustanini?

ASKOFU: Nyoka ndo alindanganya
mwanadamu. Mungu
‎alimwambia mwanadamu kuwa
‎akila atakufa. Ila nyoka
‎akamdanganya kwamba akila
‎atafanana na Mungu.

MIMI: Mbona unaanza tena
kunidanganya, baba askofu! Ndo
‎imeandikwa hivyo kwamba
‎atafanana na Mungu?

ASKOFU: We kijana vipi? Hujui ndo
imeandikwa hivyo? Imeandikwa
‎kuwa akila atafanana na
‎Mungu.

MIMI: Hebu Nisomee hilo fungu
tuonehilo fungu tuone.

ASKOFU: biblia katika Mwanzo 3:4
Inasema "Nyoka akamwambia
‎mwanamke, Hakika hamtakufa,
‎Mwanzo 3:5
kwa maana Mungu anajua ya
‎kwamba siku mtakayokula
‎matunda ya mti huo,
‎mtafumbuliwa macho, nanyi
‎MTAKUWA KAMA MUNGU,
‎mkiju mema na mabaya.

MIMI : Mbona sijaona palipoandikwa
kuwa watafanana na Mungu?

ASKOFU: Ndio, hapapo. Ila kuwa kama
Mungu ndo tulifundishwa tuwe
‎tunaitafsiri kama kufanana na
‎Mungu.

MIMI: Kwani Mwanzo 1:26 si inaonesha
kuwa Mungu alikuwa na agenda ya
‎kumuumba mtu kwa mfano wao?
‎Mbona hapa nyoka anasema
‎watakuwa kama Mungu? Ina
‎maana Hawakuumbwa kwa mfano
‎wake?

ASKOFU: Hapo sasa ndo utaanza kuona
uongo wa nyoka hehehee. Yaani
‎hapa bila macho ya kiroho
‎huwezi kuelewa. Ila tayari roho
‎ameanza kukuelekeza kwenye
‎ukweli. Nyoka ni Muongo maana
‎tayari Mwanadamu alikuwa
‎ameshaumbwa kwa Mfano wa
‎Mungu. Kwa hiyo kwa kula tunda
‎asingeweza kuwa kama Mungu.

MIMI: Kwa hiyo nyoka alidanganya kwa
kumwambia Mtu kuwa Atakuwa
‎kama Mungu akijuwa mema Na
‎mabaya?

ASKOFU: Haswaaa.. Nyoka ni Muongo na
alidanganya. Mwanzo 3:5
[5]kwa maana Mungu anajua ya
‎kwamba siku mtakayokula
‎matunda ya mti huo,
‎mtafumbuliwa macho, nanyi
‎MTAKUWA KAMA MUNGU
‎MKIJUWA MEMA NA MABAYA.

MIMI: Hebu nisomee Mwanzo 3:22.

ASKOFU: Haya sawa, hehehehee.
Mwanzo 3:22 NENO LA BABA
‎YETU LINASEMAH,

MIMI: LINASEMA NINI?

ASKOFU: [22]BWANA Mungu akasema,
Basi, huyu mtu ANEKUWA
‎KAMA MMOJA WETU, AKIJUWA
‎MEMA NA MABAYA; na sasa
‎asije
‎akanyosha mkono wake
‎akatwaa matunda ya mti wa
‎uzima, akala, akaishi milele;

MIMI : Mbona Mungu hapa
anakiri usahihi wa Kauli ya
‎shetani
‎kwa kuonesha kabisa kuwa ni
‎kweli mtu angekuwa kama
‎Mungu pindi akila tunda la
‎Mema na Mabaya?

ASKOFU: Hakuna kitu hapo, Wewe ndo
huelewi kabisa na tena Omba
‎sana Roho akufunulie uweze
‎kulijuwa neno la Baba yetu. Ni
‎kweli walikuwa kama Mungu
‎kwa kujuwa mema na mabaya,
‎ila sio kufanana naye
‎kimuonekano.

MIMI : Kwani shetani alisema kuwa
mwanadamu akila tunda
‎atakuwa kama Mungu kwa
‎kufanana naye kimuonekano.

ASKOFU: Hujanielewa... Halafu tatizo lako
huna roho ndio maana shetani
‎anakufanya uwaze mambo ya
‎kijinga mda wote. Hii sehemu ni
‎ngumu, kijana. Kuielewa ni hadi
‎uwe umesoma tioloji kwenye
‎vyuo vyetu.

MIMI : Basi hilo swali gumu. Niulize,
Mwanadamu aliumbwa kwa
‎mfano wa Mungu?

ASKOFU: Ndio. Mwanadamu aliumbwa
kwa mfano wa Mungu kabisa
‎na hilo liko wazi, ama
‎nikufungulie vitabu?

MIMI: Tutavifungua tu usijali. Je
alikuwa anajuwa mema na
‎mabaya?

ASKOFU: Alikuwa anajuwa mema tu ila
hajui mabaya.

MIMI: Mbona Mungu anakiri
mwenyewe katika Mwanzo 3:22,
‎baada ya yeye kula tunda kuwa "
‎Sasa amejuwa mema na
‎mabaya?" Huoni kuwa
‎mwanadamu bado alikuwa hajui
‎mema na mabaya?

ASKOFU: Yeah, nilikuwa nimesahau.
Nisamehe kwa hilo.
Ukisoma kwa umakini unaona
‎kabisa kuwa mwanadamu
‎alikuwa hajui mema na mabaya
‎maana yalikuwa yamefungwa
‎kwenye mti wa ujuzi wa mema
‎na mabaya.

MIMI: Sasa kama bado alikuwa hana
ujuzi wa mema na mabaya.
‎Aliwezaje kutambua kama Mungu
‎anachomuelekeza ni chema. Ama
‎nyoka anachomuelekeza ni
‎Kibaya na hila?

ASKOFU: Hapa ni wazi kuwa unaanza
sasa kukufuru. Kwa hiyo,
‎unataka kuniambia kuwa Mungu
‎alimuonea Mwanadamu,
‎kwasababu tu
‎alimpa
‎maagizo wakati ambapo
‎mwanadamu hakuwa
‎na utambuzi wa lipi jema ama
‎lipi baya? Si ndo hivo?

MIMI: Ndio. Nina mwanangu ana miezi
mitano sasa bado hajawa na.
‎utambuzi wa lipi jema na lipi
‎baya. Iwapo nitamuwekea chupa
‎ya chai mbele halafu nimpe
‎maelekezo kuwa asiishike hiyo
‎chupa maana akifanya hivyo,
‎itapasuka na ataungua. Je,
‎ataelewa kuwa maagizo
‎niliyompa ni
‎mema?

ASKOFU: Hapana. Bado hajapata
utambuzi. Itabidi umlinde sana
‎na sio kumpa majaribu. Lakini
‎adamu alikuwa
‎mtu mzima hata kama hakuwa
‎na utambuzi.

MIMI: Kwa hiyo hakupaswa kupewa
ulinzi kamili na kuepushwa na
‎majaribu kama unavyonishauri
‎nifanye kwa mwanangu?

ASKOFU: Tunakoelekea sasa tutakufuru
kijana. Staki uje upate matatizo
‎kabisa. Utapigwa mapigo
‎mabaya na Mungu kama
‎Waliyoyapata wamisri.

MIMI: Sasa mbona badala ya kunijibu
unaanza kunitisha? Kwani huoni
‎kuwa Mungu wako aliadhibu
‎watu wazima kwa makosa
‎waliyoyafanya wakati ambapo
‎walikuwa bado wachanga?

ASKOFU: Sawa walikuwa wachanga. Na
waliadhibiwa kwa kuonewa. Ila
‎hayo mambo hayamfanyi
‎Mungu wetu kuwa muonevu.
‎Mungu wetu ana huruma, ana
‎upendo, na msamaha.
‎Jinyenyekeze mbele zake la
‎sivyo Siku ya Mwisho
‎utaadhibiwa.

MIMI: Kwa hiyo hayo uliyayaona na
uliyoyataja, ni upendo ama
‎udhibiti?
Yaani ninakuambia kuwa nina
‎huruma msamaha, upendo na
‎silazimishi. Ila usiponifuata
‎nitakuangamiza? Huoni huo ni
‎udhibiti na sio uhuru?

ASKOFU: Unatafuta uhuru kwa Mungu, si
ndo hivyo? Acha Niwapigie
‎polisi waje kukupa uhuru kijana.

MIMI: 👇👇👇👇
 
Kuna swali nilimuuliza mchungaji faluni
akasema eti mimi ni pepo mchafu nimetumwa kumjaribu

aisee hizi dini!
 
Hapo hapakua na Nyoka wala baba yake Nyoka.
Hapo ilikua ni vuta nikuvute kati ya Shetani [Wale malaika walioasi], wampe Enlightment Mwanadamu, ajitambue zaidi, na ikiwezekana ajue siri zote za uMungu, ulimwengu na yeye ili kwa kujua huko wamuasi Mungu pia.Na ndo maana kwenye vitabu mfano cha Enock ambacho hakikuchapwa kwenye hii biblia, utaona kuna malaika wanafundisha watu elimu zote za dunia hii - kabla ya hapo mwanadamu alikua kama kopo tu, programmed...hujui mema, mabaya, ubaya, wewe ni kula bata tu huku uko restricted.

Hawa jamaa, wakawafundisha wanadamu uchawi, astronomy, sayansi ya vita, utabibu n.k.nk
Ikabaki kidogo tu apate siri ya kuishi milele - Mungu akaona sasa nyie wapuuzi mmezidi ..mnakoelekea mtatengeneza kiumbe ambacho hakitabiriki na kitaleta imbalances.
Mungu kapiga pin, kafungia access ya elimu na utambuzi zaidi...shetani naye akawa restricted...BinAdamu akabaki anababaika, anatangatanga na elimu nusu....hadi leo hatujielewi.

Baadae binadamu walijiorganize tena - ubishi uleule.Kwanza wakawa wanaongea lugha moja maana yake wanashare mambo...UMOJA NI NGUVU, pili wakataka kumchallenge Mungu...ooh..tutengeneze Mnara mpaka mbinguni...tukamchunguze Mungu, meaning wazidi kuchimba mambo kwa umoja watake kumjua Mungu zaidi.Mungu kawachungulia kaona hawa wajinga kwa huu umoja ni threat kabisa..kawavuruga lugha hakuna kuelewana, kawatawanya ulimwenguni kote..meaning...misuguano ikaanza, hakuna kupoa mpaka leo.
MTI WA UZIMA HATUWEZI KAMWE KUULA[TUNDA]
 
Back
Top Bottom