Mimi ni CCM, napinga Rais Magufuli kuongezewa muda

Mimi ni CCM, napinga Rais Magufuli kuongezewa muda

Magari ya kukodisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2019
Posts
412
Reaction score
696
Wakuu habari,

Nasikitishwa na ukiukwaji katiba na kanuni unaotaka kufanywa CCM.

Baba wa taifa alituasa kuwa yeye ndiye wa mwisho kutawala kwa muda mrefu kwenye nchi hii na asitokee yeyote mwenye tamaa kujaribu kutawala kwa muda mrefu.

Nimeshangazwa na mwanachama mwenzangu Mbunge Kessy wa Nkasi anaesisitiza katiba ibadilishwe ili rais aongezewe muda kwakuwa anafanya mambo mazuri.

Swali langu: Je, katika nchi hii hakuna watu wengine wenye nia njema na nchi yetu zaidi ya Magufuli?

Je, nchi hii sisi wengine hatutakiwi kuwa Marais?

Je, ule utaratibu wa kupokezana kijiti ndio unakufa?

Je, tunawafundisha nini watoto wetu?

Nakemea kwa nguvu zote na yeyeto atakayeenda kinyume na matakwa ya baba wa taifa alaaniwe kwa kumkosea heshima muasisi wa taifa hili

Lumumba kindakindaki
 
Mimi sina chama ila wanaotaka kumuongezea muda rais wanataka kuturudisha enzi za mapinduzi kwani kuna marais wangapi wamepita pamoja na wapambe wao kutaka muda uongezwe lakini waliheshimu sheria isitoshe hoja nzito kama hii ilitakiwa ianzie ndani ya chama.
 
Naomba aharakishe utaratibu huo ili CCM iondoke madarakani mkigusa katiba na kumfanya mtu huyu atawale miaka zaidi ya kumi safari yenu imeiva na utabiri wa Nyerere umetimia.

Na kwa sehemu kubwa mtu yule wa hovyo aliyesemwa na Nyerere mwenye kushauriwa na mke wake kwa sehemu kubwa tumemuona.
 
Msiogope tutapiga kura juu ya hilo, then wengi watashinda. Au mnaogopa mko wachache msiompenda mkulu?
 
Mimi sina chama ila wanaotaka kumuongezea muda rais wanataka kuturudisha enzi za mapinduzi kwani kuna marais wangapi wamepita pamoja na wapambe wao kutaka muda uongezwe lakini waliheshimu sheria isitoshe hoja nzito kama hii ilitakiwa ianzie ndani ya chama
Ukitaka kujua swala hilo liko njiani angalia maandalizi ya bunge kuwa la CCM pekee Novemba utajua kitachotokea bungeni.
 
Msiogope tutapiga kura juu ya hilo, then wengi watashinda. Au mnaogopa mko wachache msiompenda mkulu?
Kura ni ya wazi na tunataka nani hapigi ili tumshughulikie akafie mbali.
 
Matatizo ya wafugaji wakipata madaraka ndio hayo sasa ni wakati mzuri wa kujifunza hivi watu wa jamii hii wakitawala mambo ya kienyeji huwa ndio rasmi. Watu wamechoka kwa kweli na ni aibu sana kwa ushamba wa kiwango hiki.
 
Wanasiasa njaa ndo wanatamani upuuzi huu hawana uhakika na vyeo vyao baada ya jiwe kustaafu.
 
Mexican Gang,

Pamoja na rais kufanya mageuzi makubwa,kumwongezea muda ni kuchezea katiba.Je, akija rais hafai tumwondoe hata kabla ya muhula wake?
 
Mtu kashindwa kuiongoza Nchi. Nchi imejaa chuki na hofu kubwa. Mtaani ni vilio tu vya hali ngumu ya maisha. Hana sifa huyu ya kuongoza Nchi na kwa woga wake ndiyo sababu alimfukuza Membe ccm kwa kujua fika Membe angempiga chini. Hata ndani ya ccm wengi wamemchoka yeye mwenyewe alitangaza hadharani kachoka na kazi ni ngumu na ina MATESO makubwa.
 
Ndugu yangu semea humu humu kama ukijaribu kwenye kikao basi mkeo na wanao hawatakuona tena.

Waache wafanye wafanyavyo kwani wao ndiyo watawala wewe ni nani?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mantiki na msingi wa kuweka ukomo wa vipindi vya urais kuwa miaka kumi ilikuwa ni nini na je, msingi huo hauna maana tena?

Ni kweli wakati wa kuweka ukomo hapakuwa na watanzania wenye uwezo sawa na au hata zaidi ya rais wa sasa?

Ni kweli pia kuwa hivi sasa hakuna mtanzania yeyote anaeweza kuwa rais na akafanya vizuri au hata vizuri zaidi?

Bila shaka wanao pendekeza muda uongezwe wamepitiliza furaha waliyo nayo.
Na hata wakiongeza miaka mitano zaidi kwao haita tosha watatamani kuongeza zaidi.
 
Mimi sina chama ila wanaotaka kumuongezea muda rais wanataka kuturudisha enzi za mapinduzi kwani kuna marais wangapi wamepita pamoja na wapambe wao kutaka muda uongezwe lakini waliheshimu sheria isitoshe hoja nzito kama hii ilitakiwa ianzie ndani ya chama
Hatuko tayari kurudi enzi za mapinduzi
 
Msiogope tutapiga kura juu ya hilo, then wengi watashinda. Au mnaogopa mko wachache msiompenda mkulu?
Nimekuelewa mantiki yako lakin jua baba wa taifa alishatoa laana kwa yeyote atakayejaribu.
 
Matatizo ya wafugaji wakipata madaraka ndio hayo sasa ni wakati mzuri wa kujifunza hivi watu wa jamii hii wakitawala mambo ya kienyeji huwa ndio rasmi. Watu wamechoka kwa kweli na ni aibu sana kwa ushamba wa kiwango hiki.
Tukosoe kwa hoja tukishindilia kauli za baba wa taifa
 
Mantiki na msingi wa kuweka ukomo wa vipindi vya urais kuwa miaka kumi ilikuwa ni nini na je, msingi huo hauna maana tena?

Ni kweli wakati wa kuweka ukomo hapakuwa na watanzania wenye uwezo sawa na au hata zaidi ya rais wa sasa?

Ni kweli pia kuwa hivi sasa hakuna mtanzania yeyote anaeweza kuwa rais na akafanya vizuri au hata vizuri zaidi?

Bila shaka wanao pendekeza muda uongezwe wamepitiliza furaha waliyo nayo. Na hata wakiongeza miaka mitano zaidi kwao haita tosha watatamani kuongeza zaidi.
Viongozi wa Afrika wanamatatizo makubwa sana.
 
Ndugu yangu semea humu humu kama ukijaribu kwenye kikao basi mkeo na wanao hawatakuona tena.

Waache wafanye wafanyavyo kwani wao ndiyo watawala wewe ni nani..?
Kufa kila mtu atakufa lazima tuseme ukweli
 
Back
Top Bottom