Mimba imenifanya nichukie kuoga

Mimba imenifanya nichukie kuoga

Ndiyo, hii inaweza kutokea kabisa kwenye ujauzito wa wiki 10. 😅 Si lazima iwe kwamba mtu “amechukia usafi.” Katika kipindi hiki homoni za ujauzito zinaweza kuongeza sana hisia ya kunusa, na harufu fulani zinaweza kuchochea kichefuchefu au kumfanya mtu asivumilie hata maji, sabuni au shampoo. Wiki ya 10 bado ni kipindi ambacho dalili hizi huwa za kawaida.
Kwa hiyo umeamua ukimbilie ChatGPT kuchukua ya kuandika , 😂😂
 
Yaani naoga basi tu ili iwe mradi. Nimetokea kuyachukia kabisa maji ya kuoga.

Ambaye amewahi kukutana na kadhia hii anajulishe alivukaje? Mimba ina wiki 10
Wewe ni mvivu tu wa kuoga hilo halina shaka

Watu wanasingizia sana mimba imemfanya hivi au vile napenda kuwaambia kuwa mimba haimfanyi mtu kitu ukijikuta uko na tabia furani jua ndivyo ulivyo

Iko hivi binadamu wote tuna conscious mind na unconscious mind Tabia nyingi hufichwa kwenye unconscious mind sasa mimba inapoingia inasababisha hormonal imbalance hivyo tabia uliyoificha inaibuliwa na kwa kuwa utasingizia mimba unajipa tumaini kuwa mimba imesababisha hakika mimba haisababishi bali inaibua tabia yako uloificha

Kwa mfano wote binadamu tuna tabia mbaya ambazo huwa tunazikandamiza zisionekane wazi kwa watu lkn wewe unaijua na unaweza ikandamiza mpaka ikawa haionekani tena hata wewe ukajishangaa na kujipa tumaini kuwa tabia hiyo haipo tena 🤣 huko ni kujindanganya tabia ipo na ikitokea kichocheo inaamka upya

Mfano mwanamke alikuwa anamzimikia jamaa furani kabla ya mimba akipata mimba anaweza mpenda jamaa huyo mpaka hatoweza jizuia hii inatokea na wanawake kwa uongo wao wanasingizia mimba 🤣🤣🤣🤣🤣 wapendwa hiyo haipo jua ulimzimia jamaa tu kabla ya kitambi cha muda

NB msisingizie mimba tena hizo ni tabia zenu malaika ameiweka live ujione ulivo
 
kila mimba huja na tabia zake, kwa kila mwanamke.

Demu wangu wa KWANZA.
alipobeba ujauzito alizidi kunipenda sana nakunizuia nistoke awe ananiona tu machon pake.
Tulipata mtoto wa KIUME

Demu wangu wa PILI.
Alipobeba ujauzito alipenda harufu ya KIKWAPA changu tu, atakuja atajilaza nakunitanua mkono kisha ataweka pua zake humo.
nikiondoka kazin ataomba shati langu, tena lile shati lenye jasho.
nilibaki kushangaa jamani hii type...
Tulipata mtoto wa KIKE

na akinusa anasema hapo moyo umetulia.

Demu wangu wa TATU alipobeba ujauzito sasa.

wacha nicheke daaa.
ALINICHUKIAAA acha, nililala store nikichelewa hom hata saut yang hakutaka kuiskia.

Mpaka aliondoka kwenda kwao(kuna uzi niliandika aliniambukza gono na akaondoka kwao) na hata kweny simu nilipo mpigia aliongea kama tuna ugomvi.
Tumepata mtoto wa kiume mwez wa 8.
Ila hajarud bado
Aliyekupenda kabla ya mimba akipata mimba anakupenda zaidi hawezi jizuia

Anayekuchukia ila anajibaraguza kabla ya mimba akipata mimba atakuchukia live bila chenga utaona chuki yake 😂 halisi

Mimba haileti tabia ina ibua tabia ulizozificha ambazo ni tabia zako halisi 🤪🤪🤪🤪🤪
 
Aliyekupenda kabla ya mimba akipata mimba anakupenda zaidi hawezi jizuia

Anayekuchukia ila anajibaraguza kabla ya mimba akipata mimba atakuchukia live bila chenga utaona chuki yake halisi

Mimba haileti tabia ina ibua tabia ulizozificha ambazo ni tabia zako halisi
anhaaaa kumbe, ahsante mkuu umenipa mwanga angarau nimejua ABC
 
Tumewaacia mabwana kama mabinti na viherehere vyao na visebengo. Wanajuuua wanawake kuliko wanavyojijua wenyewe. Huwa nasoma comments nasema hiiiiii

Ps: sijasoma comments za hii thread
mwandko wako unaniumiza macho mkuu.

Nimesoma kwa kurudia coment yako ila sijaelewa umemaanisha nin
 
Back
Top Bottom