itagata
JF-Expert Member
- Sep 4, 2011
- 218
- 77
Mikutano ya CHADEMA inayoendelea hapa wilayani kwetu Iramba imeendelea kudoda baada ya kukosa watu kabisa. Mikutano hiyo ilifanyika katika kata ya Ndulungu, Kaselya, Kidaru, Ntwike na Mtoa. Katika mkutano wa Kidaru katika kijiji cha Tyegelo waliamua kwenda kwenye club ya pombe napo watu hawakuwasikiliza. Mingela ambako anatoka Dr Kitila Mkumbo walipata watu wasiozidi 45 tu. Hali ilikuwa mbaya sana katika kijiji cha Nsusu. Kiongozi mkuu alikuwa David Jumbe na wenzake wakiwemo Dr Mkumbo ambaye alikuwepo pia. CDM inabidi mpange mikakati mipya ya kuhakikisha Iramba mnakubalika lakini kwa hii mlionayo hamna kitu.
Poleni sana CDM wanyiramba mmeamini siyo Wachaga. Songela Zigizigi kwa kul'inga ikulukulu.
Bwana Shelui, kwanza nataka kukwambia kuwa mie sio mwanachama wa chama chochote na usijenifikiria kuwa naongelea ushabiki kama ulivyopost wewe uzi huu, kwa bahati nzuri sana mie nilikuwepo kwenye mkutano uliofanyika katika kijiji cha Nsunsu ambacho wewe umesema kuwa ni mojawapo ya vijiji ambavyo mikutano ya mkumbo haikuwa na watu, ukweli ni kuwa kwa haraka haraka mkutano ule ulikuwa na zaidi ya watu 150 na kama hao uliona wachache basi sema ulitaka wawe wangapi ndo ukubali kuwa ni wengi. Vinginevyo nashawishika kuamini kuwa umesimuliwa na watu waliokuwepo eneo hilo wenye mtizamo kama wako. kimsingi watu walikuwepo wengi na wa kutosha kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji hicho, vijiji vingine siwezi kuzungumzia kwa sababu sikuwepo.