Mkuu,
Lindi siku hizi tumeamka Sana.
Tuna misimu ya mazao Kama Sita kwa mwaka inayotufanya tutoke kwenye umasikini wa kutupwa.
Tuna msimu wa mahindi,
Msimu wa kunde,
Msimu wa ufuta,
Msimu wa mbaazi,
Msimu wa korosho,
Na mwisho kabisa msimu wa maembe ambayo kuanzia mwezi wa kumi Hadi wa 12 tunalisha miji mikubwa Kama Dar na Sasa hivi Bahresa ananumua Sana. Si umewahi kusikia "haya ni maembe ya kusini?" Basi ndiyo sisi.
Pia kwa. Maeneo yenye maji ya kutosha tunalima Sana nyanya na vitunguu ambavyo tunalisha mtwara,masasi na Dar es salaam.
Alafu Kuna mgodi wa Namungo ambao upo Ruangwa,unawanufaisha wananchi na kuongeza mzunguko wa hela maana Kuna wageni wengi Sana Sasa hivi. Rungwa inafikika kwa barababrayya lami na Kuna mahoteli kadhaa ya ghorofa yanayoupendezesha mji.
2025 nikigombea ubunge nikapita ndiyo naenda kuibadilisha moja kwa moja Lindi.
Kwa hiyo Lindi haiwezi kuwa katika hiyo list ya Kigoma,Kagera na Tabora.