Musoma mara,mwaka 2008,siwezi kusahau ile siku tarehe na mwez nimesahau ila siwezi kusahau,nimefika nikitokea Mwanza nilale asubuhi niende zangu dar kupitia sirari kipindi hicho njia ukiwa bukoba unapitia kampala kwa basi,ukiwa mwanza unapitia sirari,daaah nikachukua lodge,hapo hapo kulikuwa na bar,nikatoka enzi hizo balimi tamu balaa nikaanza kupiga balimi zangu ghafla akaja mshkaj akawa anamzingua muhudumu ambae anahusika na upande wa lodge na kaunta ya vinywa daaaah baada ya muda jamaa kaanguka kafa pale pale,cha kushangaza hakuna mlevi wala muhudumu aliostuka wakawa wanasema tu kiburi kimemponza,polisi wakaja wakachukua maiti bila kusema chochote na sisi tuliopo pale,palepale nikapata stor kuwa aliwekewa sumu ya mamba,usiku nimerudi chumbani maji yakawa hayatoki nikatoka kumgongea yule dada muhudumu,kwanza hakuitika ila aliuza nan wewe nikasema mm mpangaji wa chumba flan akauliza unataka nini,nikamwambia maji hakuna,akaniuliza kwahiyo[emoji3] daah nilipokumbuka tukio la yule jamaa aliokufa,nikamjibu hakuna kitu dada nimeuliza tu labda yatarudi na mabomba yapo wazi hivyo yatamwagika[emoji3][emoji16]