nilikwenda Zanzibar juz kati,katika harakati za kutafuta Lodge,nikaangukia lodge moja iko mbele ya kwa Mchina2, iko eneo la jeshi,ile kuingia tu getini kuna bango kubwa HILI NI ENEO LA JESHI "NIDHAMU HAIOMBWI" nikajisemea kimoyomoyo hapa pananifaa na patakuwa na ulinzi wa kutosha na utulivu. nikaingia ndani,nikaona kuna bar watu wanaangalia mpira,nikaambiwa upande wa lodge kule, niakaenda, kwanza kufika tu reception nikashtuka,nikasema mbona pamekaa hovyo hivi, kuingia zaidi nikamkuta mdada akaniambia vyumba vipo, nikamwomba nivione,kuangalia ni vitanda vya tofali na zege, vimejengwa kama kaburi,nikajisemea lahaula mbona hatari, nikamuuliza mhudumu, eeh!! chumba sh? akasema elfu30 kulala,lakini kama ni unalala tunaruhusu kulala kuanzia saa tatu ya usiku, hivyo unaweza kulipia ukaenda kuzurura akarudi saa tatu ili tukutandikie chumba chako, ila kama unataka short time hata kwa sasa unapata,kipo hicho hapo ametoka mtu sasa hivi tukutandikie. nikaona hapa hapanifai nikaondoka zangu