Tango73
JF-Expert Member
- Dec 14, 2008
- 2,128
- 1,225
Raisi wa zamani wa Urrusi Mikail Gobachev ansifa zote za kuwa mtakatifu. Ukikumbuka kwa jinsi gani siasa za kikomunisti au ujamaa na kujitegemea zilivyokuwa zinasumbua watu katika nchi zao. Huyu mrusi anstahili kabisaa kuheshimiwa kitakatifu kwa jinsi alivyo waokoa mabilion ya watu waliokuwa wanakandamizwa na siasa za kikomunisti.
Gobachev alijivua kabisaa umwinyi wa kuimbiwa kwaya na kuheshimiwa kama mungu na watu wake ingawa alikuwa katika nafasi nzuri sana ya kuwa billionea akistahafu. Kwa ujasiri wake, aliungana na Papa Paulo na Raisi wa marekani wakati huo, Ronald Regan kuhakikisha watu wote waliokuwa wanateswa na siasa za uongo na za kikatili za kikomunisti wanaokolewa na kuwa huru.
Gobachev hakutaka kabisaa kuja kuwa tajili kama walivyo wenzake waliokuwa wakuu wa KGB au Viongozi wa Chama cha kikomunisti cha Urussi-CCCCP. Gobachev aliwajali sana raia zake na watu waliokuwa wanateseka bila wao kujijua ndani ya nchi zao, ndio maana aliuchukia ukomunisti kwa nguvu zake na zakukopa zote.
Dunia lazima impatie heshima inayostahili mzee Mike' na awe anakumbukwa milele na wanyonge waliokuwa wanfanywa watumwa na wachache ndani ya nchi zao. Mkombozi siku zote hupendwa na kuabudiwa, sasa kwa nini wanadamu tusimuenzi mtu kama Gobachev? Haswa sisi watanzania ni lazima sana kumkumbuka Gobachev. Kukosa ujasili wake alioutumia kukomboa watu waliokuwa wanatwaliwa kimwinyi, hatungekuwa na upinzani kama wa CHADEMA, uhuru wa vyombo vya habari, kumiliki TV na kuona matukio makuu ya kisiasa, soka, usanii na dini duniani.na vile vile tusinge miliki Fliji,kuwa na vyuo vikuu ishirini , kuwa na mainjinia, madaktari na wanasheria wengi kuliko wansiasa..
Sasa hivi secta ya michezo, usanii na muziki zinalipa sana Tanzania na vijana wetu wanatajilika kila kukicha , hii yote ni kwa sababu ya ujasiri wa Gobachev. Jamani Gobachev anastahili kuwa Mtakatifu. nani alikuja jua kuwa ipo siku wachezaji wa Yanga wangekwenda kaunda kufanya mazoezi huku kila mmoja kapaki gari lake katika parking lot ya yanga?
Gobachev alijivua kabisaa umwinyi wa kuimbiwa kwaya na kuheshimiwa kama mungu na watu wake ingawa alikuwa katika nafasi nzuri sana ya kuwa billionea akistahafu. Kwa ujasiri wake, aliungana na Papa Paulo na Raisi wa marekani wakati huo, Ronald Regan kuhakikisha watu wote waliokuwa wanateswa na siasa za uongo na za kikatili za kikomunisti wanaokolewa na kuwa huru.
Gobachev hakutaka kabisaa kuja kuwa tajili kama walivyo wenzake waliokuwa wakuu wa KGB au Viongozi wa Chama cha kikomunisti cha Urussi-CCCCP. Gobachev aliwajali sana raia zake na watu waliokuwa wanateseka bila wao kujijua ndani ya nchi zao, ndio maana aliuchukia ukomunisti kwa nguvu zake na zakukopa zote.
Dunia lazima impatie heshima inayostahili mzee Mike' na awe anakumbukwa milele na wanyonge waliokuwa wanfanywa watumwa na wachache ndani ya nchi zao. Mkombozi siku zote hupendwa na kuabudiwa, sasa kwa nini wanadamu tusimuenzi mtu kama Gobachev? Haswa sisi watanzania ni lazima sana kumkumbuka Gobachev. Kukosa ujasili wake alioutumia kukomboa watu waliokuwa wanatwaliwa kimwinyi, hatungekuwa na upinzani kama wa CHADEMA, uhuru wa vyombo vya habari, kumiliki TV na kuona matukio makuu ya kisiasa, soka, usanii na dini duniani.na vile vile tusinge miliki Fliji,kuwa na vyuo vikuu ishirini , kuwa na mainjinia, madaktari na wanasheria wengi kuliko wansiasa..
Sasa hivi secta ya michezo, usanii na muziki zinalipa sana Tanzania na vijana wetu wanatajilika kila kukicha , hii yote ni kwa sababu ya ujasiri wa Gobachev. Jamani Gobachev anastahili kuwa Mtakatifu. nani alikuja jua kuwa ipo siku wachezaji wa Yanga wangekwenda kaunda kufanya mazoezi huku kila mmoja kapaki gari lake katika parking lot ya yanga?