Miji (sehemu) mizuri kwa mapumziko TZ

Miji (sehemu) mizuri kwa mapumziko TZ

Nenda kigoma ,fikia hilltop au lake tanganyika beach, tembelea ujiji ukajionee njia za misafara ya watumwa, uvinza, gombe kwa sokwe na jengo la Maranda wa EPA.
 
Hivi hakuna wilayani ambako ni kuzuri pia kutembelea? Lakini kuwe na usafiri wa uhakika!
Hata Ilala pia ni wilaya, Ilemela, nyamagana Arusha pia! ChaguA "Mnyewe" {don't mind just 4 a litle smile}
 
Nenda serengeti na ufikie ktk hiyo lodge ambayo majuzi tu imepata tuzo ya kuwa wildlife lodge bora kuliko zooootee duniani.
 
Kama unapenda kaa kwenye fukwe kupata sea breeze memda Nungwi Zanzibar au Mafia Island, utapata samali safi plus supu ya pweza!!
 
Mkuu nenda kijijini kwako ukaonane na uliosoma nao primary school
hakuna mtanzania anayeweza kwenda kutembea mbali
mambo yetu sio mazuri
 
Wakuu natarajia kupata Likizo August Hii inayokuja.
Na-plan kwenda mbali na Dar kupumzika kidogo angalau kwa two weeks or more....
Munaweza kunisaidia miji na sehemu nzuri kwa mapumziko marefu kama hayo? Sina tatizo ku-relocate.....
Kuhusu gharama nadhani ziwe za kawaida sio za kifisadi!


Nenda Tarime ni kuzuri sana kwa mapunziko,
 
Mkuu nenda kijijini kwako ukaonane na uliosoma nao primary schoolhakuna mtanzania anayeweza kwenda kutembea mbali mambo yetu sio mazuri
Mkuu nenda Bukoba mjini hutajuta,kwanza ni mkoa wenye hali ya hewa safi sijawahi ona,pili mkoa wa kagera ndio mkoa uliopakana na nchi nyingi kwa ukaribu kuliko mkoa wowote Afrika! Utapata fursa za kutembelea kwa urahisi uganda,rwanda na burundi na hata ukifika mipakani tu kama pale mtukula utaenjoy sana,ukifika bk kuna hoteli nyingi nzuri kama walk guard,Victorious na kuna apartment hoteli mpya jina limenitoka.utaona mazingira asili hasa upandaji wa miti mingi sana hadi utashangaa ndio mvua kule hazina msimu! Ila kila jioni hakikisha unaenda kupata kuku wa kienyeji wa kuchoma safi dunia nzima pale bukoba club huku ukipata view nzuri ya ziwa na upepo wa ukweli.lakini ulizia pia baa moja inaitwa Yasila pale omba samaki sato alietoka kuvuliwa dk 2 zilizopita ushuhudie akiwa mzima kabisa alafu wakuchomee! Kumbuka kule hakuna mgao wa umeme na kwa vile utakuwa single utapata ukarimu wa kushangaza wa wanadada warembo wa kihaya,kiganda na wakinyarwanda na pengine kama hujaoa lazima utangaze nia! Kazi kwako kiongozi
 
Mkuu nenda Bukoba mjini hutajuta,kwanza ni mkoa wenye hali ya hewa safi sijawahi ona,pili mkoa wa kagera ndio mkoa uliopakana na nchi nyingi kwa ukaribu kuliko mkoa wowote Afrika! Utapata fursa za kutembelea kwa urahisi uganda,rwanda na burundi na hata ukifika mipakani tu kama pale mtukula utaenjoy sana,ukifika bk kuna hoteli nyingi nzuri kama walk guard,Victorious na kuna apartment hoteli mpya jina limenitoka.utaona mazingira asili hasa upandaji wa miti mingi sana hadi utashangaa ndio mvua kule hazina msimu! Ila kila jioni hakikisha unaenda kupata kuku wa kienyeji wa kuchoma safi dunia nzima pale bukoba club huku ukipata view nzuri ya ziwa na upepo wa ukweli.lakini ulizia pia baa moja inaitwa Yasila pale omba samaki sato alietoka kuvuliwa dk 2 zilizopita ushuhudie akiwa mzima kabisa alafu wakuchomee! Kumbuka kule hakuna mgao wa umeme na kwa vile utakuwa single utapata ukarimu wa kushangaza wa wanadada warembo wa kihaya,kiganda na wakinyarwanda na pengine kama hujaoa lazima utangaze nia! Kazi kwako kiongozi


mkuu hao samaki sato hawani mionzi ya nyuklia??tumesikia wajapani wamezileta bongo
 
mkuu hao samaki sato hawani mionzi ya nyuklia??tumesikia wajapani wamezileta bongo
Shaka ondoa ndugu,kila utachokula bukoba ni asilia haswaa hata nyama ya ngombe ni wale walioshiba na pembe ndefu! Kule malisho yamejaa maana mvua hazina msimu kule.watu wengi hawajafahamu uzuri wa mji wa bukoba mpaka ufike na upate muda wa kuzunguka.nenda bk then utarudi na mtizamo mpya juu ya mambo mengi ikiwemo mazingira na kilimo!
 
kama wataka mapumziko kwa utulivu, wahitaji kukaa ufukweni! Option nzuri, panda ndege hadi kisiwa cha mafia, kuna aidha coastal aviation, ambayo inafanya safari kila siku saa sita na saa tisa, au tropical air saa tano kila siku, fare yao ni shiling laki moja one way! Mafia waweza kufikia butiama lodge, kama dola 100, Utende beach house, dola 20 single, mafia lodge, dola 80 single. Mafia waweza pata utulivu wa hali ya juu, security ya hali ya juu, bahari nzuri ambayo haijachafuliwa, sea foods kama, crabs, squid, fish etc.
 
Wakuu natarajia kupata Likizo August Hii inayokuja.
Na-plan kwenda mbali na Dar kupumzika kidogo angalau kwa two weeks or more....
Munaweza kunisaidia miji na sehemu nzuri kwa mapumziko marefu kama hayo? Sina tatizo ku-relocate.....
Kuhusu gharama nadhani ziwe za kawaida sio za kifisadi!
Watu wa porini bwana. Mnashindwa kujenga kwenu, na inapofika likiso maogopa kwenda. Ndio maana nimeapa mtoto wangu kamwe asiolewe na kyasaka....
 
Nenda Lushoto mkuu, utainjoy view za ukweli na hali ya kibaridi, ukarimu wa wasambaa na kama ni mkali wa gati/hedaru.
Basi we baridi itakuwa ndoto, yah ni sehemu bora sana esp. Njia ya Mlalo na place za mtae, nauli si kubwa sana, utaenjoy nyama maziwa, matunda, viazi na vngnevyo.
Japo tenga fedha kwa ajili ya familia ulioiacha.
 
tutazijua sehemu nyingi na kujifunza mengi maeneo tofauti ya tanzania kupitia thread hii,sio kuishia dar tu,weekdays ful kazi,weekends Calabash,fairway n.k!
 
Nenda Samunge loliondo pako poa ile mbaya
 
Wakuu natarajia kupata Likizo August Hii inayokuja.Na-plan kwenda mbali na Dar kupumzika kidogo angalau kwa two weeks or more....Munaweza kunisaidia miji na sehemu nzuri kwa mapumziko marefu kama hayo? Sina tatizo ku-relocate.....Kuhusu gharama nadhani ziwe za kawaida sio za kifisadi!
acha Wenge nchi inaelekea kubaya we unawaza kupumzikaa!fanya kazi
 
Bahasha la Jairo naona limeanza kukulevya, kumbe hata usafiri wako binafsi huna halafu unawaza vacation? kweli mswahili ngozi ya makalio.
Utakuwa umeupatia ukubwani na mkopo hujamaliza ndo maana unaona kama ndiyo raha ya maisha kuliko kutalii!!!!
Samahani kama nimekukwaza naongelea hapo red!!
 
Utakuwa umeupatia ukubwani na mkopo hujamaliza ndo maana unaona kama ndiyo raha ya maisha kuliko kutalii!!!!
Samahani kama nimekukwaza naongelea hapo red!!
Umesema vyema mkuu.... Hii ni mentality potofu sana imejengeka juu ya baadhi ya wa TZ, wenzetu hufanya kazi double shifts ili ku-save pesa ya kwenda vacation! Mimi nilikua nazungumzia sana sana change of environment tu. Kwani kwenda Mbeya ukapanga Guest ya elfu hamsini mpaka laki kwa wiki moja sioni kama ni big deal! Normally watu wana spend zaidi ya hiyo kwenye lager na upuuzi mwingine!
 
kuna sehemu nzuri sana nadhani Malaysia, nilimuona Vasco dagama akibembea akiwa na bibi yake, hebu mpigie muulize ni sehemu gani, nadhani patakufaa, kama la, mwambie akusaidie yeye anafahamu sehemu nyingi sana za starehe duniani, unaweza muuliza SA maana alikwenda huko na mdogo wake kwenye mwezi asali baada ya ndoa
 
Utakuwa umeupatia ukubwani na mkopo hujamaliza ndo maana unaona kama ndiyo raha ya maisha kuliko kutalii!!!!
Samahani kama nimekukwaza naongelea hapo red!!
Point za kipuuzi kabisa hizi, tena ni za kutoka kwa mtoto wa Mama, usipopatia ukubwani utotoni utawezaje kupata kitu chako? au wewe gari la urithi la Baba unaliita my car? na hiyo nyumba unayoishi ambayo kodi ya nyumba ni shikamoo unaiita my house?
Mitoto kama hii ndio inadhani hili ni jukwaa la watu wanaoishi maisha ya kula kulala.
 
Back
Top Bottom