Migogoro ya makanisani kujaa mitandaoni au nje ya kanisa hakuna mashiko, ni tabia ya hovyo

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,597
46,206
Kumekuwepo na mazoea au utamaduni wa muda mrefu wa waumini kuleta malalamiko hapa jukwaani kuhusiana na migogoro mbalimbali ambayo imakeuwa ikitokea hasa katika makanisa ya KKKT, Anglican na TAG.
Malalamiko haya sio hapa jukwaani tu bali hata katika mitandao mingine ya kijamii.

Malalamiko au migogoro hiyo mara nyingi huelezewa kuhusunia na kugombania vyeo, matumizi fedha na rasilimali nyingine, maadili na mambo yanayohusiana na siasa.

Kuleta migogoro ya makanisa mitandaoni au sehemu nyingine nje ya kanisa ni ujinga, ujuha na uwezo duni wa kufikiri. Kama kanisa ulilopo lina migogoro kwa nini msimalize wenyewe huko ndani ya kanisa washiriki na viongozi wenu husika ? Kama imeshindikana kabisa kufikia muafaka kwa nini msiachane na hilo kanisa mkaenda madhehebu mengine, kama hilo nalo ni gumu pia kwa nini msianzishe kanisa lenu wenyewe?

Tanzania ina uhuru mkubwa wa kiimani, mtu unaweza kuhamia dhehebu lingine au dini nyingine kabisa wakati wowote bila kikwazo. Pia Tanzania ni sehemu rahisi sana kuanzisha kanisa lako tofauti na nchi kama Rwanda, kama mnaona mnashindwana na wenzenu anzisheni kanisa lenu msiparuane na kulazimisha upande wenu mnaoona ni sahihi kwenu.
 
Unataka nini kiletwe mitandaoni?

Unatofautisha binadamu wa mitandaoni na binadamu wa mitaani?

Mitandao ni mitandao tu mkuu, kinachotokea kwa jamii lazima kiwe reflected kwenye mitandao kwa hali ya sasa.

Kama hivyo ndivyo ma wanasiasa watasema kuleta mambo ya siasa kwenye mitandao ni ushamba inatakiwa yamalizwe ndani ya vyama husika
 
Mambo ya vyama siasa kuwekwa mtandaoni ni sawa kwa sababu itasaidia watu kupiga kura wakati wa uchaguzi, waweze kuchagua chama bora zaidi ya kingine, Kufahamu mambo ya migogoro ya kanisani au msikitini inawasaidiaje raia walio wengi?
Unataka nini kiletwe mitandaoni?

Unatofautisha binadamu wa mitandaoni na binadamu wa mitaani?

Mitandao ni mitandao tu mkuu, kinachotokea kwa jamii lazima kiwe reflected kwenye mitandao kwa hali ya sasa.

Kama hivyo ndivyo ma wanasiasa watasema kuleta mambo ya siasa kwenye mitandao ni ushamba inatakiwa yamalizwe ndani ya vyama husika
 
ITAMBUE DINI YA KWELI
1. upendo miongoni mwao, (viongozi na waumini)
2. Dini ya kweli haiungi mkono siasa... (iepuke kuruhusu kuwa wanachama wa chama fulani cha kisiasa)
3. Dini isiunge mkono vita. ( wazia UKRAINE vs RUSSIA). Kiongoz wa dini X Anaongoza ibada ukraine kuombea jesh lao likashinde. Dini X Pia ipo urusi, nayo inaombea jesh lake. Mungu ni mmoja? Atajibu sala ipi?
4. Dini ifundishe, ionye, na ikaripie kwa kutumia BIBLIA, Sio falsafa zao binadam...
JE? UPO DINI YA KWELI?
visit, www.jw.org/sw
 
Kumekuwepo na mazoea au utamaduni wa muda mrefu wa waumini kuleta malalamiko hapa jukwaani kuhusiana na migogoro mbalimbali ambayo imakeuwa ikitokea hasa katika makanisa ya KKKT, Anglican na TAG.
Malalamiko haya sio hapa jukwaani tu bali hata katika mitandao mingine ya kijamii.

Malalamiko au migogoro hiyo mara nyingi huelezewa kuhusunia na kugombania vyeo, matumizi fedha na rasilimali nyingine, maadili na mambo yanayohusiana na siasa.

Kuleta migogoro ya makanisa mitandaoni au sehemu nyingine nje ya kanisa ni ujinga, ujuha na uwezo duni wa kufikiri. Kama kanisa ulilopo lina migogoro kwa nini msimalize wenyewe huko ndani ya kanisa washiriki na viongozi wenu husika ? Kama imeshindikana kabisa kufikia muafaka kwa nini msiachane na hilo kanisa mkaenda madhehebu mengine, kama hilo nalo ni gumu pia kwa nini msianzishe kanisa lenu wenyewe?

Tanzania ina uhuru mkubwa wa kiimani, mtu unaweza kuhamia dhehebu lingine au dini nyingine kabisa wakati wowote bila kikwazo. Pia Tanzania ni sehemu rahisi sana kuanzisha kanisa lako tofauti na nchi kama Rwanda, kama mnaona mnashindwana na wenzenu anzisheni kanisa lenu msiparuane na kulazimisha upande wenu mnaoona ni sahihi kwenu.
Ssa unataka taarifa tupataje unadhami jamii forum ninsehemu za kuleta nyuz za kula tunda kimasiara .tuache kujuwa yanaoendelea ktka maeneo menginre
 
Wengi hukimbilia huku ili kutafuta uungwaji mkono, wanataka kuaminisha watu sababu wanazoleta wao ndio za kweli kuwahusu hao wanaowasema.

Matokeo yake hiyo migogoro yao ikifika huku hugeuka siasa, wanaanza kuvutana na kuleta kero kwa wengine wasio husika na imani zao, au makanisa yao wanayosali.

Hii tabia ya kipuuzi imezidi kuota mizizi miaka ya karibuni baada ya hali ya maisha kuzidi kuwa ngumu.

Wengi wao hugombania kubaki madarakani ili waendelee kula sadaka, na wale wengine wanaokimbilia mitandaoni kuleta lawama nao kimsingi njaa zinakuwa zimewazidi hivyo huona muda wao wa kuanza kula sadaka umefika pia.

Hawa huja na mbinu nyingi; wanaweza kuzusha kiongozi fulani ana tabia mbaya [anachezea wake zao], mara anakula pesa za waumini, na sababu nyingine nyingi ilimradi wapate uhalali wa kuingia ulingoni wakabidhiwe mfuko wa sadaka wanenepe.
 
Ssa unataka taarifa tupataje unadhami jamii forum ninsehemu za kuleta nyuz za kula tunda kimasiara .tuache kujuwa yanaoendelea ktka maeneo menginre
Taarifa za ndani za KKKT dayosisi ya Meru au Karagwe zinakuhusu nini wewe Mkatoliki uliyepo Parokia ya Namtumbo au Mlutheri aliyeko Lindi?
 
Mwanzo wa binadamu kuwepo duniani.

Basi kumbe huna unalojua.

Kwa ufupi tu siasa imekuwako tangu mwanzo wa maisha, hiyo mifumo ya utawala sijui wafalme ni siasa yenyewe…. au kwako siasa ni vyama vingi?
 
Wanaleta migogoro mitandaoni kwa sababu huko makanisani wanabanwa kutoa maoni yao.
 
Basi kumbe huna unalojua.

Kwa ufupi tu siasa imekuwako tangu mwanzo wa maisha, hiyo mifumo ya utawala sijui wafalme ni siasa yenyewe…. au kwako siasa ni vyama vingi?
Hata kabla ya kuwepo mfumo wowote wa utawala, wafalme, mafarao n.k dini ilikuewepo.

Dini ilikuwepo hata kabla binadamu hawajawa na utaratibu wa kukaa pamoja kama jamii ndogo inayoshirikiana.
 
Back
Top Bottom