Mifumo Haina ushirikiano

Mifumo Haina ushirikiano

Mtu una vielelezo hivi
1. Cheti Cha kuzaliwa
2.Cheti Cha shule ya msingi
3.Cheti Cha secondary
4. Cheti Cha ufundi veta.
5.TIN number
6.Reseni ya Biashara
7.Kitambulisho Cha NIDA
8.Passport ya Tanzania

• Sasa mtu ukienda kupata Huduma ktk Hofisi za watawala wanakuambia kalete Barua ya Utambulisho wa wa Serikali ya mtaa/ Utambulisho wa mtendaji.
• Hawana uwakika kama ni mtanzania, Mifumo Haisomani na Wala Hawaziamini Documents zao.

• Kwa mtazamo wangu Hawa Hata kitambulisho chao Cha Taifa wakiamini wakati kina Taarifa zote za mtu, pia kuna ku update Taarifa za mtu. Yaani Mambo mengi Wanafanya kama tunaishi Karne 15
Hawakiamini kitambulisho chao Cha Taifa.
Hii nchi ukweli usemwe tu tunaishi kianalog mno na mbaya zaidi hatutaki kubadilika kuishi kidigitali na kujifunza hatutaki
 
Tatizo linaanzia kwa wazee wafanya maamuzi ya kisera waliojazana Serikalini hata baada ya kustaafu.
Mbinu za miaka ya 70 ndizo zinazotumika katika karne ya 21 huku vijana wanaopaswa kuendesha nchi kisasa wakiwa nje ya mfumo licha ya kusoma na kuhitimu....
Mmesoma na kuhitimu lakini ofisi mnaita hofisi?! Stupid.

Kama kiswahili kwenu shida, vipi lugha za kigeni na usomi wenu uchwara huo!
 
Mfumo wa Postal codes ukifanikiwa kikamilifu, serikali za mitaa inakufa kifo cha mende
 
Hii nchi ukweli usemwe tu tunaishi kianalog mno na mbaya zaidi hatutaki kubadilika kuishi kidigitali na kujifunza hatutaki
CCM+ taasisi zenu za kidini zinataka mambo ya Nyerere yabaki kama Yalivyo.

Watu waishi kama wapo zizini
 
Lakini nape kwenye lile zoezi la kuweka post codes, alimkwamisha Samia ,makusudi. Kijana wa hovyo sana
 
Usingalie Dosari, ndogo Tembea Uwone Nchi zingine mifumo inavyosomana,
Yaani Chumba tu ulichofikia Documents zinasomana umefika lini na unatakiwa kuondoka lini yaani sisi Watanzania tunaishi kama wanyama.
Uwone? Ni halali kudai hizo barua
 
upo mfumo unaitwa napa ambao unapata barua ya utambulisho kutoka kwa mtendaji wa kata online
Ni kama nimemwelewa hivi...hupati kitambulisho cha Taifa kama huna barua ya mtendaji, sasa ukiwa tayari unacho kitambulisho au namba ya NIDA barua ya mtendaji ya utambulisho ni ya nini tena? Nadhani ndiyo lengo lake mifumo kutosomana
 
Ukifatilia nida kwa sasa unaambiwa leta cheti cha kuzaliwa, ukienda kwenye cheti cha kuzaliwa unaambiwa leta nida, unashindwa uanzie wapi.
 
Aliyekwamishwa kashindwa kujua kuwa alikwamishwa ili arekebishe alipokwamishwa?
Haha mkuu Kuna mambo ukiyajua utaogopa sana, Kuna wana siasa wanamiliki mitandao ya kihuni

Hawatakii mifumo isomane, iwe structural organized.
 
Hii nchi ukweli usemwe tu tunaishi kianalog mno na mbaya zaidi hatutaki kubadilika kuishi kidigitali na kujifunza hatutaki
Kwa style ya utendaji wetu, maelekezo na ubunifu wote huanzia juu kuja chini. Kama kiongozi wa juu hajui nchi ielekee wapi ni vigumu sana watu wa chini kuilekeza sehemu sahihi...watz tumezoeshwa kuambiwa fanya hiki, kile na viongozi...sijui umenielewa...
 
Ni kama nimemwelewa hivi...hupati kitambulisho cha Taifa kama huna barua ya mtendaji, sasa ukiwa tayari unacho kitambulisho au namba ya NIDA barua ya mtendaji ya utambulisho ni ya nini tena? Nadhani ndiyo lengo lake mifumo kutosomana
Kujua makazi yako au unapopatikana kwa wakati huo, na anae omba ni wewe kwa uthibitisho toka kwa mtendaji au mwenyekiti wa kijiji

Kwa kuwa ina aminika Hawa viongozi huko chini ndio wanaweza thibitisha ukaazi wako eneo hilo kwa muda fulani na namba ya nyumba, mtaa

Labda huko mbele kama taarifa zikiwa Sawa sawa ndipo tunaweza kuhama taratibu

Vilevile ikumbukwe Kuna wazee wetu ambao hawana vifaa vya kidigitali kuweza kutumia ili kusaidia maswala yao ya kila siku

Mifano midogo, huduma za stationery hazijaenea, gharama ni kubwa pia.

Kuna huduma za jihudumie lakini sio wengi wanaweza kuzitumia, kijana wa kidato cha Sita hawezi kuomba cheti cha kuzaliwa au kifo, mkopo, barua ya utambulisho

Msafiri hawezi omba passport, visa application online, booking ya ndege, hotel au accommodation

Mfanyabiashara hawezi kuomba TIN online, leseni ya biashara

Mfanyakazi hawezi kuomba bima ya afya mtandaoni, kujaza majukumu yake nk

Yapo mengi, muhimu yanafanyiwa kazi taratibu
 
Niajabu mtu anaambiwa aweke cheti cha kuzaliwa, NIDA, na vingine viingiii.

Wakati NIDA peke yake ina kila taarifa, kuanzia cheti cha kuzaliwa hadi taarifa za mtaa unao ishi.

Mtoa mada uko sahihi, mifumo inatakiwa isomane kupunguza usumbufu.

Nadhani NIDA ndio ibaki kuwa hitaji kuu katika kupata baadhi ya huduma kama kupata passport, Leseni na mengine kama hayo.
 
Mmesoma na kuhitimu lakini ofisi mnaita hofisi?! Stupid.

Kama kiswahili kwenu shida, vipi lugha za kigeni na usomi wenu uchwara huo!
Najaribu kuangalia tena mahali nilipoita hofisi kwenye bandiko langu sioni..... 😳 🤔
 
Back
Top Bottom