Mwasita Moja
JF-Expert Member
- Dec 31, 2015
- 2,903
- 2,580
Ilishatabiliwa tokea mwanzo kuwa kwa Magufuli kila goti litapigwa
Watoto wa wajomba ni wengi lazima tugawane keki ya nchi. Hujiulizi kwa nini TTCL haiwezi kushindana? angalia waajiriwa wake.Kagera Sugar au Mtibwa wanazalisha tani ngapi na wameajiri wafanyakazi wangapi?
Nilisoma sehemu (stand to be corrected) kuwa MeTL ndio mwajiri mkubwa na ameajiri wafanyakazi wasiozidi 30,000 kwenye kampuni zake zote. Sasa hawa jamaa wataajiri vipi watu 100,000 (laki moja)!?
Mkuu leo nimesikia kwenye magazeti wakisema serikali imerejesha fedha ilizokopa kwenye mifuko ya jamii kiasi cha bilioni 700+ japo haijamaliza zote ina maana wemerejesha na kuchukua tena wakajengee viwanda??serikali inaandaa mazingira mazuri kwa wawekezaji mara inataka kujenga yenyewe??au wanataka kujikumbusha Enzi hizoo serikali ilimiliki viwanda vikafa vyote kifo cha mende.???Hizi pesa zetu hatujapeleka zijenge viwanda ni akiba yetu na mambo ya kuzitumia kujenga viwanda si sahihi hata kidogo nafuu wamkopeshe Mengi na Manji ndio wajenge viwanda.
Na mkoa wa katavi?Ni specialization. Kila mkoa unatakiwa ku specialize kwenye eneo moja au mbili tu. Kwa mfano mikoa ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga na Geita wata specialize kwenye viwanda vya bidhaa zitokanazo na pamba na ng'ombe. Tabora tumbaku, Kigoma mawese, Kagera bitoke & kahawa, Pwani magari & trekta nk nk. Kila mkoa na wilaya zitakuwa na viwanda vya aina yake. Nchi ya viwanda ifikapo 2025.
wanaongozwa na wanasiasa badala ya kufanya tathmini ya kina
kweli kabisa....serikali ingebaki kama regulator,wawaachie akina bakhresaKWA SABABU NDIO WANAO WAAJIRI.
Hivyo viwanda vitaishia kununuliwa na akina Manji kwa bei za kutupa kabisa
Mifuko ya hifadhi ya jamii imeanza mikakati ya kujenga viwanda ambapo kiwanda cha sukari kitajengwa Morogoro chenye uwezo wa kuzalisha tani 200,000 kwa mwaka na kuajiri watu 100,000.
Pia kuna viwanda vya kutengeneza mafuta ya alizeti na usindikaji wa nafaka mahindi ambavyo vitajengwa Dodoma na Iringa
Dodoma ni center ya alizeti saiv kati ya singida na manyara.maana mkoa wa manyara hasa kiteto wamekuwa wakulima wazuri kuzid wa singida kiasi cha alizet kuuzwa bei chini zaidi na pia watu wa singida wamekuwa wakienda kibaigwa kununua alizeti kipeleka singida kwa wingiIki cha Alzeti kwann kisijengwe Singda?
Kuzaliasha ajira laki moja inamaanisha watakaojairiwa kiwandani na wale waliopo kwenye mnyororo wa thamani ya uzalishaji sukari ambao hawapo likked na kiwanda moja kwa mojaKagera Sugar au Mtibwa wanazalisha tani ngapi na wameajiri wafanyakazi wangapi?
Nilisoma sehemu (stand to be corrected) kuwa MeTL ndio mwajiri mkubwa na ameajiri wafanyakazi wasiozidi 30,000 kwenye kampuni zake zote. Sasa hawa jamaa wataajiri vipi watu 100,000 (laki moja)!?
Iki cha Alzeti kwann kisijengwe Singda?
Singida si eneo pekee ipatikanapo alizeti.Iki cha Alzeti kwann kisijengwe Singda?
Well, basi tunaweza kusema 95% ya watanzania wameajiriwa kwa sababu kila mmoja anaingiza kipato japo kinakuwa sio direct kutoka kwa mwajiri, Ndivyo unataka kusema mkuu!?Kuzaliasha ajira laki moja inamaanisha watakaojairiwa kiwandani na wale waliopo kwenye mnyororo wa thamani ya uzalishaji sukari ambao hawapo likked na kiwanda moja kwa moja
Kwanini Singida mkuu,mimi naona kujenga Dodoma inakuwa vizuri kwani ni kati kwa kati.Iki cha Alzeti kwann kisijengwe Singda?
Kiwanda Kitazalisha tani 200000 kwa hili sawa ila kwa hili la kitaajil watu 100000? Mungu nipe uzima mpka nione haya maajabu.
Naona unaanza kupepelea nyumbani mkuuIki cha Alzeti kwann kisijengwe Singda?