Mifuko ya hifadhi ya jamii yaanza kujenga viwanda

Mifuko ya hifadhi ya jamii yaanza kujenga viwanda

Mkulukindo, post: 18150231, member: 22409"]Kagera Sugar au Mtibwa wanazalisha tani ngapi na wameajiri wafanyakazi wangapi?
Nilisoma sehemu (stand to be corrected) kuwa MeTL ndio mwajiri mkubwa na ameajiri wafanyakazi
wasiozidi 30,000 kwenye kampuni zake zote. Sasa hawa jamaa wataajiri vipi
watu 100,000 (laki moja)!?


Ni propaganda za Lumumba
Mkuu propa
 
Hizi pesa zetu hatujapeleka zijenge viwanda ni akiba yetu na mambo ya kuzitumia kujenga viwanda si sahihi hata kidogo nafuu wamkopeshe Mengi na Manji ndio wajenge viwanda.
 
Viwanda nchi hii vyote kanda moja, why?? hamuoni kuwa mnawanyima fursa wananchi wa maeneo mengine ya nchi???.

Kuna mengi ya kuangalia Kujenga viwanda

1.Ukaribu na soko kubwa la wateja.Wateja wakubwa wakiwa Dar es salaam mfano wanaotumia asilimia 90 Ya bidhaa yako ni busara kujenga kiwanda karibu na wateja wakubwa.Mfano mikoani si wanunuzi wakubwa wa unga na mchele kwani wao hula vyakula vyao wanavyolima!!! Walaji wakubwa wako Dar es salaam.Mjenzi wa kiwanda huangalia vitu kama ukaribu na wateja wakubwa.Mjenzi wa kiwanda Hajengi kiwanda kwa ajili ya kumfurahisha mbunge!!

2.Ukaribu na njia nyingi za usambazaji za uhakika za bei nafuu kusambazia wateja (Channels of distribution) Kuna mikoa ina bandari,reli,barabara na viwanja vya ndege.Viwanda vinazalisha sana wanaweza kuwa na masoko nje ya nchi hivyo hujitahidi kuweka kiwanda mahali iwe rahisi kwake kusafirisha nje ya nchi pia.

Yako mengi viwanda havijengwi holela
 
Hahahaha hakuna kiwanda cha kuajiri watu laki moja serikali I ache propaganda unless iwe forced labor concentration camp au Auschwitz au sabibo
 
Kuna mengi ya kuangalia Kujenga viwanda

1.Ukaribu na soko kubwa la wateja.Wateja wakubwa wakiwa Dar es salaam mfano wanaotumia asilimia 90 Ya bidhaa yako ni busara kujenga kiwanda karibu na wateja wakubwa.Mfano mikoani si wanunuzi wakubwa wa unga na mchele kwani wao hula vyakula vyao wanavyolima!!! Walaji wakubwa wako Dar es salaam.Mjenzi wa kiwanda huangalia vitu kama ukaribu na wateja wakubwa.Mjenzi wa kiwanda Hajengi kiwanda kwa ajili ya kumfurahisha mbunge!!

2.Ukaribu na njia nyingi za usambazaji za uhakika za bei nafuu kusambazia wateja (Channels of distribution) Kuna mikoa ina bandari,reli,barabara na viwanja vya ndege.Viwanda vinazalisha sana wanaweza kuwa na masoko nje ya nchi hivyo hujitahidi kuweka kiwanda mahali iwe rahisi kwake kusafirisha nje ya nchi pia.

Yako mengi viwanda havijengwi holela
hayo ulioandika hapo juu sawa, lakini si kwa kiwanda kama cha Alizeti mkuu! Singida imeunganishwa na mikoa yote kwa barabara za lami, utashindwaje kusafirisha mafuta ya alizeti. hata sasa kuna kiwanda cha Alizeti inyosafirishwa mpaka mwanza. Sukari ingefaa kiwanda kikae sehemu nyingine ili kurahisisha na kuwawekea wananchi urahisi wa kupata sukari badala ya kuendelea kurundika kila kitu mahala pamoja na kisha mtu wa Singida akanunua Sukari sh 6000 kwa kilo.
 
Kwa nini viwanda vya sukari vingi ni Morogoro tu? jamani sehemu nyingi miwa inapatikana sasahivi.
Ni specialization. Kila mkoa unatakiwa ku specialize kwenye eneo moja au mbili tu. Kwa mfano mikoa ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga na Geita wata specialize kwenye viwanda vya bidhaa zitokanazo na pamba na ng'ombe. Tabora tumbaku, Kigoma mawese, Kagera bitoke & kahawa, Pwani magari & trekta nk nk. Kila mkoa na wilaya zitakuwa na viwanda vya aina yake. Nchi ya viwanda ifikapo 2025.
 
hayo ulioandika hapo juu sawa, lakini si kwa kiwanda kama cha Alizeti mkuu! Singida imeunganishwa na mikoa yote kwa barabara za lami, utashindwaje kusafirisha mafuta ya alizeti.

Wateja wakubwa sana wa mafuta ya alizeti watakuwa Dodoma sio Singida baada ya serikali kuhamia Dodoma .Hivyo ni sawa kukiweka kiwanda cha mafuta ya alizeti Dodoma kwani miundo mbinu mingi ya umeme,maji,masoko,barabara itakuwa mizuri mno na rahisi kuwasambazia wateja waliozagaa kila kona ya jiji.Ukiweka singida inakuwa sehemu tu ya kuzalishia soko hamna na hata likiwepo ni dogo mno pia sina uhakika kama alizeti za Singida pekee zaweza himili kulisha hicho kiwanda.Zitahitajika alizeti kutoka mikoa mingine pia inayolima alizeti kama Iringa,dodoma,morogoro kupeleka Alizeti kwenye hicho kiwanda.Kikiwa Dodoma KITAFAIDISHA wakulima wa mikoa hiyo pia kuliko kikiwa Singida ni pembezoni mno.Yaani Alizeti itoke Iringa ,ipitie Dodoma iende singida kutengenezwa mafuta halafu mafuta yarudi Dodoma kuuzwa!! Hiyo itakuwa biashara kichaa
 
Unajengaje kiwanda cha alizeti Dom hali ya kua 70% ya alizeti unanunua singida? Hicho kiwanda hakitaweza kushindana na viwanda vidogo vilivyopo singida.Lazima mafuta yao yatakua bei ghali zaidi kuliko ya sgd.Kama mahitaji ya kiwanda hicho singida ndiyo yenye kila kitu.Maji,umeme,usafiri,soko kuzunguka maeneo yote ya nje na malighafi yenyewe.
 
Unajengaje kiwanda cha alizeti Dom hali ya kua 70% ya alizeti unanunua singida? Hicho kiwanda hakitaweza kushindana na viwanda vidogo vilivyopo singida.Lazima mafuta yao yatakua bei ghali zaidi kuliko ya sgd.Kama mahitaji ya kiwanda hicho singida ndiyo yenye kila kitu.Maji,umeme,usafiri,soko kuzunguka maeneo yote ya nje na malighafi yenyewe.

Nafikiri huna takwimu sahihi za kilimo cha alizeti.Kuna mikoa

Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na Rukwa.Hicho kiwanda kuwekwa Dodoma kitafungua chumi zilizofungwa zinazolima alizeti za mikoa hiyo mingine ili alizeti zao ziweze kufikishwa kiwandani ambapo hapo kiwandani kilipo ndipo litakuwa soko kuu la mafuta ya alizeti ambalo litakuwepo baada ya serikali kuhamia Dodoma.

Angalia ramani mikoa yote inayozunguka Dodoma ni mkulima wa Alizeti ikiwemo Dodoma yenyewe.Hivyo kiwanda kuwepo Dodoma ni sehemu sahihi kwa uzalishaji na soko pia

EDICT-2008-625-image001.jpg
 
Unajengaje kiwanda cha alizeti Dom hali ya kua 70% ya alizeti unanunua singida? Hicho kiwanda hakitaweza kushindana na viwanda vidogo vilivyopo singida.Lazima mafuta yao yatakua bei ghali zaidi kuliko ya sgd.Kama mahitaji ya kiwanda hicho singida ndiyo yenye kila kitu.Maji,umeme,usafiri,soko kuzunguka maeneo yote ya nje na malighafi yenyewe.
Bora umenisaidia kumjibu huyu Mkubwa anayedhani singida ni pembeni mno kuliko Hio Iringa.?? Watanzania mna tabia mbaya ya kudhani kila kitu kiamliwa kwa siasa.

Hamuoni hata siment tu inavyoumiza mikoa mingine kwa kuwa viwanda vyote viko ukanda mmoja. sement singida inauzwa mpaka 20,000 kwa sababu ya usafirishaji, bado tunataka kuendeleza hayo hayo! Viwanda vikijengwa angalau kwa spread ya kikanda inakuwa nafuu kwa mikoa yote nchi hii!
 
Yaan wanajenga viwanda ilihali hawana pesa za kuwalipa wastaafu tangu mwezi may?, Mungu shuka Tanzania,nchi imekwisha
 
Ni specialization. Kila mkoa unatakiwa ku specialize kwenye eneo moja au mbili tu. Kwa mfano mikoa ya Mwanza, Simiyu, Shinyanga na Geita wata specialize kwenye viwanda vya bidhaa zitokanazo na pamba na ng'ombe. Tabora tumbaku, Kigoma mawese, Kagera bitoke & kahawa, Pwani magari & trekta nk nk. Kila mkoa na wilaya zitakuwa na viwanda vya aina yake. Nchi ya viwanda ifikapo 2025.
Ok kumbe viwanda bado mpaka 2025, mi nilidhani tayari?? Basi ngoja nipate pumzi! Siasa zinatuumiza!
 
Viwanda vya serikali vitamudu ushindani kweli?Angalia TBC wanavyozidiwa mbinu na station ndogo kama clouds!sasa huko kwa kina metl na bakhrrsa tutaweza kweli?
 
Wachumi watusaidie kila mmoja atazalisha tani mbili kwa mwaka
 
Mifuko ya hifadhi ya jamii imeanza mikakati ya kujenga viwanda ambapo kiwanda cha sukari kitajengwa Morogoro chenye uwezo wa kuzalisha tani 200,000 kwa mwaka na kuajiri watu 100,000
Pia kuna viwanda vya kutengeneza mafuta ya alizeti na usindikaji wa nafaka mahindi ambavyo vitajengwa Dodoma na Iringa


upuuzi mwingine wa awamu ya tano. wamefeli kabla ya kuanza, wanamdhani kuanzisha viwanda ni sawa na kuzuia maandamano ya UKUTA
 
Kagera Sugar au Mtibwa wanazalisha tani ngapi na wameajiri wafanyakazi wangapi?
Nilisoma sehemu (stand to be corrected) kuwa MeTL ndio mwajiri mkubwa na ameajiri wafanyakazi wasiozidi 30,000 kwenye kampuni zake zote. Sasa hawa jamaa wataajiri vipi watu 100,000 (laki moja)!?
Uko sahii mkuu,kile cha kilombero K1 na K2 ukichukua permanent,temporaly na seasonal hata elfu 7 hawaipati ije ikawa hiyo 100,000.!!??
 
Uko sahii mkuu,kile cha kilombero K1 na K2 ukichukua permanent,temporaly na seasonal hata elfu 7 hawaipati ije ikawa hiyo 100,000.!!??
Hapa mkuu ndio nakuwa na mashaka makubwa kwa Watanzania. Kama waziri wa utalii kasema sisi ni wezi huwezi jua hata mimi na wewe huenda tukawa miongoni mwa hao. Lakini pia huwezi jua ule utafiti wa mtu mmoja kati ya wanne unamhusu nani mpaka aliyetoa hizi data na ahadi usimuhusu!
 
Back
Top Bottom