Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 112

Akaingia ndani ya gari hilo, alikuwa na kibegi chake kidogo kilichokuwa na pesa nyingi ambazo alizipata katika kazi yake kubwa aliyokuwa ameifanya kwa kipindi kirefu, kutembea na mabilionea wengi.

Kutoka hapo mpaka Fayad ilikuwa ni zaidi ya kilometa mia moja, hilo halikuwa tatizo, kwa kuwa barabara ilikuwa nzuri, hawakuona kama wangetumia muda mwingi mpaka kufika huko.

Garini, walikuwa wakizungumza kirafiki na Fareed alijitambulisha kama Hamad Al Hamad ambaye alitokea nchini Nigeria na kufika hapo kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Iddi ambayo ilimalizika kwa siku tano zilizopita.

“Kwa hiyo umetokea Nigeria?” aliuliza dereva yule.
“Ndiyo! Ninarudi huko keshokutwa, ninakwenda fayad kutoa mawaidha katika msikiti mkuu wa hapo kisha nitarudi Cairo,” alisema Fareed huku akimwangalia mwanaume huyo.

Walizungumza mambo mengi sana, hakukuwa na siku ambayo Fareed alijifanya kuwa mtu wa dini kama siku hiyo. Kila alipokuwa akizungumza sentensi tano, aliingizia jina la Mtume Muhammad, kila alipokuwa akizungumza sentensi tano, alizungumza kuhusu swala, jinsi Muislamu anavyoweza kuingia motoni kama tu hatokuwa akiswali swala tano kwa siku.

“Na uzninifu! Siku hizi watu wanazini sana. Wewe una wanawake wa nje wangapi?” aliuliza Fareed huku akimwangalia dereva huyo aliyeonekana kuwa mtu mzima kidogo.

“Mimi ni mwenye dhambi! Nina mahawala watatu. Allah anisamehe,” alisema dereva huyo, aliumia moyoni mwake, kwa jinsi Fareed alivyokuwa akizungumza, alionekana kuwa mtu wa swala tano.

Safari iliendelea, walikuwa wakizungumza mambo mengi njiani. Magari ya polisi yalikuwa yakiwapita kwa sana kiasi kwamba dereva yule alikuwa akishangaa tu. Muda wote Fareed alipokuwa akiyaona magari hayo, alikuwa akishangaa, aliamini kwamba hao walikuwa wakimtafuta yeye, alipokuwa akiangalia saa yake, ilikuwa ni saa 11:30 alfajiri.

Hawakuchukua muda mrefu wakaanza kuingia katika Mji wa Ismailia. Walipofika hapo, wakakutana na magari kama kumi yaliyokuwa yakikaguliwa na askari waliokuwa mahali hapo.

Dereva yule hakuogopa hata kidogo, hakujua kama msako ule ulikuwa ni kwa ajili ya abaria aliyekuwa ndani ya gari lake.
 
SEHEMU YA 113

“Kuna nini?” aliuliza Fareed huku akimwangalia dereva.
“Sijui! Nashangaa! Huwa hakuna kitu kama hiki huku,” alijibu dereva yule, alipokuwa akiwaangalia polisi wale, walishikilia karatasi mikononi mwao iliyokuwa na picha ya Fareed.

Hakutaka kujiuliza, alikuwa na jibu kichwani mwake kwamba polisi wale walikuwa mahali hapo kwa ajili yake hivyo ilikuwa ni lazima afanye kila linalowezekana aweze kuondoka mahali hapo.

“Ngoja nisogeze gari wakague wanachokitaka, wakimaliza tuondoke zetu,” alisema dereva huyo, alitamani kumwambia alirudishe gari nyuma, alichoshindwa ni kwamba kwa nyuma kulikuwa na gari jingine, na alipokuwa akiendelea kuwaangalia polisi hao, walikuwa wakizidi kusogea kule walipokuwa.

Walibakiza gari moja kabla ya kuwafikia, mbaya zaidi mikononi mwao walikuwa na picha yake.
“Mungu wangu! Nimekwisha,” alisema Fareed huku mapigo yake ya moyo yakiwa juu. Yalidunda mara mia moja kwa dakika.

**** Fareed hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya mahali hapo, polisi wale waliendelea kusogea kule gari lao lilipokuwa kwa ajili ya kulichunguza ili kuona kama mwanaume aliyekuwa akitafutwa alikuwa ndani ya gari hilo au la.

Wakati wakiwa wamebakiza hatua kama kumi kulifikia, ghafla adhana ikaanza kusikika ikiadhiniwa. Kwa haraka sana Fareed akamwambia dereva kwamba lilikuwa kosa kubwa sana kupita siku pasipo kuswali hivyo akateremka kutoka garini na kwenda pembeni kidogo.

Akasimama na kuangalia kibla, dereva yule alishangaa, ni kweli alikuwa na abiria wengi waliokuwa wakipanda ndani ya gari lake lakini huyo abiria wa siku hiyo alikuwa kiboko, aliijua dini, alipenda kuswali utadhani alikuwa ndugu yake mtume.

Polisi walipofika, wakachungulia ndani, wakamwangalia dereva ambaye aliwaambia alikuwa na safari ya kuelekea Fayed na alikuwa amempandisha ustaadhi mwenye kujua misingi ya dini na alitoka nje kwenda kuswali.

“Ndiye yule?” aliuliza polisi mmoja.
“Ndiyo! Anakwenda kwenye sherehe ya Iddi na yeye ndiye anasubiriwa,” alisema dereva yule, kitendo kile alichokifanya Fareed kikawatoa hofu polisi na kuona kwamba walikuwa wakipoteza muda kulipekua gari hilo, hivyo wakasogea mbele kwenye magari mengine.
 
A good story Shunie... the first episode and the name Fareed quickly suggests that he is a Muslim ( though he might be a Christian) .... but in the middle of the story the man wanted to change his ways and he run into a church! Now he knows how to pray in a muslim way and he seems to know many things about the religion! Here there is a lack of information ( or background information) which will easily enable the reader to grasp this dramatic change! As one of the good readers myself, I love a story even if is a fiction story .. the story iwe ina resemble the truth hapa inanoga zaidi.... My comment is not a critic but a complement to the wonderful storytelling of yours! I am your fan of course! A big apology for those who will be annoyed by this comment and mixing of languages.
 
Back
Top Bottom