Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 110

Polisi walijitahidi kumtafuta kimyakimya, hawakutaka ajue kama tayari walikuwa na picha zake lakini kitendo cha CNN kutoa picha hizo tayari kilionyesha kwamba muuaji alijua kuwa picha zake zilikuwa kila kona, hivyo alitakiwa kujificha.


Wakaacha na suala la kuficha picha zake, walichokifanya ni kuziachia mitaani, zilibandikwa kila kona, kila mmoja alitakiwa kujua kwamba mtu aliyefanya mauaji ya bilionea mkubwa nchini humo alikuwa yeye.


“Jamani! Tuhakikisheni huyu mtu anakamatwa, vinginevyo mambo yatakuwa mabaya kwetu,” alisema kamanda mkuu wa jeshi la polisi nchini humo, alikuwa akiwaambia wenzake.


“Sawa mkuu!”
“Fungeni mipaka yote, bandari, mpaka mfereji wa Suez, asije kutoroka kuelekea Ulaya,” alisema kamanda huyo.
“Sawa mkuu!”

Hilo ndilo walilolifanya, kwa haraka sana mipaka ikafungwa, walitaka kuhakikisha mtu huyo hatoki ndani ya Misri akiwa salama, ilikuwa ni lazima kumtafuta, wampate na kumfanya walichokitaka wao na kuionyeshea dunia kwamba walikuwa na uwezo wa kumtafuta mtu yeyote na kumpata.

Muda ulizidi kwenda mbele, hawakujua mahali alipokuwa Fareed, walishangaa kwani hawakuamini kama mtu huyo alipanda ndege kuondoka nchini hapo kwa kuwa tarayi taarifa zilitolewa kila kona kwamba alikuwa akitafutwa, na uzuri zaidi ni kwamba hata picha tayari ziliwekwa kila kona.

Siku ya kwanza ikapita, siku ya pili nayo ikapita, kwenye kila kona alikuwa akitafutwa, zawadi nono likawekwa la dola laki tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni moja lakini bado mtu huyo hakuonekana kitu kilichowafanya polisi kuchoka, japokuwa walishirikiana na Wamarekani kupitia Interpool lakini bado Fareed hakupatikana.
 
SEHEMU YA 111

Wakati polisi wakihangaika kumtafuta Fareed, yeye alikuwa akifikiria lake, alitaka kuondoka nchini Misri pasipo kuonekana.

Alijua kwamba endapo angeendelea kubaki humo ilikuwa ni lazima kukamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.

Alitakiwa kutoroka haraka iwezekanavyo kitu ambacho kwake hakikuwa na tatizo lolote lile, alichokuwa akihitaji ni kupata usafiri wa haraka wa kuvuka na kuingia Ulaya, sehemu ambayo aliamini ingekuwa nafuu kwake na si kuendelea kubaki Afrika.

“Ni lazima niende Ulaya, siwezi kubaki Afrika kwa sasa,” alisema Fareed.

Hakutaka kutumia ndege, aliamini kwamba katika viwanja vya ndege kulikuwa na ulinzi mkubwa na njia pekee ya kuondoka nchini humo ilikuwa ni moja tu, kwa kutumia ndege, tena si kuelekea katika bandari za Said au Ras el Bar bali alitaka kwenda katika Mji wa Fayed ambapo kulikuwa na ziwa Great Bitter lililounganishwa na mfereji wa Suez, hapo angeomba msaada wa kupanda meli za kwenda Ulaya ambapo angetokomea huko.


Safari hiyo ilitakiwa kufanyika usiku wa siku hiyo, hakutaka kubaki hapo Cairo bali alichokifanya ni kuondoka kuelekea barabarani ambapo akakodi teksi kwa ajili ya kumpeleka Fayed.

“How much?” (kiasi gani?)
“One thousand pound,” (paundi elfu moja) alijibu mwanaume aliyekuwa kwenye taksi.
“Okey!” (sawa)

Si kila mtu aliyekuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea, watu wengine walikuwa bize na kazi zao na si wote walioziona picha za Fareed katika sehemu mbalimbali zilipobandikwa.

Mmoja wa watu ambao hawakuwa wakijua kitu chochote kilichokuwa kikiendelea alikuwa dereva huyo. Ilikuwa ni vigumu kumfahamu Fareed hata kama angeona tangazo na picha zake mara kwa mara kutokana na jinsi alivyovaa.


Alikuwa na kanzu ndefu nyekundu, kichwani alivalia kiremba kikubwa huku akiwa ameshika Juzuu mkononi. Alionekana kama ustadhi ambaye alikuwa akienda sehemu fulani kutoa mawaidha au Imamu fulani aliyekuwa akiwahi sehemu fulani kuswalisha
 
SEHEMU YA 111

Wakati polisi wakihangaika kumtafuta Fareed, yeye alikuwa akifikiria lake, alitaka kuondoka nchini Misri pasipo kuonekana.

Alijua kwamba endapo angeendelea kubaki humo ilikuwa ni lazima kukamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.

Alitakiwa kutoroka haraka iwezekanavyo kitu ambacho kwake hakikuwa na tatizo lolote lile, alichokuwa akihitaji ni kupata usafiri wa haraka wa kuvuka na kuingia Ulaya, sehemu ambayo aliamini ingekuwa nafuu kwake na si kuendelea kubaki Afrika.

“Ni lazima niende Ulaya, siwezi kubaki Afrika kwa sasa,” alisema Fareed.

Hakutaka kutumia ndege, aliamini kwamba katika viwanja vya ndege kulikuwa na ulinzi mkubwa na njia pekee ya kuondoka nchini humo ilikuwa ni moja tu, kwa kutumia ndege, tena si kuelekea katika bandari za Said au Ras el Bar bali alitaka kwenda katika Mji wa Fayed ambapo kulikuwa na ziwa Great Bitter lililounganishwa na mfereji wa Suez, hapo angeomba msaada wa kupanda meli za kwenda Ulaya ambapo angetokomea huko.


Safari hiyo ilitakiwa kufanyika usiku wa siku hiyo, hakutaka kubaki hapo Cairo bali alichokifanya ni kuondoka kuelekea barabarani ambapo akakodi teksi kwa ajili ya kumpeleka Fayed.

“How much?” (kiasi gani?)
“One thousand pound,” (paundi elfu moja) alijibu mwanaume aliyekuwa kwenye taksi.
“Okey!” (sawa)

Si kila mtu aliyekuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea, watu wengine walikuwa bize na kazi zao na si wote walioziona picha za Fareed katika sehemu mbalimbali zilipobandikwa.

Mmoja wa watu ambao hawakuwa wakijua kitu chochote kilichokuwa kikiendelea alikuwa dereva huyo. Ilikuwa ni vigumu kumfahamu Fareed hata kama angeona tangazo na picha zake mara kwa mara kutokana na jinsi alivyovaa.


Alikuwa na kanzu ndefu nyekundu, kichwani alivalia kiremba kikubwa huku akiwa ameshika Juzuu mkononi. Alionekana kama ustadhi ambaye alikuwa akienda sehemu fulani kutoa mawaidha au Imamu fulani aliyekuwa akiwahi sehemu fulani kuswalisha
Mambo yanazid kunoga
 
Shunie mwezi wa 5 ndio huu sasa issue ya kuku bado unakumbuka?
 
Back
Top Bottom