Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 29

Hakutaka kuendelea kulalamika, akamvuta na kukaa kitandani. Muda wote huyo Fareed alikuwa akimwangalia Godfrey, alimpenda lakini hakuona kama mwanaume huyo alikuwa na uwezo wa kumzuia asifanye mambo yake kwani katika maisha yake hakuwa akitegemea mwanaume mmoja, alikuwa akiishi maisha ya kutegemea wanaume wengi.

“Hutoniweza. Mimi ni popo, naruka popote nipatakapo,” alisema Fareed kwa sauti ya moyoni huku akimwangalia Godfrey ambaye alionekana kuridhika kwa kile alichokuwa akifanyiwa.

***
Kwa jina aliitwa Asteria Kimaro, alikuwa mwanamke mtu mzima aliyekuwa mfanyabiashara mkubwa jijini Dar es Salaam. Alikuwa na maduka mengi ya vipodozi, alikuwa akimiliki biashara nyingi ambazo zilimuingizia kiasi kikubwa cha fedha.

Japokuwa alikuwa akifanya biashara ya halali lakini upande mwingine alikuwa akifanya biashara ya magendo. Kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwachukua wanawake kwa kisingizio cha kuwapeleka nchi mbalimbali kufanya kazi lakini mwisho wa siku alikuwa akiwauza na kuwafanyisha biashara za ngono.

Mbali na wasichana hao lakini pia kulikuwa na wengine waliokuwa wakiishi nchini Tanzania lakini kila walipokuwa wakihitajika kingono nje ya nchi, alikuwa akipigiwa simu na kuambiwa, kiasi cha fedha alichokuwa akilipwa msichana husika, na yeye alichukua chake.

Biashara hiyo ilikuwa kubwa, ilimuingizia kiasi kikubwa cha fedha. Kila siku wanawake waliendelea kujiandikisha kwake na walipotokea wanaume, walisafirishwa na kuelekea nje ya nchi kwa ajili ya ngono tu.

Hakutaka kuishia kwa wanawake bali akapanua biashara yake na kuwachukua wanaume tata na kuanza kuwasafirisha kwenda huko. Biashara hiyo ilikuwa kubwa kwa nchi za Uarabuni kwa kuwa kulikuwa na wanaume wengi waliokuwa wakitamani mapenzi ya jinsia moja hivyo alijizatiti sasa katika nchi hiyo.

Katika biashara hiyo ndipo alipokutana na Fareed. Siku ya kwanza kumuona yeye mwenyewe alishtuka. Aliwaona wanaume wengi wa aina hiyo lakini si kama alivyokuwa Fareed.
 
SEHEMU YA 30

Alikuwa mzuri wa sura, msafi, mwenye umbo maridhawa na sauti ya kuvutia. Alipoambiwa kwamba na huyo alikuwa mmoja wa wanaume tata waliotaka awe wakala wake, alichanganyikiwa kwani aliamini kwamba angepata kiasi kikubwa cha fedha kama tu angekubaliana naye na kuingia mkataba.

Wakakaa chini na kuzungumza, halikuwa tatizo, alitaka kupanua biashara yake hivyo akasaini naye mkataba na ndiye alikuwa mtu wa kwanza kufikiriwa kila dili la nje lilipokuwa likifika mezani kwake.
Akaanza kumnadi kwa wateja wake, akawatumia picha kwa kuwaambia kwamba mali mpya iliwasili, kila aliyemuona, alichanganyikiwa, hawakuamini kama kungekuwa na mtoto mashalaah kama alivyokuwa Fareed.

“How much?” (kiasi gani?) aliuliza mwanaume aliyekuwa akiishi Qatar.
“Three thousand dollars?” (dola elfu tatu)
“I want her,” (namuhitaji)
Hiyo ndiyo biashara iliyokuwa ikifanyika, Asteria aliendelea kutengeneza utajiri, serikali haikumgundua kile alichokuwa akikifanya. Wale waliopata hela, wakawaambia wenzao na hatimaye idadi ya wanaume tata ikazidi kuongezeka nchini Tanzania, hasa katika Jiji la Dar es Salaam.

Asteria aliijua biashara ya uwakala, alijitoa, alihangaika huku na kule kuwatafuta wateja, alikuwa akiwapata na malipo kufanyika. Mpaka kipindi hicho, Fareed alikuwa amekwenda nchini nyingi, hasa za Uarabuni ambapo matendo hayo yalishamiri kwa kiasi kikubwa sana.

Baada ya miezi kadhaa, Asteria akampata bilionea Saed na kumwambia kuhusu Fareed. Mwarabu huyo alichanganyikiwa zaidi baada ya kutumiwa picha. Akapata uroho, udenda ukamtoka na kuhitaji kuwasiliana naye.
Walifanya yao na siku chache mbele, wakala huyo akapokea simu kutoka nchini Marekani, kwa Bilionea Cotton Keith ambaye alimwambia kwamba alisikia mambo mengi kuhusu yeye hivyo alihitaji msichana.

“Msichana?” aliuliza Bi Asteria.
“Ndiyo!”
“Sawa. Una dola elfu tano?”
“Swali la kitoto sana hilo. Unajua unazungumza na nani?” aliuliza bilionea huyo.

“Hapana!”
“Hebu angalia Google jina la Cotton Keith,” alisikika mwanaume huyo na kukata simu.

Je, nini kitaendelea?
 
“Swali la kitoto sana hilo. Unajua unazungumza na nani?” aliuliza bilionea huyo.

“Hapana!”
“Hebu angalia Google jina la Cotton Keith,” alisikika mwanaume huyo na kukata simu.
nimestuka
 
Back
Top Bottom