Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Klabu zijilaumu kwa mawasiliano duni nasi- TFF Send to a friend Monday, 28 February 2011 20:54

Sweetbert Lukonge

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema halistahili kulaumiwa na klabu za Ligi Kuu kuwa hazijapata fedha za nauli zinazotolewa na wadhamini wakuu wa ligi hiyo, Vodacom.

Hivi karibuni baadhi ya timu za Ligi Kuu zimekuwa zikilalamika kucheleweshewa fedha hizo na kudai kuwa zimekuwa zikipa usumbufu mbalimbali wakati wakati zinapokuwa na mechi za ugenini.

Akizungumza na Mwananchi jana, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema kuwa wao hawahusiki katika suala hilo bali ni klabu zenyewe kushindwa kuwa na mawasiliano mazuri ya shirikisho hilo.

ìSiyo kweli kama kuna timu hazijapata fedha zao za nauli na kama zipo basi ni makosa ya viongozi wao kwa sababu wanatakiwa kufanya mawasiliano nasi (TFF) na kukabidhiwa hundi zao ,î alisema.

Katika hatua nyingine katibu huyo amewataka viongozi wa klabu hizo kuwa na mawasiliano na shirikisho ili kuepukana na usumbufu ambao umekuwa ukijitokeza.

Baadhi ya timu ambazo ambazo zilikuwa zililalamika kuwa bado hajapata fedha hizo za nauli ni pamoja na Toto Afrika ya Mwanza, AFC Arusha na Majimaji ya Songea.
 
Mzanzibari ateuliwa kumsaidia Julio Send to a friend Monday, 28 February 2011 20:53

Sosthenes Nyoni

CHAMA cha Soka Zanzibar (ZFA)kimemteua kocha wa timu ya Chipukizi ya Pemba, Ayubu Mohamed kuwa kocha msaidizi katika kikosi cha timu ya taifa ya vijana ya Tanzania wenye umri chini ya miaka 23 kinachojiandaa na michuano ya Olimpiki mwaka 2012.

Kuteuliwa kwa Mohamed kushika wadhifa huo ni utekelezaji wa agizo la Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) la kuitaka ZFA kuteua kocha atakayekuwa msaidizi wa Jamhuri Kihwelo 'Julio' ambaye ni kocha mkuu wa kikosi hicho kilichoingia kambini rasmi mwishoni mwa wiki.

Katibu Mkuu Msaidizi wa ZFA, Masoud Attai aliliambia Mwananchi jana kuwa tayari Mohamed amekwishaarifiwa kuhusu uteuzi huo na kwamba atajiunga na kikosi hicho muda wowote kuanzia sasa.

"Kimsingi, ZFA imemteua Mohamed ambaye ataungana na Kihwelo, taarifa amekwishapewa na muda wowote kuanzia sasa atajiunga katika kikosi hicho,"alisema Hamad.

Katika hatua nyingine Attai alisema kuwa ZFA imetangaza majina ya wachezaji 13 kutoka visiwani humo ambao wataungana na wenzao 24 walioko katika kambi ya timu ya taifa ya vijana iliyoko jijini Dar es Salaam.

Aliwataja wachezaji hao kuwa ni Mahamoud Ally, Mbaraka Suleiman, Hamis Mcha, Isihaka Othman, Amour Suleiman, Salum Said na Gharib Mussa.

Wengine ni, Salehe Ahmad, Abdulghan Ghulam, Venti Kamanya, Idrisa Abdulrahim, Awadh Juma na Abuu Omari.

Wakati huohuo,Kalunde Jamal anaripoti kuwaJulio' ameiambia Mwananchi jana kuwa kwa sasa wachezaji wake wameshaingia kambi tayari kw maandalizi hayo isipokuwa wale Simba na Yanga mbao wanatumiwa na klabu zao katika michezo wa Ligi Kuu.

Alisema kufutiai mashindano hayo kuwakilishwa na nchi nzima, timu yake itakuwa na wachezaji 44 lakini baada ya wiki moja watapunguzwa na kubakia 25.

"Maandalizi yameanza na timu imeangia kambini katika hoteli ya Bamba Beach iliyopo nje kidogo, tutakuwa na wachezaji 44 ambapo baada ya wiki moja watachujwa na kubakia 25 na tayari tumewasiliana na TFF(Shirikisho la Soka Tanzania) kuhusu mechi za kirafiki na wao wapo katika harakati za kutafutia timu za kucheza nazo, "alisema Julio.
 
bot_tabimg.gif

Internazionale yashinda 2-0 kuzidisha upinzani kwa AC Milan Send to a friend Monday, 28 February 2011 20:49

ROME, Italia
UHSINDI wa mabao 2-0 ilioupata Internazionale Milano juzi dhidi ya Sampdoria umeirejesha katika nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu ya Italia, Serie A na upinzani mkali kwa timu ya AC Milan.

Mabao ya Wesley Sneijder na Samuel Etoío yalitosha kuipa ushindi Inter Milan katika mchezo wa Jumapili wa Serie A.

Sneijder alifunga kwa mkwaju wa adhabu ndogo ambao uliupenya ukuta wa wapinzani wao dakika ya 73, kisha Etoío akaongeza jingine dakika za majeruhi na kumaliza ukame uliodumu kwa mechi nne dhidi ya Sampdoria kwenye Uwanja wa Luigi Ferraris.

ìNimeridhika. Ushindi wa leo ulistahili umetokana na juhudi na kujituma kwa kila mmoja wetu, umemaliza kipindi kigumu kwetu ,î alisema kocha Leonardo.Sneijder ambaye alikuwa majeruhi alikuwa makini katika kipindi cha pili, kiasi cha kukaribia kufunga bao la pili, pia kwa mkwaju wa aadhabu ndogo, dakika ya 80.

Naye kiungo wa Sampdoria, Andrea Poli alipiga mkwaju ambao uligonga mwamba, dakika ya 43, huku wenyeji wakitengeneza nafasi zaidi za kupata mabao kuliko Inter katika kipindi cha kwanza.

Kipa wa Inter, Julio Cesar pia alikuwa makini baada ya kulaumiwa kwa kosa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wiki jana dhidi ya Bayern Munich.

Kwa matokeo hayo, Inter imepunguza pengo la pointi na kubakia mbili kati yake na AC Milan, ambayo jana ilikuwa ikicheza na Napoli inayoshika nafasi ya tatu.

Mapema , Udinese ilikaribia kukata tiketi ya michuano ya Ulaya msimu ujao bada ya kuiadhibu Palermo kwa mabao 7-0, huku Palermo ikimaliza mchezo na wachezaji tisa, kipigo ambacho huenda kikamwondoa kibaruani kocha Delio Rossi.

Mshambuliaji raia wa Chile, Alexis Sanchez alifunga mabao manne kati ya hayo na Antonio Di Natale akiongeza matatu (hat trick) na kufikisha mabao 21, akimpiku Edinson Cavani wa Napoli kwenye orodha ya vinara wa mabao Serie A msimu huu.

Rais wa Palermo , Maurizio Zamparini alisema kuwa Rossi amepewa nafasi moja ya mwisho kujiokoa kitanzini.

ìRossi ameharibu kikosi chetu. Nimemweleza abadili safu ya ulinzi, lakini hakufanya hivyo,î alisema Zamparini. ì Timu haiwezi kucheza vibaya namna ile.î

Rossi alitangaza pia kwamba hatajiuzulu, lakini alieleza kuwa anakubali lawama kwa kipigo hicho kibaya.

Kwingineko, mshambuliaji wa zamani wa Juventus , Amauri alifunga mabao mawili kwa Parma ambayo ilitokea nyuma na kupata sare ya 2-2 dhidi ya AS Roma na kutibua mwanzo mzuri wa Vincenzo Montella kama kocha wa Roma.

Roma ilitangulia kufunga kwa penalti ya nahodha Francesco Totti, ambaye alicheza mechi yake ya 600 akiwa mjini Rome na jingine la beki Mbrazili Juan.Pia, Roma ilimpoteza kiungo wake mahiri David Pizarro aliyeumia katika mchezo huo.

Montella, amerithi mikoba ya Claudio Ranieri aliyejizulu baada ya Roma kufungwa mabao 24 msimu huu.

ìHadi dakika ya 75hatukuruhusu shuti langoni mwetu ,î alisema Montella. ìTunahitaji kuongeza kasi yetu na mfumo wa uchezaji wetu, lakini hilo haliwezi kufanyika ndani ya siku tatu.î

Jirani zao, Lazio walifungwa 1-0 na Cagliari kwa kosa la beki Andre Dias.Matokeo mengine : Bari 1-1 Fiorentina; Brescia 2-2 Lecce ; na Cesena 1-0 Chievo Verona. Catania 2-1 Genoa.
 
Ferdinand taunt to Chelsea


RivalsDM



PRINT RSS

21 comments »

Updated Mar 1, 2011 10:07 AM ET
Manchester United defender Rio Ferdinand has told Chelsea that their multi-million pound signings will not make an impact for them this season.


The £50million capture of Fernando Torres and £21million deal for David Luiz were viewed as drastic action by Carlo Ancelotti in January in an attempt to stay in the Premier League title race.
Torres has still to score since joining Chelsea as last season's Double winners now only seem set to battle for a place in the top four, while Luiz has just shown glimpses of potential in his two matches.
Ferdinand, who misses Tuesday's trip to Stamford Bridge with a calf injury, admits to being impressed by Chelsea's spending power, however, he does not expect the money to prove a rescue remedy.
The centre-back is quoted as saying in the Daily Express: "The Torres deal did make me think, 'wow, they've really gone for it'.
"But will those transfers really improve Chelsea this season? I don't know. Next season, I would say, 'yes, they will'. But it is hard to settle in quickly in January."



PRINT RSS




Member Comments

Please note by clicking on "add a comment" you acknowledge that you have read the Terms of Use and the comment you are posting is in compliance with such terms. Be polite. Inappropriate posts may be removed by the moderator.
LOG IN TO ADD A COMMENT Page 1 of 3 PREV PREV NEXT NEXT


Post Comment


  • Report Abuse redevil_83
    • 3/1/2011 9:21:40 AM
    *451 i mean. it is an away match afterall. there've been times we've played that formation at theatre of dreasm so not seeing it at the bridge would be a surprise
  • Report Abuse redevil_83
    • 3/1/2011 9:20:25 AM
    541 berbs on bench, sadly
  • Report Abuse TPink
    • 3/1/2011 9:07:54 AM
    Boy this blog has gone downhill quickly. Are all ManU "fanlets" so infantile?

    Back to the article....Agree with the other adults who posted - RivalsDM and Fox are becoming as juvenile as some of these posts. Not fair to Rio, who really has been a good leader for a few years. I was wondering what he could have said and it turns out he said what most thought and was not disrespectful at all to players or club while having his own opinion.

    Too bad Fox/Rivals has to try to turn it into something else. News Sluts!

  • Report Abuse RedWhiteAndOrange
    • 3/1/2011 8:55:16 AM
    Rooney should start at left back.
  • Report Abuse PhiladelphiaHotSpur
    • 3/1/2011 8:52:34 AM
    Berbs riding pine or does he get the start ?

    4-5-1 or 4-4-2?????

  • Report Abuse redevil_83
    • 3/1/2011 8:45:51 AM
    C'MOOONNNN YOU RED DEVILS LETS GIVE A PERFORMANCE WORHTTY OF MANCHESTER UNNIITTEEDDD
  • Report Abuse redevil_83
    • 3/1/2011 8:45:22 AM
    viva john terry
    viva john terry
    could've won the cup
    but he f*cked it up
    viva john terry

  • Report Abuse PhiladelphiaHotSpur
    • 3/1/2011 8:38:32 AM
    And if Chelsea does anything on both CL fronts, Rio is probably wrong.............

    Torres man.......I just not a fan of his. esepcially w/ that pricetag.............

  • Report Abuse RedWhiteAndOrange
    • 3/1/2011 8:38:20 AM
    I thought arsenal would win. Maybe 1-0 or 2-1. What was your prediction?
  • Report Abuse PhiladelphiaHotSpur
    • 3/1/2011 8:35:56 AM
    Yo RWO - what was your Carling Cup prediction ?
LOG IN TO ADD A COMMENT Page 1 of 3 PREV PREV
 
TAKUKURU ni maamuma wa sheria?


na Happiness Katabazi


amka2.gif
HUENDA ule utabiri ‘bubu' uliokuwa ukitolewa na baadhi ya wananchi kwamba zile kesi za rushwa zilizokufunguliwa ‘chapuchapu' kwa mbwembwe na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( TAKUKURU) dhidi ya baadhi ya waliokuwa wagombea ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM )katika kura za maoni mwaka 2010 ni kiini macho.
Sote bado tunakumbuka kwamba miongoni mwa Wana CCM walioburuzwa mahakamani na TAKUKURU kwa kudaiwa kutoa rushwa ili majina yao yapitishwe kwenye uchaguzi wa ndani ya chama chao ni aliyekuwa waziri na mbunge wa muda mrefu, Joseph Mungai na Katibu Mkuu wa (TFF), mgombea ubunge wa Jimbo la Iringa Mjini, Fredrick Mwakalebela.
Awali Wakili wa TAKUKURU, Imani Mizizi, mbele ya Hakimu Mkazi, Festo Lwiza wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa, alidai Juni 20 mwaka jana, Mwakalebela alitoa hongo ya sh 100,000 kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Mkoga, Hamis Luhanga, ili awagaie wajumbe 30 wa CCM, walioitwa kwenye kikao hicho cha kujipanga kupiga kura za maoni.
Mwanasheria alidai mshitakiwa huyo alitenda kosa kinyume cha Sheria ya Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007, kifungu cha 15(1),(b),kinachosomeka pamoja na sheria ya gharama za uchaguzi namba 6 ya mwaka 2010, kifungu cha 21(1),(a) na kifungu cha 24(8).
Hivi karibuni tumeisikia Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa kwa wakati tofauti ikitoa amri ya kuwafutia kesi washitakiwa kwa maelezo kwamba hati za mashitaka zimeonekana kuwa na dosari za kisheria. Hati hizo ziliandaliwa na mawakili wa taasisi hiyo.
Washitakiwa walishitakiwa kwa kutumia sheria mbili tofauti kwenye hati moja ya mashitaka, kitu ambacho ni kinyume cha sheria na kinaweza kusababisha washitakiwa washindwe kuandaa utetezi wao.
Kwa muktadha huo hapo juu, sasa tunaweza kuona ule utabiri umetimia, kwani hata wahenga walisema: "Lisemwalo lipo na kama halipo lina kuja."
Na kwa washitakiwa hao wawili kuachiliwa na mahakama ni wazi msemo huo wa wahenga umetimia.
TAKUKURU ndiyo chombo chetu ambacho moja ya majukumu tuliyowakabidhi ni kuchunguza, kuzuia na kupambana na rushwa na hivi sasa kina mawakili wake ambao hufika mahakamani kuendesha kesi zinazohusiana na rushwa.
Na Watanzania ndio tumeridhia tuwe na chombo hicho kwa kuhakikisha taifa letu linamtokomeza mdudu rushwa kwasababu ni adui wa haki.
Hivyo, kitendo cha baadhi ya mawakili wa TAKUKURU walioshiriki kuandaa hati hizo mbili za mashitaka dhidi ya Mungai na Mwakalebela na kubainika hati hizo zimeandaliwa ovyo, ndiko kumenisukuma kuandika mtazamo huu na kuinyoshea kidole taasisi hiyo.
Kisheria upande wa Jamhuri wanaruhusiwa muda wowote kuzifanyia mabadiliko hati zao za mashitaka pindi inapobainika kisheria.
Watanzania tujiulize, hivi umakini wa wanasheria wa TAKUKURU katika mashauri hayo uko wapi?
Haiingii akilini kabisa, Rais Jakaya Kikwete ambaye alisaini kwa haraka Sheria ya Gharama za Uchaguzi 2010 na kuiagiza taasisi hiyo iwashughulikie bila aibu wanasiasa wote hata wa CCM wanaotoa rushwa kwenye uchaguzi, halafu hawa mawakili wa taasisi hiyo washindwe kuwa makini katika kuandaa hati za mashitaka na mwisho wa siku watuhumiwa wanaachiwa na mahakama!
Tujiulize, mawakili hao ni ‘maamuma' na ‘mbumbumbu' wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya mwaka 2010?
Au taasisi hiyo iliamua kuwafungulia kesi hizo ili kumuhadaa Rais Kikwete kwamba ile sheria aliyoisaini pale Ikulu ndiyo imeanza kutumika, huku mawakili wa taasisi hiyo wakiwa wameandaa madudu katika hati hizo za mashitaka?
Kwa hiyo wananchi tumtegemee tena kumsikia Ofisa Uhusiano wa TAKUKURU, wiki hii kutoa taarifa kwa vyombo vya habari kwamba licha mahakama kumwachia Mwakalebela, taasisi yake itamshitaki tena, kwani tungali tukikumbuka kwamba hata alipoachiwa Mungai ofisa habari huyo alisema maneno hayo ambayo kwa watu wenye akili timamu kama sisi na tunajua kinachoendelea, tunaishia kupata kichefuchefu na hasira.
Vyovyote iwavyo, ninapenda kuwaasa hasa mawakili wa serikali hususan nyie mawakili na wachunguzi wa TAKUKURU, tumieni taaluma zenu vizuri na kwa haki, kwa masilahi ya taifa letu na si kwa lengo la kuwafurahisha baadhi ya wanasiasa wenye hulka za kinyang'au au watu wenye nguvu ya fedha na madaraka kuwaumiza wananchi ambao wana ugomvi wao binafsi.
Kumbukeni vyeo na taaluma mlizonazo ni dhamana, kwa hiyo baadhi yenu kwa makusudi mnavyoamua kutumia vyeo au taaluma zenu kuwaumiza wananchi, ipo siku Mungu atawalipa mshahara wa dhambi.
Nasema haya kwa uchungu, kwani nina miaka 12 sasa ya kuripoti habari za mahakamani, nimeshuhudia na ninaendelea kujifunza mambo mengi, kwamba kuna baadhi ya wananchi wenzetu wanafikishwa mahakamani kwa kubambikiwa kesi, ingawa kuna wanaofikishwa kihalali.
Kwa mtazamo wangu, ni vema mawakili wa TAKUKURU kuwa makini katika uandaaji wa hati za mashitaka na uendeshaji wa kesi zake, kwani kubainika kwa hati hizo mbili kuwa na dosari ni wazi kunachangia kuporomosha heshima ya taasisi hiyo na ndugu wa washitakiwa wataanza kujenga chuki dhidi ya taasisi hiyo na serikali yetu. Hatutaki tufike huko.
Mungu ibariki Afrika,
Mungu ibariki Tanzania.



h.sep3.gif

0716- 774494; Fukuto la Jamii
 
Yanga yaipiga kumbo Simba


*Yakaa tena kileleni

Na Nickson Mkilanya, Morogoro

MBIO za kupokezana vijiti za Ligi Kuu Tanzania Bara ziliendelea tena jana, ambapo Yanga ilikamata tena usukani wa ligi hiyo, baada ya
kuifunga Ruvu Shooting bao 1-0 katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Jamhuri.

Simba juzi ilikalia kiti hicho kwa muda, baada ya kuuchukua kutoka kwa Azam FC ambayo sasa imesukumwa hadi nafasi ya tatu.

Kwa ushindi huo Yanga, sasa ndiyo inayoongoza ligi hiyo kwa kufikisha pointi 38, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 37 na nafasi ya tatu ikikaliwa na Azam FC ambayo ina pointi 35.

Katika mechi ya jana, Yanga ilisubiri hadi dakika ya 77 ndiyo ikapata bao lake kupitia kwa Jerison Tegete, aliyefunga kwa kichwa akiunganisha kona iliyochongwa na Kiggi Makasy.

Mechi ya jana ilianza kwa timu zote kucheza kwa nguvu na kutafuta mabao haraka haraka, ambapo Yanga kupitia Davies Mwape na Tegete kuikosesha timu hiyo mabao ya wazi.

Ruvu Shooting ambayo jana ilicheza kwa tahadhari kubwa, nayo ilikosa mabao ya wazi kupitia kwa Revocatus Maliwa, Ayoub Kitala na Hassan Dilunga.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ambapo wachezaji wa Ruvu Shooting walijitahidi kutaka kufunga mabao, lakini hata hivyo washambuliaji wake hawakuwa makini kila walipolifikia lango la wapinzani wao.

Dakika ya 58, Martin Mlolele aliikosesha Ruvu bao la wazi baada ya kupiga kichwa hafifu akiwa na kipa wa Yanga Yaw Berko.

Katika kipindi hicho kila timu ilifanya mabadiliko ambapo, Yanga iliwatoa Mwape na Ernest Boakye na kuwaingiza Ibrahim Job na Idd Mbaga.

Ruvu nayo ilimtoa Hamis Yakuti na Mangasin Mangasin.

Hata hivyo mabadiliko hayo yaliinufaisha zaidi Yanga, ambayo ilipata bao lake kupitia kwa Tegete dakika ya 77.




1 Maoni:

blank.gif

Anonymous said... Yanga mwendo mdundo mpaka ubingwa!!
March 1, 2011 1:46 AM
 
Happy Drog content at the Bridge


RivalsDM



PRINT RSS

0 comments »

Updated Mar 1, 2011 9:57 AM ET
Chelsea striker Didier Drogba claims he has everything he dreams of at Stamford Bridge and has no desire to leave.
The 32-year-old, who joined the Blues in 2004 from Marseille, has been linked with a return to France since the £50million arrival of Fernando Torres from Liverpool in the winter transfer window.

The home of the best LIVE soccer and rugby awaits at FoxSoccer.tv -- don't miss a second of the action.

But Drogba, who is under contract with the Premier League champions until 2012, does not harbour any ambitions to ply his trade elsewhere.
"I have everything I dream of at Chelsea," the Ivorian said on French television channel Orange Sport.
"I'm at a great club with extraordinary team-mates, in a perfect life for my family.
"A few years ago, I could say 'I dream of playing for AC Milan, Real Madrid, Manchester United'. However, today I no longer feel the need.
"I'm at one of the best clubs in the world. These desires left me long ago."
 
Man United, Chelsea patamu leo


London, England

MIAMBA ya soka nchini England, timu za Manchester United na Chelsea, leo zinatarajia kumaliza ubishi zitakapomenyana katika mchezo wa kwanza wa
Ligi Kuu, utakaopigwa Uwanja wa Stamford Bridge baada ya awali kuahirishwa kutokana na barafu.

Awali mchezo huo ulipangwa kupigwa Desemba 19, mwaka jana lakini kutokana na baridi iliyoambatana na barafu mchezo huo ukaahirishwa hadi leo usiku.

Kwa mara ya mwisho timu hizo zilikutana katika mchezo wa Ngao ya Jamii uliopigwa Agosti, mwaka jana ambapo Man Utd iliibuka na ushindi wa mabao 3-1.

Katika michezo mitano ya ligi hiyo hivi karibuni, Chelsea inaongoza kwa kuifunga Man United ambapo imeshinda mara tatu, sare moja na kupoteza mchezo mmoja.

Ushindi wa United wa mabao 4-0 dhidi ya Wigan, mwishoni mwa wiki umeifanya United kufikisha pointi 60 wakiwa pointi nne zaidi ya Arsenal walio katika nafasi ya pili.

Katika ligi hiyo, Manchester United inaogoza ikiwa ikifuatiwa na Arsenal yenye pointi 56, huku Chelsea ikishika nafasi ya tano baada ya kujikusanyia pointi 47.

Endapo itaibuka na ushindi dhidi mabingwa watetezi Chelsea, kunaweza kuifanya United kuwa katika nafasi nzuri ya kuweza kutwaa ubingwa na kuweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza kutwaa kombe hilo mara nyingi (19).

Liverpool imetwaa ubingwa wa Uingereza mara 18 ambao ni sawa na Manchester United.

Winga aliye katika kiwango cha juu Nani, ambaye amefunga mabao 10 na kusaidia mengine 14 msimu huu, hatacheza kutokana na kuumia katika mechi dhidi ya Wigan.

Naye Kocha Mkuu wa Man Utd, Sir Alex Ferguson alisema ni vigumu kuzungumzia mchezo huo lakini hafikirii kama ataupoteza kutokana na kiwango cha timu yake.
 
amka2.gif
WASANII wa muziki pamoja na waigizaji wamekabidhi hundi ya sh mil.76 kwa waathirika wa milipuko ya mabomu iliyotokea katika kambi ya jeshi ya 511 KJ, hivi karibuni.
Fedha hizo ambazo zilipatikana kupitia mechi ya kirafiki baina ya waigizaji na wasanii wa muziki Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam na fedha hizo walizikabidhi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Akizungumza wakati wa kukabidhi fedha hizo, mwakilishi wa wasanii hao Hamis Mwinjuma ‘Mwana fa' alisema wanaungana na Watanzania wengine kutoa pole kwa wote waliofikwa na janga hilo.
Alisema kutokana na kuguswa na tukio hilo ambalo kwa namna moja ama nyingine liliwahusu na wao waliamua kushiriki katika tamasha hilo na ndipo kiasi hicho kilipopatikana.
Katika hatua nyingine, Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries (SBL) nayo imekabidhi hundi ya sh mil.10 kwa waathirika, fedha ambazo zilikabidhiwa kwa Waziri Mkuu Pinda na Mkurugenzi wa Mahusianoa wa SBL, Teddy Mapunda.



h.sep3.gif


juu
 
'Safari Nyama Choma' yapamba moto


Na Mwandishi Wetu, Mbeya

MASHINDANO ya 'Safari Lager Nyama Choma 2005', yamepamba moto jijini hapa ambapo tayari bar tano bora zimeshapatikana.Fainali ya mashindano
hayo ya mkoa yanatarajia kufanyika Jumamosi, ambapo majaji kutoka Dar es Salaam wanatarajia kuwasili leo kwa ajili ya kazi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana Meneja wa bia ya Safari, Fimbo Butallah alisema maandalizi ya fainali hizo tayari yamekamilika.

Alizitaja bar zilizopenya hatua kuwa ni Kalembo, 2000 Grocery, Mbeya Carnival Sky Club na Neabana bar.

"Kila kitu kinakwenda vyema kinachosubiriwa ni muda ufike ili mshindi aweze kupatikana na pia tunatarajia kutakuwa na burudani kemkem ikiwemo bendi TOT Plus na Marimba," alisema Butallah.




0 Maoni:
 
Extra Bongo kutambulisha wapya Leaders Jumamosi


na Dina Ismail


amka2.gif
BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo ‘Next Level' inatarajiwa kuwatambulisha rasmi wasanii wake wapya kwa mara ya kwanza kupitia bonanza la wasanii na wanamichezo litakalofanyika Jumamosi kwenye viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mbizo Entertainment inayoandaa tamasha hilo kwa kushirikiana na Tunaweza Band, Juma Mbizo, alisema jana kwamba wasanii hao wapya watatambulishwa rasmi kabla ya jioni yake kutambulishwa katika ukumbi wa TCC Chang'ombe.
Alisema kupitia bonanza hilo la kila wiki lenye lengo kuwakutanisha pamoja watu hao katika michezo, pia bonanza hilo ni kwa ajii ya kupata burudani kutoka kwa bendi mbalimbali mahiri pamoja na wasanii wa Jiji la Dar es Salaam.
"Tunataka tuwape nafasi ya kukutana pamoja, kucheza sambamba na kupata burudani, ili kuweka sawa miili na akili baada ya kazi zao za wiki nzima," alisema.
Timu zinazoshiriki katika bonaza hilo ni pamoja na Mburahati Queens, Mchangani Sisters, Magomeni Combine, DT. Dobie, TANESCO, Wagadau, Naj Contractors, Magomeni Veterani, Baker Ranger, Makuburi Sports, Kigogo Veteran, Ubungo Terminal, Dar Tallented, Kinondoni Combine, Kimara Veteran, Zimamoto na Uokoaji, PSPF na Highway Africa.
Aidha, bendi zinazotumbuiza katika bonanza hilo ni pamoja na Kalunde Band, Diamond Musica, Rufita Connection, Stone Mayiyasika, Supershine Modern Taarab, TOT Plus, Konga Moyo na TOT Taarab, Nyota Dancing Troupe, Jembe Dancing Troupe, H.Mbizo, Bushoke na Bushoke Band na Dokii.
Bendi nyingine ni pamoja na 20%, The Talent chini ya uongozi wake Hussein Jumbe, Mashujaa Musica na New Zanzibar Stars, bila kuwasahau wasanii mahiri hapa nchini katika miondoko ya Taarab, Isha Mashauzi na mama yake.



h.sep3.gif

 
'Safari Nyama Choma' yapamba moto


Na Mwandishi Wetu, Mbeya

MASHINDANO ya 'Safari Lager Nyama Choma 2005', yamepamba moto jijini hapa ambapo tayari bar tano bora zimeshapatikana.Fainali ya mashindano
hayo ya mkoa yanatarajia kufanyika Jumamosi, ambapo majaji kutoka Dar es Salaam wanatarajia kuwasili leo kwa ajili ya kazi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa jana Meneja wa bia ya Safari, Fimbo Butallah alisema maandalizi ya fainali hizo tayari yamekamilika.

Alizitaja bar zilizopenya hatua kuwa ni Kalembo, 2000 Grocery, Mbeya Carnival Sky Club na Neabana bar.

"Kila kitu kinakwenda vyema kinachosubiriwa ni muda ufike ili mshindi aweze kupatikana na pia tunatarajia kutakuwa na burudani kemkem ikiwemo bendi TOT Plus na Marimba," alisema Butallah.
 
Visura wa Tanzania wapiga vita unyanyasaji wanawake, watoto


na Dina Ismail


amka2.gif
WASHIRIKI wa shindano la kumsaka Kisura wa Tanzania mwaka 2011 wamefanya igizo maalum ambalo linazungumzia upigaji vita unyanyasaji wa wanawake na watoto.
Washiriki hao walionyesha igizo hilo katika ukumbi wa Mwinjuma ambapo walisema wamedhamiria kuunga mkono kampeni hizo kwa kuhakikisha jamii ya Kitanzania inaondokana na tatizo la kijinsia.
Akizungumza ukumbini hapo, mratibu wa onyesho hilo Easter Lwiza alisema kuwa uhamasishaji wa mapambano dhidi ya matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii ya Kitanzania ni miongoni mwa kazi kuu za warembo hao.
Alisema tangu kuanza kwa shindano hilo washiriki hao wamekuwa wakishiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kwa mfano hivi karibuni waliungana pamoja katika kusaidia wahanga wa mabomu katika hospitali ya Ilala.
Pamoja na onyesho hilo washiriki hao waliongoza mamia ya watu waliohudhuria katika onyesho hilo kupima virusi vya ukimwi ambapo mgeni rasmi alikuwa muigizaji maarufu nchini Steven Kanumba.
Kanumba aliweza kuvutiwa na vipaji vya baadhi ya washiriki hao pindi walipokuwa wakiigiza na kuahidi kuwapatia kazi pindi watakapomaliza kushiriki shindano hilo.
Shindano la kumsaka kisura lilianza rasmi Januari 30, 2011 na fainali zake zitafanyika Machi 12 katika hoteli ya Moevenpick jijini Dar es salaam.



h.sep3.gif

 
Yanga outplay Ruvu Shooting




By The guardian reporter



1st March 2011



Comments




Yanga%2822%29.jpg

Young Africans


Young Africans revived their title aspirations after edging hard fighting Ruvu Shooting by a lone goal in the Mainland Premiership return leg played at the Jamhuri Stadium in Morogoro yesterday.
It was Jerry Tegete who relieved coach Sam Timbe and the rest of the fans when he scored after connecting Athumani Idd's inswing corner kick after 77 minutes.
The tension packed encounter saw the teams share spoils at the end of the first half with Ruvu Shooting looking a well organised side.
Ruvu Shooting came a rejuvenated side as the second half resumed and took a big possession to besiege Yanga goal midway into the second half.
Yanga defence was under constant menace but Shooting's Martin Mlolere twice failed to beat Yanga's Ghanaian goalkeeper Yaw Berko much to the amazement of spectators.
Yanga midfielder Idd had released a power-packed 40-metre drive only to be parried to safety by Shooting's custodian
Mahmood Mbulu after 30 minutes.
Idd took the fruitful corner kick which Tegete made full use to take the lead after 32 minutes.
The goal was scored against the run of play as Ruvu Shooting had earlier thrown overboard more than six clear opportunities that would have seen them ahead.
Shooting's coach Charles Boniface bemoaned poor officiating by referee
Thomas Mkombozi. He said his team would have emerged winners of the game had there been impartial officiating.
Shooting are gazing at the relegation borderline with 15 points, creating a four-pint cushion over troubled Majimaji and AFC who share eleven points.
His counterpart Sam Timbe said his boys played as per the plan as they transformed the match during the second half to post the victory.
Following yesterday's victory, Yanga are leading by a point over Simba and have superior goal difference of one.
The win has psychologically boosted Yanga ahead of Saturday's return leg tie against rivals and holders Simba at the National Stadium in Dar es Salaam.
However, Simba have a game in hand as they head to Zanzibar to set up preparation camp.
Line-ups:
Ruvu Shooting: Mahmood Mbulu, Raphael Kyara, Oscar Mkulula, Ayoub Chitala, George Ossey, Hamis Maliwa/Mangasin Mangasin, Juma Jumanne, Revocatus Maliwa, Hassan Dilunga, Michael Pius/Fullzul Maganga, Martin Mlolere.
Coach: Charles Boniface

Young Africans: Yaw Berko, Shadrack Nsajigwa, Stephano Mwasika, Chacha Marwa, Nadir Haroub, Isaack Boakye, Athumani Idd, Davies Mwape, Idd Mbaga, Jerry Tegete, Nsa Job, Kigi Makasi.
Coach: Sam Timbe
Referee: Thomas Mkombozi



SOURCE: THE GUARDIAN
 
Dar heavyweight bout pushed back




By Correspondent



1st March 2011


email.png

Email



printer.png

Print



comment_bubble.png

Comments




Much touted heavyweight boxing bout between Awadh Tamim and Ashraf Suleiman that was supposed to be staged on Saturday has been pushed back by exactly a week.
The event's coordinator Shomari Kimbau said the postponement has been necessitated to pave the way for fans who would like to watch Mainland archrivals clash between Young Africans and Simba at the National Stadium.
Kimbau said the boxing bout has now been adjourned to March 12 but there is no change of the venue, Diamond Jubilee.
Kimbau said some of the boxing fans are also fans of soccer and therefore, the two sports events would distract attention of them, should they be staged on the same date.
"We need to give a wide room to fans of both soccer and boxing to attend the two events on the separate dates," said Kimbau.
Zanzibar-based boxer Suleiman remained optimistic to emerge winner of the bout while training hard.
The boxing bout between the duo was cut short when they first met last year in Dar es Salaam.
Tamim, who is based in Sweden, has not appeared in any other contest staged in the country ever since.



SOURCE: THE GUARDIAN
 
Simba custodian in psychological havoc




By The guardian reporter



1st March 2011







Comments




Simba`s first choice goalkeeper Juma Kaseja has admitted to be in psychological imbalance that has affected his performance.
Kaseja was offloaded from coach Patrick Phiri's first choice line-up replaced by Ali Mustafa.
The goalie, who won the most outstanding award during the Challenge Cup championship staged in December last year, said he is embroiled by family affairs that has drastically affected his playing-form.
Kaseja said he needs to be free of any psychological disorder for him to perform well between the posts.
He urged fans to be patient with him for the moment while he recapitulates to bounce back into his usual playing mood.
The goalkeeper downplayed any other reason for his drastic fall in form and said with time, the problem would be resolved.
Twice Kaseja was involved in controversial loss of points when his side met Azam FC on January 23 at the Uhuru Stadium in Dar es Salaam.
His loss of concentration resulted in a 2-2 draw with Toto Africa scoring deep into stoppage time at the CCM Kirumba Stadium on February 16.
Simba's head coach Patrick Phiri said Kaseja has played many matches and he needs to rest him to secure composure.
Phiri said Kaseja is being rested on the grounds to improve his performance and not loss of form as many fans have been speculating.
Phiri said his second choice goalkeeper Mustafa is most likely to be included in his first choice line-up against rivals Young Africans (Yanga) in the return leg tie of the Mainland premiership on Saturday.
"I'm expecting to alternate Kaseja and Mustafa in the next two matches between Yanga and TP Mazembe," said the Simba coach.
Simba meet Yanga on Saturday as they line up CAF Champions League first leg tie against DR Congo's TP Mazembe in a fortnight.



SOURCE: THE GUARDIAN
 
AFC meet Ruvu JKT




By The guardian reporter



1st March 2011


Comments




Relegation-haunted AFC Arusha meet JKT Ruvu in their return leg of the Mainland premier soccer league at the Uhuru Stadium in Dar es Salaam today.
The visitors will be looking forward to underline their supremacy over the army side having thumped them by 3-2 goals at the Sheikh Amri Abeid Stadium in Arusha on October 2.
Should the visitors post victory they would be making gradual ascendance towards the safe horizon from the relegation pool.
However, the victory would still confine the team inside the dreadful relegation pool as they need to win the next game as well.
AFC which regained top flight berth this season stands to be potential for demotion into the first division should they not be careful in their remaining fixtures.
JKT Ruvu are safe and have been ruled out of title race and the match will be for premiership survival. With 22 points to their kitty, JKT would only hit a ceiling of 37 points which has already been reached by both Simba and Yanga.
The army side also need to post a victory to stay safe from the relegation worries.



SOURCE: THE GUARDIAN
 
Sumu ya Teja kutoka na ‘Hotuba ya Mfungwa'


na Faisal Moshi


amka2.gif
MWANAMUZIKI Vitalis Maembe anatarajia kutoka tofauti katika nyanja ya sanaa kwa kuibuka na ‘Hotuba ya Mfungwa' ikiwa ni muendelezo wa kazi zake za sanaa alizoanza katika nyimbo mbalimbali alizowahi kuimba katika tasnia ya muziki hapa nchini.
Akizungumza katika jukwaa la sanaa jana, Maembe alisema anaomba sapoti kutoka kwa wadau mbalimbali ili kufanikisha kazi hiyo ambapo amedhamiria kufikisha ujumbe kwa jamii.
Maembe alisema ili asiende nje ya sanaa ya muziki anaopiga ameonelea atumie baadhi ya vitabu vinavyotumika kujibu maswali ya mitihani katika elimu ya sekondari.
Aidha Maembe aliweka bayana changamoto anazokutana nazo dhidi ya serikali kwa hiyo ameonelea kutumia hotuba ya Azimio la Arusha, Katiba na Vijana wa TANU.
Alisema hii ni changamoto dhidi ya rushwa, uvivu pamoja na ubinafsi ambavyo vimeikumba jamii.
Maembe alisema ujumbe wake hautoishia Dar es Salaam na badala yake atafikisha ujumbe kwa jamii hadi mikoani kupitia ‘Hotuba ya Mfungwa'.
Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Ghonche Materego alitoa wito kwa wadau wenye kazi za sanaa wajitokeze ili zihifadhiwe katika maktaba zao.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom