Michezo magazetini leo...

Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
TAKUKURU kumrejesha kortini Mwakalebela?


na Francis Godwin, Iringa


amka2.gif
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) mkoani Iringa imesema kuwa leo itatoa msimamo wake wa kuirejesha upya mahakamani kesi ya rushwa inayomkabilia kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na aliyeshinda kura za maoni katika kinyang'anyiro cha ubunge jimbo la Iringa mjini, Frederick Mwakalebela.
Uamuzi huo umekuja ikiwa ni siku tatu toka Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Iringa kumwachia huru Mwakalebela katika shtaka lake la rushwa katika mchakato wa kura za maoni na kuitaka TAKUKURU kuifungua upya kesi hiyo ama la.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwanasheria wa TAKUKURU mkoani Iringa, Ntimu Mizizi, alisema uamuzi ya mahakama hiyo chini ya hakimu Festo Lwila ameyakubali na kuwa upungufu uliokuwapo awali katika kesi hiyo 4/ 2010 taasisi hiyo inaufanyia kazi na kufungua kesi yenye maelekezo ya mahakama.
Alisema uamuzi ya mahakama katika kesi hii ya Mwakalebela umeonekana ni mzuri na wenye maelekezo ya kina zaidi kuliko ilivyokuwa kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini, Joseph Mungai, ambao mahakama haikwenda kiundani zaidi kama ilivyo katika maamuzi madogo ya kesi ya Mwakalebela.
Hata hivyo alisema leo kutakuwa na majibu sahihi dhidi ya uamuzi wa TAKUKURU katika kuendelea na kesi hiyo ama la.
Mahakama iliindoa kesi hiyo na kumwachia huru Mwakalebela baada ya kuridhika na hoja ya upande wa utetezi kwamba kulikuwa na upungufu wa kisheria kwenye hati ya mashtaka.
Mapungufu hayo ni mtuhumiwa kushtakiwa kwa makosa mawili kwenye hati moja ya mashtaka na hivyo kumfanya mtuhumiwa ashindwe kuelewa kwa usahihi kosa linalomkabili.
 
Mustafa Hassanali kufanya onyesho la wazi Viwanja vya Mnazi Mmoja


na Dina Ismail


amka2.gif
MBUNIFU maarufu wa mavazi, Mustafa Hassanali, anatarajia kufanya onyesho la wazi la mavazi katika viwanja vya Mnazi Mmoja ambalo ni sehemu ya uzinduzi wa toleo lake lenye ladha za Kiafrika kwa mwaka 2011/2012 katika maonyesho yaliyobatizwa jina la Mamma Mia.
Onyesho hilo litafanyika Machi 5 likitanguliwa na lile la Machi 4 litakalofanyika kwenye hoteli ya Movenpick ambapo ameshirikiana na shirika la Utepe Mweupe nchini, ikiwa ni katika sehemu ya kuendeleza kampeni ya uzazi salama.
Hassanali anakuwa wa kwanza kufanya maonyesho ya bure nchini ambapo kila atakayeingia katika viwanja hivyo atatakiwa kutoa mchango wa shilingi mia moja, itakayokwenda moja kwa moja katika kusaidia uzazi salama Tanzania.
"Onyesho la Mnazi Mmoja litakuwa si tu ni onyesho la kwanza la bure, bali pia litakuwa ni onyesho la kwanza katika historia ya Afrika kurushwa hewani na ‘Uhuruone' moja kwa moja kupitia mtandao wa intaneti," alisema.
Onyesho hili la Mnazi Mmoja litarushwa hewani moja kwa moja na ‘Uhuruone' kupitia mtandao wa Welcome | Kipepeo Collection by Mustafa Hassanali saa kumi kamili kwa saa za Afrika Mashariki.
Alisema katika maonyesho hayo atashiriki mbunifu maarufu kutoka visiwani Zanzibar, Farouque Abdella wa Zanzibar, pamoja na washiriki wabunifu kutoka London Fashion Week, Henrietta Ludgate na Minna Hepburn, walioshinda tuzo za ubunifu Uingereza. Aidha, pamoja na wabunifu hao, wasanii mbalimbali wa muziki nchini watatoa burudani katika onyesho hilo.
Onyesho hilo limedhaminiwa na Vodacom na Johns Hopkins Centre for Communication Programs nchini Tanzania, The Citizen, Uhuruone, Benki ya Barclays, Movenpick Royal Palm Hotel, Ultimate Security, Novamedia, Darling Hair, Vayle Springs, Eventlites, Fashion 4 Health, Image Masters and 361 Degrees.
 
Mshiriki shindano la ‘Ruka Juu' aomba kura


na Shehe Semtawa


amka2.gif
MJASIRIAMALI Idrisa Manah ‘Mc Manah' amewaomba wadau mbalimbali nchini kumpigia kura katika shindano la wajasiriamali linaloitwa ‘Ruka Juu' la kuwania kitita cha shilingi milioni tano litakalorushwa katika kipindi cha Fema TV Talk Show kuanzia Machi 5.
Mjasiriamali huyo kutoka Kibaha mkoani Pwani alisema anahitaji wadau mbalimbali kufuatilia shindano hilo katika vituo vya televisheni na kumpigia kura ili aweze kuibuka na kitita hicho kwa lengo la kupanua zaidi biashara zake.
Alisema shindano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Femina HIP litarushwa kupitia Shirika la Utangazaji nchini (TBC), linawashirikisha wajasiriamali sita kutoka mikoa tofauti huku wakiendesha biashara mbalimbali katika maeneo husika.
MC huyo aliongeza kuwa anaamini ushindi atakaoupata utasaidia pia dhima yake ya kuwasaidia wengine kupitia ajira atakayowapatia katika vituo vyake vya biashara.
 
Samatta atuma salamu Yanga
• Akandamiza tatu, aondoka na mpira

na Makuburi Ally


amka2.gif
MABAO matatu yaliyofungwa na mshambuliaji wake, Mbwana Samatta, jana yaliiwezesha Simba kuvuna pointi tatu kutoka kwa Mtibwa Sugar kwa kuitandika mabao 4-1 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo umeiwezesha Simba kupata pointi tatu tu, pia kurejea katika kiti cha uongozi wa ligi hiyo iliyoanza Agosti 21, mwaka jana, ikishindanisha timu 12.
Simba iliyoshuka dimbani jana ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi 34, sasa imekwea hadi nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 37, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 35 na Yanga pia yenye pointi kama hizo.
Hata hivyo, Simba wanaweza kupigwa kumbo katika nafasi hiyo kama mtani wake Yanga atashinda mechi yake ya leo dhidi ya Ruvu Shooting itakayochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro.
Kama Yanga itashinda, itakamata usukani wa ligi hiyo kwani itakuwa na pointi 38, lakini kinyume cha hapo, itakuwa imetoa nafasi ya kupitwa na timu nyingine zinazoshindania nafasi tatu za juu.
Katika mechi ya jana iliyokuwa na ushindani mkubwa, Simba walikuwa wa kwanza kupata bao likifungwa na Samatta kwa shuti kali lililomshinda kipa Soud Slim na kujaa wavuni katika dakika ya 13 ya mchezo huo.
Kabla ya bao hilo, katika dakika ya tatu ya mchezo, kipa Omar Ally wa Mtibwa aliumia vibaya na kukimbizwa hospitali baada ya kugongana na Amri Kiemba katika harakati za kuokoa hatari langoni kwake ambako nafasi yake ilichukuliwa na Slim.
Katika dakika ya 30, kiungo Salum Machaku almanusra afunge bao baada ya kumnyang'anya mpira beki Juma Jabu lakini shuti lake liligonga mwamba wa juu wa lango la Simba.
Bao hilo lilidumu hadi mwamuzi wa mchezo huo, Amon Paul, anapuliza filimbi ya mapumziko, Simba ilikuwa mbele kwa bao hilo.
Katika dakika ya 46, Amri Kiemba, alifunga bao la pili kwa mpira wa faulo iliyopigwa na Rashid Gumbo baada ya Shija Mkina kuangushwa na beki wa Mtibwa.
Katika dakika ya 52 Machaku alikosa bao la wazi kufuatia krosi safi ya Issa Rashid na katika dakika ya 55 Hussein Javu alifunga bao kwa kazi nzuri ya Machaku.
Simba ilipata bao la tatu katika dakika ya 65 lililofungwa na Mbwana Samata kwa kichwa kufuatia krosi ya Shija Mkina.
Katika dakika ya 76, Julius Mrope, na Omary Matuta waligongana hali ambayo ilisababisha Matuta kukimbizwa hospitali baada ya kuumia hadi kukimbizwa hospitalini.
Samata alifunga bao la nne kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 89 baada ya Mussa Hassan Mgosi kuchezewa vibaya na kipa Slim katika eneo la hatari, hadi filimbi ya mwisho walitoka kifua mbele kwa mabao 4-1.
Ushindi huo ni faraja kubwa kwa Simba kuelekea maandalizi ya mechi dhidi ya Yanga itakayochezwa Machi 5, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Mbali ya Simba kuhitaji ushindi kwa Yanga kwa lengo la kuongeza mtaji wa pointi katika kampeni ya kutetea ubingwa, pia kulipa kisasi cha kufungwa bao 1-0 katika mechi ya raundi ya kwanza.
Baada ya mchezo huo, kocha wa Simba Patrick Phiri aliipongeza Mtibwa kwa kuonyesha kiwango bora kwani walionyesha kutaka kuibuka na ushindi.
Phiri alimpongeza mshambuliaji wake Samata kwa kuonyesha mwelekeo wa kuwa mwiba mchungu wa mashindano mbalimbali ya kimataifa kwa kuonyesha njaa ya magoli.
Naye kocha wa Mtibwa Mkenya Tom Olaba alisema kipa ndiye tatizo lililoigharimu timu yake ingawa wachezaji wake walicheza kwa kiwango cha juu.
Olaba alisema amedhamiria kutoa elimu zaidi kwa wachezaji wa Tanzania baada ya kujiunga na timu hiyo.
Simba iliwakilishwa na Ally Mustafa, Haruna Shamte, Juma Jabu, Juma Nyoso, Joseph Owino/Meshack Abel, Jerry Santo, Hillary Echesa/Gumbo, Samata, Shija Mkina, Amri Kiemba na Nico Nyagawa/Mussa Mgosi.
Mtibwa iliwakilishwa na Omar Ally/Soud Slim, Juma Jafar, Issa Rashid, Obadia Mungusa, Salum Swed, Shaban Nditi, Julius Mrope, Masoud Mohamed, Hussein Javu, Salum Machaku, Vicent Barnabas/Omar Matuta/Yona Ndabila.
 
Yanga kuishusha Simba leo?


na Dina Ismail


amka2.gif
TIMU ya Yanga, leo inashuka dimba la Jamhuri mjini Morogoro kukwaana na Ruvu Shooting katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Yanga inashuka uwanjani kwa kazi moja tu ya kusaka ushindi ili kumshusha kileleni mtani wake Simba ambaye anaongoza kwa pointi 37.
Aidha, Yanga itakuwa ikipopotana vilivyo kushinda ili kujiweka kwenye mazingira mazuri kisaikolojia kabla ya kucheza na Simba hapo Machi 5.
Tayari kikosi cha Yanga kiliwasili jana mjini Morogoro kwa mechi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Kocha wa Yanga, Sam Timbe, alisema jana kwamba amekiandaa vema kikosi chake kuhakikisha kinashinda mchezo huo ili kupata pointi tatu muhimu ambazo zitawawezesha kukalia usukani wa ligi hiyo.
Hata hivyo, Timbe alisema anatarajia kupata upinzani mkubwa kutoka kwa wapinzani wao kwani nao wanahitaji kushinda ili kuondoka na pointi ambazo zitawaweka katika mazingira mazuri ya ligi hiyo.
Kwa upande wa Ruvu Shooting, msemaji wa timu hiyo, Masau Bwire, alisema kikosi chake kimejiandaa vema ili kuweza kushinda mechi hiyo muhimu kwao katika hatua hiyo ya lala salama.
"Si unajua ligi kwa sasa iko katika hatua za lala salama, hivyo hatuna budi kufanya vema katika michezo yetu ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kuepuka kushuka daraja," alisema.
Iwapo Yanga itashinda mechi ya leo itawashusha kileleni mahasimu wao wa jadi Simba ambao wanaongoza kwa pointi 37, wakifuatiwa na Azam wenye pointi 35 na Yanga wanaoshika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 35 pia.
 
Joseph Marwa amshinda Dusso


na Mwandishi wetu


amka2.gif
BONDIA Joseph Marwa juzi alidhihirisha umahiri wake baaba ya kumshinda kwa pointi mpinzani wake Chuku Dusso, katika raundi ya tatu kati ya sita za mpambabno huo.
Pambano hilo la uzani wa Cruiser lilifanyika katika ukumbi wa Heinken ulioko Mtoni, jijini Dar es Salaam, lilikuwa mahsusi katika kumpongeza bingwa wa dunia Karama Nyilawila.
Mwamuzi Omari Yazidu alimtangaza Marwa kama mshindi baada ya Dusso kushindwa kuendelea katika raundi ya tatu ya pambano hilo lililosimamiwa na Shirikisho la Masumbwi Tanzania (PST).
Aidha, bondia Abdallah Mohammed alimshinda George Mtagwa katika raundi ya pili ya pambano la raundi sita uzani wa Lightwelter, huku bondia Novart John, akimshinda Salum Saidi katika uzito wa Light.
Sultani Omari alimshinda Shaban Mtengela katika uzito wa Father, huku Bashir Salum akimtwanga Salum Mohammed katika uzito wa Fly.
 
TFF isicheze mbali lala salama Ligi Kuu

ban_tahariri.jpg

amka2.gif
LIGI Kuu ya bara iliyoanza tangu Agosti 21, mwaka jana kwa sasa imefikia penyewe ambapo kila moja imesaliwa na wastani wa takriban mechi sita kabla ya pazia kufungwa hapo Aprili 10.
Ni kipindi cha kushuhudia ushindani mkubwa kuliko kipindi chochote cha ligi hiyo kwa vile kila timu itakuwa ikipigania kufikia lengo kama ni kutwaa ubingwa kama si kumaliza nafasi ya pili.
Kwa mujibu wa kanuni, timu ya kwanza na ile ya pili, ndizo huiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa kwa bingwa kucheza Ligi ya Mabingwa na timu ya pili kucheza Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (Caf).
Ingawa pointi zimekuwa zikitafutwa tangu mechi ya kwanza ya ligi, ni ukweli pia, kipindi hiki ndicho unachoweza kusema ligi imefikia penyewe kwa maana ya ushindani wake, hivyo pia kuna mengi ambayo huambatana na hali hiyo.
Kwetu Tanzania Daima, tunatoa wito kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupitia Kamati yake ya Waamuzi, kufanya kila njia kuhakikisha mazingira ya ushindi wa haki, yanaendelea kutamalaki katika ligi hii.
Hakuna kingine kilichotusukuma kuandika maoni haya, isipokuwa shauku na kiu yetu ya kuona ligi hiyo yenye heshima na hadhi ya aina yake, ikitoa mshindi aliyestahili kwa uwezo wake dimbani si ujanja wa nje ya uwanja.
Tahadhari yetu inajikita katika msingi wa kutaka nchi kupata wawakilishi bora si bora wawakilishi kwa maana ya uwezo wao kisoka dimbani si ule wa kuishia kuzifunga Ruvu Shooting, AFC Arusha, Toto African na Majimaji tu, bali kufanya hivyo kimataifa pia.
Kwa miaka mingi, tumekuwa tukipata washindi ambao mwishowe huiwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa, lakini wamekuwa wakifanya vibaya kila mwaka, hivyo kama sehemu ya wadau wa soka na maendeleo kwa ujumla, tunadhani tunapaswa kubadilika.
Kubadilika huko ni kuhakikisha kunakuwepo udhibiti mkubwa dhidi ya vitendo vinavyoweza kuzalisha mabingwa waliotokana na umahiri wao wa kucheza soka
ya nje ya uwanja badala ya uwezo halisi wa kiuchezaji.

Hatusemi wawakilishi wetu wawe katika michuano ya kimataifa wamekuwa wakipatikana kwa mbinu za nje ya uwanja, hapana isipokuwa kitu muhimu ni TFF kufanya kila iwezalo nchi ipate washindi waliostahili kwa uwezo halisi wa soka.
Tunaamini kwa kufanya hivyo, soka yetu itakuwa imesimama kwenye mstari sahihi wa kuelekea kwenye mafanikio kabla ya kuangalia namba gani ya kuboresha maeneo mengine kwa mfano ya utawala na ufundi ambayo pia ni muhimu kwa maendeleo ya mchezo huo.
Tunasema haya kwa kuzingatia kuwa tunatarajia nini pale bingwa wa Ligi Kuu anapopatikana kwa ujanja wa nje ya uwanja?
Athari zake ni nyingi ikiwamo timu husika kushindwa kuhimili kishindo cha michuano ya kimataifa, ingawa ni ukweli pia si zote zinazoshindwa mapema, hazikupatikana kihalali.
Ndiyo maana tunaikumbusha TFF kuongeza umakini zaidi katika mechi za ligi hiyo ambapo sasa imefikia katika kipindi cha ushindani zaidi pengine kuliko wakati mwingi wa ligi hiyo kuelekea mwisho wa mbio.
Waamuzi ambao ni idara muhimu katika kukuza au kuua soka, wanao wajibu mkubwa wa kutimiza majukumu yao kwa misingi wa sheria, kanuni, taratibu huku wakiongozwa na msukumo wa uadilifu ili ligi ipate mshindi wa kweli.
Tunaamini kama waamuzi watatimiza wajibu huo, watakuwa wamesaidia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya mchezo huu ambapo kama ilivyo mingine, si burudani tu, bali ajira kwa vijana wenye vipaji na wengineo kama waamuzi na makocha.
Tunamaliza maoni haya tukisisitiza jambo hili kwamba TFF wafuatilie kwa karibu hatua hii ya lala salama kwani kutokana na umuhimu wa pointi iwe kuwania ubingwa au nafasi ya kucheza michuano ya kimataifa ama kuepuka kushuka daraja, kuna mengi yanayoweza kutokea.
 
Kwa hili la Gongo la Mboto, Yanga SC wamejidhalilisha
ban.mtazamo.jpg

Dina Ismail

amka2.gif
WIKI iliyopita msafara wa wachezaji na viongozi kadhaa wa klabu ya Yanga, ulifanya ziara kwa baadhi ya wananchi walioathiriwa na milipuko ya mabomu iliyotokea eneo la Gongo la Mboto, jijini Dar es Salaa usiku wa Februari 16.
Hilo ni tukio unaloweza kuliita ajali baada ya mabomu hayo kuanza kulipuka katika ghala kuu lililoko katika kambi ya 511 KJ, ambapo watu wapatao 24 walifariki na zaidi ya 300 kujeruhiwa.
Zaidi ya hapo, ajali hiyo imeacha adha kubwa kwa wakazi wa maeneo hayo kwa wengine kukosa makazi kutokana na nyumba zao kubaki vifusi na nyingine zikipata madhara.
Siku chache baada ya milipuko ile, wachezaji wa Yanga walifanya ziara ya kuwajulia hali wananchi waliopatwa na athari mbalimbali kama si kufiwa na ndugu na jamaa zao, basi walipoteza makazi yao.
Naomba niweke wazi kabla sijafika mbali katika Mtazamo wangu huu kwamba hatua ya wachezaji wale kwenda kuwatembelea wananchi wale walioko kwenye majonzi na simanzi, ni kitu cha kupongezwa na kuigwa.
Kutokana na kuguswa na hatua ile ya Yanga, baada ya kupata taarifa kuwa wachezaji na baadhi ya viongozi wangekwenda Gongo la Mboto, nilipata shauku ya kuambatana nao kwa maana ya kwenda kuripoti tukio hilo la kuigwa.
Siku iliyofuata, mimi na baadhi ya waandishi tukaenda eneo husika kwa lengo la kuchukua taarifa; awali kulikuwa na taarifa kuwa kungekuwa na usafiri kwa waandishi ambao ungeanzia makao makuu ya klabu hiyo, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Kariakoo jijiji Dar es Salaam.
Baada ya kuona usafiri huo unakawia, tuliamua kutangulia kwa lengo la kwenda kuripoti kile kinachotokea pia kama sehemu ya Watanzania kujionea kiwango cha athari zilizowapata wenzetu.
Tukiwa njiani, tulikuwa tukiwasiliana na viongozi wa Yanga ambao walitutaarifu kuwa timu ilikuwa inakuja, tulifika mida ya saa sita na kuendelea na mambo mengi huku tukisubiri ujio wa wachezaji wa Yanga.
Hatimaye wachezaji hao walifika majira ya saa nane mchana na kushusha walichokuja nacho na kukaa kando kusubiria ambapo muda ule alikuwepo Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha.
Kimsingi nakubaliana na usemi kuwa kutoa ni moyo wala si utajiri na Mwenyezi Mungu huweza kumbariki hata aliyetoa kidogo cha msingi tu awe amekitoa kwa moyo mkunjufu.
Hata hivyo kile kilichotolewa siku ile na wachezaji wa Yanga na viongozi wao kadhaa akiwemo Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Mohammed Bhinda, ni kuidhalilisha klabu hiyo kuanzia viongozi hadi wanachama wake.
Nasema hivi kutokana na kile kilichotolewa na wachezaji wa timu hiyo hakiendani hata kidogo na umaarufu na hadhi ya Yanga.
Ingawa cha bure hakina nyongeza, lakini wachezaji wa Yanga na viongozi wao, si wa kutoa katoni 10, sabuni na kalamu, vyote vikiwa na thamani kama ya sh 70,000!
Tuliambiwa kuwa wachezaji hao walichangishana fedha na kununua vitu, ni jambo zuri , lakini kwa upande mwingine haiingii akilini kwa timu kubwa kama ile kupeleka msaaada kama ule.
Hata baadhi ya wananchi waliokuwa pale waliuponda msaada ule na kudai haikustahili kuchoma mafuta ya gari na kupoteza muda wao kwenda kule, sana wangemuagiza hata dereva tu kuwawakilishia.
Kwa timu kubwa kama Yanga na umaarufu walionao wengi wa wachezaji hawakupaswa kwenda kutoa msaada wa kiwango kile na hasa ikizingatiwa uwezo walionao wachezaji hao ingawa si mkubwa sana.
Kwa mshahara, pamoja na posho wanazolipwa wachezaji wa Yanga hata kama wangechangishana sh 5,000 kila mchezaji nadhani wangepata kiasi cha fedha na kupeleka vitu vya maana kuliko walivyopeleka.
Hata uongozi nao unaonyesha ni jinsi gani haukuwa makini katika hilo kwani hata wajumbe wa kamati ya utendaji walioambatana na wachezaji hao Tito Ossoro, Bhinda na Katibu Celestine Mwesigwa walichukulia ni jambo la kawaida.
Ndio maana waandishi wa habari walipohoji udogo wa thamani ya vitu hivyo, waliambulia kejeli kwamba hata kama ni shilingi moja, yatosha kwa sababu ni msaaada tu.
Hivi kweli viongozi walio makini wanaweza kuruhusu mambo ya aibu kama hayo?
Cha kushangaza ni kwamba ziara ya Gongo la Mboto haikuwa ghafla, ilijulikana siku moja kabla, hivyo walipaswa kufanya maandalizi ya kutosha hata ya kuchangishana walau wapate cha kununua.
Siwezi kuwalaumu sana wachezaji wa Yanga kwani wale ni kama watoto, walipaswa kusimamiwa kwa maana ya kupewa mwongozo wa nini kifanyike, lakini kwa uzembe wa viongozi, aibu inaangukiwa kwa Yanga nzima.
Mimi nadhani, umefikia wakati viongozi kujua nini wanachokifanya, naamini wangejitambua wasingekubali
aibu kama ile, ambayo imeitia doa klabu nzima badala ya kuimwagia sifa.

Na huu ndio Mtazamo wangu, washkaji msijenge chuki!
 
Vodacom yapamba Kili Marathon 2011
ban.blank.jpg

Mwandishi wetu

amka2.gif
ZAIDI washiriki 2000 wa rika mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi wameshiriki katika mbio za Vodacom 5km Fun Run ambazo zimekuwa zikifana kila mwaka zikiwa ni sehemu ya mbio za kimataifa za Kilimanjaro Marathon ambazo hufanyika kila mwaka mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro.
Katika mbio hizo za kujiburudisha ambazo zimekuwa zikipata washiriki wengi kila mwaka, mwaka huu zilizidi kutia fora ambapo katika mbio hizo za jana, alikuwepo mshiriki mdogo kuliko wote.
Huyu ni kijana wa umri wa miaka mitatu huku mkubwa kuliko wote, alikuwa na umri wa miaka 70, wote walipewa zawadi maalum na Vodacom ambao walikuwa wadhamini wenza wa Kili Marathon.
Mgeni rasmi katika mbio hizo za 5km Fun Run, Mkuu wa wilaya ya Moshi Mjini Alhaji Mussa Samizi, ndiye alizindua mbio hizo mapema jana asubuhi ameipongeza Vodacom Tanzania kwa kudhamini mbio hizo.
Kutokana na umuhimu wa udhamini katika kukuza kiwango cha michezo nchini, ameiomba kampuni hiyo kudhamini mbio za watu wenye ulemavu ambazo zimesahaulika ambazo miaka miwili iliyopita zilikuwa sehemu ya mbio za Kilimanjaro, lakini ziliondolewa kwa kukosa mdhamini.
Aidha, mkuu huyo wa wilaya aliitaka Vodacom kuzidi kuboresha mbio hizo ambazo zinapendwa na watu wengi wenye rika mbali hasa watalii ambao huja kushiriki mbio hizo na kufanya utalii pia jambo ambalo linaongeza pato la taifa na wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro.
Akizungumza na waandishi baada ya mbio hizo, Mkurugenzi wa Vodacom kanda ya Kaskazini Nguvu Kamando alitoa wito kwa Watanzania kushiriki kwa wingi katika mbio hizo badala ya kuwaachia washiriki kutoka nje.
Aidha Kamando alisema kuwa Vodacom imejipanga kuboresha zaidi mbio hizo za kilometa tano ingawa sio kwa kiwango kikubwa ili kutowavutia wakimbiaji wakubwa kuhamia kwenye mbio hizo kufuta zawadi endapo zitakuwa kubwa.
Washindi wa mbio hizo za Vodacom 5km walipewa zawadi zifuatazo kwa wanaume na wanawake, mshindi wa kwanza akijinyakulia shilingi 100,000; wa pili shilingi 80,000; watatu shilingi 60,000; wanne shilingi 50,000; watano 40,000 na kuanzia mshindi wa tano mpaka wa tisa watapatiwa kifuta jasho cha shilingi 20,000 kila mmoja na kuwekewa muda wa maongezi kwenye simu zao wenye thamani ya shilingi 20,000.
"Pamoja na udhamini huu Vodacom inaamini kuwa itakuwa inaunga mkono juhudi za serikali za kunyanyua na kukuza vipaji vya wanamichezo hapa nchini ambao hapo baadaye wataweza kulitangaza taifa letu katika nyanja za michezo za kimataifa.
"Zaidi ya hayo, tunashiriki mashindano haya ikiwa ni kuunga mkono juhudi za serikali kukuza sekta ya utalii, hasa ukizingatia mashindano haya yanafanyika mkoani Kilimanjaro chini ya mojawapo ya vivutio vikuu vya utalii kama vile mlima mrefu barani Afrika, Mlima Kilimnjaro," anasema na kuongeza:
"Vodacom Tanzania itaendelea kudhamini michezo mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kukuza viwango vya michezo na hatimaye kuliletea taifa letu heshima katika mashindano ya kimataifa.

Kampuni ya Vodacom ni kati ya wadau wakubwa wa maendeleo ya michezo na jamii kwa ujumla ikiwemo kutumia fedha nyingi katika kuwekeza kwa mfano kwenye Ligi Kuu ya bara, shindano la Miss Tanzania, kuogelea, mmbio za boti na mbuzi.
 
Kwa nini muwatolee macho Kaseja na Nsajigwa?
ban.blank.jpg

Kenny Mwaisabula

amka2.gif
KARIBUNI tena wapenzi wa soka ambao kila Jumatatu huwa tunakutana katika kona ya Mwaisabula kama mtakumbuka wiki iliyopita nilizungumzia ujio wa TP Mazembe ambao ni mabingwa watetezi wa Afrika na jinsi Simba inavyotakiwa ifanye kupitia kocha wake mkuu Patrick Phiri kwa maana ya mfumo unaotumika.
Ni jambo la kufurahisha sana kwangu kwa maana nilipata pongezi nyingi za jinsi nilivyoona mfumo ule na jinsi unavyotakiwa uwe ili tuwaondoshe mashindanoni mabingwa watetezi kama vile tulivyowatoa Zamalek ya Misri mwaka 2003 nadhani sasa tuachane na haya tugeukie na mambo mengine.
Hivi karibuni mashabiki na wapenzi wa soka wamekuwa wakitoa maneno ya chinichini kuhusu umri wa Juma Kaseja na Shadrack Nsajigwa na si kuhusu viwango vyao vya uwanjani la hasha, ni kila makosa yanapotokea katika maeneo yao utasikia wanakwambia aha huyo bwana kaishakuwa mzee, kachoka, awapishe vijana na maneno mengi ambayo kimsingi yanakatisha tamaa kuendelea na kwamba ni soka la manyanyaso.
Hivyo matokeo yake wanajikuta uvumilivu umewashinda wanaamua kutundika daruga mapema mno kama walivyoacha wengine kama Suleman Matola akiwa na miaka 32 tu akaacha mpira zaidi ya miaka mitatu nyuma, wakati Ryan Giggs ana miaka 38 mashabiki wako kimya tu na ndio kwanza wanamwambia utu uzima dawa sisi tunawapigia kelele.
Wakati wa mashindano ya Tusker Challenge Cup 2010 yalipokuwa yakianza mashabiki, manazi na baadhi ya waandishi wa habari walikuwa wanaponda uwepo wa Shadrack Nsajigwa katika kikosi kile cha ‘Babu Poulsen' na ilifika mahali kila alipokuwa uwanjani mashabiki walikuwa wanangoja tu akosee halafu wapige kelele zao za toa huyo mzee, amekwisha, Babu huyooo na maneno mengi tu ya kejeli ambayo mwisho wa siku yangemkatisha tamaa.
Lakini Mungu si Athuman mwisho wa siku watu wenye akili timamu wanamchagua mchezaji bora wa michuano ile mikubwa kabisa katika ukanda wetu wa Afrika Mashariki na ya kati!
Nilianza kumfahamu Shadrack Nsajigwa akiwa kinda mwaka 2001 akiwa chini ya kocha marehemu Nzoyisaba Tauzan pale Mbeya akiwa na timu ya jeshi (44KJ), nikiwa nafundisha Bandari ya Mtwara tulifungwa bao 1-0, bao ambalo lilitokana na mpira wa mbali kabisa uliorushwa na kijana mdogo kabisa aliyeshiba dakika moja kabla ya mpira kwisha na kumkuta nadhani Shamte Ngecha aliyeutumbukza kimiani huyu si mwingine ni Shadrack wa Nsajigwa.
Leo mashabiki wanamwita mzee, wanataka wamtoe katika ulimwengu wa soka mapema mno, nasema usitoke mdogo wangu komaa tu!
Juma Kaseja leo kafungwa mechi tatu basi watu wanamtolea macho, mzee mzee mzee du makosa ya kina Meshack Abel, Juma Nyoso, Kelvin Yondani leo Kaseja anaitwa mzee!!!!! Du mi' ndio hapo nachoka kabisa Kaseja leo mzee? Huyu dogo niliyekuwa naye IPP juzi tu akiwa kinda leo mzee!!!!!
Naangalia magoli aliyofungwa Kaseja na Azam hata kama yeye kaomba msamaha ni uungwana tu ndio uliomfanya aombe msamaha lakini hakuna hata goli moja alilofungisha Kaseja kwa maana ya kufanya makosa yeye ya dhahiri kabla ya mabeki kufanya uzembe ambao hata timu yangu ya Majimatitu Mbagala haiwezi kufanya.
Na kama kuna mpenzi anabisha aingie katika mtandao wa Azam aangalie wameyaweka magoli yote yale kupitia mtaalamu wao Patrick Kahemela sioni kosa la Kaseja katika magoli yote yale, ingawa najua akili za watu zitakataa kukubali lakini ukweli ndio huo hakuna kosa linalomhusu Juma pale.
Ronaldo de Lima aliyekuwa kipenzi cha Wabrazil katika kutupia nyavuni, amestaafu mwaka huu baada ya kutimiza umri wa miaka 34 na amestaafu kutokana na maumivu na wala si kwa sababu ya uzee, mwaka 1994 pale mjini Marekani wakati Di Lima yuko katika Kombe la Dunia Juma Kaseja alikuwa kwao Kigoma anasoma Shule ya Msingi iweje leo tumwite mzee? Wakati Nsajigwa alikuwa Sekondari Lutengano kule Tukuyu, leo tunamwita mzee. Mashabiki tuache kuwatoa wachezaji wetu mapema katika ulimwengu wa soka.
Giggs ametua Man U mwaka 1991 mpaka leo ana miaka 38 bado yuko ulingoni; Paul Scholes yuko pale tangu 1994, Gary Neville yuko Man U tangu 1992 mwaka huu ndio kapewa kazi ya ukocha wa vijana. Kila nikiwaangalia Kaseja na Nsajigwa nawapa miaka kumi mbele ya kuwepo katika soka, ni kazi kwa mashabiki kulikubali hilo na kuwaunga mkono ili wafanye kazi ambayo tunajua wanaweza lakini kukosea ni jambo la kawaida tu mchezoni.
Navuta hisia nyuma nawaangalia wachezaji ambao walikuwepo miaka 2000 tu leo siwaoni: watu kama Ally Mayai, Ngade Chabanga, Abubakary Kombo, Athumani Majani, Hussen Baro, Bitta John, Aron Nyanda, Boniface Pawasa, Samson Mwamanda, Shabaan Kisiga, Said Sued, Waziri Mahadhi, Edibily Jonas Lunyamila, Suleiman Matola na wengine wengi tu ambao leo wangekuwa wanacheza hadi leo lakini mashabiki tunawatoa haraka mno katika ulimwengu wa soka.
Wote hao niliowataja hapo juu labda ukitoa Eddily walikuwa makinda wasiojulikana kabisa katika ulimwengu wa soka wakati Nonda Shabaan anafanya mambo yake Yanga Afrika miaka ya 1994 na 1995 lakini leo tunawaita wazee na Nonda bado kijana, hivi tutaendelea na utaratibu huo mpaka lini!!!!!!?
Najua wapenzi na wadau watasema tatizo ni wachezaji wenyewe wana mambo mengi wanayafanya ya nje ya uwanja ambayo yanawafanya watoke haraka katika soka mimi nasema si kweli, ni sisi ndio tunaosababisha yote hayo.
Mchezaji anapokuwa amekatishwa tamaa tena mbaya zaidi na watu wake wa karibu kabisa basi naye anakata tamaa, mashabiki na baadhi ya waandishi wa habari tunawaondoa mapema mno mashujaa wetu na mbaya zaidi vijana wanakuwa bado hawajajifunza vitu adimu toka kwa wakongwe hao.
Nawajua vizuri sana Kaseja na Nsajigwa na wanaowajua vizuri mno watanisaidia, ni wachezaji wasio na masihara wawapo uwanjani kuanzia katika mazoezi hadi katika mechi, si rahisi kuwakosa katika eneo lao la kazi yaani uwanjani, hawapatikani katika kumbi za starehe kwao kitu kinaitwa mvinyo ni kituo cha polisi; wenyewe ni zoezi na zoezi na wenyewe sasa leo mkiwakatisha tamaa wakakata tamaa unategemea nini tena!!!!?
Imefika wakati sasa mashabiki, wapenzi, viongozi, makocha na wadau wote tukajifunza ustaarabu wa kuheshimu na kuheshimiana katika kazi anayofanya mhusika na kimsingi tuangalie uwezo wa mchezaji uwanjani jinsi anavyotumika na muda ukifika wote tutaona.
Ndio maana leo hatumuoni uwanjani Sunday Manara wala Abdallah Kibaden na tuliwaona mtu kama Kitwana Manara akicheza kwa kipindi kirefu kuliko mchezaji yeyote ndani ya nchi yetu na tulimshuhudia Mkongwe Rogger Milla wa Cameroon akiunguruma hadi miaka 43 aliyofikia mzee wa Kiminyio, Madaraka Suleman.
George Masatu na Thomas Mashalla hakuna hata mchezaji mmoja leo anawafikia kwa umri hadi leo wanapiga soka Ughaibuni ambako mashabiki wetu hawako wangekuwa hapa wangezomewa sana. Kocha wangu Ngawina Ngawina wakati anasoma shule ya msingi alikuwa anamwona Mashala akicheza leo Ngawina aliitwa mzee toka mwaka 2006 ni ajabu na kweli!
Tuwaache kina Mohammed Banka, Fred Mbuna, Godfrey Bonny, Kaseja, Nsajigwa na wengineo waungurume hadi mwisho wa soka lao kelele za nini!!!!!!!?


h.sep3.gif

Mwandishi wa makala hii ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Bandari anapatikana 0652875794 au Email kennymwaisabula@yahoo.com
 
Safari Lager - Nyama Choma: Ladhamiria kuwapa walaji kilicho bora
ban.blank.jpg

Hellen Ngoromera

amka2.gif
HIVI karibuni Kampuni ya bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari imezindua shindano la nyama choma kwa mwaka huu lijulikanalo kama ‘Safari Lager Nyama Choma'.
Shindano hilo litaiwezesha baa mahiri kwa uchomaji nyama katika mikoa minne ya Dar es Salaam, Mbeya, Kilimanjaro na Arusha kujinyakulia kitita cha sh milioni moja kama motisha kwa washiriki.
Meneja wa Bia ya Safari, Fimbo Butallah, anasema shindano hilo ambalo limeshaanza rasmi, litamalizika Machi 27 mwaka huu.
Anasema katika shindano hilo, baa itakayoshika nafasi ya pili itazawadiwa sh 800,000, ya tatu 600,000, ya nne 400,000 wakati itakayoshika nafasi ya tano itaondoka na kifuta jasho cha sh 200,000.
Kwa mujibu wa Butallah madhumuni ya shindano hilo ambalo limekuwa kivutio kwa walaji wa nyama choma na watumiaji wa bia ni kuhakikisha wachomaji nyama hao wanatoa changamoto kwa majiko yao ili kuhakikisha walaji wanapata nyama bora.
Anasema ili kumpata mshindi wananchi watatakiwa kupiga kura na kupendekeza baa zitakazoingia tano bora kwa kutuma ujumbe mfupi kupitia simu zao za mkononi kwenda namba 15540.
"Kama unataka baa fulani ya mkoa wa Mbeya ishinde utatakiwa kufungua sehemu ya ujumbe mfupi na kuandika neno Safari ikifuatiwa na jina la baa," alisema meneja huyo.
Anasema mkoa wa Mbeya ndio utakaofungua dimba kwa shindano hilo kwani fainali zake zitafanyika Jumamosi ya machi 5 katika viwanja vya CCM Ilomba.
Anasema fainali hizo zitapambwa na burudani toka kwa bendi ya TOT na bendi ya Marimba ya mkoani Mbeya ambapo litawezesha washindi watano kupatikana.
Butallah anazungumzia sababu za TBL kudhamini shindano hilo kuwa ni kuhakikisha wanaleta changamoto kwa majiko yanayochoma nyama pamoja na walaji ili wapate kilicho bora.
"Na kwa kupitia bia yetu tunaamini kabisa mbali ya washiriki wa shindano lenyewe, lakini wanywaji wa Safari Lager siku zote hupenda kushusha vema vinywaji vyao kwa kupata nyama hivyo tumeona ipo haja ya kuwaburudisha na nyama choma yenye kiwango," anasema Butallah.
Anasema hali hiyo itawawezesha wachoma nyama hao kuboresha shughuli yao na kuibua vipaji vyao na kuchochea wachomaji nyama kutambua kuwa walaji wanastahili kupata nyama bora na inayokidhi viwango.
"Nyie ni mashahidi kwamba tumekuwa mstari wa mbele kuibua mashindano mbalimbali ambayo husaidia kubadili mitazamo hasi ya jamii kama vile shindano la ‘Shujaa wa Safari Lager, mashindano ya mbio za mitumbwi na mengine," anasema Fimbo.
Anasema wao kama moja ya makampuni yanayofanya biashara, huamua kubuni mashindano tofauti tofauti kwa lengo la kuirejesha faida waipatayo kwa jamii inayowazunguka na kwa kufanya hivyo hujikuta wakifanya mambo yaliyo na mguso kwa jamii hiyo.
Anasema kwa namna moja au nyingine mashindano hayo yamesaidia kuibadili jamii kwa kiasi kikubwa kutokana na watu wengi kunufaika kimaendeleo na wengine kupata mwanga zaidi kuhusu mambo mbalimbali wasiyoyafahamu.
Anasema kabla ya kuwapata washindi watano wa kila mkoa utakaoshiriki shindano hilo wahusika wa shindano hilo wataelekezwa mbinu mbalimbali kutoka kwa majaji kupitia semina elekezi.
Kwa Jiji la Dar es Salaam fainali zitafanyika Machi 3 mwaka huu katika Viwanja vya Leaders Club wakati Arusha zitafanyika Machi 26 na mkoani Kilimanjaro zitafanyika Machi 27.
Naye Jaji Mkuu wa shindano hilo Lawrence Salvi, anasema vigezo vitakavyozingatiwa kumpata mshindi ni iwapo baa itakidhi vigezo vya usafi, uchambuzi wa nyama na mambo mengine.
"Sisi kama majaji hatutatoa ushindi kienyeji bali kwa kuzingatia vigezo ambavyo washiriki watavitimiza, anasema Salvi.
Anasema kiutaalamu kuna nyama za aina nyingi hivyo mchomaji atanufaika na ushindi ikiwa atazingatia pia kigezo cha aina ya nyama atakayochoma na matunzo yake.
Hii si mara ya kwanza kufanyika kwa shindano hilo hapa nchini, kwani itakumbukwa namna lililovyojizolea umaarufu kwa washiriki na wananchi kwa ujumla tangu kuanza kwake mwaka 2008.
 
TFF, vyama vyaisusa Ligi ya Soka ya Wanawake
ban.blank.jpg

Mwandishi wetu

amka2.gif
MICHUANO ya Ligi Soka Wanawake Mkoa wa Dar es Salaam, inaendelea kwenye Uwanja wa Karume ulioko Ilala, ikishirikisha timu 11 kutoka wilaya za Ilala, Temeke na Kinondoni.
Ligi hiyo inaratibiwa na kusimamiwa na Chama cha Soka la Wanawake Mkoa wa Dar es Salaam, licha ya kwamba hakukuchezwa Ligi za kusaka wawakilishi wa kila wilaya.
Hii ni kutokana na vyama vya soka vya wilaya zote za Dar es Salaam, kushindwa kuendesha ligi za Wilaya kutokana na sababu kadhaa lakini kubwa zikidai hazina fedha za kuendesha Ligi hiyo.
Hata hivyo michuano hiyo, imekosa msisimko kutokana na mashabiki wachache kujitokeza kuingia uwanjani kushudia mechi hizo, licha ya kwamba uwanja wa Karume upo katikati ya jiji la Dar es Salaam.
Inasikitisha kuona kwamba pamoja na mechi hizo kupigwa kwenye uwanja unaomilikiwa na Shirikisho la soka nchini (TFF) lakini hakuna maofisa wa Shirikisho hilo wanaojitokeza kuzifuatilia mechi hizo.
Hili ni jambo linalokera hasa ukizingatia kuwa wanawategemea wachezaji kutoka kwenye michuano hiyo kuwatumia katika timu ya taifa ya wanawake ‘Twiga Stars'.
Kutojitokeza kwa maofisa wa TFF na wale wa vyama vya Wilaya husika IDFA, TEFA na KIFA, kunachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza mashabiki uwanjani hapo jambo linalotishia hata hatima ya maendeleo ya soka la wanawake nchini.
Kwa hili naona kauli za Rais wa TFF, Leodegar Tenga za kila mara mbele ya waandishi wa habari kwamba uongozi wake umedhamiria kukuza soka la wanawake ni porojo.
Inaonekana TFF ambayo hupokea fedha kutoka FIFA zikiwa ni kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya soka la wanawake katika nchi mbali mbali imekuwa ikizitumia fedha hizo kwa mambo mengine na sio kukuza soka kama ilivyokusudiwa.
Ushahidi wa hilo unathibitishwa na kukosekana kwa Ligi soka ya Taifa ya wanawake, huku TFF ikishindwa hata kuishawishi Mikoa yote kuendesha Ligi soka za wanawake.
Inatia simanzi ikizingatiwa kuwa, ni mwaka jana Twiga Stars iliitoa kimasomaso Tanzania, kwa kufuzu kibahati kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wanawake.
Juu ya kuletewa sifa na heshima na akina dada hao wa Twiga Stars bado TFF haionyeshi kulijali soka la wanawake, kana kwamba ni mchezo usiowahusu kabisa.
Naamini kama TFF ingeonyesha kujali soka la wanawake japo kwa kutoa kipaumbele kwenye Ligi hii iliyoanzishwa kiugumu ugumu, wadau wengi wangejitokeza kuunga mkono kwa njia mbali mbali.
Ni jambo baya kuona michuano hiyo ikichezwa bila hata ya kuwepo watu wa huduma ya kwanza kutoka Chama cha msalaba mwekundu wala askari wa kusaidia kuhakikisha usalama wa wachezaji na wote wanaoingia uwanjani hapo.
Nadhani kuna haja kwa Katibu Mkuu mpya wa TFF, Angetile Osiah, kuliangalia kwa umakini na umuhimu wa aina yake hili la Ligi soka ya wanawake vinginevyo tusitarajie kupiga hatua katika soka la wanawake.
Napenda kumwambia ndugu yangu Tenga kwamba sasa anapaswa kuacha unafiki badala yake achape kazi kwa kutekeleza kwa vitendo ahadi za kukuza soka la wanawake na vijana.
Kinyume na hivyo nafasi za uongozi alizozipata katika Baraza la Vyama vya soka Afrika Mashariki na kati (CECAFA) na sasa hii ya ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la soka Afrika (CAF), haitakuwa na maana kwake wala kwa Watanzania.



h.sep3.gif

 
Watanzania walivyochemsha Kilimanjaro Marathon 2011
ban.nachonga.jpg

Tullo Chambo

amka2.gif
MBIO za Tisa za Kimataifa za Kilimanjaro Marathon zilizofanyika jana mjini hapa, zilishuhudiwa Watanzania watatu pekee Banuelia Brighton, Mary Naali na Stephen Huche wakiingia tatu bora mbele ya Wakenya ambao waliteka vilivyo mbio hizo zilizozidi kujitwalia sifa na umaarufu mkubwa kitaifa na kimataifa.
Banuelia ambaye ndiye anashikilia rekodi ya Taifa ya Marathoni kamili kwa wanawake, ndiye aliyewafuta machozi Watanzania kwa kufanikiwa kumaliza nafasi ya pili katika mbio hizo za kilomita 42.
Binti huyo alikamata nafasi hiyo akitumia muda wa saa 3: 02.52, akitanguliwa na mshindi wa kwanza Anna Kamau wa Kenya aliyetumia saa 3:00.16 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Mkenya mwenzake Ophra Oruke aliyetumia muda wa saa 3:03.20.
Machungu yaliwazidi Watanzania mbele ya mgeni rasmi, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Emmanuel Nchimbi, pale kwa upande wa wanaume ambako nafasi ya kwanza ilienda kwa Mkenya, Kipkemboi Kipsang aliyetumia saa 2: 17.08 akifuatiwa na Julius Kilimo 2:17.10 huku nafasi ikinyakuliwa na mwanariadha anayechipukia hapa nchini, Steven Huche saa 2:19.24.
Kwa upande wa mbio za Nusu Marathon; wanawake Valentine Kipketer aliibuka kidedea akitumia saa 1:15.08 akifuatiwa na Loren Kitita 1:15.48 wote kutoka Kenya huku Mary Naali wa Tanzania akikamata nafasi ya tatu kwa kumaliza mbio hizo akitumia saa 1:15.55.
Kwa wanaume, Michael Kemau aliibuka mshindi wa kwanza akitumia saa 1:03.58 akifuatiwa na Leonard Muchare.
Nafasi ya tatu katika mbio hizo za nusu marathoni, imekwenda kwa Geofrey Ndungu saa 1:04.04, wote kutoka Kenya.
Kwa ujumla, matokeo ya mwaka huu katika mbio hizo yamekuwa mabaya kwa Tanzania ikilinganishwa na miaka iliyopita, hasa katika nusu marathoni ambapo Watanzania walikuwa wakitawala kwa kushika nafasi za juu, lakini mwaka huu imekuwa huzuni kwa Watanzania.
Washindi katika mbio hizo walizawadiwa zawadi zao na Waziri Nchimbi ambaye mbali ya kuwashukuru waandaaji kwa kumualika, pia alitoa shukrani za
pekee kwa wadhamini wakuu wa mbio hizi bia ya Kilimanjaro Premium Lager na wadhamini shirikishi kwa mchango wao katika kukuza mchezo wa riadha.

Alisema, jitihada zao za kuwekeza rasilimali na fedha katika mbio hizo zenye umuhimu mkubwa katika kukuza kiwango cha mchezo huo na kujenga uhusiano mzuri miongoni mwa wachezaji.
Nchimbi alisema, mbio hizo zimeleta faida kubwa ikiwamo kutoa nafasi kwa wanariadha wa Tanzania kujipima dhidi ya wengine wa kimataifa na hatimaye kukuza viwango.
"Mwaka ujao, mbio hizi zitafikisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake, pia kutakuwa na mashindano ya Olimpiki jijini London Uingereza. Nawaomba msituangushe, jitahidi mtuletee medali za dhahabu kwa upande wa marathoni," alisema Nchimbi na kusisitiza:
"Mwaka 2006, Samson Ramadhani alipotwaa medali ya dhahabu kwenye mashindano ya Madola yaliyofanyika Melbourne Australia, sote tulijisikia rah asana na tulifarijika sana. Nawaomba wajitokeze akina Samson wengine watuletee medali za dhahabu," alisema.

Alisisitiza kuwa, kufanya vema kwa wanamichezo wa hapa nchini Kimataifa kunawapa raha Watanzania, jambo ambalo ni muhimu kwani linawafanya Watanzania kufurahi na kusahau matatizo yao ya kawaida, mbali ya kulitangaza vema jina la nchi kimataifa.
Aidha, Waziri Nchimbi alielezea kuguswa na maoni ya wadau wakiwamo wa nje ya nchi juu utamaduni uliozoeleka kwa viongozi wengi kuthamini soka pekee, hivyo kusisitiza yeye si wa aina hiyo ni mdau wa michezo yote na kutoa wito kwa kampuni, taasisi na wadau mbalimbali kujikita katika kuwekeza katika riadha mchezo ambao umeliletea sifa taifa kimataifa.
Kwa upande wake Meneja Mawasiliano wa TBL, Emmy Oriyo, alisema kwa kuwa mwakani mbio hizo zinatimiza mwaka wa 10 tangu kuanzishwa kwake, Kilimanjaro Premium Lager inaahidi kuwekeza zaidi katika mbio hizo.
Alisema, lengo ni kuhakikisha maadhimisho ya kumi yanakuja na ongezeko la zawadi na udhamini mkubwa zaidi katika maeneo mengine yote.
"Tunatambua kwamba kukimbia marathoni ni jambo gumu sana, na changamoto kubwa, lakini tunafarijika kuona vijana wakiwa kwenye ari na msukumo wa aina yake kuhakikisha wanailetea heshima nchi yetu.
"Nawapongeza sana wanariadha wote walioweza kushiriki mbio hizi na wale wote walioshiriki kujifurahisha kwa kutuunga mkono, maana uwepo wenu ndio umefanya tukio hili kuwa kubwa kama ambavyo nyote mnajionea," alisema Oriyo.
Kwa upande wa burudani, bendi ya The African Stars Entertainment ‘Twanga Pepeta' TMK Wanaume Family na Joseph Payne ‘Mzungu wa BSS' walipagawisha vilivyo.
Mbio hizo za Kilimanjaro Marathoni zimefanyika kwa ufanisi mkubwa chini ya udhamini wa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambao ndio wadhamini wakuu.
Wadhamini shirikishi ni Vodacom Tanzania (5 km Fun Run), DT Dobie, TPC Sugar, Kilimanjaro Water, Tanzanite One, Simba Cement, Keys Hotel, Tanzanite One, Precisionair, KK Security na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), huku waratibu wakiwa ni Wild Frontiers ya Afrika Kusini na Executive Solution ya Dar es Salaam.
 
Rooney will face no action from FA


RivalsDM



PRINT RSS

106 comments »

Updated Feb 28, 2011 12:41 PM ET
Manchester United striker Wayne Rooney will face no action for his elbow on Wigan's James McCarthy on Saturday, the FA have confirmed.
Television replays from Saturday's match clearly showed Manchester United striker Rooney swipe McCarthy on the back of his head after the midfielder had appeared set to block his run.

Please install the latest version of the free Adobe Flash Player. Download now.

For help with Flash, see Adobe's Flash Player Support page.






At the time Clattenburg awarded a free-kick and, after contacting the official today, the Football Association have been told he feels he administered the appropriate action, which leaves the governing body powerless to launch disciplinary proceedings against the 25-year-old.
Professional Game Match Officials general manager Mike Riley said: "Mark took the correct course of action with this incident.
"Match officials are trained to prioritise following the ball, as that's where the greater majority of incidents are going to take place. However, we also do a lot of work around the area of peripheral vision to be aware of anything that might potentially happen off the ball.
"In this incident Mark was following play but caught sight of two players coming together and he awarded a free-kick because he believed one player had impeded the other.
"We should be clear that Mark did nothing wrong in officiating this incident as he acted on what he saw on the pitch."
Wigan manager Roberto Martinez claimed if Clattenburg had seen the incident properly the offence would have warranted a straight red card, a view endorsed later that evening on Match of the Day by Alan Hansen, who suggested Rooney was "in big trouble".
However, the disciplinary process is complex in the sense that the FA are not allowed by FIFA to take further action on incidents already dealt with by the referee.

Please install the latest version of the free Adobe Flash Player. Download now.

For help with Flash, see Adobe's Flash Player Support page.






In addition, world football's governing body frowns upon the idea that referees could go into a game believing they have a "get-out" of trial by video, as is the case in both codes of rugby, where Rooney would almost certainly have been cited given the severity of the incident.
It meant that Clattenburg would first of all have had to admit he did not see the incident and then explain exactly what he gave the free-kick for given the striker committed no other offence.
Sir Alex Ferguson will no doubt be gratified at knowing his £27million frontman will be available for Tuesday's trip to Chelsea and next weekend's encounter with Liverpool at Anfield, having claimed on Saturday the media would try to "electrocute" Rooney.
But the manner in which this case has been dealt with is bound to bring more calls for the widespread use of video technology.
Such demands reached a crescendo following last summer's World Cup final but so far FIFA president Sepp Blatter, whose organisation would have to give the green light for technology to be used, has been implacably resistant to such calls.
 
Usiri watanda kambi za Simba, Yanga Send to a friend Monday, 28 February 2011 21:00

patrick%20phiri.jpg
Kocha wa Simba Patrick Phiri

Jessca Nangawe na Clara Alphonce
SIKU nne kabla ya mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baina ya watani wa jadi, Simba na Yanga, usiri kuhusu kambi za timu hizo mbili ndio umetawala.

Kwa nyakati tofauti jana, uongozi wa klabu hizo ulieleza kuwa maandalizi yao yatakuwa ya siri zaidi, ingawa imethibitishwa kuwa Simba tayari wamekwenda Zanzibar na Yanga wataweka kambi yao Bagamoyo.

Kwa upande wake,Mwananchi iliarifiwa jana kuwa wachezaji wa Simba waliondoka jana alasiri kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kuweka kambi yao kujiandaa na mchezo dhidi ya watani zao, Yanga pamoja na maandalizi ya mechi ya kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe.

Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Evodius Mtawala aliiambia Mwananchi kuwa timu yao iliondoka jana mchana kwa ajili ya kwenda visiwani humo kujiandaa vyema na mchezo huo pamoja na maandalizi ya mchezo wao wa kimataifa dhidi ya Mazembe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) badaye mwezi huu.

Alisema timu imeondoka na wachezaji karibu wote isipokuwa wale ambao ni majeruhi na mara baada ya pambano lao na Yanga wataanza mikakati ya kukabiliana na Mazembe, Machi 20.

"Timu yetu inaondoka leo (jana) mchana na benchi zima la ufundi ambapo kama mnavyofahamu sisi tuna kazi kubwa mbili zilizoko mbele yetu, moja ikiwa kuhakikisha tunalipa kisasi kwa Yanga waliotufunga kule mjini Mwanza katika mzunguko wa kwanza.

Pili , ni kujiandaa na mchezo wa kimataifa ambao kwa sasa tunaupa umuhimu mkubwa dhidi ya Mazembe,"alisema Mtawala.

Naye makamu mwenyekiti wa klabu hiyo, Godfrey Nyange 'Kaburu' alithibitisha kuondoka kwa timu hiyo jana mchana kwa boti kwenda visiwani humo kwa ajili ya kuweka kambi kujiandaa na mchezo huo wa Jumamosi.

Alisema kuwa wachezaji wote waliondoka wakiwa chini ya kocha Patrick Phiri na benchi la ufundi na watarejea Dar es Salaam Ijumaa tayari kwa mchezo huo.

Phiri kwa upande wake alisema kuwa atazitumia dakika za mwanzo za mchezo huo Jumamosi kufanya mashambulizi ya mapema ili waweze kuichanganya safu ya ulinzi ya Yanga na kupata bao la mapema.

Kwa upande wao, Yanga ambao jana walikuwa wakicheza na Ruvu Shooting mjini Morogoro hawakuwa wazi watakaa wapi kwa mazoezi hayo.

Wao waligoma kueleza wazi wapi wataweka kambi yao huku katibu mkuu wao, Celestin Mwesingwa akisema kuwa mpaka jana walikuwa hawajui kambi hiyo wataweka wapi watajua baada ya kumalizika kwa mechi ya jana.

Hata hivyo, habari zilizopatikana jana zilieleza kuwa timu hiyo itakwenda Bagamoyo kama ilivyoripotiwa awali.
 
Carlo ready for 'important' game


RivalsDM



PRINT RSS

18 comments »

Updated Feb 28, 2011 3:47 PM ET
Carlo Ancelotti insists victory over Manchester United would be crucial to Chelsea's season, and says the Blues are in a "good moment".
A game with United at Stamford Bridge is perennially billed as a title decider but it appears all Ancelotti's men can achieve on that front on Tuesday night is to dent their opponents' bid to depose them as champions.
Chelsea go into the game a massive 15 points behind Sir Alex Ferguson's side, whose only realistic challengers now look like second-placed Arsenal.

Mon., Feb. 28
AC Milan 3-0 Napoli | Recap
Tue., Mar. 1
Chelsea vs. Man United

Wed., Mar. 2
Arsenal vs. Leyton Orient
Sat., Mar. 5
Arsenal vs. Sunderland
Man City vs. Wigan
Juventus vs. AC Milan
Sun., Mar. 6
Liverpool vs. Man United
Wolves vs. Tottenham
Lazio vs. Palermo
Inter Milan vs. Genoa
Fox Soccer Scores | Video | Photo


But with the Blues needing victory to climb back above Tottenham into fourth place, manager Ancelotti believes there is still plenty riding on the outcome on Tuesday night.
"It's a very important game for them, for us, for the future of Manchester United and the future of Chelsea," said Ancelotti, whose side put a three-match winless run behind them last week by beating FC Copenhagen in the Champions League.
"We are excited to play this game. We arrive at it at a good moment. We have confidence to do our best and win it. It won't be easy.
"United have been, until now, the best team in the Premier League.
"For us, it's important to win, not just for the result but to improve our confidence after the victory at Copenhagen, where we played very well."
Captain John Terry claimed after that win that Chelsea could yet benefit from a United meltdown.
But Ancelotti said: "United can decide their own destiny.
"Our aim is different at this moment. Our aim is still to compete with them.
"We are not mathematically out so we have to keep believing.
"But we need also to be honest, it would be difficult for us to close the gap.
"We want to arrive in the top four - this is our aim."
United are widely considered to lead the Premier League without having played particularly well for much of the season but Ancelotti was complimentary about their performances.
"They've played consistently," he said, acutely aware his side have failed to do the same.
"They've only lost one league game and are playing focused, concentrated.
"That's why they're top of the table."
For the fourth time in the last five games, Ancelotti's big selection decision revolves around whether to play Fernando Torres, Didier Drogba, or both.
Confirming only that both would "be involved" at some stage against United, Ancelotti added: "They can play together without problem. We're working on that in training.
"They don't have a problem playing with each other."
The Italian refused to be drawn on speculation about Drogba's Stamford Bridge future and once again backed the misfiring Torres to come good.
"Obviously, for a striker it's important to score," he said of the latter, who once again failed to find the net in Copenhagen.
"But, above all in the last game, he played very well.
"He had four opportunities to score and was denied by the goalkeeper and he moved very well for the team.
"He'd have preferred to score, but he will."
Nicolas Anelka appeared to seal his place in the starting line-up on Tuesday night with a deadly double against the Danes.
However, most of the Frenchman's goals have come away from home this season.
Ancelotti said: "Anelka can show his quality when he has space and, at home, it's more difficult for him to find the space.
"It depends on the behaviour of the team during the game.
"Against United, we won't have a lot of space but, if we can move well at the right time, we can find the space to counter-attack them.
"He can show his quality."



PRINT RSS




Member Comments

Please note by clicking on "add a comment" you acknowledge that you have read the Terms of Use and the comment you are posting is in compliance with such terms. Be polite. Inappropriate posts may be removed by the moderator.
LOG IN TO ADD A COMMENT Page 1 of 2 PREV PREV NEXT NEXT


Post Comment


  • Report Abuse eab60
    • 2/28/2011 9:47:03 PM
    *Chelsea player* says victory against *insert team name* is crucial to Chelsea's season. Sadly been hearing this way too often as of late. It's been the same statement over and over only with a different Blues player speaking about a different fixture every time. And they haven't lived up to it yet.
  • Report Abuse BluesFan7
    • 2/28/2011 7:41:35 PM
    I hear ya, but hey, maybe we can give city the boot & take last 2 CL's? lol
  • Report Abuse PhiladelphiaHotSpur
    • 2/28/2011 6:58:15 PM
    Sorry Blues..........I bleed red manana

    make my day and let me see Torres in teh SL and Drogba on teh pine........pretty plz ?

  • Report Abuse MyBlues3
    • 2/28/2011 6:27:46 PM
    Is it tomorrow yet?
  • Report Abuse BluesFan7
    • 2/28/2011 6:25:32 PM
    LOL.. Yes canadian, I will shine it with my booty! LOL 😛
  • Report Abuse Diosesdel10
    • 2/28/2011 5:29:39 PM
    Ancelotti is WYLD. i relaly can't wait to see him go to ROMA and make that team even more of a circus than it currently is.

    Chelsea is in a "good moment" - this GUys is a JOKEster i see

  • Report Abuse Arsenal_til_I_die
    • 2/28/2011 4:07:49 PM
    Blue - red- blue - red... Wait: didn't I see this in a Disney cartoon-movie?
    Hey UNLEASHED! how are you doing?

  • Report Abuse canadianunleashed
    • 2/28/2011 4:04:32 PM
    Catch ya tommorrow Blues..... please have the trophy nice and polish for the hand over lol
  • Report Abuse canadianunleashed
    • 2/28/2011 3:47:55 PM
    Oh of course i will be supporting my team and the colour will be red! I see the blue fading as the tide recedes 😉 unfortunately the current is heading out to trench lol Worst case scenario another red invades into the picture and by hell on high water Blues your team not gonna spoil our destiny.
  • Report Abuse BluesFan7
    • 2/28/2011 3:41:46 PM
    Yawning canadian EH? So much of a yawn you will be tuning into the game right? lol BLUE is the colour of the defending champs!... Until someone else holds the trophy... ITS BLUE !!!
LOG IN TO ADD A COMMENT Page 1 of 2 PREV PREV NEXT NEX
 
Fergie: Chelsea wametoka mbio za ubingwa Send to a friend Monday, 28 February 2011 20:55

LONDON, Uingereza

WAKATI Manchester United ikiwa mgeni wa Chelsea leo katika mchezo mgumu na muhimu kwenye Uwanja wa Stamford Brigde, tayari kocha Alex Ferguson ameiondoa Chelsea katika mbio za ubingwa msimu huu.

Mbali ya kuikabili Chelsea, Man United pia inasubiri kuivaa Liverpool, Jumapili kwenye Uwanja wa Anfield na baadaye Arsenal mwishoni mwa Aprili.

Lakini, ni Arsenal pekee ambayo kocha huyo mwenye umri wa miaka 69 ndiyo anaipa nafasi ya kuwazuia katika harakati zao wa kutwaa ubingwa wa 19 wa ligi hiyo.

Hadi sasa, Chelsea wapo nyuma ya Man United kwa pointi 15 kitu ambacho kinamfanya Ferguson aifikirie zaidi Arsenal kama wapinzani wao wakubwa.

Ferguson ambaye kwa kawaida huzungumzia mechi dhidi ya wapinzani wao, pia alipuuza maneno ya nahodha wa Chelsea, John Terry kwamba Man United itaporomoka kiwango, ingawa katika mchezo wa leo, mshambuliaji Fernando Torres anatazamwa na wengi kama ataibuka na kufunga bao la kwanza akiwa Chelsea.

"Kwa kawaida timu mbili zitafungua njia mwishoni mwa msimu na hiki ndicho kinachoonekana.

"Nafikiri itakuwa ni Arsenal ama sisi tutashinda taji, "alisema Ferguson.

Man United ambayo ilinyakua taji la ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya 18 msimu wa 2009 ikishinda leo inaweza kujiimarisha zaidi kileleni na katika mchezo wa juzi licha ya kucheza vibaya iliicharaza Wigan 4-0.

Ferguson amepuuza maneno ya Terry kwamba Man United inatakiwa kujizatiti zaidi ili kuhakikisha inashindana na presha ya uongozi wa ligi.

"Unajaribu kitu, wote tunajaribu ," aliongeza Ferguson

Aliongeza: "Ninasema na nilisema mara kadhaa siku zilizopita timu ambayo inawajibika ndiyo itakayoshinda taji na hii ndiyo sababu tunajizatiti kuona kunaendelea kuwa fiti ili tufikie malengo yetu."
 
NEC Yanga: Manji tuache Send to a friend Monday, 28 February 2011 20:55

Vicky Kimaro
KAMATI ya Utendaji ya klabu ya Yanga, kwa kauli moja imemtaka mfadhili wa klabu hiyo, Yusuf Manji kufunga virago vyake katika klabu hiyo baada ya kuomba kwa ridhaa yake kufanya hivyo.

Kikao hicho kilichokutana juzi, kilikuwa cha vuta nikuvute kilianza saa tisa mchana hadi saa tano usiku, huku zikiibuliwa hoja nzito ambazo zilisababisha wajumbe wa kikao hicho kugawanyika.
"Mwenyekiti (Lloyd Nchunga), alikuwa anataka uongozi ukamwangukie Manji ili aendelee kuidhamini Yanga, lakini baadhi ya wajumbe walitaka mfadhili huyo aondoke na kuiacha klabu hiyo mikononi mwa uongozi," kilieleza chanzo cha habari kimoja.

"Mvutano ulikuwa mkubwa, lakini makubaliano yalifikiwa na kubariki kujiondoa kwa Manji baada ya kupitia barua yake na hoja mbalimbali ambazo zilitolewa na baadhi ya wajumbe, tena wajumbe wa kamati hiyo ya utendaji wamemueleza wazi mwenyekiti kuhakikisha anatangaza yale ambayo yameamuliwa kwenye kikao na si vinginevyo.

Hivi karibuni Manji aliuandikia uongozi wa Yanga barua ya kutaka kujiondoa ndani ya klabu hiyo kwa madai kuwa amechoshwa na lawama ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake na baadhi ya wanachama kuwa yeye ndiye chanzo cha migogoro ndani ya klabu hiyo.

Katibu Mkuu wa Yanga, Selestine Mwesingwa alisema kwa kifupi: "Mambo yaliyojadiliwa ni mishahara ya wachezaji, hata hivyo mimi siwezi kuzungumzia hilo suala kwa undani, mwenyekiti atazungumzia kesho (leo), kuna vitu vinahitaji uthibitisho."
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom