Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,504
- 911,249
- Thread starter
- #9,041
TAKUKURU kumrejesha kortini Mwakalebela?
na Francis Godwin, Iringa
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) mkoani Iringa imesema kuwa leo itatoa msimamo wake wa kuirejesha upya mahakamani kesi ya rushwa inayomkabilia kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na aliyeshinda kura za maoni katika kinyang'anyiro cha ubunge jimbo la Iringa mjini, Frederick Mwakalebela.
Uamuzi huo umekuja ikiwa ni siku tatu toka Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Iringa kumwachia huru Mwakalebela katika shtaka lake la rushwa katika mchakato wa kura za maoni na kuitaka TAKUKURU kuifungua upya kesi hiyo ama la.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwanasheria wa TAKUKURU mkoani Iringa, Ntimu Mizizi, alisema uamuzi ya mahakama hiyo chini ya hakimu Festo Lwila ameyakubali na kuwa upungufu uliokuwapo awali katika kesi hiyo 4/ 2010 taasisi hiyo inaufanyia kazi na kufungua kesi yenye maelekezo ya mahakama.
Alisema uamuzi ya mahakama katika kesi hii ya Mwakalebela umeonekana ni mzuri na wenye maelekezo ya kina zaidi kuliko ilivyokuwa kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini, Joseph Mungai, ambao mahakama haikwenda kiundani zaidi kama ilivyo katika maamuzi madogo ya kesi ya Mwakalebela.
Hata hivyo alisema leo kutakuwa na majibu sahihi dhidi ya uamuzi wa TAKUKURU katika kuendelea na kesi hiyo ama la.
Mahakama iliindoa kesi hiyo na kumwachia huru Mwakalebela baada ya kuridhika na hoja ya upande wa utetezi kwamba kulikuwa na upungufu wa kisheria kwenye hati ya mashtaka.
Mapungufu hayo ni mtuhumiwa kushtakiwa kwa makosa mawili kwenye hati moja ya mashtaka na hivyo kumfanya mtuhumiwa ashindwe kuelewa kwa usahihi kosa linalomkabili.
na Francis Godwin, Iringa
Uamuzi huo umekuja ikiwa ni siku tatu toka Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Iringa kumwachia huru Mwakalebela katika shtaka lake la rushwa katika mchakato wa kura za maoni na kuitaka TAKUKURU kuifungua upya kesi hiyo ama la.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mwanasheria wa TAKUKURU mkoani Iringa, Ntimu Mizizi, alisema uamuzi ya mahakama hiyo chini ya hakimu Festo Lwila ameyakubali na kuwa upungufu uliokuwapo awali katika kesi hiyo 4/ 2010 taasisi hiyo inaufanyia kazi na kufungua kesi yenye maelekezo ya mahakama.
Alisema uamuzi ya mahakama katika kesi hii ya Mwakalebela umeonekana ni mzuri na wenye maelekezo ya kina zaidi kuliko ilivyokuwa kwa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Mufindi Kaskazini, Joseph Mungai, ambao mahakama haikwenda kiundani zaidi kama ilivyo katika maamuzi madogo ya kesi ya Mwakalebela.
Hata hivyo alisema leo kutakuwa na majibu sahihi dhidi ya uamuzi wa TAKUKURU katika kuendelea na kesi hiyo ama la.
Mahakama iliindoa kesi hiyo na kumwachia huru Mwakalebela baada ya kuridhika na hoja ya upande wa utetezi kwamba kulikuwa na upungufu wa kisheria kwenye hati ya mashtaka.
Mapungufu hayo ni mtuhumiwa kushtakiwa kwa makosa mawili kwenye hati moja ya mashtaka na hivyo kumfanya mtuhumiwa ashindwe kuelewa kwa usahihi kosa linalomkabili.
PRINT