Michango ya Wabunge, maswali na majibu ya Mawaziri ubora wake uko chini kabisa

Zygot

JF-Expert Member
Apr 14, 2016
2,240
2,866
Sielewi ni kwa sababu gani hali iko hivi, lakini ni wazi kwamba ubora wa walioko mjengoni uko chini. Watu wanashindwa hata kuunda maswali yanayostahili kuulizwa bungeni. Maswali mengi ni ya kuulizia miradi ya shule, urefu wa barabara, visima vya maji, n.k. vya kiwango cha wilaya na majimbo. Swali linalohusu jimbo moja linapewa sapoti na mwingine akisema, hata jimboni kwangu ni hivyo!

Sikiliza majawabu ya serikali sasa! Taaabu! Kila kinachosemwa na waziri, kinaitwa ni jawabu lakini ukweli ni kwamba mengi hayana maana kwa mwananchi wa kawadia. Tunachosikia ni vijimaneno na kuchanganya na viingereza ili tujue waziri lugha inapanda: Mtu unajibu swali la kilimo, linalowahusu wakulima wa Tanzania unaweka mipango yako kwa vijiingereza vilivyotawaliwa na matamshi ya Kiswahili!

Wenzangu mumewasikia wachangiaji wa wizara ya elimu? Taabu kabisa. Nahisi wengi wanasaka maneno yenye nadharia fulani vitabuni halafu wanakuja kwa kuvuta hewa kwa nguvu, wakitaka serikali iwasikilize; Elimu inahitaji mabadiriko, mitaala ibadirike, angalia wenzetu ulaya, elimu haiko sawa, haiwapi uwezo wa kujitegemea.

Hili siyo Bunge la miaka 60 baada ya uhuru. Wapo maprofesa kama Kabudi, atakapoanza kujibu kwa mtindo wa kufundisha kama alivyokuwa anafanya bunge liliopita, ajue hakuna wanafunzi wa kuelewa.
 
Hawa watu wangekua wanapigwa drill ya interviews kabla ya kufikia huko. Imagine bongo hakuna kazi yakipuuzi isiyo na competence test kama ubunge na uwaziri hadi huko udc ukurugenzi.

Likewise nafasi za uteuzi hizi na hisani kwa hiyo unaeza ukawa una uwezo ukatupwa nje, au huna uwezo ukatumia pesa ama princelings na undugulization.

Fikiria waziri anakua hajapitia a single drill of interview popote pale tofauti na kupendekezwa na mkuu wake wa kazi na chama.
 
Ukitaka kujua ni kwa nini JPM alikuwa anajiamulia yeye mwenyewe badala ya kutegemea maamuzi ya Bunge, wasikilize watu kama hawa. Ni watu ambao wako ignorant, halafu wanajadili mambo meeengi wanayoyatoa mitandaoni na kujidai ndo mapungufu yetu au ufumbuzi wa matatizo yetu. Mawaziri ndo hao wanapanga mambo kama vijana wa form six.

Ni kweli nimemsikia mara nyingi waziri kama Bashe anapenda sana kuchanganya maneno ya kiingereza kwenye majibu yake inagawa kwa matamshi hayo sidhani kama lugha inampenda. ni mtu ambaye anataka kuaminisha watu kwamba ana uwezo. That is not!
 
Back
Top Bottom