Zimmermann
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 2,790
- 1,232
Walipasua daraja la kwanza kidato cha sita
Wazawadiwa kitita cha fedha, kompyuta
Watambulishwa bungeni, Bunge larindima
Wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka jana wakiwa Bungeni ambapo walizawadiwa jana bungeni mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Katika jitihada za kutaka kufufua ari ya wanafunzi kusoma kwa bidii na kujenga utamaduni mpya wa kutambua juhudi za kuendeleza elimu ya taifa, Serikali jana iliweka historia kwa kuwapongeza na kuwazawadia wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka jana.
Wanafunzi hao walizawadiwa jana bungeni mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Pinda alisema serikali ina lengo la kuanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani yao ya sekondari kwenye vyuo vya elimu ya juu vya nje ya nchi.
Waziri Mkuu aliyasema hayo wakati Bunge lilipowapongeza wanafunzi hao 20 waliofanya vizuri katika mitihani yao mwaka huu.
Alisema ameiagiza Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kukaa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuangalia utaratibu huo wa kupongeza kuwa wa kudumu.
Nimeiagiza Tamisemi kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu kuhakikisha unakuwepo utaratibu huu uwe wa kudumu na ikiwezekana hata wale wa vyuo vikuu nao wanaofanya vizuri waweze kutambuliwa kama hawa.
Nia yetu ni kufanya mfuko maalum ambao utawawezesha wanafunzi hawa kusoma katika vyuo vikuu vya nje ya nchi, alisema.
Aidha, Pinda alisema wanafunzi saba wamethibitisha kuwa uamuzi wa Serikali wa kujenga shule za kata ulikuwa ni uamuzi na utabaki kuwa uamuzi sahihi.
Alisema kama shule hizi zisingekuwepo huenda vijana hao wasingeweza kuonyesha uwezo wao kitaaluma kama walivyofanya katika mitihani yao hiyo ya kidato cha sita hususan wasichana.
Alisema pia kufanya vizuri kwa wanafunzi hao kumeonyesha kuwa changamoto zilizopo zikitatuliwa wanaweza kufanya vizuri zaidi.
Alisema ni jukumu la Serikali kuendelea kuziboresha shule hizo na kuwatia moyo walimu na wanafunzi wao ili waendelee kufundisha na kujifunza kwa bidii.
Katika hafla hiyo, Pinda alitangaza zawadi kwa wanafunzi hao 20 kuwa ni kompyuta aina ya Lap Top na Sh. 150,000 pamoja na Cheti cha Ubora kwa kila mwanafunzi aliyealikwa jana.
Pia zimetolewa Sh. 500,000 pamoja na Cheti kwa Walimu 31 wa A-level waliowafundisha wanafunzi hao.
Pinda alisema Serikali imetoa Sh. milioni moja pamoja na cheti kwa kila shule walikosoma wanafunzi hao na meza ya maabara yenye thamani ya Sh. milioni tano.
Kadhalika, shule zote za kata saba ambazo wamesoma wanafunzi hao walikabidhiwa cheti.
Awali, waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema wanafunzi sita kati ya 10 kwa upande wa wasichana walifanya vizuri katika masomo ya sayansi. Alisema pia, wavulana wanane walifanya vizuri katika masomo ya sayansi.
Aliongeza kuwa wasichana sita kati ya 10 wanatoka shule za serikali, wanne wanatoka shule binafsi.
Kwa upande wa wavulana, wanafunzi sita nao wametoka shule za serikali na wanne shule binafsi.
Kati ya vijana hao, vijana saba walitajwa kuwa walimaliza kidato cha sita katika shule za kata ambazo nazo zilipewa zawadi kutokana na kuonyesha mfano mzuri.
Wanafunzi waliozawadiwa, ni Muhagachi Chacha ( Kibaha), Samwel Katwale (Mzumbe), Amir Abdallah (Feza Boys), Aron Gerson (Tabora Boys), Shaban Omary (Tabora Boys), Kudra Baruti (Feza Boys), George Assenga (Majengo), Comman Nduru (Feza Boys), Francis Joseph (Tabora Boys), George Felix (Mzumbe) na Doreen Kabuche (Benjamin W. Mkapa).
Wengine ni Rahabu Mwangamba (Kilakala), Mary Mosha (Kifungilo Girls), Nuru N. Kipato (Marian Girls), Zainabu Hassan (Al-Muntazir Islamic), Catherine E. Temu (Ashira Girls), Anthonia J. Lugomo (Usongwe), Cecilia Mviile (Kifungilo Girls), Mariam Matovolwa (Kilakala) na Suzan Makoi (Tarakea).
Wanafunzi ambao walizawadiwa na Waziri Mkuu ambao walisoma katika shule za kata katika masomo yao ya kidato cha kwanza hadi cha sita ni Samweli Katwale kutoka Sekondari ya Bukwande (Magu), Francis Josephat kutoka Sekondari ya Inchugu (Tarime), Rahabu Mwangamba kutoka Sekondari ya Vwawa (Mbeya), Zainabu Hassan kutoka Sekondari ya Uhuru (Shinyanga), Mariam Matovolwa kutoka Sekondari ya Kikuyu (Dodoma), Suzana Makoi kutoka Sekondari ya Tarakea (Rombo) na Anthonia Lugomo wa Sekondari ya Usongwe (Mbozi).
Wakitoa maoni yao kuhusu utaratibu huo wa Bunge na serikali kuwatambua wanafunzi waliofanya vizuri, baadhi ya wabunge walisema utaratibu huo utahamasisha wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao.
Mbunge wa Vunjo, (TLP), Augustine Mrema, alisema hilo ni jambo zuri kwa vile linawapa motisha wanafunzi na wenzao wanaoendelea na masomo.
Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Suzan Kiwanga, alisema ana wasiwasi na shule zilizotajwa kuwa si za kata kwa kuwa baadhi yake zimekuwepo kabla kuanzishwa kwa shule za kata.
Alisema wanaendelea kufanya utafiti zaidi ili kubaini kama kweli wanafunzi hao walimaliza masomo yao ya kidato cha nne katika shule za kata.
Mbunge wa Kibakwe (CCM), George Simbachawene, alisema tukio hilo ni zuri linachochea wengine kufanya vizuri katika mitihani yao.
Mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele, alisema amefurahi kwa kuwa mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri ametoka mkoani mwake.
Alitoa wito kwa wananchi kuziunga mkono shule hizo ili zifanye vizuri na kwamba ni matumaini yake kuwa zikifanyiwa marekebisho zitakuwa shule bora zaidi.
Mbunge wa Lulindi (CCM), Jerome Bwanausi, alisema kuwa ni changamoto kubwa kwa wanafunzi waliobaki katika shule hizo kufanya vizuri katika masono yao ili nao wapongezwe na kuzawadiwa kama wenzao.
Mbunge wa Rombo, (Chadema), Joseph Selasini, alisema kuwa ni jambo zuri kwa sababu wanafunzi wanaobakia shuleni wanapata moyo wa kufanya vizuri katika masomo yao.
Hata hivyo, alisema shule nyingi hazina vitabu, walimu na maabara na kutaka changamoto hizo zipatiwe ufumbuzi wa kina bila kubweteka.
Meneja wa Kitengo cha Habari cha Shirika lisilo la kiserikali la Haki Elimu, Nyanda Shuli, alikipongeza kitendo cha Waziri Mkuu kuwapongeza na kuwapatia zawadi vijana waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita ya mwaka huu.
Shuli alisema kutoa zawadi kwa mtu yeyote aliyefanya vizuri ni kitendo cha kutambua juhudi zake na kumhamasisha aendelee na juhudi zake hizo.
Aidha, alisema kitendo hicho pia kinawapa changamoto wanafunzi wengine ya kujibidisha katika masomo yao ili wafanye vizuri na hatimaye waweze kuzawadiwa kama walivyofanyiwa wenzao hao.
Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, alisema:
Kumzawadia mtu baada ya kufanya vizuri ni jambo jema, lakini kama CWT ugomvi wetu wa muda mrefu na serikali ni kuweza kuwatafutia zawadi walimu wote kwa kuwaboreshea mazingira mazuri sehemu zao za kazi, kwani zawadi kwa kikundi kidogo sio kuboresha elimu.
Aliongeza kuwa ili sekta ya elimu ifanye vizuri zaidi serikali inatakiwa kuwaboreshea walimu mishahara yao, vitendea kazi, maeneo ya kuishi pamoja na vivutio vingine.
Ikiwa serikali itaweza kuboresha vitu hivi vitatu sekta ya elimu itafanya vizuri zaidi kinyume cha hapo kutoa zawadi kwa watu wachache huku kundi kubwa likiwa limeachwa nyuma sio kuboresha elimu, alisema.
Mkuu wa Kitivo cha Elimu Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), Dk. Honoratha Mushi, aliunga mkono maamuzi ya kuwatunukia zawadi wanafunzi waliofanya vizuri.
Dk. Mushi alisema zawadi hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuwahamasisha wanafunzi wengine kufanya vizuri katika masomo yao.
Motisha hii ni nzuri na pia itasaidia kwa wanafunzi wengine kuhamasika kufanya vizuri katika mitihani yao huku wakijua wanapatiwa zawadi, alisema na kuongeza kuwa jambo la muhimu ambalo linatakiwa kuzingatiwa kwa wanafunzi ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na uelewa wa elimu ili iwasaidie katika maisha yao.
Alisema baadhi ya changamoto zinatakiwa kufanyiwa kazi ikiwemo marekebisho ya mitaala ya elimu ilenge kumsaidia mwanafunzi.
Imeandikwa, Sharon Sauwa na Muhibu Said (Dodoma) na Raphael Kibiriti, Romana Mallya na Beatrice Shayo (Dar).
CHANZO: NIPASHE
Wanafunzi 20 waliofanya vizuri katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka jana wakiwa Bungeni ambapo walizawadiwa jana bungeni mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Katika jitihada za kutaka kufufua ari ya wanafunzi kusoma kwa bidii na kujenga utamaduni mpya wa kutambua juhudi za kuendeleza elimu ya taifa, Serikali jana iliweka historia kwa kuwapongeza na kuwazawadia wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa Taifa wa kidato cha sita mwaka jana.
Wanafunzi hao walizawadiwa jana bungeni mjini Dodoma na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Pinda alisema serikali ina lengo la kuanzisha mfuko maalum kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani yao ya sekondari kwenye vyuo vya elimu ya juu vya nje ya nchi.
Waziri Mkuu aliyasema hayo wakati Bunge lilipowapongeza wanafunzi hao 20 waliofanya vizuri katika mitihani yao mwaka huu.
Alisema ameiagiza Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kukaa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuangalia utaratibu huo wa kupongeza kuwa wa kudumu.
Nimeiagiza Tamisemi kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu kuhakikisha unakuwepo utaratibu huu uwe wa kudumu na ikiwezekana hata wale wa vyuo vikuu nao wanaofanya vizuri waweze kutambuliwa kama hawa.
Nia yetu ni kufanya mfuko maalum ambao utawawezesha wanafunzi hawa kusoma katika vyuo vikuu vya nje ya nchi, alisema.
Aidha, Pinda alisema wanafunzi saba wamethibitisha kuwa uamuzi wa Serikali wa kujenga shule za kata ulikuwa ni uamuzi na utabaki kuwa uamuzi sahihi.
Alisema kama shule hizi zisingekuwepo huenda vijana hao wasingeweza kuonyesha uwezo wao kitaaluma kama walivyofanya katika mitihani yao hiyo ya kidato cha sita hususan wasichana.
Alisema pia kufanya vizuri kwa wanafunzi hao kumeonyesha kuwa changamoto zilizopo zikitatuliwa wanaweza kufanya vizuri zaidi.
Alisema ni jukumu la Serikali kuendelea kuziboresha shule hizo na kuwatia moyo walimu na wanafunzi wao ili waendelee kufundisha na kujifunza kwa bidii.
Katika hafla hiyo, Pinda alitangaza zawadi kwa wanafunzi hao 20 kuwa ni kompyuta aina ya Lap Top na Sh. 150,000 pamoja na Cheti cha Ubora kwa kila mwanafunzi aliyealikwa jana.
Pia zimetolewa Sh. 500,000 pamoja na Cheti kwa Walimu 31 wa A-level waliowafundisha wanafunzi hao.
Pinda alisema Serikali imetoa Sh. milioni moja pamoja na cheti kwa kila shule walikosoma wanafunzi hao na meza ya maabara yenye thamani ya Sh. milioni tano.
Kadhalika, shule zote za kata saba ambazo wamesoma wanafunzi hao walikabidhiwa cheti.
Awali, waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema wanafunzi sita kati ya 10 kwa upande wa wasichana walifanya vizuri katika masomo ya sayansi. Alisema pia, wavulana wanane walifanya vizuri katika masomo ya sayansi.
Aliongeza kuwa wasichana sita kati ya 10 wanatoka shule za serikali, wanne wanatoka shule binafsi.
Kwa upande wa wavulana, wanafunzi sita nao wametoka shule za serikali na wanne shule binafsi.
Kati ya vijana hao, vijana saba walitajwa kuwa walimaliza kidato cha sita katika shule za kata ambazo nazo zilipewa zawadi kutokana na kuonyesha mfano mzuri.
Wanafunzi waliozawadiwa, ni Muhagachi Chacha ( Kibaha), Samwel Katwale (Mzumbe), Amir Abdallah (Feza Boys), Aron Gerson (Tabora Boys), Shaban Omary (Tabora Boys), Kudra Baruti (Feza Boys), George Assenga (Majengo), Comman Nduru (Feza Boys), Francis Joseph (Tabora Boys), George Felix (Mzumbe) na Doreen Kabuche (Benjamin W. Mkapa).
Wengine ni Rahabu Mwangamba (Kilakala), Mary Mosha (Kifungilo Girls), Nuru N. Kipato (Marian Girls), Zainabu Hassan (Al-Muntazir Islamic), Catherine E. Temu (Ashira Girls), Anthonia J. Lugomo (Usongwe), Cecilia Mviile (Kifungilo Girls), Mariam Matovolwa (Kilakala) na Suzan Makoi (Tarakea).
Wanafunzi ambao walizawadiwa na Waziri Mkuu ambao walisoma katika shule za kata katika masomo yao ya kidato cha kwanza hadi cha sita ni Samweli Katwale kutoka Sekondari ya Bukwande (Magu), Francis Josephat kutoka Sekondari ya Inchugu (Tarime), Rahabu Mwangamba kutoka Sekondari ya Vwawa (Mbeya), Zainabu Hassan kutoka Sekondari ya Uhuru (Shinyanga), Mariam Matovolwa kutoka Sekondari ya Kikuyu (Dodoma), Suzana Makoi kutoka Sekondari ya Tarakea (Rombo) na Anthonia Lugomo wa Sekondari ya Usongwe (Mbozi).
Wakitoa maoni yao kuhusu utaratibu huo wa Bunge na serikali kuwatambua wanafunzi waliofanya vizuri, baadhi ya wabunge walisema utaratibu huo utahamasisha wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani yao.
Mbunge wa Vunjo, (TLP), Augustine Mrema, alisema hilo ni jambo zuri kwa vile linawapa motisha wanafunzi na wenzao wanaoendelea na masomo.
Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) Suzan Kiwanga, alisema ana wasiwasi na shule zilizotajwa kuwa si za kata kwa kuwa baadhi yake zimekuwepo kabla kuanzishwa kwa shule za kata.
Alisema wanaendelea kufanya utafiti zaidi ili kubaini kama kweli wanafunzi hao walimaliza masomo yao ya kidato cha nne katika shule za kata.
Mbunge wa Kibakwe (CCM), George Simbachawene, alisema tukio hilo ni zuri linachochea wengine kufanya vizuri katika mitihani yao.
Mbunge wa Shinyanga Mjini (CCM), Stephen Masele, alisema amefurahi kwa kuwa mmoja wa wanafunzi waliofanya vizuri ametoka mkoani mwake.
Alitoa wito kwa wananchi kuziunga mkono shule hizo ili zifanye vizuri na kwamba ni matumaini yake kuwa zikifanyiwa marekebisho zitakuwa shule bora zaidi.
Mbunge wa Lulindi (CCM), Jerome Bwanausi, alisema kuwa ni changamoto kubwa kwa wanafunzi waliobaki katika shule hizo kufanya vizuri katika masono yao ili nao wapongezwe na kuzawadiwa kama wenzao.
Mbunge wa Rombo, (Chadema), Joseph Selasini, alisema kuwa ni jambo zuri kwa sababu wanafunzi wanaobakia shuleni wanapata moyo wa kufanya vizuri katika masomo yao.
Hata hivyo, alisema shule nyingi hazina vitabu, walimu na maabara na kutaka changamoto hizo zipatiwe ufumbuzi wa kina bila kubweteka.
Meneja wa Kitengo cha Habari cha Shirika lisilo la kiserikali la Haki Elimu, Nyanda Shuli, alikipongeza kitendo cha Waziri Mkuu kuwapongeza na kuwapatia zawadi vijana waliofanya vizuri katika mitihani ya kidato cha sita ya mwaka huu.
Shuli alisema kutoa zawadi kwa mtu yeyote aliyefanya vizuri ni kitendo cha kutambua juhudi zake na kumhamasisha aendelee na juhudi zake hizo.
Aidha, alisema kitendo hicho pia kinawapa changamoto wanafunzi wengine ya kujibidisha katika masomo yao ili wafanye vizuri na hatimaye waweze kuzawadiwa kama walivyofanyiwa wenzao hao.
Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba, alisema:
Kumzawadia mtu baada ya kufanya vizuri ni jambo jema, lakini kama CWT ugomvi wetu wa muda mrefu na serikali ni kuweza kuwatafutia zawadi walimu wote kwa kuwaboreshea mazingira mazuri sehemu zao za kazi, kwani zawadi kwa kikundi kidogo sio kuboresha elimu.
Aliongeza kuwa ili sekta ya elimu ifanye vizuri zaidi serikali inatakiwa kuwaboreshea walimu mishahara yao, vitendea kazi, maeneo ya kuishi pamoja na vivutio vingine.
Ikiwa serikali itaweza kuboresha vitu hivi vitatu sekta ya elimu itafanya vizuri zaidi kinyume cha hapo kutoa zawadi kwa watu wachache huku kundi kubwa likiwa limeachwa nyuma sio kuboresha elimu, alisema.
Mkuu wa Kitivo cha Elimu Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), Dk. Honoratha Mushi, aliunga mkono maamuzi ya kuwatunukia zawadi wanafunzi waliofanya vizuri.
Dk. Mushi alisema zawadi hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kuwahamasisha wanafunzi wengine kufanya vizuri katika masomo yao.
Motisha hii ni nzuri na pia itasaidia kwa wanafunzi wengine kuhamasika kufanya vizuri katika mitihani yao huku wakijua wanapatiwa zawadi, alisema na kuongeza kuwa jambo la muhimu ambalo linatakiwa kuzingatiwa kwa wanafunzi ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na uelewa wa elimu ili iwasaidie katika maisha yao.
Alisema baadhi ya changamoto zinatakiwa kufanyiwa kazi ikiwemo marekebisho ya mitaala ya elimu ilenge kumsaidia mwanafunzi.
Imeandikwa, Sharon Sauwa na Muhibu Said (Dodoma) na Raphael Kibiriti, Romana Mallya na Beatrice Shayo (Dar).
CHANZO: NIPASHE