Miaka ya Urais ipunguzwe toka 5 hadi 4

Miaka ya Urais ipunguzwe toka 5 hadi 4

Sasa kama mmepata Rais wa hovyo, hiyo miaka 7 itakuaje?
Machineries za kumuweka sawa Rais wa hivyo kuwa Rais anayefaa zipo. Vinginevyo, tujadili hizo machineries kama ndizo za hovyo, na tufikirie plan na utekelezaji wa kuzirekebisha ziwe zinazofaa.
 
Kadri tunavyo badiri viongozi mara nyingi tunapata mawazo mapya na kadri kiongozi anavyo zidi kukaa madarakani ndivyo anavyo fanya mambo ya hovyo.

Ni wakati sasa Tanzania kubadiri utaratibu wa miaka 5 uwe wa miaka 4 kama ilivyo USA na vipindi viwili vibakie kama vilivyo sasa.

Na umri wa kuwa Rais uanzie miaka 35 badala ya 40 na mwisho kugombea Urais iwe miaka 60 kama anagombea kwa mara ya kwanza.

Mabadiriko yoyote ya katiba yasifanyike kama bunge linalo takiwa kufanya mabadiriko yoyote ya kuongeza muda wa kukaa madarakani halina 40% ya wabunge wa upinzani.

Pia Makama wa Rais asiruhusiwe kuongoza nchi zaidi ya mwaka 1 kama ikitokea Rais anafariki.. baada ya mwaka mmoja uchaguzi unatakiwa kuitishwa haraka.

Heri ya Mwaka Mpya.
🚮🚮🚮
 
Machineries za kumuweka sawa Rais wa hivyo kuwa Rais anayefaa zipo. Vinginevyo, tujadili hizo machineries kama ndizo za hovyo, na tufikirie plan na utekelezaji wa kuzirekebisha ziwe zinazofaa.
Watanzania wote tuna nafasi ya kuongoza, miaka 4 ni mingi sana kwa Rais anaye jitambua
 
Hata hiyo miaka 4 ni mingi sana iwe tu 3 inatosha sana katiba sio Bible.
 
Rais aondolewe kinga. Akifanya mambo ya hivyo apandishwe mahakamani baada ya kuachia madaraka.

Mahakama na Bunge viwe vyombo huru.
 
Kwenye umri wa kugombea miaka 35 duu, kuna watu wana 45 yrs lakini hawezi kuongoza hata ndoa yake au mkewe akipishana tu na mkewe simu kwa dada zao huyu mwanamke anataka kuniua njaa hanipi chakula haa haa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] sasa huyo akipewa nchi au PM [emoji3][emoji3] si atakuwa analia tuu ha ha ha jamani
 
Una hoja nzuri na Ubunge uwe mhula mmoja tu wa 4yrs ili watu wapunguze kulogana.
Sasa ukiwa mhula mmoja tu, mtu akipata nafasi hiyo hatafanya lolote, zaidi yakurudisha pesa alizohonga kofia na kanga
 
Hapana...! Miaka mitatu huwezi kufanya kitu chakueleweka na kikasimama. Vinginevyo, Urais iwe symbolic title tu, hivyo tubadili katiba na tuwe na msimamizi Mkuu wa masuala ya serikali kwa muda huo nilotaja wa miaka 7 ikijumuisha kuandaa serikali kufanya kazi, kukabidhi madaraka na masuala ya Uchaguzi.

Chaguzi za mara kwa mara (Tena ndani ya muda mfupi) ni ufujaji wa fedha za maendeleo ya watu kwa kisingizio cha gharama ya demokrasia. Na fedha hizi zikikusanywa za uchaguzi nyingi zinasombwo na kwenda kuwekezwa Nje ya nchi. Sasa inamaana gani kwa Wananchi wanaolitumikia Taifa kwa uaminifu?
Miaka 7 imekuwa ndoa ? Miaka 5 tu angalia inavyotutesa halafu ukaongeze 2 ? Hapana afadhali ipunguzwe
 
Watanzania wote tuna nafasi ya kuongoza, miaka 4 ni mingi sana kwa Rais anaye jitambua
Rejea majukumu ya Rais kwenye Katiba. Kisha upime kama hiyo miaka miwili (kama unataka muhula wa miaka 4) inatosha. Ukipendeza miaka minne maana yake unapendekeza Rais kufanya kazi miaka 2 effectively; endapo utazingatia sababu nilizotoa katika mabandiko yangu yaliyopita kwenye uzi huu.
 
Miaka 7 imekuwa ndoa ? Miaka 5 tu angalia inavyotutesa halafu ukaongeze 2 ? Hapana afadhali ipunguzwe
Mitano haitutesi....bali machineries ndiyo uzilaumu kama Kuna mateso umeyabaini !!!
 
Sasa ukiwa mhula mmoja tu, mtu akipata nafasi hiyo hatafanya lolote, zaidi yakurudisha pesa alizohonga kofia na kanga
Lengo watu wasifanye Siasa kuwa Ajira watu wafikirie kuwa HUDUMA.
 
Hata ukiwa mwaka mmoja hakuna litakalobadirika.

Maendeleo hayaletwi kwa kifungo cha idadi miaka wala muda wa kutawala.

Mtu kama hana maono wala mindset ya utawala na kufikiri maendeleo atayaleta vipi, hata mumpe billions of money atawale kwa muda mfupi ni kazi bure.

La msingi ni kupata mtu sahihi tu na sio hizo sheria za kijinga jinga, tena mkiweka muda mfupi ndio itaongeza upigaji na unyonyaji maana kila mwanasiasa atataka aguse kiti cha urais japo kwa muda mfupi apige apite kushoto maana hamtamlaumu kwa kisingizio alitawala muda mfupi.

Solution ni kupata kiongozi sahihi ambaye hata mkimpa uongozi wa milele hamtajutia kwakuwa analeta maendeleo
 
Kadri tunavyo badiri viongozi mara nyingi tunapata mawazo mapya na kadri kiongozi anavyo zidi kukaa madarakani ndivyo anavyo fanya mambo ya hovyo.

Ni wakati sasa Tanzania kubadiri utaratibu wa miaka 5 uwe wa miaka 4 kama ilivyo USA na vipindi viwili vibakie kama vilivyo sasa.

Na umri wa kuwa Rais uanzie miaka 35 badala ya 40 na mwisho kugombea Urais iwe miaka 60 kama anagombea kwa mara ya kwanza.

Mabadiriko yoyote ya katiba yasifanyike kama bunge linalo takiwa kufanya mabadiriko yoyote ya kuongeza muda wa kukaa madarakani halina 40% ya wabunge wa upinzani.

Pia Makama wa Rais asiruhusiwe kuongoza nchi zaidi ya mwaka 1 kama ikitokea Rais anafariki.. baada ya mwaka mmoja uchaguzi unatakiwa kuitishwa haraka.

Heri ya Mwaka Mpya.
Tubadiri= tubadili, Hoja yako ina mashiko, kwa huu uongozi mbovu wa maza mi natama iwe miaka 2 na nusu tu
 
Siungi Mkono kupunguza muhula wa Rais bali nashauri uongezwe hadi miaka Saba.

Mwaka mmoja wa kuandaa serikali kufanya kazi, mwaka mwingine wa kuandaa kukabidhi serikali na maandalizi ya chaguzi. Miaka mitano kamili kwa ajili ya kutekeleza kwa uaminifu mkubwa ahadi alizoaihidi kwa wale waliomuamini na kumpa madaraka.
Hawajui kuwa mambo ya kiserikali si kama shule wala kijiji kwamba uamke tu na uanze utekelezaji wa mambo bali kuna sheria na milolongo ya kufuata ili kumanage mipangilio mizima ya mambo kitaifa inatakiwa kwenda vipi.

Huwezi ku-skip michakato ya maendeleo kwa visingizio vya muda, hapo ni kuharibu mambo, hata hayo mataifa tajiri yalijijenga kwanza kupitia uongozi wa muda mrefu na baadae baada ya kufikia pazuri ndipo wakaanza kuzingatia hiyo demokrasia uchwara ya kupokezana uongozi, ambayo kimsingi haina maana kwa maendeleo bali ni ucheleweshaji wa maendeleo kwakuwa kila mtawala atakuwa anatawala kwa ideology yake na kuipinga ya mwenzake ama kuvuruga mambo aliyoyakuta kwa kuona hayafai na kuanzisha yake, jambo linalochelewesha maendeleo.

Demokrasia haiwezi kuleta maendeleo afrika kamwe.
 
Mi na shauri, kwanza tuyatoe ma CCM yote, harafu tufute huu utaratibu wa uchaguzi kila miaka 5! , tuwe na mfumo kama wa china,
 
Hawajui kuwa mambo ya kiserikali si kama shule wala kijiji kwamba uamke tu na uanze utekelezaji wa mambo bali kuna sheria na milolongo ya kufuata ili kumanage mipangilio mizima ya mambo kitaifa inatakiwa kwenda vipi.

Huwezi ku-skip michakato ya maendeleo kwa visingizio vya muda, hapo ni kuharibu mambo, hata hayo mataifa tajiri yalijijenga kwanza kupitia uongozi wa muda mrefu na baadae baada ya kufikia pazuri ndipo wakaanza kuzingatia hiyo demokrasia uchwara ya kupokezana uongozi, ambayo kimsingi haina maana kwa maendeleo bali ni ucheleweshaji wa maendeleo kwakuwa kila mtawala atakuwa anatawala kwa ideology yake na kuipinga ya mwenzake ama kuvuruga mambo aliyoyakuta kwa kuona hayafai na kuanzisha yake, jambo linalochelewesha maendeleo.

Demokrasia haiwezi kuleta maendeleo afrika kamwe.
Asante sana
 
Napendekeza iwe 8 kabisa na asigombee awamu 2. Akimaliza 8 asepe kuepuka gharama za uchaguzi na akiboronga baada ya hiyo 8 aishie Kisutu then Segerea.
 
Napendekeza iwe 8 kabisa na asigombee awamu 2. Akimaliza 8 asepe kuepuka gharama za uchaguzi na akiboronga baada ya hiyo 8 aishie Kisutu then Segerea.
Haaaa.. nani wa kumpeleka.. hiyo miaka 8 si atafuta kabisa na mahakama zote akijua ameboronga
 
Mi na shauri, kwanza tuyatoe ma CCM yote, harafu tufute huu utaratibu wa uchaguzi kila miaka 5! , tuwe na mfumo kama wa china,
China hakuna uchaguzi sema wana taasisi imara sana
 
Back
Top Bottom