Miaka ya Urais ipunguzwe toka 5 hadi 4

Miaka ya Urais ipunguzwe toka 5 hadi 4

Ukizingatia vijana wa miaka hii sio sawa na wa miaka ile.
Imagine Nyerere kwa umri kama wa Mwijaku alikuwa waziri mkuu. Sasa vuta picha je, Mwijaku anaweza kuwa waziri mkuu pamoja na kuwa ni msomi wa masters!
Yaani nyani mzee kakwepa mishale mingi hilo tukubali.

Eti tunampa Urais kijana wa miaka35!
Labda kama tumeichoka kabisa nchi.
 
Kwa hapa Tanzania tufanye miaka miwili tu.

Kura tuwe tunapiga kwa kutumia namba zetu za simu kama vile unatuma pesa tigo au mpesa.

Maana kama majukumu ya Rais ni kufanya ziara tu nje ya nchi miaka miwili inatosha kabisa kufanya ziara nchi zote duniani ambazo zipo 195.

Akimaliza kupiga tripu zake anakuja mwingine ni mwendo wa kupokezana tu kuruka majuu.
 
Maoni ya Warioba yamekwama, sembuse kufanya marekebisho ya katiba!

CCM watakubali miaka minne badala ya mitano?
 
Una hoja nzuri na Ubunge uwe mhula mmoja tu wa 4yrs ili watu wapunguze kulogana.
 
Naunga hoja mkono.
CCM ni nini? CCM ni taasisi na taasisi huwa si mtu.. ila mawazo ya mtu yanaweza yakaingizwa kwenye taasisi. hivyo basi naomba nieleweke kuwa tatzo si CCM kama taasisi ila watu walioingia kwa bahat mbaya kwenye taasisi ndio wanaoichafua taasisi.... fikri,awamu ya kwanza,pili,tatu,nne,tano tulkuwa tunailaum na kuipa lawama chungu nzima kama hiz za awamu hii? TAFAKARI.
 
CCM ni nini? CCM ni taasisi na taasisi huwa si mtu.. ila mawazo ya mtu yanaweza yakaingizwa kwenye taasisi. hivyo basi naomba nieleweke kuwa tatzo si CCM kama taasisi ila watu walioingia kwa bahat mbaya kwenye taasisi ndio wanaoichafua taasisi.... fikri,awamu ya kwanza,pili,tatu,nne,tano tulkuwa tunailaum na kuipa lawama chungu nzima kama hiz za awamu hii? TAFAKARI.

Kama gari ni bovu, abiria inabidi kushuka na kupanda gari zima kufika wanapokwenda.

Wakiendelea kusafiri na gari bovu na dreva mbovu, mlevi asiyejua kuendesha, ambaye hajui hata anaenda wapi hawatafika popote na kuna uwezekano mkubwa wa kupata ajali mbaya abiria wote wakapoteza maisha.
 
Siungi Mkono kupunguza muhula wa Rais bali nashauri uongezwe hadi miaka Saba.

Mwaka mmoja wa kuandaa serikali kufanya kazi, mwaka mwingine wa kuandaa kukabidhi serikali na maandalizi ya chaguzi. Miaka mitano kamili kwa ajili ya kutekeleza kwa uaminifu mkubwa ahadi alizoaihidi kwa wale waliomuamini na kumpa madaraka.
Mkuu, madikteta ndio wanataka hayo
 
Ukizingatia vijana wa miaka hii sio sawa na wa miaka ile.
Imagine Nyerere kwa umri kama wa Mwijaku alikuwa waziri mkuu. Sasa vuta picha je, Mwijaku anaweza kuwa waziri mkuu pamoja na kuwa ni msomi wa masters!
Haaaa.. sema hatuna vijana wazuri lakini tunaqeza wapata
 
Kadri tunavyo badiri viongozi mara nyingi tunapata mawazo mapya na kadri kiongozi anavyo zidi kukaa madarakani ndivyo anavyo fanya mambo ya hovyo.

Ni wakati sasa Tanzania kubadiri utaratibu wa miaka 5 uwe wa miaka 4 kama ilivyo USA na vipindi viwili vibakie kama vilivyo sasa.

Na umri wa kuwa Rais uanzie miaka 35 badala ya 40 na mwisho kugombea Urais iwe miaka 60 kama anagombea kwa mara ya kwanza.

Mabadiriko yoyote ya katiba yasifanyike kama bunge linalo takiwa kufanya mabadiriko yoyote ya kuongeza muda wa kukaa madarakani halina 40% ya wabunge wa upinzani.

Pia Makama wa Rais asiruhusiwe kuongoza nchi zaidi ya mwaka 1 kama ikitokea Rais anafariki.. baada ya mwaka mmoja uchaguzi unatakiwa kuitishwa haraka.

Heri ya Mwaka Mpya.
Wazo zuri ila mbona kiwango cha elimu hujakigusia?
 
Kiboko ni katiba mpya tu rais apunguziwe mamlaka maana kama wateule 99% anafanya yeye ndio maana tunapata machawa wengi wasaka teuzi na walioteuliwa hawafanyi kazi kwa weledi bali kusifia kulinda vyeo vyao.
 
Kadri tunavyo badiri viongozi mara nyingi tunapata mawazo mapya na kadri kiongozi anavyo zidi kukaa madarakani ndivyo anavyo fanya mambo ya hovyo.

Ni wakati sasa Tanzania kubadiri utaratibu wa miaka 5 uwe wa miaka 4 kama ilivyo USA na vipindi viwili vibakie kama vilivyo sasa.

Na umri wa kuwa Rais uanzie miaka 35 badala ya 40 na mwisho kugombea Urais iwe miaka 60 kama anagombea kwa mara ya kwanza.

Mabadiriko yoyote ya katiba yasifanyike kama bunge linalo takiwa kufanya mabadiriko yoyote ya kuongeza muda wa kukaa madarakani halina 40% ya wabunge wa upinzani.

Pia Makama wa Rais asiruhusiwe kuongoza nchi zaidi ya mwaka 1 kama ikitokea Rais anafariki.. baada ya mwaka mmoja uchaguzi unatakiwa kuitishwa haraka.

Heri ya Mwaka Mpya.
Itasaidia nini
 
Suala hili limekuzidi umri mleta mada, na wachangiaji nao wanajadili Jambo lililowazidi umri, huwezi kulinganisha wananchi wa USA na raia wa Tanzania, huku kwetu hakuna wananchi, Kuna watu tu!
 
Mkuu, madikteta ndio wanataka hayo
Hapana...! Miaka mitatu huwezi kufanya kitu chakueleweka na kikasimama. Vinginevyo, Urais iwe symbolic title tu, hivyo tubadili katiba na tuwe na msimamizi Mkuu wa masuala ya serikali kwa muda huo nilotaja wa miaka 7 ikijumuisha kuandaa serikali kufanya kazi, kukabidhi madaraka na masuala ya Uchaguzi.

Chaguzi za mara kwa mara (Tena ndani ya muda mfupi) ni ufujaji wa fedha za maendeleo ya watu kwa kisingizio cha gharama ya demokrasia. Na fedha hizi zikikusanywa za uchaguzi nyingi zinasombwo na kwenda kuwekezwa Nje ya nchi. Sasa inamaana gani kwa Wananchi wanaolitumikia Taifa kwa uaminifu?
 
Hapana...! Miaka mitatu huwezi kufanya kitu chakueleweka na kikasimama. Vinginevyo, Urais iwe symbolic title tu, hivyo tubadili katiba na tuwe na msimamizi Mkuu wa masuala ya serikali kwa muda huo nilotaja wa miaka 7 ikijumuisha kuandaa serikali kufanya kazi, kukabidhi madaraka na masuala ya Uchaguzi.

Chaguzi za mara kwa mara (Tena ndani ya muda mfupi) ni ufujaji wa fedha za maendeleo ya watu kwa kisingizio cha gharama ya demokrasia. Na fedha hizi zikikusanywa za uchaguzi nyingi zinasombwo na kwenda kuwekezwa Nje ya nchi. Sasa inamaana gani kwa Wananchi wanaolitumikia Taifa kwa uaminifu?
Sasa kama mmepata Rais wa hovyo, hiyo miaka 7 itakuaje?
 
Suala hili limekuzidi umri mleta mada, na wachangiaji nao wanajadili Jambo lililowazidi umri, huwezi kulinganisha wananchi wa USA na raia wa Tanzania, huku kwetu hakuna wananchi, Kuna watu tu!
Mkuu nimewekea mfano tuu usa lakini kuna nchi ambazo Rais ana kaa chini ya miaka 4
 
Back
Top Bottom