Miaka michache iliyopita nilibahatika kutembelea America, Washington State.
Washington huwa kuna baridi, na siku niliyofika ndio usiseme, ilikuwa baridi sana

, bahati mbaya nikawa na kikohozi huku nikiwa najisikia na kahoma fulani hivi. Haikuni simamisha kutaka kutoka na kuona mji.
Hatahivyo kama kawaida nikameza dawa yangu Panadol, na huyo nikaingia Mtaani

Nikaingia kwenye mgahawa nikavuta kigoda na kuagizia 'Tea' na uzuri nikaona "Chai Masala" kwenye menu, nikagusa tu kuashiria ndicho nilichokuwa nahitaji pale. Nilipata chai yangu, taratibu nikaanza kunywa napepesa pepesa, ghafla, nikapiga chafya, wakaniambia 'Bless you' na kwa ukarimu nikaitikia tu, 'sank you' huku mmoja wa nilio kaa naye karibu kwenye vigoda akasema 'I hope its not a cold' nikaitikia tu 'yes', 'its very cold' (sikuwa nimeelewa vizuri) Haikuishia hapo, mzee mmoja wa makamo akanisogelea na kuninong'oneza, alisema '
In Washington State, it is illegal to walk around in public if you have a common cold' hapo ndiyo ilikuwa Aha


moment yangu, kumbe, "Common cold" Yaani akimaanisha Homa ya mafua.
Aloo,nilishikwa na butwaa, nikasimama taratibu na kuondoka kurudi hotelini, ka mwendo hivi, kwa miguu, ka dakika tano sita tu lakini njiani kila nikiona Polisi naomba nisipige chafya nikakamatwa kwakuwa na homa ya mafua.

Wacheni. Duniani kuna mambo, na nimeona na kusikia mengi, lakini haya ya huyo Bro wetu Mshana Jr, Aloo ni ya kufikirisha

zaidi.