Miaka niliyoishi si haba

Miaka niliyoishi si haba

Miaka michache iliyopita nilibahatika kutembelea America, Washington State.

Washington huwa kuna baridi, na siku niliyofika ndio usiseme, ilikuwa baridi sana😱, bahati mbaya nikawa na kikohozi huku nikiwa najisikia na kahoma fulani hivi. Haikuni simamisha kutaka kutoka na kuona mji.

Hatahivyo kama kawaida nikameza dawa yangu Panadol, na huyo nikaingia Mtaani💪 Nikaingia kwenye mgahawa nikavuta kigoda na kuagizia 'Tea' na uzuri nikaona "Chai Masala" kwenye menu, nikagusa tu kuashiria ndicho nilichokuwa nahitaji pale. Nilipata chai yangu, taratibu nikaanza kunywa napepesa pepesa, ghafla, nikapiga chafya, wakaniambia 'Bless you' na kwa ukarimu nikaitikia tu, 'sank you' huku mmoja wa nilio kaa naye karibu kwenye vigoda akasema 'I hope its not a cold' nikaitikia tu 'yes', 'its very cold' (sikuwa nimeelewa vizuri) Haikuishia hapo, mzee mmoja wa makamo akanisogelea na kuninong'oneza, alisema ' In Washington State, it is illegal to walk around in public if you have a common cold' hapo ndiyo ilikuwa Aha💡🤔 moment yangu, kumbe, "Common cold" Yaani akimaanisha Homa ya mafua.
Aloo,nilishikwa na butwaa, nikasimama taratibu na kuondoka kurudi hotelini, ka mwendo hivi, kwa miguu, ka dakika tano sita tu lakini njiani kila nikiona Polisi naomba nisipige chafya nikakamatwa kwakuwa na homa ya mafua.😪🤒

Wacheni. Duniani kuna mambo, na nimeona na kusikia mengi, lakini haya ya huyo Bro wetu Mshana Jr, Aloo ni ya kufikirisha🤯 zaidi.
 
Miaka michache iliyopita nilibahatika kutembelea America, Washington State.

Washington huwa kuna baridi, na siku niliyofika ndio usiseme, ilikuwa baridi sana, bahati mbaya nikawa na kikohozi huku nikiwa najisikia na kahoma fulani hivi. Haikuni simamisha kutaka kutoka na kuona mji.
In Washington State, it is illegal to walk around in public if you have a common cold' hapo ndiyo ilikuwa Aha moment yangu, kumbe, "Common cold" Yaani akimaanisha Homa ya mafua.
 
Nmeona meanasiasa akikataza kuchanganya dini na siasa akisema hayo katika jukwaa la dini.

Pia meanasiasa huyo aliwahi Apa kwakutumia kitabu Cha DINI kutekeleza shughuli zake za kisiasa.
 
Nimeona mke wa mtu akilia kwa usaliti kwa mume wa mtu ambaye sio mumewe na kuapa kumkomesha kisa Ana mwanamke mwengine zaidi yake (unaweza ukahisi status ni za mume wake kumbe ni za mume wa mtu mwengine)
 
Kwa utoto wangu huu nami nimeona vichache pia. Nimeona marafiki wazuri wakiwa msaada mkubwa kwa mtu na ndugu wa damu wakiwa liability na maumivu kwenye maisha ya mtu.

Nimeona ndugu wakisubiri mtu afe kwa madai ya kwamba ameoza kabisa na huku pesa za michango ya msiba kupatikana haraka wakati pindi ndugu yao yuko hai pesa ya matibabu ilikua ya tabu.

Nimeona watu wakichangishana kwa tabu hela ya msiba na mambo ya kusafirisha huku hao hao wanapofika kwenye transit stations ndio wanunuaji wa bia na nyama choma kwa wingi lakini hela ya michango its a no kwao.

Nimeshuhudia ndugu wakimuacha mwanaume aliewasaidia kipindi cha pesa nyingi kwa kuwasomesha ama kuwapiga tafu lakini kwenye shida inabakia mke na watoto kupambana na hali zao huku watoto wakipiga simu wanapewa bonge la block.
Nimezoom wake za viongozi wa dini mbalimbali wakitafuta suluhisho za ashki zao nje ya ndoa huku wakiwa viongozi wa wanawake wenzao na masuala ya kifamilia ndani ya taasisi za dini zao.

Nimeona waliokufa na njaa, kukiwa na masufuria makubwa kwenye misiba yao kwa madai ya "sherehe ya mwisho ya marehemu."
Nikaona meza zikipinduka nyakati flani flani kwenye maisha ya mwanadamu. Unakuta aliyekuaga juu anashuka chini rapidly huku aliyedharaulika akipanda juu in a moment..kimbembe itokee katika ofisi.

Maybe bado sijaona...Mungu anipe uzima kuyaona mengine pia.
 
Mshana, on a serious note, mimi huyo mkaka tuu anayeimba na hiyo kofia yake.
Mwambie nimemuelewa hasa hizo ndevu. Sema tuu ana mtu wake tayari ila ningemfungia safari hadi huko aliko, mie ni mapendo daima tuu hakuna la ziada.

Back to the topic, nimeona mtoto chini ya miaka 10 ana busara kuliko wazazi wake kiasi cha kuongea na mchungaji namna aongee na wazazi wake waache mabishano kwani hayuko tayari kulelewa mtoto wa kambo na wao wanaendekeza starehe zao.
Kasie naona umekuwa wa baridi siku hizi kunani? Au sie huyu kasie mahaba matata tunaemjua?
 
1692745120265.png
I've seen 'THE MISSING LINK'!
 
Kwa utoto wangu huu nami nimeona vichache pia. Nimeona marafiki wazuri wakiwa msaada mkubwa kwa mtu na ndugu wa damu wakiwa liability na maumivu kwenye maisha ya mtu.

Nimeona ndugu wakisubiri mtu afe kwa madai ya kwamba ameoza kabisa na huku pesa za michango ya msiba kupatikana haraka wakati pindi ndugu yao yuko hai pesa ya matibabu ilikua ya tabu.

Nimeona watu wakichangishana kwa tabu hela ya msiba na mambo ya kusafirisha huku hao hao wanapofika kwenye transit stations ndio wanunuaji wa bia na nyama choma kwa wingi lakini hela ya michango its a no kwao.

Nimeshuhudia ndugu wakimuacha mwanaume aliewasaidia kipindi cha pesa nyingi kwa kuwasomesha ama kuwapiga tafu lakini kwenye shida inabakia mke na watoto kupambana na hali zao huku watoto wakipiga simu wanapewa bonge la block.
Nimezoom wake za viongozi wa dini mbalimbali wakitafuta suluhisho za ashki zao nje ya ndoa huku wakiwa viongozi wa wanawake wenzao na masuala ya kifamilia ndani ya taasisi za dini zao.

Nimeona waliokufa na njaa, kukiwa na masufuria makubwa kwenye misiba yao kwa madai ya "sherehe ya mwisho ya marehemu."
Nikaona meza zikipinduka nyakati flani flani kwenye maisha ya mwanadamu. Unakuta aliyekuaga juu anashuka chini rapidly huku aliyedharaulika akipanda juu in a moment..kimbembe itokee katika ofisi.

Maybe bado sijaona...Mungu anipe uzima kuyaona mengine pia.
Maybe bado sijaona...Mungu anipe uzima kuyaona mengine pia
 
NIMEONA;

Jambazi mbobevu akiwa mtoa mfano mzuri jinsi Jambazi mwenziye anavyopaswa kuuwawa kwa kipigo kizito.

Mcha Mungu kupita kiasi akiwa ndiye kungwi wa ufisadi, uzinzi, uchawi, uuzaji wa madawa ya kulevya, ukwepaji kodi, ubinafsi, ujambazi na hata utapeli,

Anayethamini zaidi maisha (nyumba, gari na milki za kifahari) kuliko kuishi (akijinyima kula na kupatwa vidonda vya tumbo) na kujitibu kwa gharama zaidi bila kuinjoyi pesa zake au asiishi kabisa kwenye nyumba aliyojenga kwa kufariki.

Mzee akijisifu kwenye mazishi kuwa Rafiki zake, Ndugu zake na Jamaa zake waliishi pamoja eneo flani, na wengine walimkuta hapo hapo akiishi ila wote walifariki na kumwacha yeye pekee akidunda ilihali naye ni Marehemu Mtarajiwa.
 
Walau naweza kusema nimeona mengi. Nimeona daktari akiumwa saratani ya koo kwa ajili ya matumizi ya vitu anavyokataza wengine.

Kisha nikamuona wakili aliyehukumiwa kwenda jela kwa kosa la kudhulumu mali za yatima na wajane.

Halafu nikapata ile habari yenye maumivu, habari iliyonitoa machozi na kunipa simanzi ya moyo. Kwamba rafiki yangu ambaye ni tabibu wa akili naye kajiua kwa msongo wa mawazo.

We umeona mangapi? Nimeona tabasamu kwa mtu aliyepaswa kulia, halafu nikaona maumivu katika kicheko cha mtu aliyesalitiwa.

Ukiona mtu anakupa faraja, nenda kafanye ibada, kwa kuwa haina maana kila kitu kwake kiko sawa, ila anajali hata akaamua kugawa tawi la kivuli chake katika msiba wa hisia zake.

Maisha sio yale uliyofikiri, maisha ni haya ambayo hesabu zako za shule zinakataa kujaza jedwali la upendo lililo wazi.

Kitu gani umewahi kuona? Ukitaka imani yako iwe na dosari, basi anzisha urafiki na kiongozi wa dini.

Nimeshuhudia vita katika nyumba ya balozi wa amani. Kisha nikaona uongo na ulaghai katika nafsi zilizoapa na kutii.

Halafu nikaona upendo katika sura ya kahaba, halafu baadaye nikashangazwa, nikaoneshwa ukahaba Katika sura ya aliyeitwa muumini.

Ndipo nikaamua kukubali, kuwa tukiamua kuhesabu vya kila mtu hesabu zetu daima hazitofika mwisho.

Angel Nylon View attachment 2724878
Mimi nimeona Kuishi ni Leo Jana na kesho haipo tena. na nikaona hakuna miaka Kuna siku tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom