Miaka niliyoishi si haba

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,517
Reaction score
860,567
Walau naweza kusema nimeona mengi. Nimeona daktari akiumwa saratani ya koo kwa ajili ya matumizi ya vitu anavyokataza wengine.

Kisha nikamuona wakili aliyehukumiwa kwenda jela kwa kosa la kudhulumu mali za yatima na wajane.

Halafu nikapata ile habari yenye maumivu, habari iliyonitoa machozi na kunipa simanzi ya moyo. Kwamba rafiki yangu ambaye ni tabibu wa akili naye kajiua kwa msongo wa mawazo.

We umeona mangapi? Nimeona tabasamu kwa mtu aliyepaswa kulia, halafu nikaona maumivu katika kicheko cha mtu aliyesalitiwa.

Ukiona mtu anakupa faraja, nenda kafanye ibada, kwa kuwa haina maana kila kitu kwake kiko sawa, ila anajali hata akaamua kugawa tawi la kivuli chake katika msiba wa hisia zake.

Maisha sio yale uliyofikiri, maisha ni haya ambayo hesabu zako za shule zinakataa kujaza jedwali la upendo lililo wazi.

Kitu gani umewahi kuona? Ukitaka imani yako iwe na dosari, basi anzisha urafiki na kiongozi wa dini.

Nimeshuhudia vita katika nyumba ya balozi wa amani. Kisha nikaona uongo na ulaghai katika nafsi zilizoapa na kutii.

Halafu nikaona upendo katika sura ya kahaba, halafu baadaye nikashangazwa, nikaoneshwa ukahaba Katika sura ya aliyeitwa muumini.

Ndipo nikaamua kukubali, kuwa tukiamua kuhesabu vya kila mtu hesabu zetu daima hazitofika mwisho.

Angel Nylon [emoji177]
Your browser is not able to display this video.
 
Sheikh hii ni lulu ya tamathali zako
 

Mshana, on a serious note, mimi huyo mkaka tuu anayeimba na hiyo kofia yake.
Mwambie nimemuelewa hasa hizo ndevu. Sema tuu ana mtu wake tayari ila ningemfungia safari hadi huko aliko, mie ni mapendo daima tuu hakuna la ziada.

Back to the topic, nimeona mtoto chini ya miaka 10 ana busara kuliko wazazi wake kiasi cha kuongea na mchungaji namna aongee na wazazi wake waache mabishano kwani hayuko tayari kulelewa mtoto wa kambo na wao wanaendekeza starehe zao.
 
Mwambie nimemuelewa hasa hizo ndevu. Sema tuu ana mtu wake tayari ila ningemfungia safari hadi huko aliko, mie ni mapendo daima tuu hakuna la ziada.[emoji23]
Kasie wewe..[emoji23]
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…