Leo ni siku ya Uhuru, nimefungulia redio nikatune Wasafi FM nikasikia wanapiga nyimbo ya miaka ya 60-80. Vijana wa sasa huziita zilipendwa. Sijui jina la nyimbo wala aliyeimba simjui lakini nikawa nasikiliza Kwa makini maana ujumbe wa nyimbo ulinivutia sana.
Mwimbaji wa hii nyimbo alikuwa analalamika juu ya ugumu wa maisha Kwa wakati huo. Anasema alioa wanawake wawili lakini inabidi amuache mmoja Kwa sababu maisha yamegekuwa magumu Sana.
Anataja ulanguzi wa bidhaa, akiitaka na sukari jinsi ulivyosababisha ugumu wa maisha wakati huo
Baada ya hii nyimbo kuisha nikawa nawaza tunasherekea sikukuu ya Uhuru wa Tanzania bara,ni Uhuru wa nini, mbona matatizo yaleyale ambayo huyu muimbaji wa enzi hizo aliyoyaimba bado tunayo tena makubwa sana.
Mkulima bado anatumia jembe la mkono,na inatajwa afrika ndiyo bara linaloongoza kwa kilimo duni kuliko bara lolote, Tanzania ikiwemo.
Tangu nakua tunaambiwa Tanzania ni nchi ya pili Kwa vivutio duniani ikitanguliwa na Brazil lakini tunapokea watalii chini ya milioni mbili Kwa mwaka
Leo watanzania wanakamuliwa na Kodi za kila Aina.Juzi Tu hapo wametuongezea mzigo wa Kodi isiyo rasmi, wameibatiza jina tozo.Niliwahi kumsikia mtu mmoja akisema endapo Tanzania ingepata asilimia 10 Tu ya watalii wanaotembelea Paris Ufaransa ambao hupokea watalii zaidi ya milioni 80 Kwa mwaka basi tungepiga hatua kubwa Sana Kama taifa,na masuala ya tozo tusingeyazungumzia
Tuna madini ya kila Aina lakini yamekuwa Kama laana kwwtu.Kila siku yunasikia Stori za kutoroshwa.Juzi tukajenga ukuta mererani lakini tunaambiwa Kasi ya utoroshaji imekuwa kubwa kuliko awali
Kwenye michezo bado tunaendelea kupeperusha bendera ya 'kichwa cha mwendawazimu'
Miaka 60 ya Uhuru viwanja Bora vyenye hadhi ya FIFA ni viwili tena vyote vipo Dar
Tunatajwa kuwa na ligi Bora ya 8 Africa lakini serikali haifanyi maboresho yoyote kwenye viwanja vya mikoani, viwanja vya CCM ndiyo vibovu kuliko. Azam TV anashindwa kufunga camera za kutosha Kwa sababu viwanja vingi vya mikoani havisupport, hadi wakati mwingine analazimika kufunga majukwa Kwa ajili ya studio ya kurushia matangazo Kwa gharama yake binafsi.
Serikali inalalamika ajira hakuna lakini ingeboresha sekta ya michezo vijana wengi wangejiajiri huko Ila imelala fofofo.Ila wakina mwakinyo wakishinda Kwa juhudi zao binafsi ndiyo wanawakumbuka Kwa kuwaita ikulu na bungeni kuwapongeza
Nakumbuka wiki kadhaa zilizopita Rais wa Uganda alikuja kufanya ziara Tanzania.Kwenye hotuba yake Rais wa Tanzania Mama Samia aliongelea swala la sukari,akamwambia Rais wa Uganda wafanyabkashara wa Uganda waingize sukari nchini na kuiita kauli ya waziri wake ya kuzuia sukari kutoka nje ni 'nonsense'
Niliposikia hii nyimbo ya kale hasa hiki kipande cha ulanguzi wa sukari enzi hizo niikaishia kucheka Tu maana miaka mingi baadae bado tatizo la sukari aliloliimba enzi hizo liko pale pale.Tumekwama mahali Kama taifa
Miaka ya 2013/2014 kulikuwa na makala kwenye gazeti la Tazama yenye kichwa cha habari POVERTY IN THE MIDST OF PLENTIFUL (UMASIKINI KATIKATI YA UTAJIRI)
Tumejaaliwa na mwenyezi MUNGU kila Aina ya utajiri lakini tuna umasikini wa kutupwa.Je,Tanzania tumelaaniwa?
Happy independence Day