mkaruka ataja rinu
JF-Expert Member
- Aug 27, 2016
- 3,309
- 2,218
Unashangaa kupumana uzito kwa kuning'inizwa kwenye miti wakati mabinti bado wanatahiriwa. Mboa simple tuHii habari nimesoma twitter, habari inayosema watoto wadogo wanapimwa uzito kwa kuning'inizwa kwenye mti huko wilayni Tarime mkoa wa Mara(kuna picha ikionyesha tukio hilo).
Hakika nimeshangazwa sana na hii habari, ila inaelekea hali hii ni ya kawaida tu kwa baadhi ya maeneo ya nchi yetu huku tukiwa na takribani miaka 60 ya kujitawala.
Jamani vitu vingine tuone aibu kwani haiwezekani viongozi watembee na mashangingi huku watoto wetu wananing'nizwa kwenye miti kama viroba miaka 60 baada ya uhuru na watu tunaridhika tu.
Alieturoga watanzania hakika alikuwa fundi.