Miaka 31.... Hongera sana

Kibunango

Platinum Member
Aug 29, 2006
8,419
2,270
CCM imetimiza miaka 31 tangu kuanzishwa kwake. Pengine sherehe hizi mwaka huu ndio zitazokuwa za kimya kabisa kupita miaka mingine yote.

Hongera sana CCM

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
Sina haja ya kupongeza chama ambacho kinaongoza kwa kutegemea ujinga wa watz. Hiki chama hakiwezi kudumu milele, kumbuka zile enzi za zidumu fikira za mwenyekiti wa chama, hata kama ni za kipumbavu,ziko wapi,ndio twaelekea kukizika hiki chama atii
 
CCM imetimiza miaka 31 tangu kuanzishwa kwake. Pengine sherehe hizi mwaka huu ndio zitazokuwa za kimya kabisa kupita miaka mingine yote.

Hongera sana CCM

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

CCM ipi?
Ile iliyotokana na TANU na ASP kwa misingi ya Azimio la Arusha au ile iliyotokana na Azimio la Zanzibari?

CCM ipi?
Ile iliyorithi ahadi za TANU na ASP kuwa:
Nitasema kweli Daima, Fitina kwangu mwiko,
Binadamu wote ni sawa na Afrika ni moja,
Sitapokea wala kutoa rushwa?

Cheo ni dhamana,
Sitatumia cheo changu na ofisi ya Umma kujinufaisha?

Au ndiyo CCM hii ya Utandawazi:

Chukua Chako Mapema
Kutumia ofisi ya Umma kujinufaisha
Kutoa na kupokea Rushwa na kishwa kusafishwa na TAKUKURU
Kutumia kila ghiriba na kutawala nchi hata kwa miaka 100 ijayo?

CCM ipi?
 
CCM imetimiza miaka 31 tangu kuanzishwa kwake. Pengine sherehe hizi mwaka huu ndio zitazokuwa za kimya kabisa kupita miaka mingine yote.

Hongera sana CCM

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Nakumbuka sana, CCM ikiwa inazaliwa, nilikuwa mdogo sana shule ya msingi lakini tayari nilikuwa mwumini wa siasa za TANU, ujamaa na Nyerere.

Nilikuwa na imani kubwa sana CCM. Sasa ni mtu mzima, nimesoma, nimetembea dunia na kuona kwanini wenzetu wanaendelea wakati sisi tuko pale pale.

Malengo ya CCM yalikuwa mazuri tu, hata leo bado ni mazuri tu. Bahati mbaya viongozi wetu ambao wengi walizaliwa kabla ya uhuru, hawakushiriki mapambano ya kudai uhuru, ilitakiwa ndio waendeleza mapambano ya kudai uhuru wa kiuchumi. Bahati mbaya sana wametusaliti wananchi na wamegeuka wakoloni weusi.

Kosa kubwa la Nyerere lilikuwa kuifanya CCM ishike hatamu (monopoly). Kushika hatamu huko ndiko mpaka sasa kunawafanya viongozi wetu washindwe kutofautisha kati ya kilicho cha CCM na kile cha wananchi. Hatamu hiyo hiyo ndio inavifanya vyombo kama PCCB, polisi, mahakama, nk. vitumike kama vyombo vya kulinda maslahi ya CCM na viongozi wake.

Binafsi bado nina imani na ile CCM ya Nyerere, kinachotakiwa ni kuirudisha CCM kwa wananchi. Ningependa CCM ishindwe ili iwe nafasi ya kujisafisha na kujijenga upya kama vilivyofanya vyama vya Kikomunisti kule Ulaya Mashariki.

Wakati tuna akina Malecela ambao wanailinda CCM kwa mazuri na mabaya, kuna haja ya kupata akina Gorbachev ambao wataiua au kuivunja CCM kwa faida ya ya nchi yetu na CCM yenyewe huko mbeleni.

Hali ya CCM ya leo inasikitisha sana, inaua matumaini yote ambayo kama kijana, nilikuwa tayari kuitumikia na kuilinda. Leo imegeuka kuwa chombo cha matajiri na majizi ambayo hayana visions zozote za kumkomboa Mtanzania kutoka kwenye umaskini wa ajabu. Miaka karibu 50 ya kuwa huru bado hali za wananchi wengi ni mbaya kuliko miaka ya 70. Sera za mwalimu kama mtu ni afya, kilimo bora, kujitegemea nk vyote vimekufa na sasa hatuna sera zozote za maana zaidi ya majigambo majukwaani.

Nimezaliwa kijijini, pamoja na kutokuwa na vitu muhimu kama viatu na nguo nyingi lakini miaka yote ya utoto wangu sikuwahi kushinda njaa. Tulikuwa na vyakula vya kutosha, sikuwahi kumwona mtoto wa jirani au wa ndugu anashinda njaa. Kulikuwa na zahanati ambako hata kama mtu aliumwa ghafla usiku, basi kulikuwa na uwezekano wa kwenda kumwamsha daktari na kupata matibabu bila ulalamishi wala kuombwa pesa. Kulikuwa na shule nzuri tu, shule zilizokuwa zinaendeshwa na walimu wenye nia na lengo la kuwaendeleza watanzania wenzao, shule ambazo ubora wake haukuwa tofauti na ubora wa shule walizosoma watoto wa mawaziri mijini.

Leo nikirudi kijijini naona watu wazima wamegeuka ombaomba, watoto wanakufa kwa malaria ambayo madawa yake yanajulikana miaka na miaka, shule za umma ni za maskini, viongozi wetu wanapeleka watoto wao majuu na kwenye shule za bei mbaya. Hivi kweli huu ndio uhuru na maendeleo ambayo TANU na kisha CCM walituahidi?

Wana CCM amkeni, tambueni kwamba nyie ndio mumeuza chama kwa kuchagua watu wasio na mwelekeo wala uwezo wa kutuongoza, watu ambao wanatuacha wananchi kwenye shule hoi zisizo na walimu, wao wanapeleka watoto wao Ulaya, viongozi ambao wanatumia mabilioni kwenda kufanya checkups Ulaya huku watoto na akina mama wanakufa kwa kukosa dawa ya malaria. Viongozi ambao wanawaacha vijana wetu wanahaha barabarani kwa kukosa kazi, huku wanaruhusu wageni kuajiriwa hata kwenye kazi ambazo Watanzania wanaweza kufanya bila matatizo. Viongozi ambao wanaruhusu kila takataka iagizwe toka nje, huku mananasi na matunda yetu mengine yanaoza kwa kukosa soko.

Sina cha kufurahia kuhusu uhai wa CCM na badala yake hiyo sherehe itakuja fanyika siku CCM itakapo pelekwa theatre na kufanyiwa operation ili kuondoa cancer iliyotapakaa kila sehemu. Siku ambapo CCM itakubali kuachia madaraka japo kwa muda ili ifanyiwe matibabu makubwa kwa faida yake na Watanzania wote.

Pole sana kwa wana CCM wote, huyo mwaneno ni taahira!
 
Ibra mbona hasira ndugu yangu. Taratibu, najua inaudhi sana. Tungekuwa tunamiliki silaha nchi hii sijui tungefika wapi. Maana wahusika wote wa haya maskendo wangetafutwa na kuuwawa kama Samuel Doo
 
Nadhani bwana avenue manini cjui,unachemka,unapaswa kutafuta jukwaa jingine hapa sipo
 
Nakumbuka sana, CCM ikiwa inazaliwa, nilikuwa mdogo sana shule ya msingi lakini tayari nilikuwa mwumini wa siasa za TANU, ujamaa na Nyerere.

Nilikuwa na imani kubwa sana CCM. Sasa ni mtu mzima, nimesoma, nimetembea dunia na kuona kwanini wenzetu wanaendelea wakati sisi tuko pale pale.

Malengo ya CCM yalikuwa mazuri tu, hata leo bado ni mazuri tu. Bahati mbaya viongozi wetu ambao wengi walizaliwa kabla ya uhuru, hawakushiriki mapambano ya kudai uhuru, ilitakiwa ndio waendeleza mapambano ya kudai uhuru wa kiuchumi. Bahati mbaya sana wametusaliti wananchi na wamegeuka wakoloni weusi.

Kosa kubwa la Nyerere lilikuwa kuifanya CCM ishike hatamu (monopoly). Kushika hatamu huko ndiko mpaka sasa kunawafanya viongozi wetu washindwe kutofautisha kati ya kilicho cha CCM na kile cha wananchi. Hatamu hiyo hiyo ndio inavifanya vyombo kama PCCB, polisi, mahakama, nk. vitumike kama vyombo vya kulinda maslahi ya CCM na viongozi wake.

Binafsi bado nina imani na ile CCM ya Nyerere, kinachotakiwa ni kuirudisha CCM kwa wananchi. Ningependa CCM ishindwe ili iwe nafasi ya kujisafisha na kujijenga upya kama vilivyofanya vyama vya Kikomunisti kule Ulaya Mashariki.

Wakati tuna akina Malecela ambao wanailinda CCM kwa mazuri na mabaya, kuna haja ya kupata akina Gorbachev ambao wataiua au kuivunja CCM kwa faida ya ya nchi yetu na CCM yenyewe huko mbeleni.

Hali ya CCM ya leo inasikitisha sana, inaua matumaini yote ambayo kama kijana, nilikuwa tayari kuitumikia na kuilinda. Leo imegeuka kuwa chombo cha matajiri na majizi ambayo hayana visions zozote za kumkomboa Mtanzania kutoka kwenye umaskini wa ajabu. Miaka karibu 50 ya kuwa huru bado hali za wananchi wengi ni mbaya kuliko miaka ya 70. Sera za mwalimu kama mtu ni afya, kilimo bora, kujitegemea nk vyote vimekufa na sasa hatuna sera zozote za maana zaidi ya majigambo majukwaani.

Nimezaliwa kijijini, pamoja na kutokuwa na vitu muhimu kama viatu na nguo nyingi lakini miaka yote ya utoto wangu sikuwahi kushinda njaa. Tulikuwa na vyakula vya kutosha, sikuwahi kumwona mtoto wa jirani au wa ndugu anashinda njaa. Kulikuwa na zahanati ambako hata kama mtu aliumwa ghafla usiku, basi kulikuwa na uwezekano wa kwenda kumwamsha daktari na kupata matibabu bila ulalamishi wala kuombwa pesa. Kulikuwa na shule nzuri tu, shule zilizokuwa zinaendeshwa na walimu wenye nia na lengo la kuwaendeleza watanzania wenzao, shule ambazo ubora wake haukuwa tofauti na ubora wa shule walizosoma watoto wa mawaziri mijini.

Leo nikirudi kijijini naona watu wazima wamegeuka ombaomba, watoto wanakufa kwa malaria ambayo madawa yake yanajulikana miaka na miaka, shule za umma ni za maskini, viongozi wetu wanapeleka watoto wao majuu na kwenye shule za bei mbaya. Hivi kweli huu ndio uhuru na maendeleo ambayo TANU na kisha CCM walituahidi?

Wana CCM amkeni, tambueni kwamba nyie ndio mumeuza chama kwa kuchagua watu wasio na mwelekeo wala uwezo wa kutuongoza, watu ambao wanatuacha wananchi kwenye shule hoi zisizo na walimu, wao wanapeleka watoto wao Ulaya, viongozi ambao wanatumia mabilioni kwenda kufanya checkups Ulaya huku watoto na akina mama wanakufa kwa kukosa dawa ya malaria. Viongozi ambao wanawaacha vijana wetu wanahaha barabarani kwa kukosa kazi, huku wanaruhusu wageni kuajiriwa hata kwenye kazi ambazo Watanzania wanaweza kufanya bila matatizo. Viongozi ambao wanaruhusu kila takataka iagizwe toka nje, huku mananasi na matunda yetu mengine yanaoza kwa kukosa soko.

Sina cha kufurahia kuhusu uhai wa CCM na badala yake hiyo sherehe itakuja fanyika siku CCM itakapo pelekwa theatre na kufanyiwa operation ili kuondoa cancer iliyotapakaa kila sehemu. Siku ambapo CCM itakubali kuachia madaraka japo kwa muda ili ifanyiwe matibabu makubwa kwa faida yake na Watanzania wote.

Pole sana kwa wana CCM wote, huyo mwaneno ni taahira!

Very deep indeed!

Asante mtanzania kwa insight, natumai wakulu huko dodoma watasoma hili pia kwa umakini!
 
Hilo jina lisiwapumbaze naweza kulibadilisha hata kesho.

La muhimu leo hii ni kwamba Watanzania woote popote waliopo tufurahie Chama chetu kitukufu CCM kuadhimisha miaka 31 ya kuzaliwa! Ni furaha iliyoje!! CCM Hoyee!! JK juu!! Juuu!! Juuu!! Juu zaidi!!

tz&

Kwani tatizo ni kubadilisha jina hapa au ni kutumia ID yako ile nyingine unayotumia hapa! Nadhani lile wazo la FMES la kufungia watu wenye ID zaidi ya moja hapa lilikuwa bora. Unaweza tu kurudi kwenye ile ID yako nyingine unayotumia hapa!
 
wanaumiwa na wataumia sana,ukweli CCM imefikisha miaka 31.

kuna mengi ya kujifunza na kuna mengi ambayo yanapaswa kufanyiwa marekebisho.


CCM ni chama cha mapinduzi si chama cha kihafidhina, CCM iko tayari kukosolewa na kurekebisha sera na malengo yake kwenda na wakati na haja.

sasa tunaangalia vipi tutaimarisha ushirikiano na vyama vya upinzani, tunaangalia suala la kiongozi kuwa mfanya biashara.

kutekeleza ahadi za chama na mengineo.

tumeangalia na tumeona mapungufu yetu na tunayaboresha.

kidumu chama cha mapinduzi
 
wanaumiwa na wataumia sana,ukweli CCM imefikisha miaka 31.

........

Kweli kabisa Mtu wa Pwani,

Wanaumia na wataumia sana:

1. Kina mama wajawazito wanaokufa bila huduma nzuri
2. Watoto wachanga wanaokufa kwa magonjwa yanayotibika
3. Wananchi wa Buzwagi na Bulyanhulu waliotimuliwa na ccm
4. Wananchi wa kanda ya ziwa ambayo ardhi yao imeuzwa kwa Barick
5. Watanzania wanaolipia umeme kwa bei ya kuruka
6. Watanzania wa Kigoma ambao wametengwa na Tanzania
7. Wananchi wa vijijini wasio na barabara nzuri
8. Watoto wa shule wanaokaa kwenye mavumbi kusoma
9. Mamilioni ya watanzania wanaishi kwa mulo mmoja
.......

Yeah wakati mimi na wewe tukila burger na kusaza, watanzania wengi sana wataumia na kuummia kwa serikali ya ccm:

1. Kuuza viwanda vyote kwa bei ya njugu
2. Kufilisi akiba yote ya nchi
3. Kusaini mikataba itakayowafanya watanzania kuwa watumwa
4. Kuishi maisha ghali huku mamilioni wakifa kwa njaa
5. Kuuza ardhi yote yenye madini kwa wageni
6. Kuwa na viwango vikubwa kabisa vya kodi inayofujwa
7. Kuweka mazingira safi kwa vita ya kiraia ambayo iko mbioni!

.......

Watalia na kuumia sana!.....
 
si bureeee si bureeeeee iko namna

ovyo usingetukan endelea kutukana

ccm inawatumikia wananchi na kusikiliza kilio chao


CCM chama cha watu wote na kina dhamira ya kumkomboa mtanzania
 
Kwani CCM kama Chama imewakosea nini? Why can't you join CCM to clean the house. Jiungeni kwa wingi CCM uchaguzi ukija tuwang'oe mafisadi. Tushike hatamu kwa sababu vyama vingine itatuchukuwa miaka 100 kukomaa na kuaminika kwani hata huko ni wale wale waliokimbia CCM baada ya kuzidiwa kete.
 
Nilikuwa na imani kubwa sana CCM. Sasa ni mtu mzima, nimesoma, nimetembea dunia na kuona kwanini wenzetu wanaendelea wakati sisi tuko pale pale.

Malengo ya CCM yalikuwa mazuri tu, hata leo bado ni mazuri tu. Bahati mbaya viongozi wetu ambao wengi walizaliwa kabla ya uhuru, hawakushiriki mapambano ya kudai uhuru, ilitakiwa ndio waendeleza mapambano ya kudai uhuru wa kiuchumi. Bahati mbaya sana wametusaliti wananchi na wamegeuka wakoloni weusi.

Kosa kubwa la Nyerere lilikuwa kuifanya CCM ishike hatamu (monopoly). Kushika hatamu huko ndiko mpaka sasa kunawafanya viongozi wetu washindwe kutofautisha kati ya kilicho cha CCM na kile cha wananchi. Hatamu hiyo hiyo ndio inavifanya vyombo kama PCCB, polisi, mahakama, nk. vitumike kama vyombo vya kulinda maslahi ya CCM na viongozi wake.
CCM imepita katika mengi na mengi hayo yamechangiwa na siasa za kimataifa. Wakati wa vita baridi ulikuwa ni wakati ambao kulikuwa na umuhimu mkubwa wa kuwa na chama kimoja cha kisiasa kuliko wakati mwingine wowote ule. Hivyo wazo la Mwl.Nyerere na wasaidizi wake halikuwa baya, zaidi lilirenga kwenye maslahi ya taifa, ambayo hadi leo tunaendelea kufaidika. Misingi iliyojengwa katika kipindi cha vita baridi, itachukua muda kubomaoka mna kutoweka kabisa. Katika mfumo wa sasa ambapo ni taifa moja tu lenye nguvu na kauli ya mwisho, tumeendelea kuona machafuko katika tawala za ndani katika nchi zinazoendelea. Hali hii kwa sasa inainyemelea nchi yetu.

Wakati tuna akina Malecela ambao wanailinda CCM kwa mazuri na mabaya, kuna haja ya kupata akina Gorbachev ambao wataiua au kuivunja CCM kwa faida ya ya nchi yetu na CCM yenyewe huko mbeleni.
Kipindi cha Mzee wa Ruska hapana shaka ndio kilikuwa kipindi ambacho ni sawa na kipindi cha Urusi na Gorbachev. Mabadiliko makubwa yalitokea katika kipindi hicho nchini, hata hivyo yaliweza kuwanufaisha wachache tu. Aidha baada ya Kipindi hicho kupita, Chama cha Mapinduzi kilifanikiwa kubadilisha mwelekeo wake na kwenda na wakati zaidi. Mafanikio katika hilo yaliweza kuonekana katika kipindi cha Mkapa. Tathimini nzuri itatokea mara baada ya Mwenyekiti wa sasa wa CCM kumaliza ngwe ya kwanza ya Uprez.
Nimezaliwa kijijini, pamoja na kutokuwa na vitu muhimu kama viatu na nguo nyingi lakini miaka yote ya utoto wangu sikuwahi kushinda njaa. Tulikuwa na vyakula vya kutosha, sikuwahi kumwona mtoto wa jirani au wa ndugu anashinda njaa. Kulikuwa na zahanati ambako hata kama mtu aliumwa ghafla usiku, basi kulikuwa na uwezekano wa kwenda kumwamsha daktari na kupata matibabu bila ulalamishi wala kuombwa pesa. Kulikuwa na shule nzuri tu, shule zilizokuwa zinaendeshwa na walimu wenye nia na lengo la kuwaendeleza watanzania wenzao, shule ambazo ubora wake haukuwa tofauti na ubora wa shule walizosoma watoto wa mawaziri mijini.
Hapa umeongeza chumvi Kamanda, Hakuna sehemu yoyote yenye uhakika wa kuishi kibinadamu zaidi katika Tanzania kama vijijini. Ukiondoa mabadiliko ya kiuchumi duniani, mabadiliko ya hali ya hewa na mashinikizo ya vyombo vikubwa vya fedha duniani, kijijini bado ni sehemu ambayo mtu anaweza kuishi kwa amani na kupata huduma muhimu vilevile.

Sina cha kufurahia kuhusu uhai wa CCM na badala yake hiyo sherehe itakuja fanyika siku CCM itakapo pelekwa theatre na kufanyiwa operation ili kuondoa cancer iliyotapakaa kila sehemu. Siku ambapo CCM itakubali kuachia madaraka japo kwa muda ili ifanyiwe matibabu makubwa kwa faida yake na Watanzania wote
Haupo peke yako katika hili wapo wengi na wengi wanaingia. Lakini ukweli ni kuwa CCM imefanya mengi na itaendelea kufanya mengi.
 
1. Kina mama wajawazito wanaokufa bila huduma nzuri
2. Watoto wachanga wanaokufa kwa magonjwa yanayotibika
Tusiongelee ushabiki tu, huduma za afya nchini zinazidi kuwa bora kila siku. Aidha kumekuwepo na matatizo ya watu binafsi katika kulinda afya zao na kufuata taratibu za kiafya katika kuhakikisha wanajifungua salama. Tatizo la watoto wengi kufa kabla ya kufikisha miaka 5, lipo kwa ukanda mzima wa kusini mwa jangwa la Sahara. Kwa upande wa serikali ya CCM inaendelea vema katika kupunguza na hatimae kuondoa tatizo hilo.
3. Wananchi wa Buzwagi na Bulyanhulu waliotimuliwa na ccm
4. Wananchi wa kanda ya ziwa ambayo ardhi yao imeuzwa kwa Barick
MMhm CCM haiwezi kutimua wananchi katika eneo lao pasipo kuwepo na sababu ya msingi ya kufanya hivyo. Na inapotokea kuwa watu wanaondolewa katika ardhi wanayomiliki kisheria basi taratibu zote hufuatwa.
Kwa upande mwingine wanavijiji uliowataja hapo juu, sasa wanaendelea kunufaika kwa kupata huduma bora na ongezeko la ajila kwa wanavijiji na watanzania kwa ujumla. Mambo ya kusikia kupitia redio za mbao wakati mwingine si nzuri. Ni vema siku moja ukaenda kutembelea huko na kupata ukweli.
5. Watanzania wanaolipia umeme kwa bei ya kuruka
6. Watanzania wa Kigoma ambao wametengwa na Tanzania
7. Wananchi wa vijijini wasio na barabara nzuri
8. Watoto wa shule wanaokaa kwenye mavumbi kusoma
9. Mamilioni ya watanzania wanaishi kwa mulo mmoja
Mambo mengine ni vichekesho, eti umeme wa kuruka? sijapta kusikia hilo! Ina maana kuwa Tanzania sasa kuna umeme wa magendo?
Na hilo la kigoma ndio chokochoko zingine ambazo hazina manufaa in long term.
Kwa ufupi matatizo ya madawati, barabara za vijini yamechangiwa na ongezeko la watu kuzidi hali halisi ya uchumi wa nchi. Aidha bado kuna juhudi za makusudi kabisa ya kuondoa matatizo hayo. Mifano ipo mingi katika hili. Kuhusu hao wa mlo mmoja ni wale ambao kwa makusudi kabisa wamekimbia vijijini na kuingia mjini kutafuta maisha bora. Ningependa kuwashauri kurudi huko vijini. Ile habari ya nguvu kazi haikutoka hewani, ilikuwa inakusudia watu wa aina hii.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
 
CCM imetimiza miaka 31 tangu kuanzishwa kwake. Pengine sherehe hizi mwaka huu ndio zitazokuwa za kimya kabisa kupita miaka mingine yote.

Hongera sana CCM

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI

Kidumu chama cha mapinduzi!? :confused:

No way! bora kife tu
 
Kwani CCM kama Chama imewakosea nini? Why can't you join CCM to clean the house.

Hongera kwa CCM kufikisha miaka 31, wakuu Kibunango, Mtu wa pwani, Pundamilia, ninawashukuru kwa misimamo iliyo huru, kusimamia mnacho kiamini,

Pia nimpongeze Mwafrika Wa Kike, kwa msimamo wa kupevuka kisiasa, yaaani siasa za accomodation, tunahitaji wengine humu Jf wenye kuelewa kuwa kwenye siasa za vyama vingi, dhana sio matusi tu na ugomvi, bali kushindana kihoja, maana matusi na ugomvi hufukuza wananchi wasioelewa yupi ni afadhali, kati ya vyama,

CCM imetimiza miaka 31, tunajua kuwa Roma, haikujengwa kwa siku moja, mkalengo na sera za CCM kama chama yako samba samba kabisa na mazingara tuliyonayo, kisiasa, tatizo kubwa lililotukumba CCM, ni viongozi wachache wabovu, na sio siri tena kwamba tuna mwenyekiti ambaye sio mkali, kitu ambacho kimewapa mwanya mafisadi kuharibu mipango mingi ya CCM kwa maendeleo ya wanachi. Tunategemea vyama vya siasa hasa upinzani kutukumbusha kila wakati kwenye hilo, kama wanavyofanya, maana ndio hasa nia na madhumuni ya kuwapatia ruzuku za kila mwezi ili waweze kuwa samba samba na serikali katika kuikosoa na kuirekebisha, kwenye hili natoa pongezi nyingi kwa upinzani kwa kazi ngumu waliyonayo ya kuturekebisha CCM.

Mwisho ninasema kuwa CCM tunahitaji mabadiliko makubwa sana kimaaadili, hasa ya uongozi, katiuka miaka ya karibuni tumeshusha mno vipimo vya uongozi, tumechaguana kwa kujuana, kirafiki, kindugu, bila ya kujali uwezo, hilo limtufikisha mahali pabaya sana, kama sio mwisho wa siasa kabisa, ninwashukuru wananchi kwa uvumilivu wao wa kutupa nafasi ya kujirekebisha, pamoja tutafika tu, salaam kwa wananchama wote wa CCM, popote pale mlipo, na wananchi wote wa Tanzania.

Mungu Aibariki Tanzania.
 
Back
Top Bottom