Mhh! Maskini! Wanamuomba msamaha kwa kosa lipi?

Hii nchi inavijana wengi wasomi wamezagaa mitaani, kama kunamfanyakazi anaona hatendewi haki, mara moja na haraka sana
bila shuruti aache kazi, ili kusudi waingie vijana wasomi na wachapakazi walokosa ajira, rizikeni na jiongezeni na mnachokipata.
Kaacha dokta mmoja tu Rais anapiga kelele kama zote je wakiacha wote si ndiyo atachanganyikiwa kabisa
 
Mwambie yaache kazi KBS



Akajiajiri


Uprofesa anashindwa kubuni njia mbadala ya kutoka kimaisha.

Si ndo nyie mnasema vijana mjiajiri? Au mnamaanishaga ajira ni za wazee?
Ndio maana amesema kwa niaba ya wafanyakazi wote
 
Hii nchi inavijana wengi wasomi wamezagaa mitaani, kama kunamfanyakazi anaona hatendewi haki, mara moja na haraka sana
bila shuruti aache kazi, ili kusudi waingie vijana wasomi na wachapakazi walokosa ajira, rizikeni na jiongezeni na mnachokipata.
Ukute huyo mfanyakazi ndio anawalisha hao vijana wasio na kazi mtaani Tanzania ni nchi ya kijamaa
 
Sio suala la kuridhika ni suala la haki ya mhusika, nchi hii tungejifunza kuacha ubinafsi wa kila mtu kudai chake kwa wakati wake tungefika mbali, tungesaidiana katika kudai kwa makundi makundi, mathalani leo waalimu kesho madaktari, kesho mapolisi keshokutwa watendaji wa vijiji.

Uchumi hautaki ubinafsi, hawa walipwa mshahara wakiongezewa ni faida kwao directly, na ni faida kwa wengine indirectly, akiwa na ziada ataspend zaidi pesa yake itazunguka mpaka kumfikia muuza urojo pale chumbageni.

Hata wewe jobless utajiajiri na biashara yako itasimama sababu kuna mtu kule usiyemjua purchasing power yake ni kubwa!
True said
 
Wewe kwa chuki zako ndo maana ulitumbuliwa mapema tu.
Mwache rais apambane kuweka uchumi wa hii nchi vyema, hata siku mishahara ikipandishwa thamani yake ionekane.

Bila kudhibiti mifumuko ya bei kwa bidhaa, mshahara hata upande bado mzigo utakuwa mkubwa tu kwa watumishi.

WAVUMILIE KIDOGO TU MAMBO YATAKUWA MSWANO.
Sasa mbona bidhaa zinazid kupanda bei mbali ya kwamba mshahara hajaongeza jwa miaka mingi?

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Mkuu hapa naona umeweka ubaguzi. mfanyakazi ni mfanyakazi bila kujali yupo serikalini au kampuni binafsi.
kwa ufahamu wangu mdogo,mliopo serikalini hasa hasa mamlaka(EWURA,PURA,LATRA,TRA,TCRA n.k) nao wamekutuma uombe msamaha?
Umechunguza wafanyakazi waliopo makampuni ya wahindi na wachina wanalipwaje ukilinganisha na mliopo serikalini ?

kwa ufupi sisi tuliopo makampuni binafsi tunawaonea wivu,sema tu nafasi za kuajiriwa serikalini ni kidogo tunalazimika kwenda makampuni binafsi. Suala la mfanya kazi kuwa na TIN nampongeza rais maana hata tulipokuwa hatuna TIN tulilipa pay as you earn wakati mamalaka hazikutambui kama mlipa kodi,utaratibu uliopo kwa sasa ni mzuri maana hata mimi natambulika kama mlipa kodi.

Ukienda dukani kkoo kwa kiasi fulani thamani ya fedha yako ndogo unaiona,ikilinganishwa na zamani ambapo fedha ndogo ya mshahara ilipambanishwa na fedha ya vigogo waliopiga mabilioni ya fedha na kwenda shopping ambapo wafanya biashara waliuza kwa faida zaidi ya mara mbili. Ni kweli kwa sasa mishahara haijaongezeka lakini kitu kinaitwa value for money kinaonekana.
Thamani ya fedha sina uhakika kama inaonekana, hivi nakupa mfano hai, kabla rais Kikwete hajaondoka madarakani kanda ya ziwa (Kagera) mfuko wa saruji wa kg 50 uliuzwa kati ya elf 14/15 hadi 16. Leo hii mfuko wa saruji huo huo unauzwa elf 22 kg 50. Hiv mwananchi wa kawaida ambaye sina uelewa na masuala ya fedha leo unaniambia thamani ya fedha inaonekana sidhan kama naweza kukuelewa. Saruji nimekupa mfano tu. Lakini jambo la ajabu sasa huko mpakani mwa nchi ya Tanzani-Uganda mfuko wa saruji kg 50 ni elf 16 TzS

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
 
Mawazo ya kukata tamaa hayo yaani utafikiri mtu katoka uzingizini kisa tu tamaa ya ajira,unapofanya kazi malipo ya halali ni haki yako wala siyo ombi kwa sababu ni jasho lako.
Hawajitambui na wana hasira za kutoajiriwa. UKWELI haukosewi. Uzalendo si kufanya kazi halafu usilipe ujira halali.
 
Kama nakuona vile,nani mbinafsi kati yangu mimi na wewe?
Vuta taswira yako nyuma kabla ya 2015 ulivyokuwa unatetea watawala, sasa umewekwa kando unatema cheche?
mimi nikiulizwa nimtaje mtu mwenye sura mbili siweziacha kukutaja wewe Salary Slip
Nimewahi kutetea watawala wa nchi hii hata siku moja? Watawala hawa wanaotoka na CCM ni lini niliwahi kuwatetea humu? Wewe kama una chuki na mimi au watumishi wa umma, uwe muwazi na si kuwa muongo,mzushi na mnafiki.
 
Nimewahi kutetea watawala wa nchi hii hata siku moja? Watawala hawa wanaotoka na CCM ni lini niliwahi kuwatetea humu? Wewe kama una chuki na mimi au watumishi wa umma, uwe muwazi na si kuwa muongo,mzushi na mnafiki.
Ninachoshukuru hujabadilisha jina, rudi nyuma kwenye post zako kabla ya 2015,hasa hasa post zinazohusu siasa.
Lakini sikulazimishi kuamini ushauri wangu. Nafsi ya mtu ndo shahidi namba moja wa mhusika.
kama imekuudhi nisamehe bure tuendelee kufurahia jamii forums.
 
Thamani ya fedha sina uhakika kama inaonekana, hivi nakupa mfano hai, kabla rais Kikwete hajaondoka madarakani kanda ya ziwa (Kagera) mfuko wa saruji wa kg 50 uliuzwa kati ya elf 14/15 hadi 16. Leo hii mfuko wa saruji huo huo unauzwa elf 22 kg 50. Hiv mwananchi wa kawaida ambaye sina uelewa na masuala ya fedha leo unaniambia thamani ya fedha inaonekana sidhan kama naweza kukuelewa. Saruji nimekupa mfano tu. Lakini jambo la ajabu sasa huko mpakani mwa nchi ya Tanzani-Uganda mfuko wa saruji kg 50 ni elf 16 TzS

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
Nadhani pia watu wa kagera wanauza ndizi hadi dodoma zinafika the same day tofauti na zamani ambapo ulikuwa ukibeba ndizi unazifikisha zimeishaiva,
tusiangalie upande mmoja wa shilingi tuangalie pande zote.kipindi ulichokitaja hapo juu fedha ya ufisadi ilikuwa nyingi mtaani ikikimbiza
vitu vichache,na hapa wafanyakazi tuliumizwa sana unless upo kwenye position ya kupiga deal,mfanyakazi wa kawaida tulisota sana.
ukienda dukani kununua nguo,unagombelezea ushushiwe bei mwingine anaomba afungiwe 5
 
Back
Top Bottom